Serikali yasikia kilio cha wanafunzi wa vyuo

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Serikali yasikia kilio cha wanafunzi wa vyuo
Veronica Mheta
Daily News; Friday,November 21, 2008 @20:21

Kutokana na kukithiri kwa vitendo vya migomo katika vyuo vya elimu ya juu hasa vya umma, Serikali imeamua kuunda kamati kupitia na kutoa mapendekezo ya namna ya kuboresha utekelezaji wa Sera ya Uchangiaji wa Elimu ya Juu.

Kamati hiyo inajumuisha wajumbe saba ambao wanatoka katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, mwanafunzi mmoja kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), mwanafunzi mmoja kutoka Umoja wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu (TAHLISO), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, pamoja na wataalamu kutoka Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT).

Hayo yalisema jana Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Gaudentia Kabaka wakati alipokuwa akitoa tamko la serikali kuhusu kufungwa kwa vyuo vikuu vya umma. Kabaka alisema si rahisi kurekebisha sera ya uchangiaji wa elimu kwa mara moja, ni lazima mchakato ufanyike kisha ujadiliwe na wataalamu mbalimbali na kupelekwa bungeni kujadiliwa tena na hatimaye sera iweze kubadilishwa.

“Lakini huu ni mchakato na hatua hii inachukua muda,” alisema Kabaka. Aliongeza kuwa sera ya uchangiaji inalenga kutumia rasilimali na fedha kidogo za serikali ili kuwawezesha wanafunzi wengi zaidi kupata elimu ya juu. Alisema hivyo si busara kwa serikali kwa sasa kuwalipia wanafunzi asilimia 100 kama wanavyotaka hata kwa wale wanafunzi wanaotoka kwenye familia zenye uwezo.

Wanafunzi wa vyuo wamelazimika kugoma kuingia madarasani kutokana na kugomea sera ya uchangiaji wanayodai kuwa ina upungufu mwingi na kwamba haiwatendei haki wanafunzi hasa wanaotoka katika familia za watu ambao hawana uwezo wa kifedha. Wanafunzi hao wanadai baadhi ya wanafunzi wanaotoka familia moja wanapewa madaraja tofauti ya mikopo, hali inayoonyesha kuwa bodi ya mikopo haiko makini wakati wa kuchambua vigezo vya kutoa mikopo hiyo.

Sababu hizo ndizo zimesababisha wanafunzi hao kugoma kwani wengi wao wameshindwa kuendelea na masomo kutokana na kushindwa kulipa ada wanayotakiwa kuchangia baada ya kupewa mkopo. Kwa upande wake, Kabaka alisema bajeti ya mwaka 2008/2009 ni Sh bilioni 117, ambazo zinatosheleza wanafunzi 42,000 tu ambao wangeweza kukopeshwa kama serikali ingekuwa inatoa asilimia 100.

Lakini alisema kwa sasa wanafunzi 60,000 wapo vyuoni. “Kuwapatia wanafunzi 60,000 mkopo wa asilimia 100 kungehitaji kiasi cha Sh bilioni 163.7 ambazo serikali haina uwezo wa kuzipata fedha.” Kabaka alisema hivi sasa kila chuo kipo kwenye mchakato wa kuwabaini wanafunzi wanaokubaliana na sera ya uchangiaji wa elimu ili waweze kurudi vyuoni kwa kutumia sheria na taratibu zilizowekwa na vyuo.

Alisisitiza kuwa wanafunzi watakaokubaliana na sera ya uchangiaji wa elimu ndio wataoweza kuingia madarasani kusoma; lakini wanafunzi ambao hawatakubaliana na sera hiyo wataendelea kukaa nyumbani hadi hapo watakapokubali wenyewe.

“Kubadilisha sera ya uchangiaji si kwa haraka kama wanavyodai wanafunzi, kunahitaji muda na Bunge kupitia marekebisho hayo hivyo wanafunzi watakaokubaliana na sera ya uchangiaji wa elimu ndio wataweza kurudi vyuoni endapo wasipokubaliana nayo wataendelea kukaa nyumbani kwao hadi hapo watakapoamua kuikubaliana nayo”.

Pia Kabaka alisema gharama inayotozwa na vyuo vikuu vya umma siyo halisi na serikali inachangia gharama kwa kiasi kikubwa na kueleza kuwa gharama halisi ya kozi ya udaktari wa binadamu kwa Chuo Kikuu cha Muhimbili ni Sh milioni 4.3 lakini mwanafunzi hulipa Sh milioni 1.0 kwa mwaka.

Pia ada halisi kwa kozi ya udaktari wa Tiba ya Wanyama, Chuo Kikuu cha Sokoine ni Sh milioni 32 kwa mwaka; lakini mwanafunzi hulipa Sh milioni 1.2 na kwa upande wa Shahada ya Biashara, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam gharama halisi ni Sh milioni tatu ila mwanafunzi analipa Sh milioni 1.25.

Hadi sasa wanafunzi wa vyuo vikuu saba wamerudishwa nyumbani kwa muda usiojulikana kwa madai ya kutaka sera ya uchangiaji wa gharama za elimu ya juu ifutwe au kufanyiwa marekebisho ili wanafunzi wote wapewe mikopo kwa asilimia 100 ambapo chanzo chake ni wanafunzi hao kuendelea na migomo hata baada ya uongozi wa vyuo kuasihi wasitishe migomo hiyo ilishindikana.

Akizungumzia hasara inayoipata serikali kutokana na migomo hiyo, Kabaka alisema wanasubiri takwimu sahihi toka vyuo mbalimbali vilivyogoma ili kujua hasara inayoendelea kuipata serikali juu ya migomo hiyo na kusisitiza kuwa migomo hiyo imesababisha wanafunzi wanaohitaji elimu kuikosa kwa wakati unaotakiwa.
 
Sioni kama kuna ufumbuzi wowote hapo. Bado tutajikuta tena kwenye migomo. Naibu waziri anasema wale watakaokubaliana na sera ya kuchangia ndio watarudi, na wale wasiokubali watakaa nyumbani mpaka wakubali. Mimi nadhani hapa hatujatatua kitu. Maana mgomo umesababishwa na wale wanaopinga kuchangia kwa 100%.

Wafanye hiyo research yao tuone watakuja na jipya lipi. Maana tukumbuke katika kuunda bodi wa mikopo kwa elimu ya juu, research pia ilifanyika na ikaja na majibu ya huu utumbo ulioko sasa.
 
Kama kawaida serikali haina solution mbali na vitisho. Wanasahau kwamba sasa wakati wa vitisho umefika mwisho.
Urusi mambo yalipofika mwisho ujamaa ulikufa. China pia. Na ujerumani mashariki mambo yalipochacha ukuta ule ulitelemshwa chini na nchi ikabaki moja si mbili tena.
Nimesikia na IGP naye kawa mwanasiasa siku hizi. Anatangaza vitisho. Huko sijui kunamhusu nini. Dalili ya ujinga na kutumiwa na watawala badala ya kufanya kazi ya kutulind raia tunaopigwa mabomu ndani ya nyumba zetu. Na kuingiliwa na majambazi.
Alijaribu Tarime akashindwa. Asubiri kushindwa hata kwa hili la wanafunzi.
Jamani viongozi wetu wasome nyakati. Hapa kutishana mwisho. Wabadilike au tuwabadili.
 
Naupenda sana huu utaratibu wa tume, kamati nk

Pengine Pinda aweke utaratibi wa kuomba "kibali" kabla ya kuunda hizi tume kama ilivyo kwenye makongamano, semina na warsha
 
billion 163 mboni ni karibu sana na zile za EPA. Kwa vile ni emergency case, watumie pesa za EPA zilizorudishwa. Pia wabunge wajitolee kutopata perdiems kikao kijacho cha bunge, wasilipwe pesa za wasaidizi na mafuta ya gari. Watumie mshahara wao tu ambao ni Tshs 1.5m kwa mwenzi na mambo mengine.

Mbona pesa za kuisaidia TRL zilipatikana fasta? na hizi zipatikane tu. Huo mchakato nahisi umetake into account fedha ambazo tayari wanafunzi wameshapewa kwa sasa. Hivyo wanahitaji kafungu ka nyongeza tu.

Zaidi ya hivyo, wanafunzi waliofukuzwa kwa mgomo tu ndio waongezewe hicho kiwango kwani wao ndio wameonyesha kutoridhika na kiasi wanachokipata.
 
Kama una moyo mwepesi usisome ripoti hii na msidhanie mko kwenye back to the future..!!!
 

Attachments

  • RIPOTI YA MATATIZO YA MIGOMO ELIMU YA JUU.doc
    388 KB · Views: 435
Kwa nini ni wazimu? Au sitakiwi kuuliza kwa nini ni wazimu?

Angalia jibu moja kabla ya hilo la mama hapo juu... utaona kwanini ni wazimu kuunda tume kuchunguza matatizo ya elimu ya juu na kutoa mapendekezo ya suala zima la uchangiaji elimu ya juu!
 
Angalia jibu moja kabla ya hilo la mama hapo juu... utaona kwanini ni wazimu kuunda tume kuchunguza matatizo ya elimu ya juu na kutoa mapendekezo ya suala zima la uchangiaji elimu ya juu!

Okay...sasa kama ni wazimu tufanye nini ili tuondokane nao?
 
Tutaunda kamati ngapi? Maana kila kitu kinaundiwa kamati na hatuoni matunda yake....

.... na ndiyo huo wazimu aliousema!!!


.... by the way, mmeona heading hiyo kwenye gazeti la serikali?.... eti "serikali yasikia kilio" what a joke :(
 
.... na ndiyo huo wazimu aliousema!!!
.... by the way, mmeona heading hiyo kwenye gazeti la serikali?.... eti "serikali yasikia kilio" what a joke :(

Ukisikia usanii ndio huu, ukisikia ubabaishaji ndio huu, ukisikia upofu ndio huu, na ukisikia ujinga ndio huu. Lakini kibaya zaidi ni kwa watanzania kukubali, kuruhusu na kukumbatia fedheha kama hizi. Kwenye nchi za wenzetu serikali kama hii ya kwetu kamwe haingedumu hata kwa siku moja - ndio wazimu wenyewe na unasikitisha.
 
NI KWELI HUU SASA NI WAZIMU,

Kuna mtu mmoja humu JF huwa anasema, "miafrika ndivyo tulivyo" watu wanapinga, pia mtaalam wa DNA alitoa comment moja ya kuwa-undermine Waafrica hee watu walikuwa wakali kweli kweli, hata hivyo 'miafrika ndivyo tulivyo'

Kama hatuko hivyo, Tuonyeshe kwa vitendo!!
 
Kwangu mimi kichwa kizuri cha habari hiyo kingekuwa "serikali yajibu mapigo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu juu"
Nimependezwa na suala la uwakilishi wa wanavyuo katika hiyo kamati,ila sijui ni kivipi watawachagua/wamewachagua hao wawakilishi.Maana wanaweza kujipa mtereko kwa kuwa_pick akina 'yes sir' kind of person!
 
.... na ndiyo huo wazimu aliousema!!!


.... by the way, mmeona heading hiyo kwenye gazeti la serikali?.... eti "serikali yasikia kilio" what a joke :(

'Siri kali' lazima itafute mlango wa kutokea kwenye kasheshe hii na mlango huo ni kupitia kwenye kuunda tume nyingine!!!! Tume kila kukicha na hatuoni la maana lolote kutoka kwenye tume hizo. Tume ya Mwakyembe ilishauri Hosea wa TAKUKURU na Mwanasheria Mkuu wastaafishwe lakini hadi hii leo bado wanapeta na mapendekezo chungu nzima ya tume hiyo hayafanyiwa kazi. Tume ya madini ambayo iliangalia mambo mbali mbali ikiwemo mikataba na Kiwira bado mpaka leo mengi ndani ya ripoti ya tume hiyo ni siri na Ngeleja hajasema lolote kuhusu Kiwira kama umiliki wake utarudishwa kwa Watanzania au fisadi Mkapa ataendelea kuimiliki. Usanii kila kukicha!!! halafu Msekwa bila woga wala aibu anadai JK kafanya mengi mazuri tangu aingie madarakani!!!!! kwa hiyo anastahili tena kupewa awamu nyingine!!!! :confused:
 
Ushauri wangu kwa Mh. Gaudensia Kabaka. Srea ya uchangiaji katika elimu ya juu kwa Tanzania umeshindwa kutekelezeka kama inavyoonyeshwa katika makabrasha. Kwa sasa Watanzania wako wa matabaka mbali mbali, kiufupi wapo matajiri sana, matajiri, masikini sana na masikini wastani. Katika mchakato mzima kumekuwa kukifanyika viini macho ambavyo ndiyo chanzo cha migomo. Unakuta watoto wanaotoka familia masikini ndiyo hao wanaotakiwa kuchangia asilimia kubwa zaidi ya mtoto anayetoka familia tajiri. Kutokana na ukiukwaji huu wa utaratibu uliowekwa, ndipo wanafunzi wameitaka serikali iwakopeshe kwa asilimia mia moja kila mwanachuo ili kuepusha malalamiko kama haya. Hii itasaidia sana hata katika ufuatiliaji wake kwani mwanafunzi atatakiwa kulipa asilimia mia moja mara amalizapo masomo yake. Hii ingesaidia hata kama kumbu kumbu zinapotea. KABAKA ELEWA UNDANI WA KILIO CHA WANAFUNZI HAWA SIYO JUU JUU KAMA ULIVYO AINISHA- GO DEEP KABAKA.
 
Back
Top Bottom