Serikali yakiri makosa kuwalazimisha Wafanyakazi wa Umma kununua laini ya simu ya TTCL

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,789
218,421
1647259898075.png

Wakati wa utawala wa awamu ya 5 chini ya Dr Magufuli, viongozi wa serikali, wakiwemo Mawaziri na wafanyakazi wa serikali walilazimishwa kununua line ya simu ya TTCL kibabe, huku wengine wakipigwa mkwara kwamba wasipokuwa na line ya TTCL watang'olewa kwenye uongozi, lengo la jambo hilo kwa akili ya viongozi wa wakati ule ilikuwa kulazimisha mtandao wa TTCL kupata wateja wengi, hata hivyo idadi ya wafanyakazi wote wa serikali ya Tanzania inakadiriwa kufikia laki 6 tu.

Nchi yenye Raia wanaotajwa kuzidi mil 60, hata ukichukua wafanyakazi wote ukawapelekea line za TTCL kwa mtutu wa bunduki mtandao huo hauwezi kuteka soko kwa idadi hiyo ya wateja, Binafsi nilipinga vibaya sana jambo hilo na nikashauri viongozi wa wakati ule kwamba, ikiwa wanataka TTCL ishamiri basi Wanaccm wote waliodaiwa kuwa wengi sana nchini Tanzania ndio walazimishwe kununua line za TTCL, pamoja na kwamba Mwenyekiti wa ccm alikuwa Magufuli huyohuyo lakini ushauri wangu hakuufuata .

Leo Waziri Nape amekiri hadharani kwamba uamuzi ule haukuwa na lolote la maana.

===

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema kwamba haukuwa utaratibu sahihi kuwalazimisha viongozi wa serikali kumiliki na kutumia laini za Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL).

Amesema kufanya hivyo kunaweza kusiwe na matunda yanayotarajiwa kwani kiongozi anaweza kuinunua kwa sababu amelazimishwa, lakini akatumia ya mtandao ambao yeye anaupenda.

“Huduma hizi hazilazimishwi. Ukiwalazimisha watu wachukue laini, watachukua hiyo uliyowalazimisha halafu watachukua na ile wanayoipenda,” amesema Nape na kuongeza kwamba “I don’t think if it was a good model [sidhani kama ulikuwa utaratibu mazuri.”

Nape amesema hayo akijibu swali la mmoja wa waandishi wa habari aliyetaka kujua wizara ina mpango gani kuhakikisha kwamba TTCL inafikisha mawasiliano vijijini ikizingatiwa kwamba Hayati Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliagiza awatumishi wote wa serikali kuwa na laini za TTCL.

Aidha, katika mkutano huo wa kueleza mafanikio ya wizara kwa mwaka mmoja wa uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan iliibuliwa tena hoja ya gharama za intaneti na waziri akasema kwamba gharama zilivyo sasa zipo chini ya kiwango kinachokubalika kisheria.

“… Kwa presha ya siasa tumeshuka hadi tukapitiliza kiwango kilichoiwekwa kisheria. Sasa hatuwezi kuendelea kushuka kama tunahitaji huduma bora,” amesema.

Amesema kuwa ukitaka huduma bora sharti ukubali kuigharamikia kidogo na kuwataka wananchi kuacha malalamiko, kujiona wanyongea au kudhani kwamba wanaonewa.

Hata hivyo, amesema Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaendelea na mazungumzo na wadau kuona namna ya kuboresha gharama hizo ili kuimarisha na kukuza matumizi ya huduma za intaneti nchini.


Pia soma: Serikali: Sio Watumishi wote wa Umma wanatakiwa kuwa na laini ya TTCL bali Viongozi wanaopewa vocha watapewa za TTCL
 
Wakati wa utawala wa awamu ya 5 chini ya Dr Magufuli, viongozi wa serikali, wakiwemo Mawaziri na wafanyakazi wa serikali walilazimishwa kununua line ya simu ya TTCL kibabe, huku wengine wakipigwa mkwara kwamba wasipokuwa na line ya TTCL watang'olewa kwenye uongozi, lengo la jambo hilo kwa akili ya viongozi wa wakati ule ilikuwa kulazimisha mtandao wa TTCL kupata wateja wengi, hata hivyo idadi ya wafanyakazi wote wa serikali
CCM ni genge la matapeli tupu
 
Back
Top Bottom