nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
*Maige amsimamisha mkurugenzi wanyamapori
*Msekwa ajibu tuhuma za ufisadi Ngorongoro
*Mgawo wa umeme walalamikiwa upya bungeni
Na Waandishi Wetu
SAKATA la kutorosha wanyamapori kwenda nje ya nchi limeishtua serikali kutoka usingizini baada ya Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Bw. Obeid Mbwangwa na watendaji wengine wawili kusimamishwa kazi na serikali ili kupisha uchunguzi.
Bw. Mbwangwa amekumbwa na hali hiyo zikiwa ni siku chache baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo, na siku moja baada ya wabunge kutaka hatua zichukuliwe haraka kwa wahusika, akiwamo mkurugenzi huyo na wanyama walioibwa warejeshwe ama wakiwa hai au wamekufa.
Kutokana na agizo la Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wa mkurugenzi wa awali, Bw. Erasmus Tarimo Februari 8, mwaka huu na kumpatia likizo ya kusubiria kustaafu ambapo kwa mujibu wa sheria Julai 7, mwaka huu ndipo Bw. Mbwangwa alishika wadhifa huo kutoka nafasi ya Mkurugenzi Msaidizi wa wizara hiyo.
Tamko la kusimamishwa kazi kwa Bw. Mbwangwa na wenzake wawili ambao hawakutajwa majina ili kupisha uchunguzi, lilitolewa jana bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii, Bw. Ezekiel Maige wakati akifanya majumuisho ya makadirio na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2011 na 2012.
"Mheshimiwa Spika kutokana na malalamiko mengi ambayo waheshimiwa wamelizungumzia ni suala la kutoroshwa kwa wanyamapori, ninashukuru sana na maoni ya kamati juu ya suala hili ni nimeyazingatia," alisema Bw. Maige
"Hivyo basi kuanzia leo Agosti 18, 2011 Mkurugenzi wa Maliasili na Utalii, Obeid Mbwangwa na wenzake wawili ambao kutokana na uchunguzi wa jambo hili sitawataja hapa, nimewasimamisha kazi rasmi, ili kupisha uchunguzi wa utoroshaji wa wanyamapori hao," aliongeza.
Kilio cha wabunge
Wabunge jana waliendelea kuchangoa bajeti hiyo, wakiitaka serikali kuwarudisha wanyama 116 waliotoroshwa, wawe hai au mizoga kwa kuwa na kama itashindwa kufanya hivyo itakuwa imeonesha udhaifu mkubwa.
Walisema kwa kitendo hicho, serikali imeingia doa ambalo ni tishio kwa usalama wa taifa kwa kuruhusu ndege ya kijeshi ya Qatar kuingia nchini na kuruhusiwa kukaa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa kuwapakia wanyama hao na kuwasafirisha.
Mbunge wa Simanjiro, Bw. Christopher Ole Sendeka (CCM) alisema utoroshwaji wa wanyama hao ulifanyika kwa sababu viongozi wengi wamezoea njia za kufanya mambo kwa mkato.
Mbunge huyo alisema nyara za taifa zinaporwa kwa kiasi cha kufedhehesha, hivyo leseni 180 za uuzaji wanyama nje zifutwe na zichomwe moto kuanzia jana.
"Mkurugenzi wa Wanyamapori Bw. Mbangwa hawezi kukanusha kuhusika katika utoroshwaji wa wanyama hai na ndege hai kwa kutumia ndege ya jeshi la Qatar kutoka Uwanja wa Ndege KIA, kuna matatizo katika idara hiyo likiwemo suala la ukabila, hivyo waziri ana kazi ngumu kuibadilisha idara hiyo," alisema Bw. Sendeka.
Alisema kama Bw. Maige anataka kuwafahamu ama kupata ukweli kuhusu wanyama na ndege waliotoroshwa, aandike barua Geneva Uswisi na waliohusika wataumbuka na kuchukuliwa hatua za kisheria.
"Tupo tayari kuwapokea wanyamapori wetu wakiwa hai au mizoga, Mheshimiwa Spika bila kusita wanyama wote waliotoroshwa hapa nchini tunahitaji warejeshwe mara moja, hiki ni kibarua kizito kwa kuwa ilichangiwa na tabia mbaya serikalini, lakini lazima iwe hivyo," alisema Bw. Sendeka.
"Ni mbaya sana kuona ndege ya jeshi la Qatar inaingia hapa nchini katika uwanja wa ndege wa KIA bila kibali na kufanya kazi yake kisha kuondoka na wanyamapori wetu wakati nchi zingine haiwezekani ndege ya kijeshi kutua na kufanya hivyo, hali ya usalama wa nchi iko hatarini," alisema Bw. Sendeka.
Aidha mbunge wa Maswa Magharibi Bw. John Shibuda (CHADEMA) akichangia katika hotuba hiyo alisema utoroshaji wa wanyama hao ni doa kwa taifa hivyo haoni sababu ya kumsifia kiongozi yeyote kwa kuwa wanaipeleka nchi katika hali mbaya kiusalama.
"Kutoroshwa kwa wanyamapori hao kumeidhalilisha Idara ya Usalama wa Taifa, Polisi, na mamlaka nyingine za usalama na hawa wanaoitwa intelijensia taarifa zao zilikuwa wapi tangu wanyama hao walipokuwa wanakusanywa," alisema Bw. Sibuda.
Aidha Mbunge wa Kilindi Bi. Beatrice Shelukindo (CCM) alisema matatizo yote ya kuuza wanyamapori yanatokana na viongozi wasio waadilifu.
"Mheshimiwa spika Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori hastahili kuwepo kwenye nafasi hiyo kwa kuwa yeye ndiye aliyetoa vibali 180 kwa wafanyabiashara kuuza wanyamapori nje ya nchi.
Serikali yasitisha vibali
Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda jana katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo aliwaeleza wabunge kuwa serikali imesitisha vibali vya usafirishaji na uuzaji wanyama nje ya nchi kwa kuwa biashara hiyo haina manufaa kwa taifa.
Bw. Pinda alisema biashara hiyo itatazamwa upya, na itakapoanza masharti yatabadilika ikiwa ni pamoja na kiwango cha tozo kwa kuwa wafanyabiashara wanapata faida kubwa kuliko serikali
Msekwa akanusha tuhuma dhidi yake
Wakati huo huo Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. Pius Msekwa amepuuza vikali tuhuma zilizotolewa na baadhi ya wabunge na kusema kuwa ni maneno ya 'kijinga na kipumbavu'.
Akizungumza kwa njia ya simu akiwa Dodoma jana, Bw. Msekwa alisema kwamba yupo kwenye ziara ya kikazi na madai yanayotolewa juu yake kwamba anatumia vibaya nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Hifadhi ya Ngorongoro kugawa maeneo kwa wafanyabiashara ni ya kipuuzi.
"Ndugu mwandishi nisikilize vizuri, madai hayo ni ya kipuuzi lakini nitaitisha mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia ukweli wa jambo hilo," alisema Bw. Msekwa.
Umeme walalamikiwa upya
Spika wa Bunge, Bi. Anne Makinda ameitaka serikali itoe maelezo kuhusu kukosekana kwa umeme usiku na mchana katika maeneo mbalimbali kwa siku kadhaa licha ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kupitishwa wakati ikionesha matumaini makubwa.
Bi. Makinda alitoa agizo hilo jana bungeni mjini Dodoma baada ya Mbunge wa Nyamagana, Bw. Ezekiah Wenje (CHADEMA) kuomba mwongozo wa spika, ili bunge lijadili jambo la dharura kwa kutumia kanuni ya 87(1).
Wakati anaomba mwongozo huo Bw. Wenje alilieleza Bunge kuwa, hakuna umeme Mwanza kwa siku nne sasa usiku na mchana, na pia tatizo hilo lipo kwenye maeneo mengi nchini ukiwemo mkoa wa Arusha, Kigoma na Dar es Salaam.
Imeandikwa na Godfrey Ismaely, Rachel Balama, Dar na Pendo Mtibuche, Dodoma
*Msekwa ajibu tuhuma za ufisadi Ngorongoro
*Mgawo wa umeme walalamikiwa upya bungeni
Na Waandishi Wetu
SAKATA la kutorosha wanyamapori kwenda nje ya nchi limeishtua serikali kutoka usingizini baada ya Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Bw. Obeid Mbwangwa na watendaji wengine wawili kusimamishwa kazi na serikali ili kupisha uchunguzi.
Bw. Mbwangwa amekumbwa na hali hiyo zikiwa ni siku chache baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo, na siku moja baada ya wabunge kutaka hatua zichukuliwe haraka kwa wahusika, akiwamo mkurugenzi huyo na wanyama walioibwa warejeshwe ama wakiwa hai au wamekufa.
Kutokana na agizo la Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wa mkurugenzi wa awali, Bw. Erasmus Tarimo Februari 8, mwaka huu na kumpatia likizo ya kusubiria kustaafu ambapo kwa mujibu wa sheria Julai 7, mwaka huu ndipo Bw. Mbwangwa alishika wadhifa huo kutoka nafasi ya Mkurugenzi Msaidizi wa wizara hiyo.
Tamko la kusimamishwa kazi kwa Bw. Mbwangwa na wenzake wawili ambao hawakutajwa majina ili kupisha uchunguzi, lilitolewa jana bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii, Bw. Ezekiel Maige wakati akifanya majumuisho ya makadirio na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2011 na 2012.
"Mheshimiwa Spika kutokana na malalamiko mengi ambayo waheshimiwa wamelizungumzia ni suala la kutoroshwa kwa wanyamapori, ninashukuru sana na maoni ya kamati juu ya suala hili ni nimeyazingatia," alisema Bw. Maige
"Hivyo basi kuanzia leo Agosti 18, 2011 Mkurugenzi wa Maliasili na Utalii, Obeid Mbwangwa na wenzake wawili ambao kutokana na uchunguzi wa jambo hili sitawataja hapa, nimewasimamisha kazi rasmi, ili kupisha uchunguzi wa utoroshaji wa wanyamapori hao," aliongeza.
Kilio cha wabunge
Wabunge jana waliendelea kuchangoa bajeti hiyo, wakiitaka serikali kuwarudisha wanyama 116 waliotoroshwa, wawe hai au mizoga kwa kuwa na kama itashindwa kufanya hivyo itakuwa imeonesha udhaifu mkubwa.
Walisema kwa kitendo hicho, serikali imeingia doa ambalo ni tishio kwa usalama wa taifa kwa kuruhusu ndege ya kijeshi ya Qatar kuingia nchini na kuruhusiwa kukaa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa kuwapakia wanyama hao na kuwasafirisha.
Mbunge wa Simanjiro, Bw. Christopher Ole Sendeka (CCM) alisema utoroshwaji wa wanyama hao ulifanyika kwa sababu viongozi wengi wamezoea njia za kufanya mambo kwa mkato.
Mbunge huyo alisema nyara za taifa zinaporwa kwa kiasi cha kufedhehesha, hivyo leseni 180 za uuzaji wanyama nje zifutwe na zichomwe moto kuanzia jana.
"Mkurugenzi wa Wanyamapori Bw. Mbangwa hawezi kukanusha kuhusika katika utoroshwaji wa wanyama hai na ndege hai kwa kutumia ndege ya jeshi la Qatar kutoka Uwanja wa Ndege KIA, kuna matatizo katika idara hiyo likiwemo suala la ukabila, hivyo waziri ana kazi ngumu kuibadilisha idara hiyo," alisema Bw. Sendeka.
Alisema kama Bw. Maige anataka kuwafahamu ama kupata ukweli kuhusu wanyama na ndege waliotoroshwa, aandike barua Geneva Uswisi na waliohusika wataumbuka na kuchukuliwa hatua za kisheria.
"Tupo tayari kuwapokea wanyamapori wetu wakiwa hai au mizoga, Mheshimiwa Spika bila kusita wanyama wote waliotoroshwa hapa nchini tunahitaji warejeshwe mara moja, hiki ni kibarua kizito kwa kuwa ilichangiwa na tabia mbaya serikalini, lakini lazima iwe hivyo," alisema Bw. Sendeka.
"Ni mbaya sana kuona ndege ya jeshi la Qatar inaingia hapa nchini katika uwanja wa ndege wa KIA bila kibali na kufanya kazi yake kisha kuondoka na wanyamapori wetu wakati nchi zingine haiwezekani ndege ya kijeshi kutua na kufanya hivyo, hali ya usalama wa nchi iko hatarini," alisema Bw. Sendeka.
Aidha mbunge wa Maswa Magharibi Bw. John Shibuda (CHADEMA) akichangia katika hotuba hiyo alisema utoroshaji wa wanyama hao ni doa kwa taifa hivyo haoni sababu ya kumsifia kiongozi yeyote kwa kuwa wanaipeleka nchi katika hali mbaya kiusalama.
"Kutoroshwa kwa wanyamapori hao kumeidhalilisha Idara ya Usalama wa Taifa, Polisi, na mamlaka nyingine za usalama na hawa wanaoitwa intelijensia taarifa zao zilikuwa wapi tangu wanyama hao walipokuwa wanakusanywa," alisema Bw. Sibuda.
Aidha Mbunge wa Kilindi Bi. Beatrice Shelukindo (CCM) alisema matatizo yote ya kuuza wanyamapori yanatokana na viongozi wasio waadilifu.
"Mheshimiwa spika Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori hastahili kuwepo kwenye nafasi hiyo kwa kuwa yeye ndiye aliyetoa vibali 180 kwa wafanyabiashara kuuza wanyamapori nje ya nchi.
Serikali yasitisha vibali
Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda jana katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo aliwaeleza wabunge kuwa serikali imesitisha vibali vya usafirishaji na uuzaji wanyama nje ya nchi kwa kuwa biashara hiyo haina manufaa kwa taifa.
Bw. Pinda alisema biashara hiyo itatazamwa upya, na itakapoanza masharti yatabadilika ikiwa ni pamoja na kiwango cha tozo kwa kuwa wafanyabiashara wanapata faida kubwa kuliko serikali
Msekwa akanusha tuhuma dhidi yake
Wakati huo huo Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. Pius Msekwa amepuuza vikali tuhuma zilizotolewa na baadhi ya wabunge na kusema kuwa ni maneno ya 'kijinga na kipumbavu'.
Akizungumza kwa njia ya simu akiwa Dodoma jana, Bw. Msekwa alisema kwamba yupo kwenye ziara ya kikazi na madai yanayotolewa juu yake kwamba anatumia vibaya nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Hifadhi ya Ngorongoro kugawa maeneo kwa wafanyabiashara ni ya kipuuzi.
"Ndugu mwandishi nisikilize vizuri, madai hayo ni ya kipuuzi lakini nitaitisha mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia ukweli wa jambo hilo," alisema Bw. Msekwa.
Umeme walalamikiwa upya
Spika wa Bunge, Bi. Anne Makinda ameitaka serikali itoe maelezo kuhusu kukosekana kwa umeme usiku na mchana katika maeneo mbalimbali kwa siku kadhaa licha ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kupitishwa wakati ikionesha matumaini makubwa.
Bi. Makinda alitoa agizo hilo jana bungeni mjini Dodoma baada ya Mbunge wa Nyamagana, Bw. Ezekiah Wenje (CHADEMA) kuomba mwongozo wa spika, ili bunge lijadili jambo la dharura kwa kutumia kanuni ya 87(1).
Wakati anaomba mwongozo huo Bw. Wenje alilieleza Bunge kuwa, hakuna umeme Mwanza kwa siku nne sasa usiku na mchana, na pia tatizo hilo lipo kwenye maeneo mengi nchini ukiwemo mkoa wa Arusha, Kigoma na Dar es Salaam.
Imeandikwa na Godfrey Ismaely, Rachel Balama, Dar na Pendo Mtibuche, Dodoma