Rubani wa Uholanzi Afanya Kituko Ambacho Hakijawahi Kutokea

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
2385902.jpg


Thursday, July 02, 2009 8:32 AM

Rubani wa ndege ya shirika la ndege la Arkefly la Uholanzi ametoa kali ya mwaka kwa kuwashusha abiria wote kwenye ndege na kuendelea na safari ndege ikiwa tupu baada ya kukasirishwa na baadhi ya abiria ambao waligoma kufunga mikanda. Tukio hilo lilitokea ijumaa kwenye uwanja wa ndege wa Schiphol wa jijini Amsterdam, Uholanzi wakati ndege hiyo ilipokuwa ikijiandaa kupaa kutoka Uholanzi kuelekea Uturuki.

Wakati ndege ikiwa iko kwenye hatua za mwisho za kupaa huku taratibu za usalama kwenye ndege zikitolewa, abiria wapatao 10 walikataa kukaa kwenye viti vyao na pia walikataa kufunga mikanda yao.

Tukio hilo lilimkasirisha rubani wa ndege hiyo raia wa Uholanzi ambaye aliamua kuirudisha ndege hiyo kwenye terminal na kuwashusha abiria wote waliokuwemo kwenye ndege hiyo na kuanza safari ya kuelekea Uturuki ndege hiyo ikiwa tupu haina abiria hata mmoja.

Abiria walioachwa uwanja wa ndege walipandishwa ndege nyingine siku iliyofuatia na kuendelea na safari zao.

Shirika la ndege la Arkefly halijasema chochote juu ya rubani wao huyo ambaye amekuwa gumzo kutokana na hatua yake hiyo.


Source: nifahamishe.com
 
Pia rubani akisha toa order lazima ifuatwe maana anaweza fanya lolote...hapo rubani anaweza akakosa kazi au adhabu tu za kiutendaji wao wana sheria zao....maana hata hvy atajiteetea sababu za kiusalama ndg haiwezi kuruka abiria wamesimama....ila kosa kuzira kuwashusha na kuwaacha.
 
So alienda Uturuki kufanya nini? au ndio kutimiza ratiba?

maana hapa bongo ni upuuzi kulinda ratiba afu uchome mafuta bure
 
mwe, hiki ni kituko atii. ila ni sawa, nadhani angewashusha wale waliogoma kukaa na kufunga mikanda tu. kosa lake ni kuwashusha wote!!!
 
So alienda Uturuki kufanya nini? au ndio kutimiza ratiba?

maana hapa bongo ni upuuzi kulinda ratiba afu uchome mafuta bure

Ndege ilikuwa na aratiba ya kurudi na abiria kutoka uturuki. Fikiria kama KLM au BA haijaja hapo bongo kwasababu jamaa alikuwa hana abiria wa kuwaleta wangapi wataathirika hapo DSM.
 
So alienda Uturuki kufanya nini? au ndio kutimiza ratiba?

maana hapa bongo ni upuuzi kulinda ratiba afu uchome mafuta bure

Nimeelewa, alienda Uturuki kuchukua abiria wasiokuwa na hatia, hao Wa-dutch walimletea za kuleta akasema aende zake Istanbul akachukue abiria wapole.
 
Teteheeete! amejitahidi kuonyesha nini adhabu ya wasio na nidhamu!!!
 
Teteheeete! amejitahidi kuonyesha nini adhabu ya wasio na nidhamu!!!

Pia hawa jamaa wanaweza kuchukuliwa hatua kwa kuhatarisha usalama wa ndege na abiria wengine kwa kukataa kufuata taratibu za kiusalama (safety measures) Pia kulitia hasara shirika kwani ilibidi watafutiwe usafiri mwingine
 
Rubani ana haki ya kumkataa abiria ndani ya ndege anayorusha. Aidha, rubani ana haki ya kukataa kusafiri na mtu ambaye yeye anadhani ata-impair utendaji wake akiwa angani.

Katika tukio hili, kampuni husika ya ndege ilitakiwa itafute rubani mwingine na ambaye angerusha ndege minus wale walio-violate safety rules, lakini kama hakukuwa na replacement ya rubani basi ni wazi ndege ililazimika kwenda huko bila ya abiria ili waweze ku-maintain schedule kwa abiria wengine.
 
Pia hawa jamaa wanaweza kuchukuliwa hatua kwa kuhatarisha usalama wa ndege na abiria wengine kwa kukataa kufuata taratibu za kiusalama (safety measures) Pia kulitia hasara shirika kwani ilibidi watafutiwe usafiri mwingine
Issue ya insurance vipi! hasara ya ndege inaweza kulipwa na insurance policy. sijui hiyo imekaaje kisheria?
 
In my opinion the pilot lacks professionalism. If you work with people (customers) you are bound to meet misfits or people who are not going to follow the rules. The trick is to make them respect you enough to let you work with them. It can be done. It takes training, patience and hard work.
 
In my opinion the pilot lacks professionalism. If you work with people (customers) you are bound to meet misfits or people who are not going to follow the rules. The trick is to make them respect you enough to let you work with them. It can be done. It takes training, patience and hard work.

Lunanilo,
On this particular case, your opinion is baseless because you don't have any investigation report to quantify your statement that 'the pilot lacks professionalism'. As I narrated above, the pilot of any commercial flight may refuse any person on board if he or she feels that person can impair or interfear the operation of the aircraft/ship. Therefore, don't jump to the conclusion while you have little information to support your statement.
 
Hey thanks for your contribution. Please do not take this personal, when I replied to the post I did not mean to single you out. I am just appalled at the poor customer service that is sometimes given because people have no patience or skills of dealing with unruly customers that we should expect in the world of information. If there is a problem customer or passenger in this case, just throw him/ her out rather than delay all passengers.
Remember there are people in the plane who have to meet deadlines in their destinations. True that I do not have any more information other than what is given on this thread, but still, you do not refuse service to the rest of the shop because a couple of nutcases have entered your brain. As I pointed out above my response is not addressed to you in particular. It is for the pilot, seriously if every worker refused to give their services,because of unruly customers, nothing will be done. I know doctors who are driven nuts by their patients, engineers who are constantly criticized by their clients and the list goes on. the professional has to learn about how to provide good customer service to his clients, while at the same time he pacifies and educates the unruly customers.

Also quantitative analysis is probably a good tool but sometimes it fails and one has to use qualitative analysis. What was there to quantify in the thread?

I am aware of the danger of air travel and the powers that pilots are given etc. But if you wear a uniform for a company, you are basically a sales person for the company and your duty is good customer service, whether you are a doctor, pilot or cleaner.

The bottom line is the BOTTOM LINE

Have a good one.
 
Pia rubani akisha toa order lazima ifuatwe maana anaweza fanya lolote...hapo rubani anaweza akakosa kazi au adhabu tu za kiutendaji wao wana sheria zao....maana hata hvy atajiteetea sababu za kiusalama ndg haiwezi kuruka abiria wamesimama....ila kosa kuzira kuwashusha na kuwaacha.

Hilo kosa wewe umetoa wapi?

Rubani ana haki ya kumkataa abiria ndani ya ndege anayorusha. Aidha, rubani ana haki ya kukataa kusafiri na mtu ambaye yeye anadhani ata-impair utendaji wake akiwa angani.

Katika tukio hili, kampuni husika ya ndege ilitakiwa itafute rubani mwingine na ambaye angerusha ndege minus wale walio-violate safety rules, lakini kama hakukuwa na replacement ya rubani basi ni wazi ndege ililazimika kwenda huko bila ya abiria ili waweze ku-maintain schedule kwa abiria wengine.

ni maneno yako au una-source ya ku-support claims zako?
 
Back
Top Bottom