DOKEZO Serikali iko wapi masoko yanakuwa machafu kiasi hiki? Kipindupindu kitatuacha?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Anonymous

Senior Member
Feb 3, 2006
124
321
Hali ya masoko kwa kweli ni mbaya sana, yaani unaweza kununua bidhaa ukaharibu viatu na ukapata magonjwa mazingira ya masoko yetu. Kila mfanya biashara analipa ushuru wa kuwepo sokoni, hata hivyo inashindwa kubainika hela zinatumikaje? Mbona masoko machafu hadi yanatia kinyaa, na mengine hutoa harufu mbaya kabisa.

1705403162861.png
photo_3_2024-01-16_20-37-53.jpg
photo_7_2024-01-16_20-37-53.jpg

Leo nimetembelea soko la Tegeta Nyuki aisee, sijui kama kipindupindu kimetuacha au kinatuvutia kasi tu. Maeneo machafu hata kutembea ni shida. Angalia kama hali ya wauzaji matunda hapa na hayo maji machafu ya pembeni.

photo_12_2024-01-16_20-37-53.jpg
photo_13_2024-01-16_20-37-53.jpg
photo_17_2024-01-16_20-37-53.jpg
Fikiria uchafu huo halafu bado tupo comfortable kununua bidhaa bila kujali afya zetu. Mimi nadhani ni wakati kwa wafanyabiashara kudai matumizi ya fedha za ushuru zinazolipwa kila siku.

1705403223698.png
photo_24_2024-01-16_20-37-53.jpg
photo_16_2024-01-16_20-37-53.jpg
Kwa sasa kasi ya magonjwa yasiyoambukiza pia iko juu, kwa uchafu huu magonjwa ya upumuaji yanakosekanaje maana kutakuwa na hewa nzito mfanyabiashara anaivuta kutwa nzima.

1705402371970.png

Hebu angalia kama hapo, mtu unapitaje, yaani unatoka sokoni kama umetoka shamba miguu imechafuka matope matupu.

Ni kweli tumeshindwa kutumia hela za ushuru kutengeneza mitaro vizuri ili mvua zisilete athari kwa kiasi hiki cha kuhatarisha afya za watu.

Tunasubiri kupindupindu?
 
Maeneo mengi yalipojengwa Masoko, ni Maeneo ya CCM... Usiniulize ushuru unaenda wapi...!
 
Kumbe hatuna haja yakulaumu sana milipuko ya magonjwa maana mazingira tushayatengeneza wenyewe 😂😂milipuko inatuachaje kwa mfano
 
Ndio maana bima ya afya kwa wote itafail. Hata usafi tu umetushinda. Masikini na mtu asiye na elimu ni mzigo kwa bima.

Mtu mchafu, hali balanced diet, kazi ngumu ni lazima akipata nafasi ya kwenda bure aende kila siku.

Watu wengi wanaumwa lakiní wanakomaa kwasababu hospital gharama wanaishia duka la dawa. Wape bima uone sasa.
 
Yote na yote jamii pia inalo jukumu la kuimalisha usafi
Sio kila kitu selikali iwafanyie, Jamii sasa wao jukumu lao litakua lipi?
 
Yote na yote jamii pia inalo jukumu la kuimalisha usafi
Sio kila kitu selikali iwafanyie, Jamii sasa wao jukumu lao litakua lipi?
Kwanini inawatoza kodi kama wanataka wafanye usafi wao? Hizo tozo wanazipeleka wapi? Kununua ma V8?
 
Back
Top Bottom