drphone
JF-Expert Member
- Sep 29, 2009
- 3,542
- 281
Naona wewe hujui unachokiongea!! Maswali yetu ni haya;
1. Je mkuu wa mkoa alipaswa asome ile risala? Kwa nini isisomwe na mkuu wa shele ama mwenyekiti wa bodi ya shule? (iko wapi itifaki hapo kama si kujipendekeza?)
2. Anavyohutubia wananchi anahutubia kama nani na kwa minajiri ipi?
3. Je mke wa Rais ana mamlaka yoyote kikatiba hapa kwetu?
4. Je WAMA ni taasisi ya serikali? Kwa nini inatumia resources za serikali kama magari n.k.
5. Kwa nafasi yake kama mke wa Rais, je tutapimaje kama misaada inayotolewa kwa WAMA (based on her influence as the first lady) haitumiki kwa maslahi binafsi ya kwake na familia yake?
6. Kwa nini wakimaliza muda wao wa uongozi wanaondoka na taasisi zao?
7. Je huoni kwamba WAMA inatakiwa iwe responsible kwetu wananchi kwa sababu inatumia resources zetu kuanzia magari mpaka ofisi, sina uhakika na payroll, inawezekana pengine inatoka ikulu!!
Binafsi naona nchi hii inaendeshwa bila kufuata taratibu na best practice, mke wa rais ni mke kama walivyo wake zetu. Naamini anastahili ulinzi, mshahara na posho akisafiri basi. Haya mengine tunayoyaona ni mbwembwe tu za kikwere na yote yanatokana na watanzania kufubaa kiakili!
Vinginevyo tunatakiwa kuhoji haya mambo, kinyume na hapo siku Mama atakuja kumfukuza kazi waziri ama ofisa yoyote wa serikali kwa sababu naamini yeye na Mr. hawajui kama anavyofanya sasa si sahihi!! Wasaidizi wa rais pale ikulu wanajua haya si sahihi lakini hakuna mwenye ujasiri wa kumwambia Mama Salma wala Mkuu mwenyewe!
mkuu mm nasema ni kujikomba kwa wabongo kwa mkuu mpaka wanasahau majukumu yao