Serikali ya CCM kuhusika na Kifo Cha Zao la Pamba

Tony Almeda

JF-Expert Member
Sep 18, 2011
397
122
Zao la pamba lililokuwa linategemewa sana katika mikoa ya kanda ya ziwa, liko hatarini kutolimwa kabisa kutokana na serikali kuonekana haiwathamini wakulima wa zao hilo na kuwakumbatia wanunuzi.

Kikao kilichofanyika wiki hii baina ya serikali na wanunuzi hao wa pamba, kilionyesha udhaifu wa serikali baada ya kushindwa kufikia muafaka wa bei elekezi, baada ya Wanunuzi hao kung'ang'ania bei ya kuanzia iwe shillingi 450 kwa kilo moja ya pamba isiyochambuliwa, wakati serikali ilikuja na bei ya kuanzia ya shillingi 700 kwa kilo moja ya pamba isiyochambuliwa.

Mwaka 2011 bei ya pamba ilishuka ghafla kutoka shillingi 1400 kwa kilo moja hadi kufikia shillingi 700 kwa kilo na serikali kushindwa kufanya lolote la kuwanusuru wakulima hao wa pamba wakati bei waliipanga wao wenyewe.

Habari kutoka Bariadi zinasema ya kuwa. Kwa kuwa Serikali ya CCM imeshindwa kuwatetea wakulima wa pamba, Basi watageukia kulima mazao mbadala kama alizeti na choroko kuliko kuumia na wakati huo huo gharama za kulilima zao hilo zikiongezeka maradufu

My take:
Serikali inatakiwa iliangalie kwa umakini hili suala, tusije kutafuta mchawi hili zo pindi litakapokufa,kuna bahadhi ya maeneo hivi sasa hawalimi kabisa au kama wanalima basi ni kidogo sana tofauti na zamani.
Source ni mimi mwenyewe mdau wa pamba
 
Bei ya Tsh. 1,400@kilo ya pamba-mbegu haijawahi kuwepo hapa TZ tangu zao lianze kulimwa. We umeitoa wapi? km sio kuchonganisha serikali na wananchi. Visit web. hii (Cotton - Daily Price - Commodity Prices - Price Charts, Data, and News - IndexMundi) halafu uniambie kwa vigezo vyako bei itakuwaje msimu huu. Kama hujafanya utafiti usipost uongo hapa JF, ni aibu.

Eng. Willy
Wacha dharau bw mdogo! Kama hauna kumbukumbu na wewe usikurupuke.

Mwaka 2011 bodi ya pamba ilitangaza bei elekezi ni shillingi 1,400 kwa kilo moja. Na kampuni ya NIDA ilinunua mpaka kwa bei ya 1,700/= kwa kilo mwaka 2010

Hizi data zako za kwenye soko la dunia zinaanzia mwezi Nov 2011, kama unajua zaidi lete data za BODI ya Pamba Usijifanye mjuaji....! kikao cha mwisho kati ya bodi na Wadau wa pamba kimeshindwa kupata muafaka wa bei, hilo ndio nazungumza hapa.

 
Wacha dharau bw mdogo! Kama hauna kumbukumbu na wewe usikurupuke.
Mwaka 2011 bodi ya pamba ilitangaza bei elekezi ni shillingi 1,400 kwa kilo moja. na kampuni ya NIDA ilinunua mpaka kwa bei ya 1,700/= kwa kilo mwaka 2010

Hizi data zako za kwenye soko la dunia zinaanzia mwezi Nov 2011, kama unajua zaidi lete data za BODI ya Pamba Usijifanye mjuaji....! kikao cha mwisho kati ya bodi na Wadau wa pamba kimeshindwa kupata muafaka wa bei, hilo ndio nazungumza hapa.

Mkuu, hilo la ubwana-mdogo linatoka wapi? umejuaje km mi ni mdogo kiasi cha kutojua chochote? Niombe msamaha, kwa sababu niko kwenye Cotton Industry na nina updates za kila siku kuhusu zao la pamba.

Mwaka 2011 unaosema bei elekezi ilikuwa Tsh. 1,100 wakati kwenye world market ikiwa US cents 120. Baadae bei ilishuka kwenye world market nakuwa 80 US Cents ndipo Bodi ya Pamba ilikaa tena na wadau na ku-review bei ikawa Tsh 800. Eti data zinaanzia mwezi Nov., 2011 umesoma kuanzia juu au umeangalia trend tu..?

Hiyo kampuni ya NIDA unayoisema mwaka 2011 haikununua pamba, na kiwanda chake ilikikodisha kwa Fresho Investments Co. Ltd baada ya kupata hasara mwaka 2010. Hicho kikao cha wadau kilichoshindwa kupata muafaka wa bei mi nilikuwepo. Hivyo, kama huna taarifa sahihi kaa kimya au uliza sio kujidhalilisha hapa JF.

Eng. Willy
 
haya mpambano uendeleeee ..........................eeeeehhhhh ikawaje tena?,tuendeleeeeeeeeeeeeeee..............
 
haya mpambano uendeleeee ..........................eeeeehhhhh ikawaje tena?,tuendeleeeeeeeeeeeeeee..............

Tony, find the possible cotton producer price as at 7 June 2012:

1. Basic information:

2. Revenues:
  • Lint price = 1.4045USD/kg (63.71*2.2045) = Tsh. 2,232/kg (1.4045*1,589)
  • Seeds price = 300*2 = Tsh. 600/2 kg.

  • Total revenues (1kg of lint + 2kg of seeds) = Tsh. 2,832 (equivalent to 3kg of raw-cotton)
  • Divide by 3 to get the price/kg of raw-cotton = Tsh. 944.
  • Less Tsh. 200 (Ginner expenses as per PWC) for the ginnery operating at optimum efficiency = Tsh. 744.

3. Bodi ya Pamba stands for Tsh. 700/kg as an indicative price.
4. Wakulima and Politicians stands for Tsh. 1,000/kg
(below that piga mawe; source: John Cheyo - MP).
5. Ginners stands for Tsh. 500/kg
(most of them operate at cost of Tsh. 400/kg due to inefficiency).

So, there is where the misunderstanding btn these cotton stakeholders comes from.

Eng. Willy
 
Back
Top Bottom