Kulingana na baadhi ya hizi sheria za mafao ya viongozi zimekaa kimtego zaidi . Inabidi zifanyiwe marekebisho hili kulinda maslahi ya Taifa. Mfano mtu aliyeshindwa uongozi kwa uzembe au ufisadi anaweza kuishia kujiuzulu na kuendelea kufaidi pesa ya walipa kodi.This will be hard but 'yes we can get there' if there is a political will accompanied by a public pressure through our representatives and civic sociaties
Serikali :Lowassa na wenzake waliojiuzulu walilipwa mafao
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imesema viongozi wa kisiasa waliojiuzulu kutokana na sababu mbalimbali, walilipwa mafao yao kwa kuzingatia sheria za kazi pamoja na katiba ya nchi.
Viongozi waliojiuzulu ni pamoja na aliyekuwa waziri mkuu wa awamu ya nne, Edward Lowassa.
Akijibu swali la Mbunge wa Karatu, Dk. Wilibrod Slaa (Chadema), Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari, alisema kumekuwepo na utata wa kutafsiri juu mtu kufukuzwa kazi na kujiuzulu.
Alisema kuwa suala hilo halijafafanuliwa katika sheria za mafao ya viongozi wa kisiasa namba tatu ya mwaka 1999 kifungu cha tano na sheria ya pensheni ya mafao kwa watumishi wa
umma namba mbili ya mwaka 1999, kifungu cha 16.
Pamoja na utata huo, Sumari alisema: Viongozi wa kisiasa wanaojiuzulu wanastahili kulipwa mafao kama ilivyoainishwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa sababu hiyo, alisema viongozi wote wa kisiasa waliojiuzulu walilipwa mafao yao kwa kuzingatia sheria namba tatu ya mwaka 1999 kifungu cha tano.
Sumari aliwataja waliofaidika na sheria hiyo kuwa ni rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, makamu wa rais wa serikali ya awamu ya tatu, Hayati Dk. Omar Juma.
Wengine ni waliowahi kuwa mawaziri wakuu, Lowassa (awamu ya nne) na Frederick Sumaye (awamu ya tatu).
Wengine ni spika wa bunge la serikali ya awamu ya tatu, Pius Msekwa, mawaziri na manaibu wa serikali ya awamu ya nne na tatu, wakuu wa mikoa na wilaya (awamu ya tatu) na
wabunge wote walioishia katika kipindi cha mwaka 2000 na 2005.
Katika kuuliza swali lake, Dk. Slaa alisema kuwa kifungu cha nne cha sheria ya mafao ya viongozi wa kisiasa, kinatoa tafsiri ya viongozi wastaafu kwa maneno ya aliyeshika nafasi na aliyeacha kushika nafasi hiyo.
Katika kujenga hoja yake, Dk. Slaa alisema kuwa tafsiri inaacha utata jinsi mhusika anavyoacha uongozi yaani kwa kustaafu, kustaafishwa, kufukuzwa au kujiuzulu mwenyewe na hasa ikizingatiwa kuwa kwa mujibu wa sheria maneno hayo yanatofautiana kuhusiana na malipo ya mafao.
Dk. Slaa alitaka kufahamu tafsiri inayostahili malipo ya mafao, taratibu za mafao zinazotumika kwa viongozi hao na pia idadi ya viongozi ambao wamefaidika kwa majina na vyeo pamoja na kiasi walicholipwa.
Hata hivyo, Sumari alikataa kutaja kiwango cha fedha walizolipwa viongozi hao wa kisiasa kwa maelezo kuwa walilipwa kulingana na stahili zao.
Mwananchi Read News
Serikali :Lowassa na wenzake waliojiuzulu walilipwa mafao
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imesema viongozi wa kisiasa waliojiuzulu kutokana na sababu mbalimbali, walilipwa mafao yao kwa kuzingatia sheria za kazi pamoja na katiba ya nchi.
Viongozi waliojiuzulu ni pamoja na aliyekuwa waziri mkuu wa awamu ya nne, Edward Lowassa.
Akijibu swali la Mbunge wa Karatu, Dk. Wilibrod Slaa (Chadema), Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari, alisema kumekuwepo na utata wa kutafsiri juu mtu kufukuzwa kazi na kujiuzulu.
Alisema kuwa suala hilo halijafafanuliwa katika sheria za mafao ya viongozi wa kisiasa namba tatu ya mwaka 1999 kifungu cha tano na sheria ya pensheni ya mafao kwa watumishi wa
umma namba mbili ya mwaka 1999, kifungu cha 16.
Pamoja na utata huo, Sumari alisema: Viongozi wa kisiasa wanaojiuzulu wanastahili kulipwa mafao kama ilivyoainishwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa sababu hiyo, alisema viongozi wote wa kisiasa waliojiuzulu walilipwa mafao yao kwa kuzingatia sheria namba tatu ya mwaka 1999 kifungu cha tano.
Sumari aliwataja waliofaidika na sheria hiyo kuwa ni rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, makamu wa rais wa serikali ya awamu ya tatu, Hayati Dk. Omar Juma.
Wengine ni waliowahi kuwa mawaziri wakuu, Lowassa (awamu ya nne) na Frederick Sumaye (awamu ya tatu).
Wengine ni spika wa bunge la serikali ya awamu ya tatu, Pius Msekwa, mawaziri na manaibu wa serikali ya awamu ya nne na tatu, wakuu wa mikoa na wilaya (awamu ya tatu) na
wabunge wote walioishia katika kipindi cha mwaka 2000 na 2005.
Katika kuuliza swali lake, Dk. Slaa alisema kuwa kifungu cha nne cha sheria ya mafao ya viongozi wa kisiasa, kinatoa tafsiri ya viongozi wastaafu kwa maneno ya aliyeshika nafasi na aliyeacha kushika nafasi hiyo.
Katika kujenga hoja yake, Dk. Slaa alisema kuwa tafsiri inaacha utata jinsi mhusika anavyoacha uongozi yaani kwa kustaafu, kustaafishwa, kufukuzwa au kujiuzulu mwenyewe na hasa ikizingatiwa kuwa kwa mujibu wa sheria maneno hayo yanatofautiana kuhusiana na malipo ya mafao.
Dk. Slaa alitaka kufahamu tafsiri inayostahili malipo ya mafao, taratibu za mafao zinazotumika kwa viongozi hao na pia idadi ya viongozi ambao wamefaidika kwa majina na vyeo pamoja na kiasi walicholipwa.
Hata hivyo, Sumari alikataa kutaja kiwango cha fedha walizolipwa viongozi hao wa kisiasa kwa maelezo kuwa walilipwa kulingana na stahili zao.
Mwananchi Read News