Serikali yapiga marufuku utumiaji wa maji ya chemchem Shehenia ya Msuka Pemba sababu ya kuwa na bakteria hatari

USSR

JF-Expert Member
Jul 15, 2015
9,896
22,666
SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR,
WIZARA YA AFYA.


TAARIFA YA TAHADHARI KWA UMMA KUHUSU MAJI YA CHEMCHEM YA ILIYOPO PEMBENI MWA BAHARI YA HINDI KATIKA SHEHIA YA MSUKA, MASHARIKI, WILAYA YA MICHEWENI MKOA WA KASKAZINI PEMBA
TAREHE: 05/04/2023

Ndugu wananchi, Hivi karibuni kupitia mitandao ya kijamii zilisambaa taarifa za kuwepo Chemchem inayotoa maji ambayo ukinywa maji hayo ni tiba ya magonjwa mbali mbali.

Maji haya yanapatikana katika chemchem iliyopo ndani ya bahari katika Shehia ya Msuka Mashariki Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Ndugu wananchi, wamejitokeza watu mbali mbali kutoka Kisiwa cha Pemba na nje ya Kisiwa hicho ambao hufika kwa wingi katika eneo lenye chemchem hiyo na kuchukua maji hayo katika vyombo tofauti ikiwemo madumu, chupa na ndoo na kunywa maji hayo wakiamini kwamba maji hayo ni tiba ya magonjwa mbali mbali.

Ndugu wananchi, baada kupata taarifa hiyo, Wizara ya Afya ilituma wataalamu wake kwenda kuchukua sampuli ya maji hayo kwa lengo la kuyafanyia uchunguzi ili iweze kuthibisha kwamba maji hayo ni tiba kama inavyoaminika katika jamii.

Sampuli zilizochuliwa zilipelekwa kwa Mkenia Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ajili ya uchunguzi wa maabara ili tuweze kuthibisha madai ya kuwa maji haya ni tiba kwa magonjwa mbali mbali na yapo salama kunywewa.

Ndugu wananchi, Baada ya uchunguzi na uchambuzi wa kina wa maji hayo, uchunguzi umebainisha mambo yafuatayo;-

1. Uwepo wa vimelea vinavyosababisha magonjwa ya kuharisha (bacteria wa E. Coli) wa idadi kubwa kati ya mia mbili na ishirini hadi elfu moja na mia nane kwa kila lita mia moja (220 hadi 1800 kwa kila lita 100), kwa kawaida maji ya kunywa hayatakiwi kuwepo na hata kimelea kimoja cha aina hiyo.

2. Pia uchunguzi umebaini kuwepo vimelea vinavyosababisha ugonjwa wa kuharisha aina ya “Coliforms” wa zaidi ya elfu moja mia nane kwa kila lita moja za maji (1800 kwa kila lita 100). Kwa kawaida vimeilea hivi vinahitajika viwemo kwenye maji ya kunywa, lakini isiwe zaidi ya watatu kwa lita mia moja kwa kila lita mia moja ya maji.

3. Uchunguzi huu vile vile umebaini uwepo wa Chloride kwa kiwango kikubwa ambapo wataalamu wetu wemebaini kiasi cha upimo wa kuanzia elfu moja mia nne na tisiini milligram kwa kila lita hadi mpaka elfu mbili na khamsini na tisa milligram kwa lita moja (1490.88 mg/L hadi 2059.36 mg/L). kiwango kinachokubalika ni kipimo kisichozidi mia mbili na khamsini milligram kwa kila lita moja (250 mg/L).

4. Kiwango cha Chumvi chumvi (Salinity) kimebainika kwa kiwango cha kupima ukali wa chumvi cha baina ya mbili nukta nane na tatu nukta nane (2.827 hadi 3.827 psu) ambapo ni zaidi ya kiwango kinachokubalika katika maji ya kunywa cha sufuri, (0 psu).

Ndugu wananchi, Kutokana na matokeo hayo yatuthibitishia kwamba maji haya yamechafuliwa na kinyeshi cha viumbe hai na pia kuna kiwango kikubwa cha Kemikali ambazo sio salama katika mwili wa binadamu. Kwa maana hio maji haya sio salama kwa kunywa na kama tukiendekea kuyatumia yanaweza kuathiri Afya zetu na kupelekea matatizo ya kiafya yafuatayo:-

1. Magonjwa ya kuharisha ikiwemo Kipindupindu, kutapika na kupoteza maji mengi mwilini.

2. Kupata maumivu makali ya tumbo na baadae unaweza kupata vidonda vya tumbo hapo baadae.

Ndugu wananchi, Napenda kuchukua fursa hii kuwaomba Wazanzibari wenzangu kwamba taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii hapa nchi kwamba maji yanayopatikana katika Chemchem iliyopo katika Bahari ya Hindi katika Shehia ya Msuka Mashariki, Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba hayawezi kutibu ugonjwa wowote na tuzipuuze taarifa hizi kwa hazina ukweli wowote.

Ndugu wananchi, Aidha, napenda niwasihi wananchi wote kwamba mtu yoyote mwenye matatizo ya kiafya afike katika Kituo cha Afya au Hospitali iliyokaribu kwa ajili uchunguzi na matibabu na tuache kutumia maji haya kama tiba kwani yanaweza kutuletea athari zaidi katika Afya zetu.

Ndugu wananchi, Mwisho kabisa nitoe wito wangu kwa Wanzanzibari wenzangu kwa tuache kuyatumia maji haya tukiamini ni tiba ya magonjwa mbali mbali kwani athari yake inaweza kuwa kubwa na kusabisha matatizo ya kichumi na kijamii.

Ahsanteni kwa kunisikiliza.

NASSOR AHMED MAZRUI,
WAZIRI WA AFYA,
ZANZIBAR.

USSR

FB_IMG_1680681077554.jpg
 
Kuna nuka huko Wizarani?

Je, kuna upotoshaji wa hali ya juu kuhusu upatikanaji wa E-Coli na Coliform bacteria katika maji ya chemichemi?

Kunani huko? Nani atakayekwenda kufaidika na Marufuku hiyo?

Kwa kukurupuka na kwa mtazamo wa haraka haraka, mara nyingi nikiona vitu kama hivi, yaani, matumizi ya mamlaka kutoa marufuku ya matumizi ya maji n.k. ndipo nakutaga kuna jambo/suala la kiaina nyuma yake.

Aidha, tathmini iliyofanyika ni ya kweli na sahihi na ya haki ikiwa na maana matokeo yake ni ya kweli na yanaipa mamlaka haki ya kutoa ban au kuna uwongo na ulaghai mpana na mrefu yaliyopigwa(botched).kwa makusudi ili kudiskareji wenyeji na kuwatenga katika mchakato mzima(issue nzima) kuhusu chemchemu hiyo. Na kuwapa wanufaika wa utafiti na matokeo yake,mkono mrefu na usemi kuhusu eneo husika.

Maji sasa hivi ni kama Dhahabu.
Hasa maji safi ya kunywa na kwa kiasi fulani Biashara ya maji ya chemchemi ambayo kwa sasa ipo duniani imefikia wastani wa Dola za Marekani Bilioni 7 kwa mwaka kulingana na vyanzo vyangu ambavyo biashara zinafanywa na makampuni makubwa kabisa duniani.

Nina imani kubwa kwamba kuna dokezo la ufisadi katika suala hili, tena labda la ukubwa wa juu kuliko ninavyoamini kunapo.

Nashauri kwamba, kuwe na uchunguzi huru na au Utafiti/Vipimo wa maji hayo tena (mara nyingine)ili kubaini Ukweli. We need an investigative and Journalistic and scientific approach ++ to acertain madai ya wote. Wizara pamoja na Wanaodai the healing properties ndani ya maji hayo.

wadadavue

1.Sifa za maji sijui php na vimbwanga vyote na madini yaliyomo humo na
2.Vyanzo vya bakteria hawa katika maji ya chemchemi hiyo huko.

Haiingii akilini kabisa.



TISS mpo?
 
Kuna nuka huko Wizarani?

Je, kuna upotoshaji wa hali ya juu kuhusu upatikanaji wa E-Coli na Coliform bacteria katika maji ya chemichemi?

Kunani huko? Nani atakayekwenda kufaidika na Marufuku hiyo?

Kwa kukurupuka na kwa mtazamo wa haraka haraka, mara nyingi nikiona vitu kama hivi, yaani, matumizi ya mamlaka kutoa marufuku ya matumizi ya maji n.k. ndipo nakutaga kuna jambo/suala la kiaina nyuma yake.

Aidha, tathmini iliyofanyika ni ya kweli na sahihi na ya haki ikiwa na maana matokeo yake ni ya kweli na yanaipa mamlaka haki ya kutoa ban au kuna uwongo na ulaghai mpana na mrefu yaliyopigwa(botched).kwa makusudi ili kudiskareji wenyeji na kuwatenga katika mchakato mzima(issue nzima) kuhusu chemchemu hiyo. Na kuwapa wanufaika wa utafiti na matokeo yake,mkono mrefu na usemi kuhusu eneo husika.

Maji sasa hivi ni kama Dhahabu.
Hasa maji safi ya kunywa na kwa kiasi fulani Biashara ya maji ya chemchemi ambayo kwa sasa ipo duniani imefikia wastani wa Dola za Marekani Bilioni 7 kwa mwaka kulingana na vyanzo vyangu ambavyo biashara zinafanywa na makampuni makubwa kabisa duniani.

Nina imani kubwa kwamba kuna dokezo la ufisadi katika suala hili, tena labda la ukubwa wa juu kuliko ninavyoamini kunapo.

Nashauri kwamba, kuwe na uchunguzi huru na au Utafiti/Vipimo wa maji hayo tena (mara nyingine)ili kubaini Ukweli. We need an investigative and Journalistic and scientific approach ++ to acertain madai ya wote. Wizara pamoja na Wanaodai the healing properties ndani ya maji hayo.

wadadavue

1.Sifa za maji sijui php na vimbwanga vyote na madini yaliyomo humo na
2.Vyanzo vya bakteria hawa katika maji ya chemchemi hiyo huko.

Haiingii akilini kabisa.



TISS mpo?
Hebu nyoosha maelezo, kwamba hayo maji hayana madhara?! Na je, hiyo chem chem imekuwapo kwa muda gani?
 
Muda hauniruhusu kufanya hivyo.
Hatahivyo Zema, hoja ya uwepo au kutokuwepo na madhara kwenye maji ya chemichemi, hayo yanajadilika.
 
SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR,
WIZARA YA AFYA.


TAARIFA YA TAHADHARI KWA UMMA KUHUSU MAJI YA CHEMCHEM YA ILIYOPO PEMBENI MWA BAHARI YA HINDI KATIKA SHEHIA YA MSUKA, MASHARIKI, WILAYA YA MICHEWENI MKOA WA KASKAZINI PEMBA
TAREHE: 05/04/2023

Ndugu wananchi, Hivi karibuni kupitia mitandao ya kijamii zilisambaa taarifa za kuwepo Chemchem inayotoa maji ambayo ukinywa maji hayo ni tiba ya magonjwa mbali mbali.

Maji haya yanapatikana katika chemchem iliyopo ndani ya bahari katika Shehia ya Msuka Mashariki Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Ndugu wananchi, wamejitokeza watu mbali mbali kutoka Kisiwa cha Pemba na nje ya Kisiwa hicho ambao hufika kwa wingi katika eneo lenye chemchem hiyo na kuchukua maji hayo katika vyombo tofauti ikiwemo madumu, chupa na ndoo na kunywa maji hayo wakiamini kwamba maji hayo ni tiba ya magonjwa mbali mbali.

Ndugu wananchi, baada kupata taarifa hiyo, Wizara ya Afya ilituma wataalamu wake kwenda kuchukua sampuli ya maji hayo kwa lengo la kuyafanyia uchunguzi ili iweze kuthibisha kwamba maji hayo ni tiba kama inavyoaminika katika jamii.

Sampuli zilizochuliwa zilipelekwa kwa Mkenia Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ajili ya uchunguzi wa maabara ili tuweze kuthibisha madai ya kuwa maji haya ni tiba kwa magonjwa mbali mbali na yapo salama kunywewa.

Ndugu wananchi, Baada ya uchunguzi na uchambuzi wa kina wa maji hayo, uchunguzi umebainisha mambo yafuatayo;-

1. Uwepo wa vimelea vinavyosababisha magonjwa ya kuharisha (bacteria wa E. Coli) wa idadi kubwa kati ya mia mbili na ishirini hadi elfu moja na mia nane kwa kila lita mia moja (220 hadi 1800 kwa kila lita 100), kwa kawaida maji ya kunywa hayatakiwi kuwepo na hata kimelea kimoja cha aina hiyo.

2. Pia uchunguzi umebaini kuwepo vimelea vinavyosababisha ugonjwa wa kuharisha aina ya “Coliforms” wa zaidi ya elfu moja mia nane kwa kila lita moja za maji (1800 kwa kila lita 100). Kwa kawaida vimeilea hivi vinahitajika viwemo kwenye maji ya kunywa, lakini isiwe zaidi ya watatu kwa lita mia moja kwa kila lita mia moja ya maji.

3. Uchunguzi huu vile vile umebaini uwepo wa Chloride kwa kiwango kikubwa ambapo wataalamu wetu wemebaini kiasi cha upimo wa kuanzia elfu moja mia nne na tisiini milligram kwa kila lita hadi mpaka elfu mbili na khamsini na tisa milligram kwa lita moja (1490.88 mg/L hadi 2059.36 mg/L). kiwango kinachokubalika ni kipimo kisichozidi mia mbili na khamsini milligram kwa kila lita moja (250 mg/L).

4. Kiwango cha Chumvi chumvi (Salinity) kimebainika kwa kiwango cha kupima ukali wa chumvi cha baina ya mbili nukta nane na tatu nukta nane (2.827 hadi 3.827 psu) ambapo ni zaidi ya kiwango kinachokubalika katika maji ya kunywa cha sufuri, (0 psu).

Ndugu wananchi, Kutokana na matokeo hayo yatuthibitishia kwamba maji haya yamechafuliwa na kinyeshi cha viumbe hai na pia kuna kiwango kikubwa cha Kemikali ambazo sio salama katika mwili wa binadamu. Kwa maana hio maji haya sio salama kwa kunywa na kama tukiendekea kuyatumia yanaweza kuathiri Afya zetu na kupelekea matatizo ya kiafya yafuatayo:-

1. Magonjwa ya kuharisha ikiwemo Kipindupindu, kutapika na kupoteza maji mengi mwilini.

2. Kupata maumivu makali ya tumbo na baadae unaweza kupata vidonda vya tumbo hapo baadae.

Ndugu wananchi, Napenda kuchukua fursa hii kuwaomba Wazanzibari wenzangu kwamba taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii hapa nchi kwamba maji yanayopatikana katika Chemchem iliyopo katika Bahari ya Hindi katika Shehia ya Msuka Mashariki, Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba hayawezi kutibu ugonjwa wowote na tuzipuuze taarifa hizi kwa hazina ukweli wowote.

Ndugu wananchi, Aidha, napenda niwasihi wananchi wote kwamba mtu yoyote mwenye matatizo ya kiafya afike katika Kituo cha Afya au Hospitali iliyokaribu kwa ajili uchunguzi na matibabu na tuache kutumia maji haya kama tiba kwani yanaweza kutuletea athari zaidi katika Afya zetu.

Ndugu wananchi, Mwisho kabisa nitoe wito wangu kwa Wanzanzibari wenzangu kwa tuache kuyatumia maji haya tukiamini ni tiba ya magonjwa mbali mbali kwani athari yake inaweza kuwa kubwa na kusabisha matatizo ya kichumi na kijamii.

Ahsanteni kwa kunisikiliza.

NASSOR AHMED MAZRUI,
WAZIRI WA AFYA,
ZANZIBAR.

USSR

View attachment 2578204
Dar maeneo mengi tunakunywa maji yasiyopimwa ya visima vya wapemba, zaidi ya miaka 60 baada ya uhuru mama hajatoa pesa za kutuachisha maji ya visima.
 
Dar maeneo mengi tunakunywa maji yasiyopimwa ya visima vya wapemba, zaidi ya miaka 60 baada ya uhuru mama hajatoa pesa za kutuachisha maji ya visima.
Mkuu kuna kitu hakiko sawa huko....umesikia wapi maji ya chemichemi yamejaa bacteria ya e-coli?
Kwanini wapige marufuku tuu? Kwanini wasiseme wachemshe maji?
 
Mkuu kuna kitu hakiko sawa huko....umesikia wapi maji ya chemichemi yamejaa bacteria ya e-coli?
Kwanini wapige marufuku tuu? Kwanini wasiseme wachemshe maji?
Ni mwananchi gani atachemsha, muda na nishati ya kuchemshia atapata wapi na kiwango cha joto la maji kuweza kuviua atalijulia wapi! Sisi tunakunywa ya visima visivyotiwa dawa huku serikali ya wapigaji ikijivuna mafanikio ya kusambaza maji ambayo kasambaza mpemba!
 
Ni mwananchi gani atachemsha, muda na nishati ya kuchemshia atapata wapi na kiwango cha joto la maji kuweza kuviua atalijulia wapi! Sisi tunakunywa ya visima visivyotiwa dawa huku serikali ya wapigaji ikijivuna mafanikio ya kusambaza maji ambayo kasambaza mpemba!


Sawa, uwezekano wa kukosa muda au nishati mie naona haupo....hayo kutokea ni kama mtu ameenda pale na kiu kwani sidhani kama kuna mtu alienda pale kunywa maji akiwa na kiu. Hicho sicho kilichokuwa kinaendelea pale watu wanaofika pale wanaenda kwasababu wanaamini maji hayo ni tiba ya magonjwa ...hiyo peke yake inadhihirisha wanaofika pale wana muda na raslimali... mtu afunge safari kutoka Dar aende pemba, ina maana ana muda na ana rasilimali za kutosha za kuweza kuchemsha maji hayo.

Haya kama huko unapodai mnakunywa maji ya visima visivyotiwa dawa, je serikali inayajua hayo? Visima vimepigwa marufuku? Kuna watu wameugua kwa bacteria hizo mbili zilizotajwa?
 
SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR,
WIZARA YA AFYA.


TAARIFA YA TAHADHARI KWA UMMA KUHUSU MAJI YA CHEMCHEM YA ILIYOPO PEMBENI MWA BAHARI YA HINDI KATIKA SHEHIA YA MSUKA, MASHARIKI, WILAYA YA MICHEWENI MKOA WA KASKAZINI PEMBA
TAREHE: 05/04/2023

Ndugu wananchi, Hivi karibuni kupitia mitandao ya kijamii zilisambaa taarifa za kuwepo Chemchem inayotoa maji ambayo ukinywa maji hayo ni tiba ya magonjwa mbali mbali.

Maji haya yanapatikana katika chemchem iliyopo ndani ya bahari katika Shehia ya Msuka Mashariki Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Ndugu wananchi, wamejitokeza watu mbali mbali kutoka Kisiwa cha Pemba na nje ya Kisiwa hicho ambao hufika kwa wingi katika eneo lenye chemchem hiyo na kuchukua maji hayo katika vyombo tofauti ikiwemo madumu, chupa na ndoo na kunywa maji hayo wakiamini kwamba maji hayo ni tiba ya magonjwa mbali mbali.

Ndugu wananchi, baada kupata taarifa hiyo, Wizara ya Afya ilituma wataalamu wake kwenda kuchukua sampuli ya maji hayo kwa lengo la kuyafanyia uchunguzi ili iweze kuthibisha kwamba maji hayo ni tiba kama inavyoaminika katika jamii.

Sampuli zilizochuliwa zilipelekwa kwa Mkenia Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ajili ya uchunguzi wa maabara ili tuweze kuthibisha madai ya kuwa maji haya ni tiba kwa magonjwa mbali mbali na yapo salama kunywewa.

Ndugu wananchi, Baada ya uchunguzi na uchambuzi wa kina wa maji hayo, uchunguzi umebainisha mambo yafuatayo;-

1. Uwepo wa vimelea vinavyosababisha magonjwa ya kuharisha (bacteria wa E. Coli) wa idadi kubwa kati ya mia mbili na ishirini hadi elfu moja na mia nane kwa kila lita mia moja (220 hadi 1800 kwa kila lita 100), kwa kawaida maji ya kunywa hayatakiwi kuwepo na hata kimelea kimoja cha aina hiyo.

2. Pia uchunguzi umebaini kuwepo vimelea vinavyosababisha ugonjwa wa kuharisha aina ya “Coliforms” wa zaidi ya elfu moja mia nane kwa kila lita moja za maji (1800 kwa kila lita 100). Kwa kawaida vimeilea hivi vinahitajika viwemo kwenye maji ya kunywa, lakini isiwe zaidi ya watatu kwa lita mia moja kwa kila lita mia moja ya maji.

3. Uchunguzi huu vile vile umebaini uwepo wa Chloride kwa kiwango kikubwa ambapo wataalamu wetu wemebaini kiasi cha upimo wa kuanzia elfu moja mia nne na tisiini milligram kwa kila lita hadi mpaka elfu mbili na khamsini na tisa milligram kwa lita moja (1490.88 mg/L hadi 2059.36 mg/L). kiwango kinachokubalika ni kipimo kisichozidi mia mbili na khamsini milligram kwa kila lita moja (250 mg/L).

4. Kiwango cha Chumvi chumvi (Salinity) kimebainika kwa kiwango cha kupima ukali wa chumvi cha baina ya mbili nukta nane na tatu nukta nane (2.827 hadi 3.827 psu) ambapo ni zaidi ya kiwango kinachokubalika katika maji ya kunywa cha sufuri, (0 psu).

Ndugu wananchi, Kutokana na matokeo hayo yatuthibitishia kwamba maji haya yamechafuliwa na kinyeshi cha viumbe hai na pia kuna kiwango kikubwa cha Kemikali ambazo sio salama katika mwili wa binadamu. Kwa maana hio maji haya sio salama kwa kunywa na kama tukiendekea kuyatumia yanaweza kuathiri Afya zetu na kupelekea matatizo ya kiafya yafuatayo:-

1. Magonjwa ya kuharisha ikiwemo Kipindupindu, kutapika na kupoteza maji mengi mwilini.

2. Kupata maumivu makali ya tumbo na baadae unaweza kupata vidonda vya tumbo hapo baadae.

Ndugu wananchi, Napenda kuchukua fursa hii kuwaomba Wazanzibari wenzangu kwamba taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii hapa nchi kwamba maji yanayopatikana katika Chemchem iliyopo katika Bahari ya Hindi katika Shehia ya Msuka Mashariki, Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba hayawezi kutibu ugonjwa wowote na tuzipuuze taarifa hizi kwa hazina ukweli wowote.

Ndugu wananchi, Aidha, napenda niwasihi wananchi wote kwamba mtu yoyote mwenye matatizo ya kiafya afike katika Kituo cha Afya au Hospitali iliyokaribu kwa ajili uchunguzi na matibabu na tuache kutumia maji haya kama tiba kwani yanaweza kutuletea athari zaidi katika Afya zetu.

Ndugu wananchi, Mwisho kabisa nitoe wito wangu kwa Wanzanzibari wenzangu kwa tuache kuyatumia maji haya tukiamini ni tiba ya magonjwa mbali mbali kwani athari yake inaweza kuwa kubwa na kusabisha matatizo ya kichumi na kijamii.

Ahsanteni kwa kunisikiliza.

NASSOR AHMED MAZRUI,
WAZIRI WA AFYA,
ZANZIBAR.

USSR

View attachment 2578204

Kitu ambacho nakiona:

Kutaja ugonjwa ambao mdudu husika hajapatikana mpaka ripoti ilipowasilishwa kipindupindu.

Labda kama ni ugonjwa ni wa matarajio na si hali ya sasa. Sina uhakika mtoa ripoti alilenga nini hasa yaliyomo au matarajio ya kimazingira?
 
Back
Top Bottom