Sakata la hereni za ng'ombe bungeni, Msukuma amtaja mbunge wa Kibaha kufaidika na mradi huo

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Wakati wa kuwasilishwa na kujadiliwa kwa hoja ya Bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, moja kati ya mambo yaliyochangiwa na wabunge wengi hasa wanaotoka maeneo ya wafugaji ni suala la HERENI ZA KIELEKTRONIKI KWA MIFUGO HASA NG'OMBE
Katika hotuba iliyowasilishwa ilielezwa kuwa hadi kufikia Oktoba 30, 2022, jumla ya mifugo 5,292,738 ambao ni ng'ombe 4,460,354, punda 66,863, mbuzi 513,729 na kondoo 251,792 wametambuliwa na kusajiliwa kwenye mfumo wa utambuzi. Ingawa pia ilielezwa kuwa , tarehe 3 Novemba, 2022 Serikali ilisitisha zoezi la Utambuzi wa mifugo kwa muda ili kurekebisha kasoro

Baada ya mjadala mrefu mimi, nimevutiwa na sehemu ya mchango wa Mbunge wa Geita, Joseph Kasheku Musukuma ambaye mara kadhaa wakati akichangia amemtaja Mbunge wa Kibaha (Akimtaja kwa jimbo lake bila jina) kuwa "ana-lobby" wabunge wengine wakubali suala la ng'ombe kuwekewa hereni kwani yeye ni "mnufaika" wa zoezi hilo.

Mara kadhaa "Msukuma" amemtaka Mbunge huyo wa Kibaha aacahane na suala la "Ku-lobby" wabunge ili wakubali suala la kuwekea ng'ombe hereni akisisitiza kuwa Jimboni kwake Kibaha kuna Kuku wengi sana kama anaona suala hilo ni la muhimu basi ni vyema akawekee hereni kuku katika jimbo lake.

Hoja yangu ni kama kweli Mbunge wa Kibaha anawahadaa wabunge waunge mkono huduma ambayo inamnufaisha yeye binafsi (KUWEKEA HERENI KWENYE MIFUGO) je hili sio suala linaloleta MGONGANO WA KIMASLAHI, NA LINALOPASWA KUTOLEWA MAJIBU NA WAHUSIKA.

Video iko hapa unaweza kutazama:



 
Mfano mmoja tu huu; tena mfano halisi kabisa unaoonyesha udhaifu mkubwa sana wa nchi hii.

Kwamba hata jambo dogo tu kulitekeleza kwa ufanisi haiwezekani.

Sasa kwa mwendo kama huu unategemea tutapata maendeleo kwa vipi?

Kipande cha reli (SGR) toka Dar hadi Morogoro, sasa imebaki kuwa ni hadithi ya kusimuliwa tu, haijulikani ni lini kazi hiyo itakamilika!

Mifano ya namna hii ni mingi sana
 
Usanii kila sehemu
Kila mmoja anaongea lake
Kuna mambo mengi yamewashinda ila wao wanakomaa na Hereni
Sasa si wavae wao tuwatambue pia

Marehemu alikuwa anatoa idadi mpaka ya samaki waliomo baharini kitu ambacho hata waliotutangulia hiyo technology hawana
Ila mzee wetu alitaja na idadi kabisa

Nchi ina wajinga hii
 
Kipande cha reli (SGR) toka Dar hadi Morogoro, sasa imebaki kuwa ni hadithi ya kusimuliwa tu, haijulikani ni lini kazi hiyo itakamilika!
Nasikia hakuna kazi zinaendelea huko(sijadhibitisha). Yawezekana, lengo ni kutimiza matakwa ya wapinzani wa maendeleo ya watanzania ya kuonyesha miradi yote ya maendeleo iliyoanzishwa kwa uzalendo.mkubwa ni "ndovu weupe"/white elephant.

Kwa namna moja ni kama watanzania tumezungukwa na kuweka mtu kati kibaya sisi wengi tumezungukwa na wachache. Mungu tunusuru na dhahama hii.
 
Nasikia hakuna kazi zinaendelea huko(sijadhibitisha). Yawezekana, lengo ni kutimiza matakwa ya wapinzani wa maendeleo ya watanzania ya kuonyesha miradi yote ya maendeleo iliyoanzishwa kwa uzalendo.mkubwa ni "ndovu weupe"/white elephant.

Kwa namna moja ni kama watanzania tumezungukwa na kuweka mtu kati kibaya sisi wengi tumezungukwa na wachache. Mungu tunusuru na dhahama hii.
Kama ni hivyo, hawa viongozi wanaoruhusu hujuma hii hawaoni kwamba matokeo yake ni kujivunjia heshima kwa wananchi wao wenyewe?
Mbona wangeheshimika zaidi kwa kuhakikisha kwamba miradi hii inakamilika mapema, na kama ni huko kutafuta ulaji, basi ufanyike nje ya miradi yenyewe?
Kamilisha miradi kama ilivyopangwa, halafu wafurahishe hao waliokuweka mifukoni mwao baadae!
 
Yaani nchi imejaa wapiga deal balaa

CCM ndo inafaidika na viongozi mafisadi
Hawa ni wabunge wa CCM, ni hawa hawa waliingiza kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama chao, nii hawa hawa walipitisha sheria hii ya Treceability: sasa kwanini wanapinga?
 
Madudu ya kwenye hiyo project ya hereni/tag za ng'ombe yanatia kinyaa. Kuna uroho wa pesa kupitiliza kutoka kwa viongozi wetu. Ninaifahamu vyema hii project, itoshe kusema kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake
 
Hawa ni wabunge wa CCM, ni hawa hawa waliingiza kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama chao, nii hawa hawa walipitisha sheria hii ya Treceability: sasa kwanini wanapinga?
Mkuu
Kwa hali ya sasa, ukiona muswada unapelekwa Bungeni na una hela ndani basi fahamu ni wizi unafanyika kwa mujibu wa sheria
 
Wakati wa kuwasilishwa na kujadiliwa kwa hoja ya Bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, moja kati ya mambo yaliyochangiwa na wabunge wengi hasa wanaotoka maeneo ya wafugaji ni suala la HERENI ZA KIELEKTRONIKI KWA MIFUGO HASA NG'OMBE
Katika hotuba iliyowasilishwa ilielezwa kuwa hadi kufikia Oktoba 30, 2022, jumla ya mifugo 5,292,738 ambao ni ng'ombe 4,460,354, punda 66,863, mbuzi 513,729 na kondoo 251,792 wametambuliwa na kusajiliwa kwenye mfumo wa utambuzi. Ingawa pia ilielezwa kuwa , tarehe 3 Novemba, 2022 Serikali ilisitisha zoezi la Utambuzi wa mifugo kwa muda ili kurekebisha kasoro

Baada ya mjadala mrefu mimi, nimevutiwa na sehemu ya mchango wa Mbunge wa Geita, Joseph Kasheku Musukuma ambaye mara kadhaa wakati akichangia amemtaja Mbunge wa Kibaha (Akimtaja kwa jimbo lake bila jina) kuwa "ana-lobby" wabunge wengine wakubali suala la ng'ombe kuwekewa hereni kwani yeye ni "mnufaika" wa zoezi hilo.

Mara kadhaa "Msukuma" amemtaka Mbunge huyo wa Kibaha aacahane na suala la "Ku-lobby" wabunge ili wakubali suala la kuwekea ng'ombe hereni akisisitiza kuwa Jimboni kwake Kibaha kuna Kuku wengi sana kama anaona suala hilo ni la muhimu basi ni vyema akawekee hereni kuku katika jimbo lake.

Hoja yangu ni kama kweli Mbunge wa Kibaha anawahadaa wabunge waunge mkono huduma ambayo inamnufaisha yeye binafsi (KUWEKEA HERENI KWENYE MIFUGO) je hili sio suala linaloleta MGONGANO WA KIMASLAHI, NA LINALOPASWA KUTOLEWA MAJIBU NA WAHUSIKA.

Video iko hapa unaweza kutazama:





Mbunge wa kibaha mh. Silvesrty Koka ana group of companies inaitwa S.F ambayo ndani yake kuna kampun yake ya IT inaitwa Equipoint itakuwa ndo inaitaka hiyo tenda. Naamin hapo Kasheku naye atakuwa ni chawa wa kampuni fulan Koka akimfuata akimlambisha asali kesho utamkuta akiisifia Equipoint kuwa wana uwezo ni kampuni ya kitanzania so wapewe tenda hiyo.
 
Mkuu
Kwa hali ya sasa, ukiona muswada unapelekwa Bungeni na una hela ndani basi fahamu ni wizi unafanyika kwa mujibu wa sheria
Mimi nimejaribu kufanya homework kidogo kupata chimbuko la Sheria. Moja kubwa ni kuwa ni international requirement kutokana na agreements tulizo ratify, sijaona sababu ya watu kuipinga kwa kejeri - wabunge wana nguvu ya kufanya jambo liende linavyotakiwa. Ukiacha Sheria kumbuka kiuwa jambo hilo liliweka katika Ilani ya uchaguzi wa chama chao wenyewe
 
Back
Top Bottom