Sekondari ya wavulana Tabora irudishwe katika mfumo wake

senzighe

JF-Expert Member
Jan 1, 2012
1,983
1,521
Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na malalamiko mengi ya kupotea kwa uzalendo miongoni mwa watanzania kutokana na tabia na mienendo mbalimbali iliyokuwa na inayoendelea kujitokeza.Mengi yamezungumzwa na kutafsiriwa kama ni ukosefu wa uzalendo hasa yanapojitokeza kwenye nyanja za kisiasa katika mikutano,washa,makongamano na hata bungeni.

Kuelekea mwishoni mwa miaka ya 1990 tulishuhudia kusimamishwa kwa uchukuaji wa vijana wa JKT kwa mujibu wa sheria kwa sababu zilizotolewa kwa wakati huo lakini miaka ya hivi karibuni baada ya serikali kung'amua mmomonyoko wa maadili na ukosefu wa uzalendo miongoni mwa vijana ,serikali iliamua angalau baadhi ya vijana wanaohitimu elimu ya juu ya sekondari huchaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria .Tuna imani hapo baadae wote wanaohitimu watashirikishwa kwenye mafunzo hayo.

Kati ya mwanzoni mwa miaka ya 1970 na miaka ya 1990 sekondari ya wavulana ya Tabora maarufu kama Tabora Boys' ilikuwa ni shule inayochukua vijana kutoka kila mkoa wa Tanzania ambapo mbali ya kufundishwa masomo ya kawaida ,vijana walifundishwa na kuiva kikamilifu katika masuala ya siasa na ulinzi wa nchi yao na ni vijana waliokuwa wamejaa uzalendo wa dhati kwa nchi yao kwa muelekeo na vitendo vyao.

Siyo kwa uzalendo huu wa sasa wa watu kujinasibu wenyewe wakati wa mchana lakini ifikapo usiku hubadilika .Matunda ya vijana hao wa miaka hiyo kutoka Tabora Boys' yanaonekana mpaka sasa kwani wengi ni viongozi katika taasisi ,makampuni ,taasisi za elimu ya juu,makamanda wakubwa katika majeshi yetu nakadhalika wakiwa bado wamejawa na heshima ya uzalendo wa nchi yao.

Tunaiomba serikali kwa jinsi ilivyofikiria umuhimu wa kuanzisha tena mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria basi ione tena umuhimu wa kuirudisha shule ya sekondari ya wavulana Tabora katika mfumo wake ule ili tuendelee kuzalisha vijana wenye maadili mazuri na wenye uzalendo kwa Taifa lao.
 
Mada ya msingi sana katika kipindi hiki ambacho taifa lina nia ya kujenga kwa dhati uzalendo.JKT uliasisiwa na majemedari wa awamu ya kwanza mara baada ya Uhuru.Haikuwa na maana yoyote kulifuta au kuliendesha kunusuru nusu kama ilivyo sasa Mwaka mmoja ndani ya JKT ilitosha kuhitimisha kumjenga kijana kutambua na kuishi maisha ya Kitanzania Kinachopatikana ni kuboresha na kuongeza ari ya kulitumikia taifa.Kuwepo kwa shule zenye michepuko ya kijeshi pia kutumike kuwaandaa hata viongozi wa vizazi vijavyo .
 
Sio Tabora Boys pekee shule kadhaa zinatakiwa zirejeshwe kwenye michepuo iliyopangwa wakati huwo

Shule za kilimo zirejeshwe japo taratibu taratibu Hadi ziwe na mifumo ya michepuo husika, kibaha, galanos, bagamoyo, nk kilimo

Tanga ufundi nk

Nashauri wasichelewe kuchukua maoni haya ya maana kabisa.
 
It's too late......Wenyewe wanajiita The head of Tanzania..... Kilichobaki sasa hivi pale wanafunzi wenyewe wanaulewa mdogo katika masuala mbali mbali kiuchumi,siasa na hata kijamii pale wamekalia kukesha madarasani na kushiriki kwenye religious issues tu

Labda ikitokea sherehe wamealikwa tabora girls basi kuwaza upumbavu tu na kutongozana .

Kimsingi mamlaka zinazohusika ikiwemo maafisa elimu waliangalie mtoa mada ametoa point moja safi sana.
 
Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na malalamiko mengi ya kupotea kwa uzalendo miongoni mwa watanzania kutokana na tabia na mienendo mbalimbali iliyokuwa na inayoendelea kujitokeza.Mengi yamezungumzwa na kutafsiriwa kama ni ukosefu wa uzalendo hasa yanapojitokeza kwenye nyanja za kisiasa katika mikutano,washa,makongamano na hata bungeni.

Kuelekea mwishoni mwa miaka ya 1990 tulishuhudia kusimamishwa kwa uchukuaji wa vijana wa JKT kwa mujibu wa sheria kwa sababu zilizotolewa kwa wakati huo lakini miaka ya hivi karibuni baada ya serikali kung'amua mmomonyoko wa maadili na ukosefu wa uzalendo miongoni mwa vijana ,serikali iliamua angalau baadhi ya vijana wanaohitimu elimu ya juu ya sekondari huchaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria .Tuna imani hapo baadae wote wanaohitimu watashirikishwa kwenye mafunzo hayo.

Kati ya mwanzoni mwa miaka ya 1970 na miaka ya 1990 sekondari ya wavulana ya Tabora maarufu kama Tabora Boys' ilikuwa ni shule inayochukua vijana kutoka kila mkoa wa Tanzania ambapo mbali ya kufundishwa masomo ya kawaida ,vijana walifundishwa na kuiva kikamilifu katika masuala ya siasa na ulinzi wa nchi yao na ni vijana waliokuwa wamejaa uzalendo wa dhati kwa nchi yao kwa muelekeo na vitendo vyao.

Siyo kwa uzalendo huu wa sasa wa watu kujinasibu wenyewe wakati wa mchana lakini ifikapo usiku hubadilika .Matunda ya vijana hao wa miaka hiyo kutoka Tabora Boys' yanaonekana mpaka sasa kwani wengi ni viongozi katika taasisi ,makampuni ,taasisi za elimu ya juu,makamanda wakubwa katika majeshi yetu nakadhalika wakiwa bado wamejawa na heshima ya uzalendo wa nchi yao.

Tunaiomba serikali kwa jinsi ilivyofikiria umuhimu wa kuanzisha tena mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria basi ione tena umuhimu wa kuirudisha shule ya sekondari ya wavulana Tabora katika mfumo wake ule ili tuendelee kuzalisha vijana wenye maadili mazuri na wenye uzalendo kwa Taifa lao.
Hauwezi kujenga uzalendo wakati huohuo unawabagua baadhi ya wananchi, kisa haukipendi chama chao.
 
It's too late......Wenyewe wanajiita The head of Tanzania..... Kilichobaki sasa hivi pale wanafunzi wenyewe wanaulewa mdogo katika masuala mbali mbali kiuchumi,siasa na hata kijamii pale wamekalia kukesha madarasani na kushiriki kwenye religious issues tu

Labda ikitokea sherehe wamealikwa tabora girls basi kuwaza upumbavu tu na kutongozana .

Kimsingi mamlaka zinazohusika ikiwemo maafisa elimu waliangalie mtoa mada ametoa point moja safi sana.
Tabora school alumni wote wanapaswa kujiorganize wakajenge library ya kisasa pale. Ikiwezekana laboratory kubwa za kisasa shule iendelee kuzalisha vichwa vya taifa.
 
It's too late......Wenyewe wanajiita The head of Tanzania..... Kilichobaki sasa hivi pale wanafunzi wenyewe wanaulewa mdogo katika masuala mbali mbali kiuchumi,siasa na hata kijamii pale wamekalia kukesha madarasani na kushiriki kwenye religious issues tu

Labda ikitokea sherehe wamealikwa tabora girls basi kuwaza upumbavu tu na kutongozana .

Kimsingi mamlaka zinazohusika ikiwemo maafisa elimu waliangalie mtoa mada ametoa point moja safi sana.
Japo kwa mambo uliyoyataja vijana wale wako tofauti sana na vichwa panzi wanaotokea shule zingine hasa Milambo and co.
 
Ninachokiona mimi sio Tabora boys tu ila iwe ni kwa shile zote zilizokuwa zikiitwa za Vipaji Maalum, zirudi upyaa. Binafsi huwa najiuliza, hivi serikali inawezaje kuiacha Elimu yetu ikining'inia shimoni huku ikinunua magari ya Kifahari kila mwaka kwa pesa nyingi?!!!!?
 
Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na malalamiko mengi ya kupotea kwa uzalendo miongoni mwa watanzania kutokana na tabia na mienendo mbalimbali iliyokuwa na inayoendelea kujitokeza.Mengi yamezungumzwa na kutafsiriwa kama ni ukosefu wa uzalendo hasa yanapojitokeza kwenye nyanja za kisiasa katika mikutano,washa,makongamano na hata bungeni.

Kuelekea mwishoni mwa miaka ya 1990 tulishuhudia kusimamishwa kwa uchukuaji wa vijana wa JKT kwa mujibu wa sheria kwa sababu zilizotolewa kwa wakati huo lakini miaka ya hivi karibuni baada ya serikali kung'amua mmomonyoko wa maadili na ukosefu wa uzalendo miongoni mwa vijana ,serikali iliamua angalau baadhi ya vijana wanaohitimu elimu ya juu ya sekondari huchaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria .Tuna imani hapo baadae wote wanaohitimu watashirikishwa kwenye mafunzo hayo.

Kati ya mwanzoni mwa miaka ya 1970 na miaka ya 1990 sekondari ya wavulana ya Tabora maarufu kama Tabora Boys' ilikuwa ni shule inayochukua vijana kutoka kila mkoa wa Tanzania ambapo mbali ya kufundishwa masomo ya kawaida ,vijana walifundishwa na kuiva kikamilifu katika masuala ya siasa na ulinzi wa nchi yao na ni vijana waliokuwa wamejaa uzalendo wa dhati kwa nchi yao kwa muelekeo na vitendo vyao.

Siyo kwa uzalendo huu wa sasa wa watu kujinasibu wenyewe wakati wa mchana lakini ifikapo usiku hubadilika .Matunda ya vijana hao wa miaka hiyo kutoka Tabora Boys' yanaonekana mpaka sasa kwani wengi ni viongozi katika taasisi ,makampuni ,taasisi za elimu ya juu,makamanda wakubwa katika majeshi yetu nakadhalika wakiwa bado wamejawa na heshima ya uzalendo wa nchi yao.

Tunaiomba serikali kwa jinsi ilivyofikiria umuhimu wa kuanzisha tena mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria basi ione tena umuhimu wa kuirudisha shule ya sekondari ya wavulana Tabora katika mfumo wake ule ili tuendelee kuzalisha vijana wenye maadili mazuri na wenye uzalendo kwa Taifa lao.
Tatizo maana ya uzalendo imetekwa na wanyonyaji .
Wale waliosoma hapo miaka ya sabini na Sitini ndio waliozihujumu kwa sababu ya uzalendo wao feki.

Uzalendo kwa sasa umekua ni kama tiketi ya kuwa Mkoloni mweusi.

Umewahi kujiuliza kati ya mgambo wanaofanya kazi kubwa kabisa za ulinzi bila kulipwa mshahara wowote na wale wengine wa juu wanaojiita wazalendo ndani ya mamiwani na maVX badala ya jeep nani mzalendo wa kweli?

Hakuna mtu wa juu mzalendo .
Never on earth.
Ni watu wanaopigania maslahi yao na watoto wao ili wawarithishe watoto wao Mali na vyeo kama wao.

Kaa ufikiri na uweke pembeni ushabiki wa kisiasa, utajua kweli , nayo kweli itakuweka huru mbali na dhambi.

Uzalendo ungekuwepo kwa waliopita JKT ,Shule kama Mazengo Technical School isingezimwa na kuwa Chuo cha Kata wakati ni shule iliyokuwa inachukua Wanafunzi toka Tanzania nzima hasa upande wa Ufundi na masomo ya PGM na EGM.
Shule kama Mkwawa pia ziliuawa na wazalendo wabinafsi na waoga. Walioamua kuua fursa ya watoto maskini kupata elimu ya uhakika na iliyokua inawajenga vijana kuwa na ujasiri na umoja na kuanza kujifunza uongozi wa kuwatumikia watanzania bila Ubaguzi.

Hizi shule ziliwaunganisha vijana wa Tanzania nzima kitaaluma. Woga wa wazalendo feki baada ya kuona kuwa vijana wengi wanapata elimu na wakati wa uchaguzi kwenye vituo ndani ya maeneo ya shule walikua hawapati kura wakahofia vyeo vyao , wakaamua wazifute shule nyingi za Umma zilizokua bora kabisa na kuanzisha shule dhaifu za Kata.

Kama tunataka kujenga Uzalendo basi turudi enzi za kina Kawawa . Nchi ijengwe na wenye moyo. Sio wenye meno.
Ili tuwe wazalendo wa kweli basi Waziri awe Tayari kufanya kazi ya Uwaziri kwa mshahara kama ya watumishi wengine wenye elimu sawa na ya kwake mana kazi zote zinafanywa na waliopo chini yake as a team work.
TRA / Hazina / BOT wawe na mishahara sawa na idara nyingine wenye elimu sawa na za kwao. Ama yakwao iwashushwe au wengine ipandishwe ifikie yakwao. Wakulima wa Mbaazi na mahimdi ,mazao yao nayo yanunuliwe na serikali.
Wafanyabiashara walipiwe fidia kwenye bidhaa walizoweka madukani na kukosa wateja kwa muda mrefu kwa kupunguziwa au kusamehewa kodi.

Watanzania wafanye kazi kizalendo sio kama ilivyo sasa watu wananyemelea nafasi zenye maslahi makubwa wakishazipata wanakejeli wenzao kwa kijikinai kuwa wao ni wazalendo ,ndio wanaopiga kelele za kejeli na vitisho na dhihaka kwa watumishi wengine na watanzania wenye maslahi duni.
Kila mtu afaidi maisha ya hapa duniani kama. Huo utakua ni ujamaa wa kweli na kujitegemea ambao utazaa uzalendo wa kweli na usawa bila kuwa na wanyonyaji na matabaka ndani ya nchi moja kuna mabwana na watwana kupitia rasilimali za umma.

Uzalendo sio kukimbia mchakamchaka maporini ,uzalendo ni kujenga mazingira yenye usawa na haki kwa wote.
Kama uchumi ni mdogo wote waonje joto ya jiwe. Kama uchumi umekua wote wafurahiye.
 
Wapi ifunda tech shule iliyonipa maujanja ya mkate wa kila siku ila now imebakia magofu
 
Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na malalamiko mengi ya kupotea kwa uzalendo miongoni mwa watanzania kutokana na tabia na mienendo mbalimbali iliyokuwa na inayoendelea kujitokeza.Mengi yamezungumzwa na kutafsiriwa kama ni ukosefu wa uzalendo hasa yanapojitokeza kwenye nyanja za kisiasa katika mikutano,washa,makongamano na hata bungeni.

Kuelekea mwishoni mwa miaka ya 1990 tulishuhudia kusimamishwa kwa uchukuaji wa vijana wa JKT kwa mujibu wa sheria kwa sababu zilizotolewa kwa wakati huo lakini miaka ya hivi karibuni baada ya serikali kung'amua mmomonyoko wa maadili na ukosefu wa uzalendo miongoni mwa vijana ,serikali iliamua angalau baadhi ya vijana wanaohitimu elimu ya juu ya sekondari huchaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria .Tuna imani hapo baadae wote wanaohitimu watashirikishwa kwenye mafunzo hayo.

Kati ya mwanzoni mwa miaka ya 1970 na miaka ya 1990 sekondari ya wavulana ya Tabora maarufu kama Tabora Boys' ilikuwa ni shule inayochukua vijana kutoka kila mkoa wa Tanzania ambapo mbali ya kufundishwa masomo ya kawaida ,vijana walifundishwa na kuiva kikamilifu katika masuala ya siasa na ulinzi wa nchi yao na ni vijana waliokuwa wamejaa uzalendo wa dhati kwa nchi yao kwa muelekeo na vitendo vyao.

Siyo kwa uzalendo huu wa sasa wa watu kujinasibu wenyewe wakati wa mchana lakini ifikapo usiku hubadilika .Matunda ya vijana hao wa miaka hiyo kutoka Tabora Boys' yanaonekana mpaka sasa kwani wengi ni viongozi katika taasisi ,makampuni ,taasisi za elimu ya juu,makamanda wakubwa katika majeshi yetu nakadhalika wakiwa bado wamejawa na heshima ya uzalendo wa nchi yao.

Tunaiomba serikali kwa jinsi ilivyofikiria umuhimu wa kuanzisha tena mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria basi ione tena umuhimu wa kuirudisha shule ya sekondari ya wavulana Tabora katika mfumo wake ule ili tuendelee kuzalisha vijana wenye maadili mazuri na wenye uzalendo kwa Taifa lao.
Inawezekana nawe umepita hapa sio kwa madini haya ya namna hii
 
Back
Top Bottom