Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Serikali Daruso yavunjwa
na Chalila Kibuda
SERIKALI ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es es Salaam (DARUSO), imevunjwa juzi baada ya Rais wake, Mathias Kipara, kuitoa serikali hiyo katika Umoja wa Vyuo Vikuu na Taasisi Tanzania (TAHLISO) bila kupitia maamuzi ya bunge.
Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Spika wa Bunge wa DARUSO, Goodruck Mwangomango, alisema kutokana na rais kukiuka Katiba ya Daruso kunachangia serikali yake kuvunjika mpaka uchaguzi utakapofika kwa ajili ya kupata viongozo wapya.
Spika Mwangomango alisema rais alitumia mamlaka yake vibaya kujitoa Tahiliso pasipo kushirikisha bunge ambalo ndilo lenye maamuzi; hii imechangia serikali ya Darsuso kuvunja uaminifu kwa wanafunzi waliowachagua.
Alisema serikali ya Daruso ilijiunga kupitia bunge, hivyo hata kujitoa ilihitajika bunge kutoa maamzi yake kama chombo cha mwisho cha maamuzi.
Aidha, alisema serikali hiyo kwa sasa itaongozwa na wenyeviti wa vitivo mpaka uchaguzi utakapoitishwa tena kwa ajili ya kuchagua viongozi wapya.
Mwangomango alisema kuwa rais wa Daruso alijiunga Tahliso kwa kutumia bunge, hivyo hata suala la kujitoa bunge ndilo lingepaswa kutoa maamuzi.
Aidha, alieleza kesho watatoa tamko rasmi juu ya kuvunja serikali hiyo ya wanafunzi wa Daruso na kukabidhi kwa wenyeviti wa vitivo.
Serikali hiyo iliyokuwa na mawaziri 30, rais alikuwa Mathias Kipara, Waziri Mkuu, Paul Mapuri na Makamu wa Rais, Jacqueline Materu.
na Chalila Kibuda
Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Spika wa Bunge wa DARUSO, Goodruck Mwangomango, alisema kutokana na rais kukiuka Katiba ya Daruso kunachangia serikali yake kuvunjika mpaka uchaguzi utakapofika kwa ajili ya kupata viongozo wapya.
Spika Mwangomango alisema rais alitumia mamlaka yake vibaya kujitoa Tahiliso pasipo kushirikisha bunge ambalo ndilo lenye maamuzi; hii imechangia serikali ya Darsuso kuvunja uaminifu kwa wanafunzi waliowachagua.
Alisema serikali ya Daruso ilijiunga kupitia bunge, hivyo hata kujitoa ilihitajika bunge kutoa maamzi yake kama chombo cha mwisho cha maamuzi.
Aidha, alisema serikali hiyo kwa sasa itaongozwa na wenyeviti wa vitivo mpaka uchaguzi utakapoitishwa tena kwa ajili ya kuchagua viongozi wapya.
Mwangomango alisema kuwa rais wa Daruso alijiunga Tahliso kwa kutumia bunge, hivyo hata suala la kujitoa bunge ndilo lingepaswa kutoa maamuzi.
Aidha, alieleza kesho watatoa tamko rasmi juu ya kuvunja serikali hiyo ya wanafunzi wa Daruso na kukabidhi kwa wenyeviti wa vitivo.
Serikali hiyo iliyokuwa na mawaziri 30, rais alikuwa Mathias Kipara, Waziri Mkuu, Paul Mapuri na Makamu wa Rais, Jacqueline Materu.