Sasa kutuonyesha tupu zenu ndio nini!?

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Tafiti nyingi zinaonesha kwamba, mwanamke ambaye anavaa kwa njia yenye kuchokoza hisia, hawezi kutazamwa kama aliye na uwezo sawa na wengine mahali. Hii iko duniani kote, bila kujali kama ina ukweli au haina.

Njia rahisi kwa wanawake wasiopenda kuwajibika kwa maisha yao ni kuwalaumu wanaume, na ndio maana mie hata sishangai ninaposhambuliwa pale ninapoweka mada kuwakosoa wanawake. Mtu anazungumzia kuhusu kuvaa vibaya kwa wanawake kwamba, kunachangia kuwafanya waonekane ni bidhaa, wanawake wengine wanabisha. Kubisha huku ni kukataa kuwajibika. Lakini hata wakibisha, bado jamii zote zinaushikilia huo wanaoukataa kuwa ndiyo ukweli.

Mtu akijichukulia kwa udhati fulani, wengine nao watamchukulia kwa udhati huo. Akishindwa, wengine nao watashindwa kumchukulia kwa udhati unaostahili. Kama unataka kubishana na hao wengine, ni suala la kujaribu kuipinga hali halisi na kupinga kuwajibika kwa maisha yake. Hebu fikiria, hata kama ni mwanaume. Leo hii mwanasheria wa kiume amevaa 'pensi' huku akiwa ameteremsha mlegezo mpaka makalio yanaonekana na shati la 'ki-modo' na makobazi, unadhani ni nani atamkabidhi kesi yake. Hata kama ni mwanasheria mzuri vipi, labda tu kama mtu anamjua vizuri sana tangu hapo kabla.

Mwanamke ambaye ni afisa mahali kama Mamndenyi, akienda ofisini na kimini na kitopu chenye kuonesha kitovu, hakuna atakayetilia maanani maneno yake. Mhuni hatiliwi maanani. Kwa jamii, hizo ni nguo za kihuni, iwe ni kweli au sio kweli, ndiyo tafsiri yake. Mwanamke anapovaa kama kifaa, wanaume wanapomzonga au kumchukulia kama kifaa, hilo sio suala la unyanyasaji kijinsia, bali ndiyo hali halisi. Mtu wa zima-moto tunamjua kwa mavazi, mcheza mpira tunamtambua kwa mavazi, mwanafunzi hivyohivyo. Ndiyo maana kuna wakati makahaba wa jijini Dar walikuwa wanavaa kama wanafunzi na mashugadadi wakawa wanawachangamkia sana. Mavazi husema sisi ni nani na ni jamii imepanga siyo wanaume.

Huwa tunawaambia wengine sisi ni akina nani kwa lugha za ishara za aina mbalimbali, na ndio maana wengi hawashangazwi na majibu ya baadhi ya wana JF wanapojibu hoja humu jamvini, mfano mzuri kama, mzee mwenzangu Rejao, rafiki yangu Bujubuji, Ndyoko, au Washawasha. Hawa wamejijengea sifa moja kubwa humu jamvini, huwa hawamung'unyi maneno. Inawezekana wasichana wengi siku hizi hawajui kwamba huwa wanasema wao ni nani kupitia mavazi. Wanachojua wao ni fasheni ambayo wameiyona kwa wanawake fulani maarufu hususan wa nchi za Magharibi, lakini hawajui jamii inapokea ujumbe gani kwa mavazi yao.
 
Hata wewe umeona eh! Leo huenda nitakiona cha mtema kuni, ngoja waje Wabeijing hapa!

unajishtukia tu

binafsi linapokuja suala la uvaaji kila mtu kuna anachoangalia (labda umbo lake na rangi ya ngozi yake) na najua pia kuwa kila vazi lina sehemu yake. na hili si kwa wanawake tu hata wanaume mbona wengi tunawaona wanaacha maungo yao wazi (na mnavyotisha sasa...yak)
 
kuna uzi umeanziswa wa mapepo/majini/masabuli/masijui nn umeniboa jamani!! samahani babu kwa kuichakachua sledi yako !
 

Huwa tunawaambia wengine sisi ni akina nani kwa lugha za ishara za aina mbalimbali, na ndio maana wengi hawashangazwi na majibu ya baadhi ya wana JF wanapojibu hoja humu jamvini, mfano mzuri kama, mzee mwenzangu Rejao, rafiki yangu Bujubuji, Ndyoko, au Washawasha. Hawa wamejijengea sifa moja kubwa humu jamvini, huwa hawamung'unyi maneno. Inawezekana wasichana wengi siku hizi hawajui kwamba huwa wanasema wao ni nani kupitia mavazi. Wanachojua wao ni fasheni ambayo wameiyona kwa wanawake fulani maarufu hususan wa nchi za Magharibi, lakini hawajui jamii inapokea ujumbe gani kwa mavazi yao.
dah! Mtambuzi..hii research yako uliifanya saa ngapi? kumbe ni hivi! ...nilikuwa sijui aisee!
 
'.............Mwanamke ambaye ni afisa mahali kama Mamndenyi, akienda ofisini na kimini na kitopu chenye kuonesha kitovu, hakuna atakayetilia maanani maneno yake. Mhuni hatiliwi maanani .................'

Mkuu nimekukubali sana,
mkono wako ukipona tu mkuu lazima nikakupe ile kitu roho yako itapenda,
kwa sasa naendelea kukuombea tu.
 
unajishtukia tu

binafsi linapokuja suala la uvaaji kila mtu kuna anachoangalia (labda umbo lake na rangi ya ngozi yake) na najua pia kuwa kila vazi lina sehemu yake. na hili si kwa wanawake tu hata wanaume mbona wengi tunawaona wanaacha maungo yao wazi (na mnavyotisha sasa...yak)

Bee umeongea

Mwanamke na Mwanamme wote wanatakiwa kuvaa mavazi yanayoendana na matukio au mahala walipo.
 
  • Thanks
Reactions: bht
Bee umeongea

Mwanamke na Mwanamme wote wanatakiwa kuvaa mavazi yanayoendana na matukio au mahala walipo.

sasa Mtambuzi asilete mambo za 'blame game' hapa ilhali hili liko wazi kabisa...
kwa mwanamke au mwanaume linapokuja suala la mavazi, it is all about what, when and where to wear what u want to... (this should tell you how you should get dressed).
 
thatha kama joto limezidi, watafanyaje? inabidi tu wavae hivyo vimini, mgongo mgongo na naiti dress mchana! "Just jokin........"
 
yaan umenena kila kitu kwa usahihi na wengi eti ujiita ni watu wanaokwenda na wakati jamani c kila kitu uigwa tamaduni nyingine c zetu tunakopi na kupesti,message sent
 
Hahahahaa mtambuzi bana, naona leo umeanza na defence kwanza!! Mi naona issue hapo ni aina ya mavazi, wakati na sehemu uliyopo. Kwa sababu hata huyo mamndenyi mwenyewe hawezi kwenda ofisini juu kavaa mtishirt mkuubwaa, chini kajifunga kanga halafu miguuni kavaa raba mtoni, kisa tu ni nguo ya heshima!!!
 
Back
Top Bottom