Robertinho: Nawapongeza Yanga kwa kushinda dabi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Akizungumza baada ya timu yake kufungwa magoli 5-1 katika mchezo dhidi ya Yanga, Kocha wa Simba, Roberto Oliveira “Robertinho” amesema kipindi cha pili wachezaji wake walipoteza umakini.

Amesema “Magoli mawili tuliyofungwa kipindi cha pili wachezaji wetu (Simba) walizubaa na kupoteza umakini, walifikiri kuna faulo wenzetu wakaendelea kucheza na wakafunga, nawapongeza wapinzani wetu (Yanga) kwa kushinda ‘Dabi’ na sisi tumepoteza mchezo muhimu.”

Kipigo hicho ni cha kwanza kwa Simba msimu huu katika Ligi Kuu Bara, pia ni cha kwanza kwa Robertinho dhidi ya Yanga tangu akutane na wapinzani hao katika mechi 4 ikiwemo pamoja na zile alizokuwa Vipers.
 
Akizungumza baada ya timu yake kufungwa magoli 5-1 katika mchezo dhidi ya Yanga, Kocha wa Simba, Roberto Oliveira “Robertinho” amesema kipindi cha pili wachezaji wake walipoteza umakini.

Amesema “Magoli mawili tuliyofungwa kipindi cha pili wachezaji wetu (Simba) walizubaa na kupoteza umakini, walifikiri kuna faulo wenzetu wakaendelea kucheza na wakafunga, nawapongeza wapinzani wetu (Yanga) kwa kushinda ‘Dabi’ na sisi tumepoteza mchezo muhimu.”

Kipigo hicho ni cha kwanza kwa Simba msimu huu katika Ligi Kuu Bara, pia ni cha kwanza kwa Robertinho dhidi ya Yanga tangu akutane na wapinzani hao katika mechi 4 ikiwemo pamoja na zile alizokuwa Vipers.
Ile kamati aliyoiteua rais wa heshima imeshindwa kufanya kazi? Ila Mo janja sana alishaona kitakachotokea . Kukwepa lawama akawateua wanazi wa Simba
 
Ile kamati aliyoiteua rais wa heshima imeshindwa kufanya kazi? Ila Mo janja sana alishaona kitakachotokea . Kukwepa lawama akawateua wanazi wa Simba
Nililisema hili hapa wanazi wakasema kuwa MO ni mtaalamu wa fitna za Dabi.
 
“Goli la pili Wachezaji wangu walijua ni faulo, wanashangaa tu ghafla Yanga wanaenda kufunga, nawapongeza wameshinda lakini pia majeraha ya Mchezaji wangu Kibu yameniathiri”

- Coach Robertinho baada ya Derby!

Tunapokea maelezo ya Kocha ama tukutane Terminal 3?_
 
Robetino amedhihirisha kuwa ni kocha mzuri akipewa average players kama ilivyokuwa msimu uliopita. Lakini msimu huu kapewa kila kitu kuanzia wachezaji na wasaidizi wake aliowataka yeye mwenyewe lakini hata kupanga timu anashindwa. Timu haina mfumo wa kujilinda kabisa ikishambuliwa na Simba washukuru maana vipigo kama vya leo vilikuwa vitokee vingi kabla ya mechi ya leo ila Mungu tu ndio alikuwa anasaidia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom