Sababu kuu 4 zilizowafanya CCM waendelee kukamata dola awamu ya 5

makoye2009

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
2,638
1,218
Wana JF na Watanzania wote,

Nimetafakari kwa kina sana na kugundua kuwa CCM walianza mapema sana kuweka mbinu za kimkakati za kuchukua Dola kwa awamu hii ya 5. Kuna sababu kadha wa kadha lakini zilizo muhimu sana ziko kama 4 na nitaziainisha hapa chini. Kuna watu watajaribu kupinga kwa interest zao lakini ubaki utabaki kama ulivyo na historia itakuja kuhukumu siku moja. Nitazitaja hapa chini na kutolea maelezo mafupi.

1. SHERIA YA CYBER CRIME ILIYOWASILISHWA KWA HATI YA DHARURA BUNGE LA MWISHO NA KUPITISHWA.

2. SHERIA YA TAKWIMU ILIYOWASILISHWA SAMBAMBA NA HIYO YA KWANZA.
3. MATUMIZI MABAYA YA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWATIA HOFU NA KUWATISHA WAPIGA KURA.

4. MATUMIZI MABAYA YA TAKUKURU(PCCB) KWA KUFUMBIA MACHO RUSHWA KWA WAGOMBEA WA CCM.

1. Sheria ya Cyber Crime. Kwa Mtanzania yeyote mwenye akili timamu kwa sasa anajua kwanini sheria hii
iliwasilishwa kwenye Bunge la mwisho kwa Hati ya dharura kana kwamba nchi ilikuwa inaelekea kwenye
kiyama kwamba sheria hiyo ilikuwa lazima itungwe, ipitishwe, isainiwe na Rais na ianze kutumika mara
moja.Sheria hii ilitungwa maksudi ili kuisaidia CCM kwa kudhibiti wale wote ambao wangeweza kutoa
taarifa tafauti na matokeo ya Tume yaliyokuwa yamekusudiwa(Uchakachuaji)! Tumeshuhudia matokeo ya
kwenye vituo vya kupigia kura yakipokelewa na Tume tofauti na matokeo halisi ya vituoni na hapohapo
Tume ikishirikiana na Serikali kuwadhibiti wengine wote wasifanye TALLYING(Majumuisho) ili kuficha siri hiyo.Pamoja na Wabunge wa upinzani kuipinga na baadhi ya wale wa CCM ilipitishwa.

2. Sheria ua Takwimu: Sheria hii ya Takwimu kama ilivo ile ya kwanza hapo juu ilitungwa kwa mtindo uleule kwa

masksudi maalumu ili kulinda maslahi ya CCM na Serikali iliyoko Madarakani. Sheria hii ilipitishwa kwa
lazima ili kuhakikisha kwamba Takwimu za Tume kwa maana ya idadi ya wapiga kura na matokeo
vinadhibitiwa na sheria hii. Kwamba mtu mwingine yeyote asije na matokeo tofauti na yale ya Tume
hata kama ni ya uongo! Hili wamefanikiwa kwa vile tumeona idadi ya Kura zilizopigwa vituoni haindeni
na kile Tume ilikuwa ikiwsilisha kwenye Majumuisho yake. Yote hii ilikuwa ni kuhakikisha Wapinzani
hawaji na takwimu zile za ukweli toka Vituoni ili kuficha kushindwa kwa CCM.

3. Matumizi mabaya ya vyombo vya Ulinzi na Usalama:
Tangu mwanzo kabisa wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2015 tulianza kuona mazoezi ya Ndege za Kivita,
Wanajeshi, Polisi na Watu wa Usalama wakifanya mazoezi makali kana kwamba nchi ilikuwa inaenda
kuingia vitani. Kuna jamaa yangu mmoja aliniambia kabla ya Uchaguzi kuwa Jeshi la Wananchi(JWTZ)
lilikuwa limewekwa katika hali ya tahadhari kana kwamba chochote kingeliweza kutokea kabla au baada ya Uchaguzi. Alisema kwamba wakubwa wa Jeshi walikuwa wanajua zaidi nini kilikuwa kikiendelea! Hali hiyo ilipelekea baadhi ya watu kutoenda kupiga kura na kuna waliokimbilia nchi za jirani mpaka Uchaguzi uishe salama.

4. Matumizi mabaya ya TAKUKURU (PCCB):
TAKUKURU kikiwa ni chombo chenye kupambana na Kuzuia Rushwa kilionywa kisiingilie kabisa mtandao wa Wapiga Kura wa CCM tangu kura za Maoni mpaka Upigaji kura ili kuwapa nafasi Waheshimiwa wenye nchi wafanye vitu vyao pasipo bughudha. Ndicho kilichotokea, hakuna asiyejua kuwa Watia nia wa Urahisi na Wagombeaji wote wa Ubunge waliachwa watembeze rushwa pasipo kuguswa ili washinde kiulaini. Mpaka sasa hakuna kesi yoyote ya Kigogo wa CCM kwa kosa la kutoa rushwa au kupokea
rushwa pamoja na matukio kama hayo kuwepo!!!

Hiyo ndiyo itakayokuwa Serikali ya Magufuli awamu ya 5 ambayo imeinga kwa mizengwe, wizi wa kura na kamatakamata ya Watanzania hasa wale wote waliokuwa wanaonyesha dalili za kutaka mabadiliko kupitia UKAWA/CHADEMA na LOWASSA.

Mungu ibariki Tanzania nchi yangu. Nina hakika kuna siku utaondokana na minyororo hii ya Watawala na Makaburu weusi wa CCM. Amina.
 
Uloi nga mâché68;14507923 said:
5.ukawa kuitupa ajenda ya ufisadi

Uloi nga;

Kwa taarifa yako hiyo siyo sababu iliyowafanya CCM kushinda dola hata kidogo.
Hilo la Ufisadi ni sehemu ya sera za CCM na litaendelea kuwatafuna Watanzania mpaka siku mtakapotia akili ya kuiweka CCM pembeni. Kwa taarifa yako tu ni kwamba Rais wako Magufuli anaenda kuanza na kashfa ya Ufisadi kuhusu Feri Fake alilonunua linalofanya kazi ya kusuasua kati ya DAR na Bagamoyo. Wewe subiria tu wataaalamu wa kuibua hoja na kashfa nzito toka UKAWA mara ya Bungeni kuanza.
 
Namba 1 weka mfano Wa matokeo ambayo yamebabdikwa vituoni tofauti na iliyotangaza tume. Inyo usiweke matokeo waliyochakachua ma IT wenu yale ya Tunduma, bumbuli, ndanda pamoja na haya ya ushindi wa jumla sheria itachukua mkondo wake
 
Niliwahi kusema humu January Makamba kuwa naibu waziri mawasiliano haikuwa bahati ni mkakati uliopangwa toka kitambo kufanikisha insu ya uchaguzi na dili la kampuni ya halotel.
Adui/rafiki namba 1 wa hi nchi ukimtoa Mkapa na kikwete ni January makamba.
Kila kizuri au kibaya ambacho kimetokea kwenye utawala wa awamu ya 4 kipo chini ya hawa watu 3 (three legged cup hawa ndio waamuzi wa kila kitu)
 
All in all NEC kua partisan,haiwezekani m/kiti na viongozi wengine wa nec wachaguliwe na rais half chama chake kishindwe!NEVER NEVER NEVER
 
Tanzania ilikwama ilipokubali vyama vingi bila kubadili sheria ili ziendane na mfumo wa vyama vingi. Haiwezekani kuwe na vyama vingi alafu mwenyekiti wa chama kimojawapo achague watendaji wa tume ya uchaguzi, wakuu wa mikoa na wilaya zisingekuwa nafasi za kisiasa.
 
Uloi nga;

Kwa taarifa yako hiyo siyo sababu iliyowafanya CCM kushinda dola hata kidogo.
Hilo la Ufisadi ni sehemu ya sera za CCM na litaendelea kuwatafuna Watanzania mpaka siku mtakapotia akili ya kuiweka CCM pembeni. Kwa taarifa yako tu ni kwamba Rais wako Magufuli anaenda kuanza na kashfa ya Ufisadi kuhusu Feri Fake alilonunua linalofanya kazi ya kusuasua kati ya DAR na Bagamoyo. Wewe subiria tu wataaalamu wa kuibua hoja na kashfa nzito toka UKAWA mara ya Bungeni kuanza.

Mtaalamu Kafulila Mbunge wa kuteuliwa!
 
Uloi nga mâché68;14507923 said:
5.ukawa kuitupa ajenda ya ufisadi

Kama agenda ya UFISADI ina nguvu ya kukitoa chama madarakani si CCM ilipaswa kuwekwa pembeni 1995 nchi ilivyokuwa inanuka ufisadi hata Mwl Nyerere akaingilia kati? Au 2010 wakati EPA na yale madudu mengine yaliposhika kasi? Lakini pamoja na madudu hayo CCM si ilishinda 2010?Na pamoja na uchafu wote iliyonayo CCM leo hii si CCM imeshinda tenda?Pamoja na kutuhumiwa na ufisadi wa ESCROW leo hii Prof. Tibaijuka si amepata kura nyingi huko Muleba kusini? Kama ambavyo agenda ya UFISADI isivyoweza kuitoa CCM madarakani ndivyo ambavyo haiwezi kuiingiza UKAWA madarakani. Kuna mambo mengine yanayoshindisha CCM na kuikosesha UKAWA. Tafakari.

Kama wewe si zuzu au bazazi nadhani umeelewa
 
Tanzania ilikwama ilipokubali vyama vingi bila kubadili sheria ili ziendane na mfumo wa vyama vingi. Haiwezekani kuwe na vyama vingi alafu mwenyekiti wa chama kimojawapo achague watendaji wa tume ya uchaguzi, wakuu wa mikoa na wilaya zisingekuwa nafasi za kisiasa.

Wewe uliyempiga Warioba umesababisha matatizo haya!
 
Hizo sababu hazikuisaidia ccm Bali ilikuwa ni hofu yao tu, ninavyojua 80% ya watanzania wanaishi vijijini na ni 40% yenye nishati ya umeme, waliobaki 60% hawajui nini kinaendelea dunian. Leo hii au dakika hii ukiwauliza matokeo ya Zanzibar yamekuwaje au lowasa amesema nini juu ya uchaguzi huu hakuna anayeweza kukupa jibu.
 
Khaa!! Sababu kuu ni moja tu. Kuikana ajenda ya ufisadi ambayo kwa miaka Zaidi ya 10 ilikuwa ndiyo silaha iliyoiangamiza na kuidhoofisha CCM. Wanalaaniwe wote waliyouuwa upinzani wa dhati kwa maslahi yao binafsi :angry:
 
5. Kumkaribisha bubu (lowassa) CHADEMA na kumpa nafasi ya kugombea urais baada ya siku moja tu ya kujiunga na CHADEMA.
6. Kumkaribisha na kumpokea Mr. Zero (Sumaye) na kumfanya kuwa mzungumzaji mkuu wa CHADEMA katika mikutano yake.
7. Kumuacha kamanda Dr Slaa, mpiganaji wa kweli kuondoka katika chama na kumruhusu nabii feki (Gwajima) kumdhalilisha kamanda huyu na shujaa wa ukweli. Hii iliwatia Chadema asilia hasira kali sana.
8. Kuwaweka M4C pembeni na kuwakabidhi 4U Movement majukumu ya M4C.
 
Back
Top Bottom