BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Hili lilishazungumziwa zaidi ya miezi 12 iliyopita, lakini hakuna chochote kilichofanyika. Serikali ya kisanii imeliibua tena sijui kama sasa hivi watakuwa serious.
Angalia hapa.
Date::9/3/2008
Serikali yashtukia uzito wa mzigo wa mashangingi ya viongozi
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
SERIKALI inafanya marekebisho makubwa ya namna ya udhibiti wa uendeshaji wa magari ya kifahari kwa mawaziri na viongozi wengine kuondokana na matumizi mabaya ya mali za umma.
Hayo yamo katika ripoti ya Mpango wa Serikali kuhusu Orodha ya Magari yake na Kudhibiti Matumizi ambayo imependekezwa pamoja na mambo mengine magari ya kifahari ya mawaziri maarufu kama mashangingi yanunuliwe kila baada ya miaka saba badala ya miwili ya sasa.
Utaratibu wa sasa ni kwamba, gari la waziri huweza kununuliwa kila baada ya miaka miwili tangu linunuliwe na kuanza kutumika, kisha hutumiwa na watendaji wa ngazi ya chini, au kuuzwa au waziri 'kujiuzia'.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya serikali ya mwezi Aprili 2008, ambayo gazeti hili imefanikiwa kuona nakala yake mapema wiki hii, jumla ya magari yote ya serikali nchini yamebainika ni kati ya 35,000 hadi 40,000.
Ndani ya ripoti hiyo ambayo tayari nakala anayo Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo, kati ya orodha hiyo magari ya kifahari ya Toyota Landcruiser Vx na Gx na aina nyingine ya Landcruiser ni kati ya 10,000 hadi 15,000.
Takwimu za sasa, gari moja aina Toyota VX au Toyota GX, hadi kuliingiza nchini ni kati ya Sh 80 hadi 120 milioni ambayo ni kwa ajili ya serikali, huku gharama za operesheni ikiwa ni pamoja na matengenezo ya kila wiki na mafuta ni kati ya Sh moja hadi 1.5 milioni, kutegemea safari.
Ripoti hiyo ya kitaalamu ambayo inalenga kuishauri serikali namna ya kupunguza matumizi mabaya ya fedha za umma katika ununuzi na uendeshaji magari ikiwemo hayo ya kifahari, katika mapendekezo yake inaonyesha pia haja ya kupunguzwa kwa orodha hiyo ya magari kwa kiwango cha nusu.
Katika ripoti hiyo, magari hayo 40,000 ni kuanzia Serikali Kuu na Halmashauri za Wilaya, miji, manispaa na majiji, ambayo ni pamoja na yale ya miradi maarufu kama DFP ambayo hutokana na wafadhili.
Orodha hiyo inaonyesha sehemu kubwa ya magari hayo ni Toyota Pickup na Hard Top, ambazo zimekuwa zikitumika zaidi vijijini huku mashangingi ya Vx na Gx yakirandaranda mijini.
Kutokana na mapendekezo ya Ripoti hiyo, chini ya mpango huo pia serikali inashauriwa kupunguza matumizi ya magari hayo ya Gx na Vx katika ngazi za Serikali za Mitaa.
Pendekezo hilo katika ngazi ya Serikali za Mitaa, linataka Mkuu wa Mkoa pekee ndiye atumie Vx ili kuwezesha Rais anapofika aweze kulitumia huku Wakuu wa Wilaya na watendaji wengine wakitakiwa kupatiwa gari za kawaida kama Toyota Landcruiser si Vx.
Katika mapendekezo hayo ya kitaalamu ambayo ni dira ya kupunguza matumizi mabaya ya fedha za umma, yanataka pia wakurugenzi wa wizara na watendaji wa mashirika mbalimbali na taasisi za umma, wasitumie Vx badala yake watumie magari ya kawaida.
Iwapo Ripoti hiyo itatekelezwa, serikali itaweza kupunguza magari yake kwa kiasi cha nusu hivyo pia kuweza kuokoa mabilioni ya shilingi katika kuendesha magari hayo na ununuzi.
Ripoti hiyo yenye kurasa zaidi ya 100, pamoja na mambo mengine imeanisha magari ya kila wizara, idara, taasisi mbalimbali ikiwemo yale ya miradi.
Baadhi ya wizara kama Afya na Ustawi wa Jamii, zimeonekana kuwa na magari mengi makao makuu huku katika ngazi za Serikali za Mitaa kukikosekana magari ya kutosha kuhudumia wananchi.
Pia Ripoti hiyo imeonyesha kwamba, wakati kukiwa na magari mengi makao makuu ya wizara mbalimbali, bado Jeshi la Polisi limekuwa na uhaba wa magari katika maeneo mengi nchini ikiwemo ya mipakani.
Ripoti hiyo imekamilika wakati kukiwa na malalamiko kutoka kwa wananchi, kuhusu matumizi ya serikali katika kununua magari ya kifahari wakati nchi ni maskini.
Kutokana na malalamiko hayo, mwaka jana serikali iliamua kuunda timu ya wataalamu ikimhusisha Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu, ili kuona na kupata ushauri wa namna bora ya kupunguza matumizi katika kununua na kuendesha magari ya kifahari na mengine bila sababu za msingi.
Angalia hapa.
Date::9/3/2008
Serikali yashtukia uzito wa mzigo wa mashangingi ya viongozi
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
SERIKALI inafanya marekebisho makubwa ya namna ya udhibiti wa uendeshaji wa magari ya kifahari kwa mawaziri na viongozi wengine kuondokana na matumizi mabaya ya mali za umma.
Hayo yamo katika ripoti ya Mpango wa Serikali kuhusu Orodha ya Magari yake na Kudhibiti Matumizi ambayo imependekezwa pamoja na mambo mengine magari ya kifahari ya mawaziri maarufu kama mashangingi yanunuliwe kila baada ya miaka saba badala ya miwili ya sasa.
Utaratibu wa sasa ni kwamba, gari la waziri huweza kununuliwa kila baada ya miaka miwili tangu linunuliwe na kuanza kutumika, kisha hutumiwa na watendaji wa ngazi ya chini, au kuuzwa au waziri 'kujiuzia'.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya serikali ya mwezi Aprili 2008, ambayo gazeti hili imefanikiwa kuona nakala yake mapema wiki hii, jumla ya magari yote ya serikali nchini yamebainika ni kati ya 35,000 hadi 40,000.
Ndani ya ripoti hiyo ambayo tayari nakala anayo Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo, kati ya orodha hiyo magari ya kifahari ya Toyota Landcruiser Vx na Gx na aina nyingine ya Landcruiser ni kati ya 10,000 hadi 15,000.
Takwimu za sasa, gari moja aina Toyota VX au Toyota GX, hadi kuliingiza nchini ni kati ya Sh 80 hadi 120 milioni ambayo ni kwa ajili ya serikali, huku gharama za operesheni ikiwa ni pamoja na matengenezo ya kila wiki na mafuta ni kati ya Sh moja hadi 1.5 milioni, kutegemea safari.
Ripoti hiyo ya kitaalamu ambayo inalenga kuishauri serikali namna ya kupunguza matumizi mabaya ya fedha za umma katika ununuzi na uendeshaji magari ikiwemo hayo ya kifahari, katika mapendekezo yake inaonyesha pia haja ya kupunguzwa kwa orodha hiyo ya magari kwa kiwango cha nusu.
Katika ripoti hiyo, magari hayo 40,000 ni kuanzia Serikali Kuu na Halmashauri za Wilaya, miji, manispaa na majiji, ambayo ni pamoja na yale ya miradi maarufu kama DFP ambayo hutokana na wafadhili.
Orodha hiyo inaonyesha sehemu kubwa ya magari hayo ni Toyota Pickup na Hard Top, ambazo zimekuwa zikitumika zaidi vijijini huku mashangingi ya Vx na Gx yakirandaranda mijini.
Kutokana na mapendekezo ya Ripoti hiyo, chini ya mpango huo pia serikali inashauriwa kupunguza matumizi ya magari hayo ya Gx na Vx katika ngazi za Serikali za Mitaa.
Pendekezo hilo katika ngazi ya Serikali za Mitaa, linataka Mkuu wa Mkoa pekee ndiye atumie Vx ili kuwezesha Rais anapofika aweze kulitumia huku Wakuu wa Wilaya na watendaji wengine wakitakiwa kupatiwa gari za kawaida kama Toyota Landcruiser si Vx.
Katika mapendekezo hayo ya kitaalamu ambayo ni dira ya kupunguza matumizi mabaya ya fedha za umma, yanataka pia wakurugenzi wa wizara na watendaji wa mashirika mbalimbali na taasisi za umma, wasitumie Vx badala yake watumie magari ya kawaida.
Iwapo Ripoti hiyo itatekelezwa, serikali itaweza kupunguza magari yake kwa kiasi cha nusu hivyo pia kuweza kuokoa mabilioni ya shilingi katika kuendesha magari hayo na ununuzi.
Ripoti hiyo yenye kurasa zaidi ya 100, pamoja na mambo mengine imeanisha magari ya kila wizara, idara, taasisi mbalimbali ikiwemo yale ya miradi.
Baadhi ya wizara kama Afya na Ustawi wa Jamii, zimeonekana kuwa na magari mengi makao makuu huku katika ngazi za Serikali za Mitaa kukikosekana magari ya kutosha kuhudumia wananchi.
Pia Ripoti hiyo imeonyesha kwamba, wakati kukiwa na magari mengi makao makuu ya wizara mbalimbali, bado Jeshi la Polisi limekuwa na uhaba wa magari katika maeneo mengi nchini ikiwemo ya mipakani.
Ripoti hiyo imekamilika wakati kukiwa na malalamiko kutoka kwa wananchi, kuhusu matumizi ya serikali katika kununua magari ya kifahari wakati nchi ni maskini.
Kutokana na malalamiko hayo, mwaka jana serikali iliamua kuunda timu ya wataalamu ikimhusisha Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu, ili kuona na kupata ushauri wa namna bora ya kupunguza matumizi katika kununua na kuendesha magari ya kifahari na mengine bila sababu za msingi.