Gluk
JF-Expert Member
- Mar 23, 2017
- 1,856
- 2,954
Habari wanajukwa.
Leo acha niwasanue wasimamizi wa kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha nyegezi mkoani mwanza.
Huenda hawajui haya au wanajua ila wanafumbia macho
Kwanza wale wanaokatisha tiketi za kuingia ndani kituoni mara nyingi ukiwapa pesa kubwa wanakata shilingi 300 badala ya sh 200 halali na kukwambia kuwa hawana shilingi 100 na kutokana kuwa watu ni wengi na ww una haraka unaamua kuacha hiyo sh 100.
Cha pili baada ya abiria kupewa tiketi ya kuingia ndani kituoni kuna watu ambao kazi yao ni kuchukua zile tiketi na kuzichana, ila hawafanyi hivyo kwa tiketi zote na matokeo yake baadhi ya tiketi hurudishwa katika mzunguko na kuuzwa kwa mara ya pili.
Wahusika chukueni hatua kama mlizochukua katika kituo cha mabasi Magufuli kwa kuweka mfumo wa kadi badala ya tiketi.
Jumapili njema nyote.
Leo acha niwasanue wasimamizi wa kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha nyegezi mkoani mwanza.
Huenda hawajui haya au wanajua ila wanafumbia macho
Kwanza wale wanaokatisha tiketi za kuingia ndani kituoni mara nyingi ukiwapa pesa kubwa wanakata shilingi 300 badala ya sh 200 halali na kukwambia kuwa hawana shilingi 100 na kutokana kuwa watu ni wengi na ww una haraka unaamua kuacha hiyo sh 100.
Cha pili baada ya abiria kupewa tiketi ya kuingia ndani kituoni kuna watu ambao kazi yao ni kuchukua zile tiketi na kuzichana, ila hawafanyi hivyo kwa tiketi zote na matokeo yake baadhi ya tiketi hurudishwa katika mzunguko na kuuzwa kwa mara ya pili.
Wahusika chukueni hatua kama mlizochukua katika kituo cha mabasi Magufuli kwa kuweka mfumo wa kadi badala ya tiketi.
Jumapili njema nyote.