Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Baada ya waziri wa makazi,ardhi na nyumba prof.Anna Tibaijuka kuwasilisha ombi la Tanzania kuongezewa eneo la mita kadhaa za mraba baharini,SMZ imekuja juu.Serikali ya mapinduzi ya zanzibar imedai kwamba haikushirikishwa katika mpango huo.Pia SMZ imesema kwamba katika hali halisi,wao Zanzibar ndo wenye haki ya kwenda kuomba kuongezewa eneo baharini tena bila hata kuingiliwa na serikali ya jamhuri ya muungano ya Tanzania.SMZ imesema bara hawana haki yoyote katika suala hili na wamepotoka kwa kuchukua uamuzi huu.