NAIBU Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Makongoro Mahanga, mapungufu yaliyoko katika sheria za kazi hapa nchini, yanasababisha baadhi ya kampuni binafsi, kuajiri watu wageni hata kwa kazi zinazostahili kufanywa na Watanzania.
Dk Mahanga aliyasema hayo juzi kufuatia hoja iliyowasilishwa na Ofisa Kazi wa Mkoa wa Mara,Venance Kadago, ambaye alisema idara yake imekuwa ikifanya ukaguzi katika kampuni binafsi na kukuta wafanyakazi wa kigeni walioajiriwa kwa mikataba ya muda mfupi bila kuwa na vibali kutoka Wizara ya Kazi.
Ofisa huyo alisema vibali wanavyopewa wageni ili kuwaruhusu kuishi nchini, vinatoa mwanya kwa watu hao, kufanya kazi ambazo vinginevyo, zinaweza kufanywa na Watanzania.
"Mapungufu yaliyoko katika sheria ya sasa ndiyo yanayosababisha matatizo haya yote. Maofisa uhamiaji huko mikoani, wamekuwa wakitoa vibali vya kuwaruhusu wageni kuishi nchin," alisema Dk Mahanga.
Alisema kwa kutambua tatizo hilo, wizara yake inaandaa marekebisho ya sheria za kazi, itakayoainisha vizuri majukumu ya wizara katika kutoa vibali vya kazi na majukumu ya maofisa uhamiaji katika kutoa vibali vya wageni kuishi nchini.
Alisema hatua hiyo itasaidia kuondoa mwingiliano na mgongano wa majukumu ya wizara na uhamiaji.
Dk Mahanga alikuwa akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo wa Mkoa wa Mara ambapo alisema pamoja na utandawazi na nchi kuingia kwenye ushirikiano wa kikanda wa kiuchumi, biashara na ajira, si vyema kuruhusu kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania, kufanywa na wageni.
Alitumia mwanya huo kutoa rai kwa Wizara ya Mambo ya Ndani, kupitia Idara ya Uhamiaji, kushirikisha na wizara yake, kushughulikia matatizo yanayohusu ajira kwa wageni hata kama sheria bado zina mapungufu.
Source: Mwananchi.
Mtazamo: Hili jambo serikali yetu isiendeleze siasa kwa wingi na kusababisha jamii yetu iangamie. Latest statistics zinasema kila mwaka it is estimated around 700,000 graduates wanamaliza vyuoni na just 5.7% ndio wanaajiriwa katika kazi za maana (World Bank Figures). ILO wanasema kuwa 40% of youth population katika maeneo ya mijini kama Dar hawana kazi.
Wenzetu in developed economies wanakuwa na mikakati inaoleweka kuhusu hili swala hasa likija katika maendeleo ya nchi. Wazawa wanapokuwa na kazi unaongeza kiwango cha watu wenye kuwa na uwezo wa kumudu gharama za maisha na hilo linaongeza pia kiwango cha watu wenye kufanya matumizi na pia kuchangia katika kukua kwa sekta za viwanda na kilimo. Kutokana na hilo basi ajira ni sekta muhimu sana nchini kuweza kutoa nafasi ya maendeleo ya kweli kwa watanzania.
Tukiangalia dunia ya leo ajira za nchi zilizoendelea huwa zinaenda kwa mpangilio unaoeleweka. Kuna ajira wanaweza kupewa wazawa kwani supply yake iko kubwa sana. Mfano sekta ya kilimo (casual labourers) Serikali ingelitoa kipaumbele zaidi kwa wazawa kupewa hizo kazi ili kupunguza hili tatizo la watu kukosa kazi.
Vile vile kazi za maofisini kuna sekta kama biashara, Information technology particularly katika user-end services, Engineering, wazawa wangelipewa mkazo na makampuni binafsi yangeliambiwa kuwa watoekipaumbele kutoa ajira kwa watoto wetu wanaomaliza vyuoni kupata kazi katika maeneo hayo. Kukitokea makampuni binafsi yanadai hawajapata mtu wangelitakiwa wamfanyie recruitment mzawa wakati wamemuajiri mgeni ili akimaliza katika kipindi maalum aje kurithi nafasi ya yule expatriate.
Kuna sekta zina mapungufu ya wafanyakazi kwasababu soko la wafanyakazi halikidhi mahitaji. Mfano waalimu hasa waalimu wa masomo ya hisabati na kiingereza hapo wangeliruhusu kuleta foreign nationals waje kufundisha (kwa limited period mfano 5 years basi). Hilo lingelisaidia kutoa nafasi ya wazawa yaani waalimu wetu kuwa wamesomea wakafuzu kuja kufidia hii kiu ya mahitaji ya watu katika sekta hiyo. Pia sekta nyengine kama kilimo pia wangelifanya hivyo hivyo.
Wawekezaji nadhani ni wakati muafaka serikali yetu ikafafanua nani anaweza kujulikana kama muekezaji tanzania. Wawekezaji njaa kama wachina wanaofanya biashara za umachinga kariakoo ni wakati muafaka wangelidhibitiwa kutoa nafasi kwa vijana wetu waweze kujiajiri. Pia small scale business should be protected ili wapate vijana wetu waweze kujiajiri na kutoa nafasi ya kukua kwa mzunguko wa pesa. Binafsi wawekezaji Tanzania wangelitakiwa wawe na si chini ya milioni 100 na wawe wanaajiri wazawa katika shughuli zao. Hili lingelisaidia kuondoa tatizo.
Naibu waziri angelitakiwa kufahamu kuwa ijapokuwa analivutia pumzi swala hili pia afahamu kuwa vijana wengi hawana kazi. Director wa Youth Development kutoka wizara kazi alisema 60% ya vijana wengi hawana kazi Tanzania. Hili sio jambo zuri kwani hawa vijana ndio nguvu kazi ya taifa inayopotea na kodi inayoyoma. Ni vema serikali ikajaribu kuwatafutia namna waweze kupunguza hili tatizo at the same time walinde zile kazi chache zilizopo nchini.
Failure do this inapelekea kuongezeka kwa vijana mitaani wasio na shughuli maalum, kukua kwa uhalifu nchini kwasababu hawana njia za kujipatia kipato, Kuongezeka kwa maradhi kama vile ukimwi kutokana na wengine kujitafutia riziki kwa njia zisizo rasmi (ukahaba), Kukua kwa watoto wengi mitaani kutokana na wazazi kushindwa kumudu gharama za maisha, na mwisho wa siku jamii yetu kupotea kwasababu nguvu kazi haijatumika kabisa. Ni mtazamo tu. Nilikuwapo!!!!
Dk Mahanga aliyasema hayo juzi kufuatia hoja iliyowasilishwa na Ofisa Kazi wa Mkoa wa Mara,Venance Kadago, ambaye alisema idara yake imekuwa ikifanya ukaguzi katika kampuni binafsi na kukuta wafanyakazi wa kigeni walioajiriwa kwa mikataba ya muda mfupi bila kuwa na vibali kutoka Wizara ya Kazi.
Ofisa huyo alisema vibali wanavyopewa wageni ili kuwaruhusu kuishi nchini, vinatoa mwanya kwa watu hao, kufanya kazi ambazo vinginevyo, zinaweza kufanywa na Watanzania.
"Mapungufu yaliyoko katika sheria ya sasa ndiyo yanayosababisha matatizo haya yote. Maofisa uhamiaji huko mikoani, wamekuwa wakitoa vibali vya kuwaruhusu wageni kuishi nchin," alisema Dk Mahanga.
Alisema kwa kutambua tatizo hilo, wizara yake inaandaa marekebisho ya sheria za kazi, itakayoainisha vizuri majukumu ya wizara katika kutoa vibali vya kazi na majukumu ya maofisa uhamiaji katika kutoa vibali vya wageni kuishi nchini.
Alisema hatua hiyo itasaidia kuondoa mwingiliano na mgongano wa majukumu ya wizara na uhamiaji.
Dk Mahanga alikuwa akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo wa Mkoa wa Mara ambapo alisema pamoja na utandawazi na nchi kuingia kwenye ushirikiano wa kikanda wa kiuchumi, biashara na ajira, si vyema kuruhusu kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania, kufanywa na wageni.
Alitumia mwanya huo kutoa rai kwa Wizara ya Mambo ya Ndani, kupitia Idara ya Uhamiaji, kushirikisha na wizara yake, kushughulikia matatizo yanayohusu ajira kwa wageni hata kama sheria bado zina mapungufu.
Source: Mwananchi.
Mtazamo: Hili jambo serikali yetu isiendeleze siasa kwa wingi na kusababisha jamii yetu iangamie. Latest statistics zinasema kila mwaka it is estimated around 700,000 graduates wanamaliza vyuoni na just 5.7% ndio wanaajiriwa katika kazi za maana (World Bank Figures). ILO wanasema kuwa 40% of youth population katika maeneo ya mijini kama Dar hawana kazi.
Wenzetu in developed economies wanakuwa na mikakati inaoleweka kuhusu hili swala hasa likija katika maendeleo ya nchi. Wazawa wanapokuwa na kazi unaongeza kiwango cha watu wenye kuwa na uwezo wa kumudu gharama za maisha na hilo linaongeza pia kiwango cha watu wenye kufanya matumizi na pia kuchangia katika kukua kwa sekta za viwanda na kilimo. Kutokana na hilo basi ajira ni sekta muhimu sana nchini kuweza kutoa nafasi ya maendeleo ya kweli kwa watanzania.
Tukiangalia dunia ya leo ajira za nchi zilizoendelea huwa zinaenda kwa mpangilio unaoeleweka. Kuna ajira wanaweza kupewa wazawa kwani supply yake iko kubwa sana. Mfano sekta ya kilimo (casual labourers) Serikali ingelitoa kipaumbele zaidi kwa wazawa kupewa hizo kazi ili kupunguza hili tatizo la watu kukosa kazi.
Vile vile kazi za maofisini kuna sekta kama biashara, Information technology particularly katika user-end services, Engineering, wazawa wangelipewa mkazo na makampuni binafsi yangeliambiwa kuwa watoekipaumbele kutoa ajira kwa watoto wetu wanaomaliza vyuoni kupata kazi katika maeneo hayo. Kukitokea makampuni binafsi yanadai hawajapata mtu wangelitakiwa wamfanyie recruitment mzawa wakati wamemuajiri mgeni ili akimaliza katika kipindi maalum aje kurithi nafasi ya yule expatriate.
Kuna sekta zina mapungufu ya wafanyakazi kwasababu soko la wafanyakazi halikidhi mahitaji. Mfano waalimu hasa waalimu wa masomo ya hisabati na kiingereza hapo wangeliruhusu kuleta foreign nationals waje kufundisha (kwa limited period mfano 5 years basi). Hilo lingelisaidia kutoa nafasi ya wazawa yaani waalimu wetu kuwa wamesomea wakafuzu kuja kufidia hii kiu ya mahitaji ya watu katika sekta hiyo. Pia sekta nyengine kama kilimo pia wangelifanya hivyo hivyo.
Wawekezaji nadhani ni wakati muafaka serikali yetu ikafafanua nani anaweza kujulikana kama muekezaji tanzania. Wawekezaji njaa kama wachina wanaofanya biashara za umachinga kariakoo ni wakati muafaka wangelidhibitiwa kutoa nafasi kwa vijana wetu waweze kujiajiri. Pia small scale business should be protected ili wapate vijana wetu waweze kujiajiri na kutoa nafasi ya kukua kwa mzunguko wa pesa. Binafsi wawekezaji Tanzania wangelitakiwa wawe na si chini ya milioni 100 na wawe wanaajiri wazawa katika shughuli zao. Hili lingelisaidia kuondoa tatizo.
Naibu waziri angelitakiwa kufahamu kuwa ijapokuwa analivutia pumzi swala hili pia afahamu kuwa vijana wengi hawana kazi. Director wa Youth Development kutoka wizara kazi alisema 60% ya vijana wengi hawana kazi Tanzania. Hili sio jambo zuri kwani hawa vijana ndio nguvu kazi ya taifa inayopotea na kodi inayoyoma. Ni vema serikali ikajaribu kuwatafutia namna waweze kupunguza hili tatizo at the same time walinde zile kazi chache zilizopo nchini.
Failure do this inapelekea kuongezeka kwa vijana mitaani wasio na shughuli maalum, kukua kwa uhalifu nchini kwasababu hawana njia za kujipatia kipato, Kuongezeka kwa maradhi kama vile ukimwi kutokana na wengine kujitafutia riziki kwa njia zisizo rasmi (ukahaba), Kukua kwa watoto wengi mitaani kutokana na wazazi kushindwa kumudu gharama za maisha, na mwisho wa siku jamii yetu kupotea kwasababu nguvu kazi haijatumika kabisa. Ni mtazamo tu. Nilikuwapo!!!!