The Informer
Senior Member
- Jun 14, 2010
- 119
- 29
Hodi JF,
Kuna taarifa za uhakika kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salva Rweyemamu, pamoja na business partner na rafiki wake wa siku nyingi, Dk. Gideon Shoo, wameanzisha gazeti la kila wiki la Kiswahili, TAFAKARI, ambalo linalenga uchaguzi mkuu ujao.
Hivi sasa inaelezwa kuwa kuna amri ya Ikulu kuwa Idara ya Habari, Maelezo, isitishe kusajili magazeti mapya eti mpaka sheria mpya ya Habari itakapopitishwa. Ni wazi hii ni mbinu ya kudhibiti media kwenye uchaguzi mkuu.
Hivi sasa Salva na Shoo wamekodi gazeti hilo la TAFAKARI kutoka kwa mmiliki wake halisi ili waliendeshe kwa muda kwenye kipindi hiki cha mavuno cha kuelekea uchaguzi mkuu.
Lengo la kuanzisha gazeti hillo ni kupata matangazo ya Bajeti za wizara za serikali kwenye Bunge linaloendelea sasa ili wavune at least 300 million shillings za matangazo.
Pia, gazeti hili linategemea kupata matangazo mengine zaidi kutoka serikalini na msaada wa system kwa makubaliano kuwa litakuwa linaandika habari za kumpamba Rais Jakaya Kikwete na chama cha CCM ili wapate ushindi wa kishindo 2010.
Watu walio karibu na 'wajanja' hawa wawili wanasema kuwa lengo haswa ni kwa Salva na Shoo kuvuna pesa za matangazo ya bajeti na uchaguzi mkuu kwa kupitia mgongo wa kumsaidia JK na CCM.
Inasemekena kuwa gazeti hili linaendeshwa kutoka ofisi iliyopo Sinza, Dar es Salaam, na lina idadi chache sana ya waandishi wa habari na wafanyakazi wengine. Salva na Shoo husemekana kuwa nao wanasaidia kuandika baadhi ya makala kwenye gazeti hilo.
Pamoja na kuwa na waandishi wachache mno, bado uongozi huo unachelewa kuwalipa mishahara yao na huenda kukawa na matatizo makubwa zaidi pesa za matangazo ya bajeti na uchaguzi zitakavyoanza kumiminika. Gazeti hili limejipa mategemeo makubwa ya kupata matangazo serikali kwa kujinadi kuwa ni "Special Project" ya kuhakikisha ushindi wa Kikwete na CCM kwenye uchaguzi wa 2010.
Ikumbukwe kuwa Salva na Shoo zamani walikuwa wakurugenzi wa Habari Corporation inayochapisha magazeti ya Mtanzania, Rai na mengineyo kabla ya kuuza kampuni hiyo kwa mbulushi Rostam Aziz -- yule mbunge wa Igunga anayehusishwa na Richmond, Kagoda, import support, kashfa ya kodi kwenye uagizaji mchele, mbolea, pembejeo, n.k.
Salva na swahiba wake, Shoo, wana kampuni ya Public Relations inayoitwa
G&S Media Consultancy. Hii kampuni ndiyo ilifanya kazi ya kuitangaza kampuni ya kitapeli ya Richmond Development Company LLC kupitia vyombo vya habari wakati ilipoingia Tanzania kufanya upigaji.
Katika mradi huu, Shoo ndiyo yuko front na Salva anaonekana kujificha kwa mbali asionekene kuhusika moja kwa moja.
Kweli nchi hii wajinga ndiyo huliwa!
Kuna taarifa za uhakika kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salva Rweyemamu, pamoja na business partner na rafiki wake wa siku nyingi, Dk. Gideon Shoo, wameanzisha gazeti la kila wiki la Kiswahili, TAFAKARI, ambalo linalenga uchaguzi mkuu ujao.
Hivi sasa inaelezwa kuwa kuna amri ya Ikulu kuwa Idara ya Habari, Maelezo, isitishe kusajili magazeti mapya eti mpaka sheria mpya ya Habari itakapopitishwa. Ni wazi hii ni mbinu ya kudhibiti media kwenye uchaguzi mkuu.
Hivi sasa Salva na Shoo wamekodi gazeti hilo la TAFAKARI kutoka kwa mmiliki wake halisi ili waliendeshe kwa muda kwenye kipindi hiki cha mavuno cha kuelekea uchaguzi mkuu.
Lengo la kuanzisha gazeti hillo ni kupata matangazo ya Bajeti za wizara za serikali kwenye Bunge linaloendelea sasa ili wavune at least 300 million shillings za matangazo.
Pia, gazeti hili linategemea kupata matangazo mengine zaidi kutoka serikalini na msaada wa system kwa makubaliano kuwa litakuwa linaandika habari za kumpamba Rais Jakaya Kikwete na chama cha CCM ili wapate ushindi wa kishindo 2010.
Watu walio karibu na 'wajanja' hawa wawili wanasema kuwa lengo haswa ni kwa Salva na Shoo kuvuna pesa za matangazo ya bajeti na uchaguzi mkuu kwa kupitia mgongo wa kumsaidia JK na CCM.
Inasemekena kuwa gazeti hili linaendeshwa kutoka ofisi iliyopo Sinza, Dar es Salaam, na lina idadi chache sana ya waandishi wa habari na wafanyakazi wengine. Salva na Shoo husemekana kuwa nao wanasaidia kuandika baadhi ya makala kwenye gazeti hilo.
Pamoja na kuwa na waandishi wachache mno, bado uongozi huo unachelewa kuwalipa mishahara yao na huenda kukawa na matatizo makubwa zaidi pesa za matangazo ya bajeti na uchaguzi zitakavyoanza kumiminika. Gazeti hili limejipa mategemeo makubwa ya kupata matangazo serikali kwa kujinadi kuwa ni "Special Project" ya kuhakikisha ushindi wa Kikwete na CCM kwenye uchaguzi wa 2010.
Ikumbukwe kuwa Salva na Shoo zamani walikuwa wakurugenzi wa Habari Corporation inayochapisha magazeti ya Mtanzania, Rai na mengineyo kabla ya kuuza kampuni hiyo kwa mbulushi Rostam Aziz -- yule mbunge wa Igunga anayehusishwa na Richmond, Kagoda, import support, kashfa ya kodi kwenye uagizaji mchele, mbolea, pembejeo, n.k.
Salva na swahiba wake, Shoo, wana kampuni ya Public Relations inayoitwa
G&S Media Consultancy. Hii kampuni ndiyo ilifanya kazi ya kuitangaza kampuni ya kitapeli ya Richmond Development Company LLC kupitia vyombo vya habari wakati ilipoingia Tanzania kufanya upigaji.
Katika mradi huu, Shoo ndiyo yuko front na Salva anaonekana kujificha kwa mbali asionekene kuhusika moja kwa moja.
Kweli nchi hii wajinga ndiyo huliwa!