Sakata la mchezaji Hassan Kessy, Simba wako sahihi

Mkuu, angalau hapa haki imeonekanabkutendeka tofauti na swala la Mbuyu, Yondani, Ramadhani sing'ano orodha inaendelea...halafu kumbuka ilikuwa imebaki siku nne mkataba uishe halafu tulikuwa tumemfungia ingawa kimkataba hata kama ilikuwa imebaki sekunde...
tutawapa 50 watoto wazuri kama haitoshi semeni tutawaongeza,mnataka hii 50 tuwape lini?
 
Hamsini tu. Mkude naye tutamsainisha kwa mfumo huo huo. Mkipiga sana kelele mtakuja kulipwa million 50 nyingine.
Wapiga dili wa mikia tayari wameishajua mgawo wao6katika hizo 50.
Rahisi sana kusema hivyo. Pesa sio zako hivyo rahisi sana kuzipangia budget. Kama unafikiri mhindi atalipa fidia bila hatua kuchukuliwa kwa mzembe aliyefanya ujinga huu unajidanganya.
 
Wengine hata pesa za vocha mgogoro bado wanashabikia ohh tutalipa. Anayelipa mhindi nyie wengine mnashobokea kulipiwa. Deni lilikuwa bilioni 11 siku mhindi akichoka jengo limekwenda na maji kwa mnada.
 
WATU WANASAHAU HARAKA SANA, HATA NGASA ALILIPIWA NA MHINDI ILI ACHEZE LAKINI KILA MWISHO WA MWEZI AKIENDA KUANGALIA MSHAHARA ANAKUTA NUSU, NUSU ILIYOBAKI ILIKUWA INALIPIA DENI. NA HUYO KESI AJIANDAE KAMA ALISHAPEWA ZA USJILI LAZIMA MHINDI AMKATE KAMA HAJAMALIZIWA ASUBIRI TU MAUMIVU.
 
Cha mijinga huliwa na mjanja. Mlijitia wajuaji. Mngeandika barua tu ya kuomba kuidhinishiwa. Siku 5 za mkataba zimezaa milioni 50.Mhindi sidhani kama atakubali kulipa kirahisi.Lazima vichwa vita roll kwa ujinga huu.
Huenda Rage alitumia zaidi kwa Mbuyu Twite wakati ule. Ndiyo viongozi wetu. Angalau kwa hili Simba wamepata pa kushikia baada ya kulizwa miaka mingi sana
 
Wengine hata pesa za vocha mgogoro bado wanashabikia ohh tutalipa. Anayelipa mhindi nyie wengine mnashobokea kulipiwa. Deni lilikuwa bilioni 11 siku mhindi akichoka jengo limekwenda na maji kwa mnada.
moo moo mooo mooo,mmekua ng'ombe???
 
Huenda Rage alitumia zaidi kwa Mbuyu Twite wakati ule. Ndiyo viongozi wetu. Angalau kwa hili Simba wamepata pa kushikia baada ya kulizwa miaka mingi sana
Mbuyu Twite pia Simba walirudishiwa millioni 30 na milioni 2 extra. Ngassa zilirudishwa na Yanga wakamkata kwenye mshahara.
 
Kuna mshauri mmoja mgongo wazi yeye kazi yake ni kuishauri Simba kuhusu usajili.Angeanza kushauri migongo wazi wenzake kwa madudu ya kusajili wachezaji wenye mikataba.Wana bahati jag ikienda FIFA adhabu itakuwa pamoja na kufungiwa kusajili.
 
Hiyo pesa ni ndogo., na adhabu kwa Yanga haitosherezi,, ni lazima Yanga wapokwe point I zote walizo mchezesha mchezaji ambaye si wao,,

Hapo sasa pamekuwa patamu hii kesi ya Kessy lazima ifike mbali zaidi ya hapa.,
 
Wangeongezewa adhabu maana wamekuwa malimbukeni sana kwa wachezaji wa Simba

Na bado...!
 
Usajiri wa Yanga vpl uko sawa kwani alikuwa amemaliza mkataba ndiyo maana kipengelebkilichowabana ni kupeleka jina cuf tarehe 10.6.2016 wakati mkataba wa Kessy na Simba ulikuwa unaisha tarehe 15.6.2016.
Yanga hadi hapo hawapo salama Kama jina walilipeleka CAF Tarehe 10.6.2016 hali mkataba wake ulikuwa unakoma 15.6 ni dhahiri walianza kumtumia akiwa ndani ya mkataba wa Simba.

Hapo sasa IPO hatar ya kunyang,anywa point zote alizocheza Kessy akiwa ndani ya kesi hii.
Yanga hapa wakae mkao wa kutoa hizo point kwa mujibu wa kifingu fulani cha Caf na Fifa ambacho Simba na timu zingine wakizihitaji hizi point basi wanitafute ili waibane Yanga kisheria wapewe point zao.
 
Cha mijinga huliwa na mjanja. Mlijitia wajuaji. Mngeandika barua tu ya kuomba kuidhinishiwa. Siku 5 za mkataba zimezaa milioni 50.Mhindi sidhani kama atakubali kulipa kirahisi.Lazima vichwa vita roll kwa ujinga huu.
Lakini unajua kipengele cha Mkataba wa Kessy na Simba kinataka alipe kiasi gani akivunja mkataba? Unajua kama hizo ndizo walizodai Simba kutoka kwa Yanga? Unajua Simba wakapunguza hizo hadi kiasi gani kwenye mazungumzo yaliyofuatia, ambazo Yanga walikataa kulipa? Unajua Simba watakushangaaje wakisikia unafurahia kiwango hicho ambacho ni cha chini mno kuliko thamani halisi ya Kessy? Kwa mnasaba huo, unajua nani aliyemshinda mwenzake kwenye kadhia hii?
 
Peleka hao Yanga FIFA maana hapa kuna mambo ya ajabu ajabu hapa wanadhani ni mambo kama ya ccm na ukawa
 
Tehe tehe, fidia ya bilio 2 aliyo kuwa anaitaka hanzpopo imeota mbaya na kuwa 50m,
 
Yaani serious hii kesi ilikuwa ni ya kupoteza miezi kadhaa ikijadiliwa? Kweli TFF hii imeamua kufanya kazi kinyume na na maendeleo ya mpira kwa kukumbatia mapenzi ya timu zao badala ya kufanya kazi waliyoomba wao wenyewe.

Masuala ya michezo yaliachwa kulalamikiwa ktk mahakama za kawaida ili mambo yaende haraka, badala yake kamati hii ya sheria inatumia miezi sita kujadili kitu kilicho wazi.

Natamani kuona siku mamlaka za soka nchini zitakapoamua kufanya kazi kwa kanuni zao ili na sisi tupige hatua
 
Yanga hadi hapo hawapo salama Kama jina walilipeleka CAF Tarehe 10.6.2016 hali mkataba wake ulikuwa unakoma 15.6 ni dhahiri walianza kumtumia akiwa ndani ya mkataba wa Simba.

Hapo sasa IPO hatar ya kunyang,anywa point zote alizocheza Kessy akiwa ndani ya kesi hii.
Yanga hapa wakae mkao wa kutoa hizo point kwa mujibu wa kifingu fulani cha Caf na Fifa ambacho Simba na timu zingine wakizihitaji hizi point basi wanitafute ili waibane Yanga kisheria wapewe point zao.
Uzidai baada ya ligi.. Wakati roho zinawauma
 
Lakini unajua kipengele cha Mkataba wa Kessy na Simba kinataka alipe kiasi gani akivunja mkataba? Unajua kama hizo ndizo walizodai Simba kutoka kwa Yanga? Unajua Simba wakapunguza hizo hadi kiasi gani kwenye mazungumzo yaliyofuatia, ambazo Yanga walikataa kulipa? Unajua Simba watakushangaaje wakisikia unafurahia kiwango hicho ambacho ni cha chini mno kuliko thamani halisi ya Kessy? Kwa mnasaba huo, unajua nani aliyemshinda mwenzake kwenye kadhia hii?
Simba bado wanaweza kuendelea na kumdai Kessy.Kwani mkataba unasema akivunja mkataba sio Yanga kama timu bali Kessy kama mchezaji. Aliyevunja masharti ya mkataba ni Kessy. Na habari za ndani ni kwamba Simba itaendelea kukomaa naye ili iwe fundisho kwa wachezaji wasioheshimu mikataba.
 
SIMBA WAMESHAONEWA SANA NA KUNYANYASWA TENA KWA MIAKA MINGI. KWA HILI VIONGOZI WASIKUBALI HIYO FIDIA KABISA KWA SABABU HAILINGANI KABISA NA KOSA LILILOFANYIKA. NA ZAIDI WAKATE RUFAA CAF/FIFA KUPINGA HIYO ADHABU NDOGO IKIWEZEKANA YANGA WANYANGA'NYWE POINTI ZOTE KWA MECHI ALIZOCHEZA KESSY ILI LIWE FUNDISHO KWA BAADHI YA VIONGOZI WA TFF NA KLABU YANGA.
Heeee ili mpate ubingwa subutuuuu....!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom