Nyakageni
JF-Expert Member
- Feb 1, 2011
- 15,045
- 5,093
Hivi Kawe na Ubungo mmekosa nini? Ni 'uongo' gani waliwaambia? Au Mnyika na Mdee waliiba kura? Kwa miaka 50 ya uhuru CCM imeifanya Dar kuwa peponi, wanakaa malaika, wenye heri na watakatifu!
Kichwa huuma zaidi kuona CCM inachaguliwa mikoani. Mikoani wanakaa mashetani, misukule na mazimwi kwa mtizamo wa CCM! Mtwara wameanza kujitoa 'usukule', hongera sana japo gharama yake ni kubwa, mmepigwa, mmebakwa, mmeuliwa!
Kwa upendeleo huu wa wazi, si chama pendwa CHADEMA kinachoweza kutuokoa, kwani hata Mbowe ana miradi peponi! Upendeleo wa wazi ni kama:
1. AFYA
Muhimbili iko Dar na wala siyo Dodoma au Singida! Ziada wana Ocean Road, Heart Institute, Temeke, Amana, Mwananyamala! Hadhi ya hospitali za wilaya za Dar ni bora kuliko zetu mikoani kama Kitete pale Tabora
2. USAFIRI
Kila kona ya Dar lami zenye service road! Service road ziko Dar tu, kwa malaika! Barabara zote ziko chini ya TANROADS.
Treni mikoani haziendi ila Dar kila siku zinapiga kazi!
Barabara za mbinguni zinajengwa na magari ya kasi (BRT) kubeba malaika, sisi kule Shinyanga usafiri baiskeli! Kigoma wamelia machozi ya damu kwa miaka 50 ya daraja la Malagarasi, Kigamboni hata hawajaomba linajengwa! Gharama kama mara kumi ya lile ya Malagarasi
3. MAKAZI
Dar umeme upo kila kona, 100%. Kigoma toka uhuru hakuna!! Lindi na Mtwara ni 3%. Shirika la nyumba la taifa (NHC) miradi yake iko Dar tu, jumla ya miradi yote ya mikoani ni sawa na Dar! Shida ya maji Dar ni nafuu kuliko Kigoma wenye mito, ziwa na chemchem. Kanda yote ya ziwa na magharibi hakuna hata kiwanda cha cement kimoja, nobody cares!
Dr. Slaa alizunguka kwa ndege akaona tembe akapaza sauti kushusha bei, CCM kutudhihaki eti nyumba zetu za tembe wanazijenga pale Makumbusho-Kijitonyama kama kumbukumbu!
4. ELIMU
Dar ina vyuo zaidi ya 40 vya elimu ya juu! Mwanza jiji la pili lina vitano tu!
Mwisho: Kauli za mawaziri wetu ndo kero zaidi, mi huwaita mawaziri wa Dar!
*@Anna Tibaijuka: Kigamboni iwe kama London, Jangwani pawe city garden ya kisasa Afrika! Manzese nyumba zibomolewe na kujengwa maghorofa! Dar iwe satellite city!
*Magufuli: Dar ijenge vertical, barabara za juu! Wanaoandamana wapite kwenye lami!-Kibondo je kwa wanaoandamana?
NI DHAMBI KWA MIKOANI KUCHAGUA CCM
__________
Mbowe_ ni m/kiti na KUB kauli yake ikulu lazima wakae vikao
Mnyika_ ni mkurugenzi uenezi na sera CDM
Mdee_ ni waziri kivuli wa ardhi awaambie watoe baadhi ya vyuo Dar na viwanda vijengwe mikoani.
Kichwa huuma zaidi kuona CCM inachaguliwa mikoani. Mikoani wanakaa mashetani, misukule na mazimwi kwa mtizamo wa CCM! Mtwara wameanza kujitoa 'usukule', hongera sana japo gharama yake ni kubwa, mmepigwa, mmebakwa, mmeuliwa!
Kwa upendeleo huu wa wazi, si chama pendwa CHADEMA kinachoweza kutuokoa, kwani hata Mbowe ana miradi peponi! Upendeleo wa wazi ni kama:
1. AFYA
Muhimbili iko Dar na wala siyo Dodoma au Singida! Ziada wana Ocean Road, Heart Institute, Temeke, Amana, Mwananyamala! Hadhi ya hospitali za wilaya za Dar ni bora kuliko zetu mikoani kama Kitete pale Tabora
2. USAFIRI
Kila kona ya Dar lami zenye service road! Service road ziko Dar tu, kwa malaika! Barabara zote ziko chini ya TANROADS.
Treni mikoani haziendi ila Dar kila siku zinapiga kazi!
Barabara za mbinguni zinajengwa na magari ya kasi (BRT) kubeba malaika, sisi kule Shinyanga usafiri baiskeli! Kigoma wamelia machozi ya damu kwa miaka 50 ya daraja la Malagarasi, Kigamboni hata hawajaomba linajengwa! Gharama kama mara kumi ya lile ya Malagarasi
3. MAKAZI
Dar umeme upo kila kona, 100%. Kigoma toka uhuru hakuna!! Lindi na Mtwara ni 3%. Shirika la nyumba la taifa (NHC) miradi yake iko Dar tu, jumla ya miradi yote ya mikoani ni sawa na Dar! Shida ya maji Dar ni nafuu kuliko Kigoma wenye mito, ziwa na chemchem. Kanda yote ya ziwa na magharibi hakuna hata kiwanda cha cement kimoja, nobody cares!
Dr. Slaa alizunguka kwa ndege akaona tembe akapaza sauti kushusha bei, CCM kutudhihaki eti nyumba zetu za tembe wanazijenga pale Makumbusho-Kijitonyama kama kumbukumbu!
4. ELIMU
Dar ina vyuo zaidi ya 40 vya elimu ya juu! Mwanza jiji la pili lina vitano tu!
Mwisho: Kauli za mawaziri wetu ndo kero zaidi, mi huwaita mawaziri wa Dar!
*@Anna Tibaijuka: Kigamboni iwe kama London, Jangwani pawe city garden ya kisasa Afrika! Manzese nyumba zibomolewe na kujengwa maghorofa! Dar iwe satellite city!
*Magufuli: Dar ijenge vertical, barabara za juu! Wanaoandamana wapite kwenye lami!-Kibondo je kwa wanaoandamana?
NI DHAMBI KWA MIKOANI KUCHAGUA CCM
__________
Mbowe_ ni m/kiti na KUB kauli yake ikulu lazima wakae vikao
Mnyika_ ni mkurugenzi uenezi na sera CDM
Mdee_ ni waziri kivuli wa ardhi awaambie watoe baadhi ya vyuo Dar na viwanda vijengwe mikoani.