Rufaa ya Sioi yatinga NEC

@Bobuk, tusichanganye mambo, sheria ya Tanzania haitoi UBAGUZI. Hakuna mahali sheria inasema kuwa anayetakiwa kuapa ni yule ambaye amezaliwa kwenye nchi ambayo haikumpa uraia. hakuna. Ili mradi umezaliwa nje ya territorial za Republic unatakiwa ama uape au utoe evidence(uthibitisho) kuwa hauna uraia wa nchi nyingine yoyote. Mbele ya sheria za Tanzania aliyezaliwa Kenya na aliyezaliwa USA wote wanakuwa kwenye kundi moja. Foreign citizen until proven otherwise.

Kwa ruhusa ya mdau Jagermaster naomba niweke ufafanuzi wake ili uone exactly tatizo liko wapi.

"Tanzania tuna uraia wa aina tatu,
(1) Uraia wa Kuzaliwa (citizenship by birth)-Huu napatikana kwa mtu yoyote aliyezaliwa Tanzania with a condition that, mzazi mmoja wapo au (wote) awe either raia wa kuzaliwa au raia wa kwandikishwa.

(2) Raia wa kuandikishwa (citizeship by naturalisation)- Huu hupatikana kwa kuomba, ikiwa raia yoyote wa kigeni anayeishi Tanzania kwa muda usiopungua miaka kumi, au pungufu ya hapo kama waziri ataona inafaa, ambaye anania kubaki Tanzania kwa muda wote wa maisha yake. Huu ndio mara nyingi tunauona kwenye magazeti watu wakiomba

(3) Uraia wa kurithi (citizenship by descent)- Huu ni uraia mtu yoyote aliyezaliwa nje ya Tanzania huku wazazi wake wakiwa Watanzania raia wa kuzaliwa au wa kuandikishwa. Watu wanaozaliwa ikiwa wazazi wao wanafanya kazi kwenye balozi hao watu wanahesabika wamezaliwa Tanzania. Pia ileweke kuwa mtu ukizaliwa kwenye chombo cha usafiri (ndege, meli.e.t.c) unahesabika umezaliwa kwenye nchi ambayo hicho chombo kimeandikishwa

Ileweke kuwa sheria ya uraia ya Tanzania, haitambuwi uraia wa nchi mbili au tatu, with exception kwa mtu mwenye uraia wa kurithi. Raia wa kurithi anaruhusiwa kuwa na uraia wa nchi mbili mpaka pale atakapofikisha umri wa miaka kumi na nane (18) anatakiwa kukana uraia wa nchi nyingine na kubaki na uraia wa Tanzania pekee. Hiki kitendo watu wengi hawakifanyi na price yake wanaipata pale wanapotaka uongozi wa kisiasa

Pia hakuna mahara popote pale ambapo sheria ya uraia ya Tanzania inatoa exception katika kukana uraia kwa mtu mwenye uraia wa kurithi, kwamba either kama huyo mtu kazaliwa kwenye nchi ambayo inatoa automatic citizeship kama US au conditional citizeship kama Kenya kwamba aukane uraia wake wa awali au hapana. Sheria ya Tanzania inawataka watu wote wenye uraia wa kurithi kuukana uraia wa nchi walizozaliwa pale wanapofikisha umri wa miaka kumi na nane, without exception kama Mh Mchemba unavyotaka tuamini. Naona hapo Mh umetumia common sence na sio sheria unavyosema, ni vizuri kama ukaweka ushahidi wa hayo mnayoyaamini. Pia sheria inatoa mwanya wa mtu kupewa uraia hata kama hajakana uraia wa nchi nyingine, ikiwa atathibitisha tu kuwa ni vigumu au haiwezekani kukana uraia wa nchi nyingine ambayo inamtambuwa au haimtambui kuwa ni raia wake

What about SIYOI?
Kwa kesi ya Siyoi ilivyo, yeye anafall katika category ya tatu yaani raia wa Kurithi kwa kuwa alizaliwa Kenya na wazazi watanzania. Wazazi wake walikuwa hawafanyi kazi za ubalozi huko Kenya wakati jamaa anazaliwa.
Pasipo kujali kuwa either Kenya walikuwa wanamtabua kuwa raia wao au hapana, Tanzania ilikuwa inamtambua Siyoi kama raia wa Kurithi yaani alikuwa na uraia wa Kenya na Tanzania na alivyofikisha umri wa miaka 18 kama alishindwa kuukana uraia wa Kenya alipoteza sifa za kuwa raia wa Tanzania. Kwa mazingira yake kama inaonekana ilikuwa ni vigumu kwa yeye kukana uraia wa Kenya kwa kuwa Kenya walikuwa 'hawamtambui' kama raia, alipaswa kupeleka maelezo hayo idara ya Uhamiaji ili wamwelewe kuwa kwa kesi yake hawezi kukana uraia na wa mpe uraia wa Tanzania

Kwa jinsi nilivyosoma sheria ya uraia ya Kenya, Siyoi pia hana sifa ya kuwa raia wa Kenya kwa umri alionaona. Swali sasa linakuja Siyoi ni raia wa aina gani?
Jibu ni jepesi SIYOI SUMARI hana Uraia wa nchi yoyote ile Duniani (Stateless). Watu wa aina hii wapo wengi tu duniani ambao wanaishi kwa kutokuwa na uraia wa nchi yoyote kisheria. Ila kwa Tanzania I know anything can happen

NB
Issue hii ni tofauti na Kesi ya Ulimwengu, licha ya mwamba wote Siyoi na Generali wanajikuta wanakuwa sio raia wa nchi yoyote ile Duniani, Siyoi anapaswa kuukana uraia wa Kenya, kwa kuwa yeye alishawahi kuwa raia wa kurithi mpaka alipofikisha umri wa miaka 18 ndipo uraia wake ulikoma, Ulimwengu hakuwahi kuwa raia wa Tanzania kwani hata Wazazi wake hawakuwahi kuwa raia wa Tanzania, ndio maana yeye aliambiwa aombe uraia wala hakuambiwa aukane tu uraia wa Rwanda.

Kwa maoni yangu sheria ya Uhamiaji ya Tanzania inamapungufu mengi. Ikifika stage kama hizi ndio mapungufu yake yanaonekana. Kwa mfano mpaka sasa raia yoyote wa kurithi, mwenye mke au mume ambaye sio raia wa Tanzania au ni raia wa kurithi, akizaa mtoto nje ya nchi huyo mtoto anakuwa sio raia wa Tanzania, wala uraia wa kurithi haupati. Itampasa huyo mtoto amuombee uraia wa kwandikishwa kama anataka awe Mtanzania.

Wito kwa Watanzania wote wenye uraia wa kurithi nendeni mkakane uraia wa nchi mlizozaliwa, maana kwamtindo huu mkekalia kuti kavu bila kujiju" (MWISHO WA KUNUKUU).

Mkuu FJM, shukrani kwa maelezo ya kina ambayo yametuelimisha wengi juu ya mambo ya uraia na sheria zake.

Hii ndo raha na faida ya JF, ni kisima cha elimu.
 
Kama hujui sheria kuhusiana na uraia wa Tanzania inasemaje si unakaa kimya ndugu ya nini kujiaibisha na maneno mengiutafikiri unaelewa kumbe hamna kitu.kama kitu hujui unauliza si lazima uchangie hapa au unaongeza idadi ya post zako JF?

Sasa wewe "UNAYEJUA" mbona huelezi hicho unachokijua insteady unatoa SWEEPING & INCOHERENT statement like a intoxicated madman!
 
Chadema kimekata rufaa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kikitaka kuenguliwa katika uchaguzi huo, mgombea wa CCM, Siyoi Sumari kwa maelezo kwamba si raia wa Tanzania.

Hatua ya Chadema imekuja saa chache baada ya Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Trasias Kagenzi kutupa mapingamizi yote ya wagombea katika uchaguzi huo mdogo.

Kwa mujibu wa nyaraka za Chadema, ambazo zina nukuu, barua ya siri ya OfisaUhamiaji Mkoa wa Arusha, D. Namomba kwenda kwa Mkuu wa Mkoa, aliyetaka kujua uraia wa Siyoi, mgombea huyo wa CCM anadaiwa kuzaliwa Thika, Kenya na kunautata kama aliwahi kuukana uraia wake wa awali.

Meneja wa Kampeni wa Chadema, Vicent Nyerere alisema wana ushahidi kuwa uraiawa Siyoi una tata hivyo, hawakubaliani na uamuzi wa Kagenzi... “Tunakata rufani NEC kwani tuna ushahidi kuwa uraia wa mgombea wa CCM una utata.”

Source: Mwananchi

watampaisha bila wao kujijua. tusubiri tuone. wengi tunakumbuka jinsi WENJE wa Mwanza alivyowekea pingamizi la namna hiyo na MASHA matokeo yake ndo walivyosaidia kumtangaza kwa wananchi na mwisho akashinda
 
Ngongo naomba nikujibu pamoja na Politiki.

... Ndiyo Uraia wa Sioyi utaamuliwa kwa kufuata SHERIA za Tanzania. Lakini pia utaangalia sheria za URAIA wa Kenya alikozaliwa HASA Kabla ya Katiba mpya.
Mkuu acha kupotosha, uraia wa Tanzania unaamuliwa kwa sheria za Tanzania, si za Kenya wala nchi nyingine yoyote. Vinginevyo tungekuwa na raia wa Tanzania ambao katiba ya Tanzania haiwatambui lakini katiba za nchi ya nje inawatambua, jambo ambalo lingekuwa ni vurugu. Ukitaka kuamini kwamba uraia wa Tanzania unaamuliwa kwa sheria za Tanzania wala si za nchi nyingine, ujiulize kwa nini Uhamiaji wakifukuza mtu nchini huwa hawamwambii nchi ya kwenda, ila wanachojali aondoke Tanzania!!
 
vita unatakiwa utumie kila mbinu na silaha uliyo nayo pia uchaguzi lazima ucheze na propaganda, siasa na mambo ya kisheria yote hayo ni malengo ya kupata ushindi, unapoanza kuchokonoa uraia possible yakaibuka mwngine ambayo yanakuwa karata muhimu kwenye kampeni na hatimaye kupatikana ushindi!!

kuongezea hapo timu zinanapocheza mpira wanategemea defender wa timu pinzani atakosea na wao kufunga kirahisi,kwenye siasa kuna kamati ya ufundi kazi yake ni kutafuta makosa na chance kama hizo
 
@Bobuk, tusichanganye mambo, sheria ya Tanzania haitoi UBAGUZI. Hakuna mahali sheria inasema kuwa anayetakiwa kuapa ni yule ambaye amezaliwa kwenye nchi ambayo haikumpa uraia. hakuna. Ili mradi umezaliwa nje ya territorial za Republic unatakiwa ama uape au utoe evidence(uthibitisho) kuwa hauna uraia wa nchi nyingine yoyote. Mbele ya sheria za Tanzania aliyezaliwa Kenya na aliyezaliwa USA wote wanakuwa kwenye kundi moja. Foreign citizen until proven otherwise.

Kwa ruhusa ya mdau Jagermaster naomba niweke ufafanuzi wake ili uone exactly tatizo liko wapi.

"Tanzania tuna uraia wa aina tatu,
(1) Uraia wa Kuzaliwa (citizenship by birth)-Huu napatikana kwa mtu yoyote aliyezaliwa Tanzania with a condition that, mzazi mmoja wapo au (wote) awe either raia wa kuzaliwa au raia wa kwandikishwa.

(2) Raia wa kuandikishwa (citizeship by naturalisation)- Huu hupatikana kwa kuomba, ikiwa raia yoyote wa kigeni anayeishi Tanzania kwa muda usiopungua miaka kumi, au pungufu ya hapo kama waziri ataona inafaa, ambaye anania kubaki Tanzania kwa muda wote wa maisha yake. Huu ndio mara nyingi tunauona kwenye magazeti watu wakiomba

(3) Uraia wa kurithi (citizenship by descent)- Huu ni uraia mtu yoyote aliyezaliwa nje ya Tanzania huku wazazi wake wakiwa Watanzania raia wa kuzaliwa au wa kuandikishwa. Watu wanaozaliwa ikiwa wazazi wao wanafanya kazi kwenye balozi hao watu wanahesabika wamezaliwa Tanzania. Pia ileweke kuwa mtu ukizaliwa kwenye chombo cha usafiri (ndege, meli.e.t.c) unahesabika umezaliwa kwenye nchi ambayo hicho chombo kimeandikishwa

Ileweke kuwa sheria ya uraia ya Tanzania, haitambuwi uraia wa nchi mbili au tatu, with exception kwa mtu mwenye uraia wa kurithi. Raia wa kurithi anaruhusiwa kuwa na uraia wa nchi mbili mpaka pale atakapofikisha umri wa miaka kumi na nane (18) anatakiwa kukana uraia wa nchi nyingine na kubaki na uraia wa Tanzania pekee. Hiki kitendo watu wengi hawakifanyi na price yake wanaipata pale wanapotaka uongozi wa kisiasa

Pia hakuna mahara popote pale ambapo sheria ya uraia ya Tanzania inatoa exception katika kukana uraia kwa mtu mwenye uraia wa kurithi, kwamba either kama huyo mtu kazaliwa kwenye nchi ambayo inatoa automatic citizeship kama US au conditional citizeship kama Kenya kwamba aukane uraia wake wa awali au hapana. Sheria ya Tanzania inawataka watu wote wenye uraia wa kurithi kuukana uraia wa nchi walizozaliwa pale wanapofikisha umri wa miaka kumi na nane, without exception kama Mh Mchemba unavyotaka tuamini. Naona hapo Mh umetumia common sence na sio sheria unavyosema, ni vizuri kama ukaweka ushahidi wa hayo mnayoyaamini. Pia sheria inatoa mwanya wa mtu kupewa uraia hata kama hajakana uraia wa nchi nyingine, ikiwa atathibitisha tu kuwa ni vigumu au haiwezekani kukana uraia wa nchi nyingine ambayo inamtambuwa au haimtambui kuwa ni raia wake

What about SIYOI?
Kwa kesi ya Siyoi ilivyo, yeye anafall katika category ya tatu yaani raia wa Kurithi kwa kuwa alizaliwa Kenya na wazazi watanzania. Wazazi wake walikuwa hawafanyi kazi za ubalozi huko Kenya wakati jamaa anazaliwa.
Pasipo kujali kuwa either Kenya walikuwa wanamtabua kuwa raia wao au hapana, Tanzania ilikuwa inamtambua Siyoi kama raia wa Kurithi yaani alikuwa na uraia wa Kenya na Tanzania na alivyofikisha umri wa miaka 18 kama alishindwa kuukana uraia wa Kenya alipoteza sifa za kuwa raia wa Tanzania. Kwa mazingira yake kama inaonekana ilikuwa ni vigumu kwa yeye kukana uraia wa Kenya kwa kuwa Kenya walikuwa 'hawamtambui' kama raia, alipaswa kupeleka maelezo hayo idara ya Uhamiaji ili wamwelewe kuwa kwa kesi yake hawezi kukana uraia na wa mpe uraia wa Tanzania

Kwa jinsi nilivyosoma sheria ya uraia ya Kenya, Siyoi pia hana sifa ya kuwa raia wa Kenya kwa umri alionaona. Swali sasa linakuja Siyoi ni raia wa aina gani?
Jibu ni jepesi SIYOI SUMARI hana Uraia wa nchi yoyote ile Duniani (Stateless). Watu wa aina hii wapo wengi tu duniani ambao wanaishi kwa kutokuwa na uraia wa nchi yoyote kisheria. Ila kwa Tanzania I know anything can happen

NB
Issue hii ni tofauti na Kesi ya Ulimwengu, licha ya mwamba wote Siyoi na Generali wanajikuta wanakuwa sio raia wa nchi yoyote ile Duniani, Siyoi anapaswa kuukana uraia wa Kenya, kwa kuwa yeye alishawahi kuwa raia wa kurithi mpaka alipofikisha umri wa miaka 18 ndipo uraia wake ulikoma, Ulimwengu hakuwahi kuwa raia wa Tanzania kwani hata Wazazi wake hawakuwahi kuwa raia wa Tanzania, ndio maana yeye aliambiwa aombe uraia wala hakuambiwa aukane tu uraia wa Rwanda.

Kwa maoni yangu sheria ya Uhamiaji ya Tanzania inamapungufu mengi. Ikifika stage kama hizi ndio mapungufu yake yanaonekana. Kwa mfano mpaka sasa raia yoyote wa kurithi, mwenye mke au mume ambaye sio raia wa Tanzania au ni raia wa kurithi, akizaa mtoto nje ya nchi huyo mtoto anakuwa sio raia wa Tanzania, wala uraia wa kurithi haupati. Itampasa huyo mtoto amuombee uraia wa kwandikishwa kama anataka awe Mtanzania.

Wito kwa Watanzania wote wenye uraia wa kurithi nendeni mkakane uraia wa nchi mlizozaliwa, maana kwamtindo huu mkekalia kuti kavu bila kujiju" (MWISHO WA KUNUKUU).

Mkuu FJM,

Naheshimu mchango wako maana umeenda shule. Umesoma vifungu mbalimbali na kuviandika kwa lugha nyepesi. Hiyo ndiyo JF ya zamani ambayo wengi tulikuwa tunajivunia kuwa sehemu yake. Ambapo watu walikuwa wanaingia chini kusoma na kuelewa na kisha kutufundisha sisi sote hapa.

Ninapingana na wewe kwenye tafsiri hiyo ya kwamba mtoto akizaliwa nje ya nchi na wazazi wote wawili au mmoja Mtanzania basi serikali ya TZ kwa miaka 18 ya mwanzo inamtambua kama ana uraia wa nchi mbili. Kwa mawazo yangu naona hilo sio sahihi. Ukitaka kuona sio sahihi angalia form ya kiapo ambayo iko kwenye act hiyo hiyo ya uraia ya 1995. Unapoapa lazima utaje nchi nyingine ambayo una uraia wake. Sasa kama huna na hujawahi kuwa na uraia wa nchi nyingine, utataja nini?

Sheria yoyote hapa duniani ni ngumu ku cover scenarios zote na ndio maana kunakuwa na mahakama za kutafsiri sheria. Hapa muhimu ni kurudi nyuma na kuangalia je waliotunga hii sheria walikuwa wanataka ku achieve nini? Ukisoma documents zote unagundua lengo lao lilikuwa kuzuia Mtanzania kuwa na uraia wa nchi nyingine kwa kujua au kutokujua. Na njia kubwa ya kupata uraia wa nchi nyingine waliainisha kama kupitia mzazi mmoja kuwa wa hiyo nchi nyingine au kuzaliwa kwenye hiyo nchi nyingine. Hapo ndipo suala lote hili linapotakiwa kukaa.

Ninaamini kabisa hawakuwa na lengo la kuwalenga watu kama akina Siyoi. In fact tafsiri ya sasa ya kifungu hiki ni faraja kwa Watanzania wengi sana hasa wale wanaoishi sehemu za mipakani. Mkuu, mimi nataoka wilaya ya mpakani na ninaelewa hili jambo likiangaliwa kisiasa litaleta usumbufu kwa watu wengi sana. Kule mipakani ni kawaida watu wa upande mmoja kwenda kutibiwa upande mwingine kutegemeana na ubora wa huduma za sehemu hiyo nyingine. kwa mfano kati ya Tanzania na Malawi, kuna kipindi huduma za Malawi zilikuwa bora zaidi, Watanzania wengi wa Kyela walikuwa wanaenda kutibiwa huko ikiwa na pamoja na hata kujifungua. Hivyo hivyo kuna kipindi watu wa Malawi walikuwa wanakuja TZ kutibiwa.

Ukiachia hiyo, angalia wafanyakazi wote waliokuwa wanafanyakazi kwenye jumuia ya Afrika Mashariki. Kulikuwa na maelfu ya watanzania waliopelekwa kenya au Uganda kikazi. Kuna wengine walizaa watoto wao huko na kurudi TZ watoto wao wakiwa wachanga. Kuna wengi wao wamekufa na si ajabu hata watoto hawajui walizaliwa Kenya au Uganda. wanachojua Wazazi wao wote wawili walikuwa Watanzania.

Ndio maana tokea mwanzoni na mpaka sasa binafsi naamini tafsiri iliyotolewa na mkuu wa uhamiaji ndio sahii na ndiyo ilikuwa lengo la kutungwa kwa sheria hii. Kama umezaliwa nje na wazazi wote wawili ambao ni Watanzania basi sharti pekee liwe kuangalia kama wakati unazaliwa je hiyo nchi ulikozaliwa ilikuwa inatoa uraia automatically?

haya majadiliano yatakuwa na maana kama kuna watanzania wenzetu watajifunza na kuzuia mikanganyiko kama hii.
 
Napenda sana jitihada za CDM juu ya swala hilo ila kwakuwa tunao uwezo wa kushinda kwa kura, basi nashauri tusipoteze muda na akili katika kuweka pingamizi badala yake tuweke nguvu na akili yote katika mbinu za ushindi wa kura. Lini fisadi akamtosa fisadi mwenzio? Hawa wote lao moja kama Tendwa yuko radhi kueneza chuki na husda dhidi ya kamanda Lema, leo aseme Siyoi sio raia? Haiwezekani na bado Siyoi atatakatishwa mpaka awe mgombea tu.

yote lazima yaende sambamba ili kuwadhoofisha kotekote
 
Back
Top Bottom