Ishaka
Member
- Nov 1, 2011
- 74
- 12
Kinachoendelea sasa hivi katika kampuni ya tiGO in ubabaishaji mtupu uliosheheni wizi na dhuruma kwa wateja kwa zaidi ya miezi miwili sasa! Hivi hawa tiGO mikataba yao ya uwekezaji hapa nchini inasemaje mbona watanzania tunafanyiwa vituko kama vile nchi haina serikali?!
TiGO wamechoka mbaya nahisi wanaweza kutimka wakati wowote wakaiacha serikali solemba kama ilivyotokea kwa Meridian Beao Bank miaka ya nyuma.
Kama mitambo ya mtandao wa tiGO ni mibovu isiyotengenezeka na hawana uwezo wa kununua mipya basi ni vema wafunge virago watanzania tumechoshwa kuibiwa na kunyimwa huduma tulizozitarajia.
Fikiria hata kuongeza muda wa maongezi inakuwa taabu, watu kupiga simu hamsikilizani lakini pesa inakwenda, ukiweka sh. 2,000 ukatuma meseji 14 tu salio limekwisha, ukiongeza salio kutumia tiGO Pesa yaani ujue umekwisha! na usilogwe ukawakopa unapoishiwa salio maana wataendelea kukukata pesa yako kila unapoweka bila wewe kujua.
Halafu wanakela na mi-message yao ya kijinga ya promotion na upatu kila wakati mchana na usiku wa manane. Naomba mamlaka zinazohusika kuifungia mara moja hii kampuni kimeo ya tiGO.
Naomba kuwakilisha.
TiGO wamechoka mbaya nahisi wanaweza kutimka wakati wowote wakaiacha serikali solemba kama ilivyotokea kwa Meridian Beao Bank miaka ya nyuma.
Kama mitambo ya mtandao wa tiGO ni mibovu isiyotengenezeka na hawana uwezo wa kununua mipya basi ni vema wafunge virago watanzania tumechoshwa kuibiwa na kunyimwa huduma tulizozitarajia.
Fikiria hata kuongeza muda wa maongezi inakuwa taabu, watu kupiga simu hamsikilizani lakini pesa inakwenda, ukiweka sh. 2,000 ukatuma meseji 14 tu salio limekwisha, ukiongeza salio kutumia tiGO Pesa yaani ujue umekwisha! na usilogwe ukawakopa unapoishiwa salio maana wataendelea kukukata pesa yako kila unapoweka bila wewe kujua.
Halafu wanakela na mi-message yao ya kijinga ya promotion na upatu kila wakati mchana na usiku wa manane. Naomba mamlaka zinazohusika kuifungia mara moja hii kampuni kimeo ya tiGO.
Naomba kuwakilisha.