Serikali ya Daruso yavunjwa

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174
Serikali Daruso yavunjwa


na Chalila Kibuda


amka2.gif
SERIKALI ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es es Salaam (DARUSO), imevunjwa juzi baada ya Rais wake, Mathias Kipara, kuitoa serikali hiyo katika Umoja wa Vyuo Vikuu na Taasisi Tanzania (TAHLISO) bila kupitia maamuzi ya bunge.
Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Spika wa Bunge wa DARUSO, Goodruck Mwangomango, alisema kutokana na rais kukiuka Katiba ya Daruso kunachangia serikali yake kuvunjika mpaka uchaguzi utakapofika kwa ajili ya kupata viongozo wapya.
Spika Mwangomango alisema rais alitumia mamlaka yake vibaya kujitoa Tahiliso pasipo kushirikisha bunge ambalo ndilo lenye maamuzi; hii imechangia serikali ya Darsuso kuvunja uaminifu kwa wanafunzi waliowachagua.
Alisema serikali ya Daruso ilijiunga kupitia bunge, hivyo hata kujitoa ilihitajika bunge kutoa maamzi yake kama chombo cha mwisho cha maamuzi.
Aidha, alisema serikali hiyo kwa sasa itaongozwa na wenyeviti wa vitivo mpaka uchaguzi utakapoitishwa tena kwa ajili ya kuchagua viongozi wapya.
Mwangomango alisema kuwa rais wa Daruso alijiunga Tahliso kwa kutumia bunge, hivyo hata suala la kujitoa bunge ndilo lingepaswa kutoa maamuzi.
Aidha, alieleza kesho watatoa tamko rasmi juu ya kuvunja serikali hiyo ya wanafunzi wa Daruso na kukabidhi kwa wenyeviti wa vitivo.
Serikali hiyo iliyokuwa na mawaziri 30, rais alikuwa Mathias Kipara, Waziri Mkuu, Paul Mapuri na Makamu wa Rais, Jacqueline Materu.
 
Hi Daruso si ndiyo walimpa JK siku saba atengue kauli yake ya kuukwepa mkutano wa kikatiba katika kuiandika katiba mpya pale alipotangaza nia yake ya kujiundia Tume yake mwenyewe?

Sasa kama uongozi wao umevunjwa wataandaaje maandamano yao ya kupinga Tume kuandika katiba mpya?
 
Vyuo vikuu miaka hii imebaki tu majina, huko nyuma kitendo cha serikali kuua hata raia mmoja tu wasomi wa vyuo vikuu wangekua waachii nafasi hata ya kunywa maji wadhalimu walioko madarakani bila kuwajibika.

Asiyefahamu hilo aulize kulichomfanya mzee mwinyi kujiuzulu miaka hiyo.

Leo hii vyuo vikuu si taasisi za kutetea wanyonge tena.
 

SERIKALI ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es es Salaam (DARUSO), imevunjwa juzi baada ya Rais wake, Mathias Kipara, kuitoa serikali hiyo katika Umoja wa Vyuo Vikuu na Taasisi Tanzania (TAHLISO) bila kupitia maamuzi ya bunge.
Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Spika wa Bunge wa DARUSO, Goodruck Mwangomango, alisema kutokana na rais kukiuka Katiba ya Daruso kunachangia serikali yake kuvunjika mpaka uchaguzi utakapofika kwa ajili ya kupata viongozo wapya.
Spika Mwangomango alisema rais alitumia mamlaka yake vibaya kujitoa Tahiliso pasipo kushirikisha bunge ambalo ndilo lenye maamuzi; hii imechangia serikali ya Darsuso kuvunja uaminifu kwa wanafunzi waliowachagua.
Alisema serikali ya Daruso ilijiunga kupitia bunge, hivyo hata kujitoa ilihitajika bunge kutoa maamzi yake kama chombo cha mwisho cha maamuzi.
Aidha, alisema serikali hiyo kwa sasa itaongozwa na wenyeviti wa vitivo mpaka uchaguzi utakapoitishwa tena kwa ajili ya kuchagua viongozi wapya.
Mwangomango alisema kuwa rais wa Daruso alijiunga Tahliso kwa kutumia bunge, hivyo hata suala la kujitoa bunge ndilo lingepaswa kutoa maamuzi.
Aidha, alieleza kesho watatoa tamko rasmi juu ya kuvunja serikali hiyo ya wanafunzi wa Daruso na kukabidhi kwa wenyeviti wa vitivo.
Serikali hiyo iliyokuwa na mawaziri 30, rais alikuwa Mathias Kipara, Waziri Mkuu, Paul Mapuri na Makamu wa Rais, Jacqueline Materu.

Mmmh, Serikali ya wanafunzi tu mawaziri 30.,ama kweli mtoto wa nyoka ni nyoka
 
Back
Top Bottom