RO7 ZA MGOS
JF-Expert Member
- Sep 27, 2016
- 1,663
- 4,570
ZIFAHAMU SEHEMU SABA HATARI ZAIDI DUNIANI KATIKA MAISHA YAKO.
Kwa fikra za kawaida tunadhani ya kwamba sehemu zinalindwa zaidi duniani ni Benki,Ikulu,kambi za jeshi na Bungeni labda kwa sababu ya kuwepo viongozi wakubwa wa taifa au hela zinazopatikana Benki hizo.
Leo nakuletea sehemu saba ambazo ni hatari zaidi duniani ambazo ukifika sehemu hizo kama siyo mhusika lazima uuwawe!.Sehemu hizo zinaulinzi wa hali ya juu sana.
1:BENKI YA FEDERAL RESERVE:- Hii ni Benki iliyopo katika jiji la New York,Marekani ambayo inatumika kuhifadhi zaida ya 25% ya dhahabu zote duniani.Benki hii ni moja kati ya sehemu zenye ulinzi mkali zaidi duniani ikiwa imejengwa kwa urefu wa futi hamsini kutoka usawa bahari na inalindwa na zaidi ya wanajeshi 5,000.
2: JUMBA LA GREENBRIER:- Jumba hili linapatikana katika mji wa Virginia,Marekani ambapo unaambiwa linatumika kuhifadhi vifaa vya nyuklia vya Marekani.Unaambiwa katika jumba hili ndipo viongozi wa juu wa Serikali na kijeshi hufanyia mkutano na kuamua wapi watashambulia.
3: MPAKA WA KOREA KUSINI NA KOREA KASKAZINI:- Huu ni mpaka ambao unazitenganisha nchi mbili mahasimu duniani.Ni moja kati ya sehemu ambazo zinalindwa zaidi duniani ambapo kuna zaidi ya wanajeshi 2,000 ambao hufanya doria.Ni vigumu kwa mtu kufika kwenye mpaka huu kwa sababu kufanya hivyo ni kuhatarisha maisha yako.
4: INAPOHIFADHIWA MITAMBO YA WIKILEAKES:- Miongoni mwa sehemu zinazopewa ulinzi mkubwa duniani ni pamoja na mahali panapohifadhiwa mitambo ya kundi la wanahabari wachunguzi ambao hutoa siri za nchi mbalimbali duniani wakiwemo viongozi wakubwa wanaotenda kinyume na taratibu za kiuongozi ikiwa ni pamoja na rushwa na matumizi mabaya ya ofisi.Mitambo hii ipo katika milima ya Sweden ambapo unaambiwa ina uwezo wa kuzia mabomu ya nyuklia.
5: GHALA LA DOOMSDAY:- Ghala la Doomsday lipo katika kisiwa cha Spitsbergen, Norway ikiwa ni moja kati ya sehemu zinazopewa ulinzi wa hali ya juu zaidi duniani.Ulinzi unaopewa ghala hili ni kwa sababu ndimo zilimohifadhiwa zaidi ya aina 3,000 za mbegu.Hii ni kulinda dunia iwapo kutatokea vita au majanga ya asili yatakayosababisha uhaba wa chakula duniani.
6: AREA 51:- Najua na kuamini kuwa ni watu wengi ambao wamewahi kusikia sehemu hii,ni moja kati ya sehemu zenye ulinzi mkali zaidi dunia.Ni eneo ambalo hutumika kutengeneza ndege za kivita za Marekani,mabomu ya nyuklia na vifaa vya kitekinolojia vilivyotumika katika safari ya mwezini mwaka 1945,na hii sehemu inahusishwa na kuhifadhi viumbe aina ya Aliens.Hawa ni viumbe wenye tekinolojia ya hali ya juu sana.
7: MLIMA WA CHUMA:- Mlima huu upo Pennsylvania, Marekani ambao unatumika kuhifadhi mitambo inayoendesha mitambo ya 'Internet'.Sehemu hii pia hutumika kuhifadhi data na nyaraka za siri za Serikali ya Marekani.
Ahsanteni sana 🙏🙏🙏.
C&P
Kwa fikra za kawaida tunadhani ya kwamba sehemu zinalindwa zaidi duniani ni Benki,Ikulu,kambi za jeshi na Bungeni labda kwa sababu ya kuwepo viongozi wakubwa wa taifa au hela zinazopatikana Benki hizo.
Leo nakuletea sehemu saba ambazo ni hatari zaidi duniani ambazo ukifika sehemu hizo kama siyo mhusika lazima uuwawe!.Sehemu hizo zinaulinzi wa hali ya juu sana.
1:BENKI YA FEDERAL RESERVE:- Hii ni Benki iliyopo katika jiji la New York,Marekani ambayo inatumika kuhifadhi zaida ya 25% ya dhahabu zote duniani.Benki hii ni moja kati ya sehemu zenye ulinzi mkali zaidi duniani ikiwa imejengwa kwa urefu wa futi hamsini kutoka usawa bahari na inalindwa na zaidi ya wanajeshi 5,000.
2: JUMBA LA GREENBRIER:- Jumba hili linapatikana katika mji wa Virginia,Marekani ambapo unaambiwa linatumika kuhifadhi vifaa vya nyuklia vya Marekani.Unaambiwa katika jumba hili ndipo viongozi wa juu wa Serikali na kijeshi hufanyia mkutano na kuamua wapi watashambulia.
3: MPAKA WA KOREA KUSINI NA KOREA KASKAZINI:- Huu ni mpaka ambao unazitenganisha nchi mbili mahasimu duniani.Ni moja kati ya sehemu ambazo zinalindwa zaidi duniani ambapo kuna zaidi ya wanajeshi 2,000 ambao hufanya doria.Ni vigumu kwa mtu kufika kwenye mpaka huu kwa sababu kufanya hivyo ni kuhatarisha maisha yako.
4: INAPOHIFADHIWA MITAMBO YA WIKILEAKES:- Miongoni mwa sehemu zinazopewa ulinzi mkubwa duniani ni pamoja na mahali panapohifadhiwa mitambo ya kundi la wanahabari wachunguzi ambao hutoa siri za nchi mbalimbali duniani wakiwemo viongozi wakubwa wanaotenda kinyume na taratibu za kiuongozi ikiwa ni pamoja na rushwa na matumizi mabaya ya ofisi.Mitambo hii ipo katika milima ya Sweden ambapo unaambiwa ina uwezo wa kuzia mabomu ya nyuklia.
5: GHALA LA DOOMSDAY:- Ghala la Doomsday lipo katika kisiwa cha Spitsbergen, Norway ikiwa ni moja kati ya sehemu zinazopewa ulinzi wa hali ya juu zaidi duniani.Ulinzi unaopewa ghala hili ni kwa sababu ndimo zilimohifadhiwa zaidi ya aina 3,000 za mbegu.Hii ni kulinda dunia iwapo kutatokea vita au majanga ya asili yatakayosababisha uhaba wa chakula duniani.
6: AREA 51:- Najua na kuamini kuwa ni watu wengi ambao wamewahi kusikia sehemu hii,ni moja kati ya sehemu zenye ulinzi mkali zaidi dunia.Ni eneo ambalo hutumika kutengeneza ndege za kivita za Marekani,mabomu ya nyuklia na vifaa vya kitekinolojia vilivyotumika katika safari ya mwezini mwaka 1945,na hii sehemu inahusishwa na kuhifadhi viumbe aina ya Aliens.Hawa ni viumbe wenye tekinolojia ya hali ya juu sana.
7: MLIMA WA CHUMA:- Mlima huu upo Pennsylvania, Marekani ambao unatumika kuhifadhi mitambo inayoendesha mitambo ya 'Internet'.Sehemu hii pia hutumika kuhifadhi data na nyaraka za siri za Serikali ya Marekani.
Ahsanteni sana 🙏🙏🙏.
C&P