Sakata la kuficha Mabilioni Uswisi lachukua Sura mpya

Source: Mwananchi

Maoni yangu

Kwa maelezo ya Mkuchika inaonesha dhahiri kuwa ameshaandaa majibu ya hatma ya hili sakata ila sasa hivi anatafuta njia tu ya kumfikisha kwenye majibu yake. Hivi serikali gan inafanya uchunguziwa suala zito kwa kuwaita watu barabaran wapeleke taarifa za uhalifu?? hivi vyombo vyote vya usalama hawawezi kweli kufanya kazi hiyo???Hapa mwisho wa siku anataka kusema tuliwaomba wenye majina ya waloficha fedha Uswiss hawakujitokeza, hivyo km serikali tuliona habar hizo ni majungu tukaamua kuachana na hilo suala mana tulishindwa timiza kigezo vya serikali ya Uswiss.

Na je hata km majina hayo yatapelekwa kwake, je! tutakuwa na uhakuka gan kama atayafikisha Uswiss?? Najaribu kuimagine kwenye hayo majina kwa mfano katajwa JK na Pinda, hivi kweli Mkuchika atayapeleka Uswiss?? au anataka kutueleza nn hasa hapa??? Hapa suluhisho ni Tume maalum ya wabunge, tukimtegemea Mkuchika apeleke jina la aliyemteua Uswiss au mtoto wa aliyemteua Uswiss tutakuwa WENDAWAZIMU. CCM ni genge linaloongozwa na wezi hivyo tusitegemee km wanaweza wakakaangana mana wote ni wachafu. Hii kesi naona mtuhumiwa ni ngedele na hakimu ni Nyani.
asante kwa kuandika vizuri na kuonyesha uchungu ulionao kwa nchi yako. Tusipoteze muda mwingi kufikiri juu ya utatuzi wa haya matatizo na mengine kama hatujaanzia hapo kwenye kiini cha tatizo. Hapo kwenye red asiyepaelewa na aende akalale, asilalamike!
 
ر من خمسة عشرCUF مشكلة من مشاكل مسجلCCM النظام وضمن Chademaمزاياه ما يل

Tena wakome kabisaaa wasitueleze

Mkuu Ta Muganyizi naomba tafsiri kwani siyo wote twajua lugha hiyo.
 
Last edited by a moderator:
Ndani ya serikali hii ya CCM hamtapata jibu lolote lamaana, maana wahusika ndiyo wachunguzi: kuna EPA, KAGODA...Mpaka leohii kuna nini cha maana kilichofanyika, tunapoteza muda wetu, kama hatuta weza kuandamana maandamano ya "liwalo na liwe" ili tupate majibu ya maana tutakuwa tuna twanga maji kutafuta unga, hawa jamaa ni wendawazimu!
 
Wabongo bwana rahisi kweli kuwatawala, yaani wote humu wanaamini kuwa Bw.Zito Kabwe ana uwezo wa kupenya ngome ya secret banking ya Uswisi na kupata majina ya watu walioweka fedha huko, sasa nimeamini kwa nini mikutano ya CHADEMA inajaa lakini ikija kwenye kupiga kura wote wanaojaa kwenye mikutano wana mambo muhimu ya kufanya zaidi ya kwenda kupiga kura!
 
Mwishowe utasikia waziri akituambia "Uswizi imekana kuyajua majina ya hao vigogo walioficha pesa huko".
Na atamalizia kwa kusema "Uswizi imesema hakuna mtanzania yoyote mwenye akaunti usuzwi".

AKILI KUMKICHWA
KICHWA CHA MWENADAWAZIMU
kumkosoa Mwenyezi Mungu sio vizuri lakini angelisema kuwa "hakika na asemaye uongo afe hapo hapo" ingekuwa bora maana wengine tungeona japo aibu kuusema hadharani. Hiyo adhabu ingemfaa sana huyu waziri, unafiki wa kjupindukia huu!
 
hapa tuendelee tu na M4C haya mambo mengine ni kuchezeana akili,muda ukifika kila kitu kitakua sawa.Tusikate tamaa wa ipo siku pesa zetu zitarudi tu.!!!
 
Yaani wenye majina wampe! Si yameandikwa kwenye magazeti. Kwani yeye hajui kusoma.

magazeti wameyatoa wapi?.
Unajua kwamba bank za uswis zina sheria ya kulinda majina ya wenye account?.
Au magazeti walihack website za mabenk ya swizland.
 
Kwani maana ya ku-hire private investigator ni nini?! Asikudanganye mtu, kuna URASIMU wa kutisha kwenye banking system ya Uswisi hususani linapokuja suala la CONFIDETIALITY. N pamoja na kwamba tayari wana secrecy ya hali ya juu, lakini bado wana kitu kingine kinachoitwa Numbered Accounts ambapo akaunt husika hupewa extra ordinary secrecy to the point that can only be accessed by ONLY Senior Bank Officials and not ANY Bank Official! Hii TIGHT CONFIDENTIALITY kwa muda mrefu imekuwa ikitumika kama cempetiting edge ya Swiss Banks.
Suala la ugumu wa kupata taarifa za wateja wenye akaunti za Uswis limekuwa ni burning issue duniani kote na nchi nyingi zimekuwa zikigonga mwamba. Hivi karibuni, Mamlaka za Ujerumani ilibidi hadi watumie njia za kununua(bribing) banking infos za Wajeruman wenye akaunti zao Uswis baada ya Wajeruman hao kuhisiwa ukwepaji kodi!! Sio kwamba Mamlaka za Ujeruman hazikutaka kupitia legal channels; walitaka sana na in fact walifanya lakini wakagonga mwamba na kuamua kutumia short cut. Na kwavile Uswis wanafahamu wazi kwamba sheria zao zinapingwa na mataifa mbalimbali; basi wanaamua kuji-insulate kwa kutoegemea kokote kule(may be ili msije mkajifanya ni marafiki zenu ili wawasaidie)! Na katika kuhakikisha hilo, ndo maana utakuta hadi leo Uswis sio member wa European Union kwani wanaogopa wasije wakabanwa na baadhi ya sheria za EU ambazo zita-affect sysytem yao. Hata huko Umoja wa Mataifa; Uswis imeanza kuwa mwanachama miaka 10 tu iliyopita.

Hata hivyo, si kwamba there's no legal channel itakayowezesha kutolewa kwa information hizo. Legal channels zipo BUT zina-involve a series of channels zinazopitia kabla ya kujiridhisha na kutoa nafasi kwa mamlaka husika kutoa search warrant!! Here, is not ONLY the issue ya General Attorney na Director of PCCB kusaini legal documents na kuzipeleka benki za Uswisi kisha benki hizo ziamue ku-release customer's information.....NEVER!! Hata kama zitaongezeka na saini za Rais, Gavana, Ministry of Fiannce .....! Swiss banks are not abide by Tanzanians regulations, but by their only regulations na ndio maana ili wakupatie hizo infos lazima pamoja na mambo mengine utaje unataka infos za nani(mteja gani!) na inabidi uthibitishe kosa husika! Huwa hawa-deal na collective cases.....kwamba tunataka infos za WATANZANIA; wana-deal na individual cases!

Na ndio maana nikasema the only easier solution na kwa kuajiri Private Investigator......njia hii imekuwa ikitumiwa na nchi mbalimbali!! Huyo Private Investigator ndie anayefahamu nani(Bank Officials) wapo for sale!!
 
shame upon mkuchika hivi nchi hii haina usalama wa taifa je wanafanya nini kama usalama wa taifa hawawezi kushughulikia hili basi hakuna haja ya kuwa na usalama wa taifa. Hivi waziri anaweza kuwapa raia kazi ya kuchunguza watu wanaohujumu uchumi wa nchi je hii inaingia akilini kweli? kama ni wajibu wa raia kuchunguza uhalifu basi hakuna haja ya kuwa na vyombo vya usalama kama polisi na usalama wa taifa ni bora vikavunjwa kuliko kuendelea kutumia pesa za walipa kodi kuendesha vyombo hivyo ambavyo havitimizi wajibu wake ipasavyo.
 
Hao wenye majina yao waliohusika kwenye scandals zingine wamewafanyaje? Hamna mpya kwa sirikali hii.

Hata wakiwapata watazirudisha kinyemela kama zile za EPA ama tutangojea change kama ile ya rada?

afadhali hata zikirudi na ziende kuchimba visima vijijini, kuliko zirudi halafu zikasaidie kuumaliza upinzani 2015 kama pes za rada zinavyopigwa danadana
 
Mkuchika anamdanganya nani? Uswisi wanayo majina hivyo hawahitaji hayo "majina" ya Mkuchika. Kwanini wasiseme ukweli kuwa hawana mpango wa kujifichua kwa vile ni wale wale? Ukiona hivyo jua zengwe lilishapikwa.

Yaani ajabu eti pesa ziwekwe uswisi halafu wao waseme hawana majina duh. wako nyuma kiasi hicho kiteknolojia?
 
Yaani jana kwenye taarifa ya habari ya ITV nilimcikia Boc wa Takukuru Hosea akisema tena with sneer in his voice kwamba.. ninanukuu.. "wanaosema viongozi wameficha hela huko Swiss ci wana uchungu.. waje wawataje hao viongozi".. Wanatufanya sie ni mapuruzai wa kutupwa..! Damn..
 
Kama uswis wametaka majina ya matapeli wetu ujue nao wanashirikiana na vibaka nyangumi hao. Kwa kuwa kwa taifa letu ni dhambi kuwa na akaunti nje bila taarifa na kibali,ni kwa nini uswis isiwataje matapeli wote au raia wote wenye akaunti uko na sisi ndo tuchambua nani katutapeli nani anamiliki kihalali? Watz tusiangalie nje tu,hata kwenye benki za apa apa,wakuu wetu wana akaunti za hatari.
 
Zitto kama hujipendi toa majina, wengine wanatoka bagamoyo, wengine Sumbawanga kule ambako mwewe alimbeba ngombe mzimamzima, we dogo nguvu yako ndogo, usipime maji ya mto kwa mguu yatakughalikisha!
 
Kama uswis wametaka majina ya matapeli wetu ujue nao wanashirikiana na vibaka nyangumi hao. Kwa kuwa kwa taifa letu ni dhambi kuwa na akaunti nje bila taarifa na kibali,ni kwa nini uswis isiwataje matapeli wote au raia wote wenye akaunti uko na sisi ndo tuchambua nani katutapeli nani anamiliki kihalali? Watz tusiangalie nje tu,hata kwenye benki za apa apa,wakuu wetu wana akaunti za hatari.[/QUOTE

Nahisi mchezo mchafu zaidi unataka kuchezwa hapa
 
Back
Top Bottom