Ripoti ya Uchunguzi vifo vya watoto Tabora

Lakini kama kuna major structural au technical failure, inayofanya jengo lisiweze kutumika ipasavyo, kinyume cha maagizo ya mshitiri hii sifahamu lakini naamini inadumu kwa uhai wa jengo. Kwa mfano, kama kuna conference room ghorofani iliyotakiwa kuchukuwa watu mia lakini haijawahi kuchukuwa watu hao hadi miaka kumi kupita. Ikiwa baada ya miaka kumi, mshitiri akapata mkutano wa watu mia na jengo kuanguka kutokana na uzito wao, basi wataalam wote watakuwa liable (kuanzia msanifu majengo hadi mhandisi wa structures). Hasa ikiwa walikagua na kupitisha kazi ya mkandarasi kuwa ilifanyika kama walivyomuagiza.

Hivyo ndivyo ninavyoelewa. Labda nimekosea.
Umenena vema mkuu FM,

Lakini bado pia Structural Designer anaweza kuwa hana hatia endapo Design span ilishapitiliza.

Wasiwasi wangu ni huu, jengo hili ukiliangalia vema utaona kuwa watoto wote walianza kutegemea sehemu moja ya kutolea hewa kama inavyoonekana kwenye picha hapa chini, siamini kama professional designer yeyote anaweza ku-recommend upupu huu:

i2_DSC02279.JPG
 
Sijui. Sijawahi kuiona kwenye consultancy agreement yeyote. .................................. Lakini kama kuna major structural au technical failure, inayofanya jengo lisiweze kutumika ipasavyo, kinyume cha maagizo ya mshitiri hii sifahamu lakini naamini inadumu kwa uhai wa jengo. Kwa mfano, kama kuna conference room ghorofani iliyotakiwa kuchukuwa watu mia lakini haijawahi kuchukuwa watu hao hadi miaka kumi kupita. Ikiwa baada ya miaka kumi, mshitiri akapata mkutano wa watu mia na jengo kuanguka kutokana na uzito wao, basi wataalam wote watakuwa liable (kuanzia msanifu majengo hadi mhandisi wa structures). Hasa ikiwa walikagua na kupitisha kazi ya mkandarasi kuwa ilifanyika kama walivyomuagiza.

Hivyo ndivyo ninavyoelewa. Labda nimekosea.

.........exactly........thats the point im talking about........yes waweza kutumia professional wengine.........at the same time huwezi kumuacha msanifu original wa jengo.......unless kuna indemnification of some sort....kwa sababu design liability anakuw anayo bado.......na ndio maana mnaitwa Mafundi Mchundos (professionals)..........kuna kitu chaitwa "Life span"......je hiyo inakuwaje Fundi Mchundo!!
 
kuna mtu anaweza kuangalia ripoti hiyo inasema nini kuhusu kuwajibiwa kwa NSSF maana wengine walisema miye nimekurupuka na wao hadi hivi sasa wamejificha hawataki hata kuinua vichwa vyao. Walikuwa wa kwanza kudai ripoti imetoka lakini hawathubutu kuijadili...
 
Umenena vema mkuu FM,

Lakini bado pia Structural Designer anaweza kuwa hana hatia endapo Design span ilishapitiliza.

..............


....ooops....kumbe Fundi Mchundo Mkuu alishaliona hilo....thats where i was driving to................ya kwamba liability ya design inaishia pale life span ya structure inapofikiwa
 
.........exactly........thats the point im talking about........yes waweza kutumia professional wengine.........at the same time huwezi kumuacha msanifu original wa jengo.......unless kuna indemnification of some sort....kwa sababu design liability anakuw anayo bado.......na ndio maana mnaitwa Mafundi Mchundos (professionals)..........kuna kitu chaitwa "Life span"......je hiyo inakuwaje Fundi Mchundo!!

Hapana, Mkuu. Unaweza kumuacha msanifu original hata kama life span ya jengo ( mimi nilitumia neno, uhai wa jengo) bado haijaisha ili mradi uhakikishe kuwa huyo unayemchukua badala yake ni competent na legally recognised. Kwa kufanya hivyo, utakuwa umemuondolea liability yule wa kwanza katika sehemu unayoifanyia mabadiliko na sehemu nyingine itakayokuwa affected. Kwa sababu hii liability ina kick- in pale tuu panapotokea matatizo, linakuwa ni jukumu la arbitrator kuamua ni yupi katika waliohusika alikuwa negligent katika utendaji wake wa kazi na kusababisha damage kwa mshitiri.

Kama nilivyosema hapo awali, ingawa ni busara kama mshitiri atamhusisha msanifu original kwenye kazi za baadae lakini halazimiki. Miradi mingi tuu imefanyika nyumbani bila kumshirikisha msanifu original tukianzia upanuzi wa Maktaba ya Taifa, mabadilko katika jengo la Long Room, mabadiliko katika jengo la makao makuu ya NDC, n.k.

Ni kawaida vile vile kwa mshitiri ku-engage interior designer tofauti na msanifu original. Muhimu hapa vile vile ni competence ya huyo anayekuwa engaged.

Kwenye hili jengo, ukiangalia picha aliyobandika Mkuu Invisible, competence ya yeyote aliyekuwa appointed is to be doubted. Ile vent inawezekana ni kutoka jikoni na ilitakiwa ivuke paa kwa kiasi kikubwa na sio kama ilivyowekwa. Kama hizo ngazi ndiyo escape route ya pekee, basi tatizo ni more fundamental kuliko ilivyojitokeza kwenye ripoti. Ukiangalia kwa mfano, kuna mlango unafungukia ndani. Katika fire escape route mlango unatakiwa kufungikia nje ili kurahisisha watu kutoka (ni rahisi zaidi kusukuma mlango nje kuliko kuuvutia ndani hasa kama kuna msongamano mlangoni)! Ni hatari vile kuwa na ngazi ya wazi kuanzia pale ambapo mlango unafungukia. Hii itawafanya watu wa-trip wakati wanakimbia maafa.

Mawazo yangu tuu.

Amandla.........
 
1. Kama kuna modification zilifanyika.........je zilifanywa na nani
2. Kwanini mtu ui-discredit taarifa inayo-suggest........original designer awe consulted (this is where im troubled)....unapo-assume kuwa kutakuwa na ulaji......how do one substatiate this......i mean this argument is very very weak......how do you know the next consultant ndio hakutakuwa na ulaji.........
3.......unapompa designer mwingine afanye modification...........liability inahama!!........just kirahisi rahisi namna hiyo........ok....ndio Tanzania yetu hii.......tutafanyeje......na nyie ndio Mafundi Mchundos wetu
 


Hivi Tanzania kuna legal age ya kunywa pombe? ...Kama ipo, ni mahali gani ambapo inatumika?


Nadhani kuna sheria. Ipo, lakini haionekani? Kwenye mabango yanayotangaza tusker, kilimanjaro na serengeti, nimeona imeandikwa: Ni marufuku kuuzwa kwa mtu aliye chini ya miaka 18.

Sina hakika kama hiyo ni sheria/sera ya kitaifa, au watengeneza ulabu wamejitungia.

THE INTOXICATING LIQUORS ACT, 1968/28
PART VII, Sections 68 and 69, Subsect. (1)(a),(b)


OFFENSES

Supplying Intoxicating Liquor to any Person Under the Age of Sixteen Years

Any licensee who supplies intoxicating liquor to any person under the apparent age of sixteen years shall be guilty of an offence.

Any licensee who employs any person under the apparent age of sixteen years to:
(a) sell or control or supervise the sale of intoxicating liquor;​

b) have the custody or control of any intoxicating liquor on the premises, shall be guilty of an offence.​

Any licensee who permits any person under the apparent age of sixteen years to remain present on his licensed premises in any room, courtyard or other place in which intoxicating liquor is being served for consumption shall be guilty of an offence.


Iko current (haijatenguliwa, na imenukuliwa Bungeni in modern times).
 
1. Kama kuna modification zilifanyika.........je zilifanywa na nani
2. Kwanini mtu ui-discredit taarifa inayo-suggest........original designer awe consulted (this is where im troubled)....unapo-assume kuwa kutakuwa na ulaji......how do one substatiate this......i mean this argument is very very weak......how do you know the next consultant ndio hakutakuwa na ulaji.........
3.......unapompa designer mwingine afanye modification...........liability inahama!!........just kirahisi rahisi namna hiyo........ok....ndio Tanzania yetu hii.......tutafanyeje......na nyie ndio Mafundi Mchundos wetu

Hapana Ogah.Hautuelewi.
Hakuna mtu anayepinga msanifu original kuwa consulted. Tatizo ni pale wanaposema kuwa mabidiliko yoyote yalitakiwa kufanywa na msanifu original. Hii ndiyo tunayoona kuwa ni kupenyeza ulaji maana si lazima msanifu original apewe kila kazi itakayofanyika katika jengo aliloli-design. Huu ni uamuzi wa mshitiri na hapaswi kulazimishwa. Kwa kumlazimisha amchukue mtu ambae pengine hakumridhia ndio tunaona inaweza kuwa ni njia ya kumtengenezea ulaji msanifu original. Huyu bwana/bibi atakuwa amepata kazi in perpetuity kwa sababu tuu ali-design jengo la awali! Huku ni kum-hold to ransom mshitiri! Mshitiri awe na uhuru wa kumpa kazi yeyote amtakaye (hata msanifu original) bila kushinikwa. Hii ni haki yake maana yeye ndiye anayeingiza pesa yake na ni lazima aridhike kuwa anapata value for his/her money. Mbaya anapochukua short cut na kuacha kutumia wataalamu waliohalalishwa kihalali kwa kazi anayokusudia!

Si Tanzania peke yake ambapo mabadiliko yanafanywa na asiye msanifu original. Hii inatokana na pengine mshitiri kutopendezwa na kazi aliyomfanyia msanifu original au wakati mwingine ni kutaka mtazamo mpya tuu. Inaruhusiwa na haina noma. Ila kama huyo anayembadili msanifu original ni competent ni lazima ataheshimu na kutilia maanani alichokikuta.

Kilichofanyika katika jengo hili ni interior design na si kazi ngumu isipokuwa walioifanya hawakuwa competent. Hauhitaji kuwa msanifu original kujua umuhimu wa escape routes katika public space!
 

THE INTOXICATING LIQUORS ACT, 1968
PART VII Sections 68 and 69, Subsect. (1)(a),(b)


OFFENSES

Supplying Intoxicating Liquor to any Person Under the Age of Sixteen Years

Any licensee who supplies intoxicating liquor to any person under the apparent age of sixteen years shall be guilty of an offence.

Any licensee who employs any person under the apparent age of sixteen years to:
(a) sell or control or supervise the sale of intoxicating liquor;​

b) have the custody or control of any intoxicating liquor on the premises, shall be guilty of an offence.​

Any licensee who permits any person under the apparent age of sixteen years to remain present on his licensed premises in any room, courtyard or other place in which intoxicating liquor is being served for consumption shall be guilty of an offence.


Iko current (haijatenguliwa, na imenukuliwa Bungeni in modern times).

Hii aparent age ndio nini hasa? Mimi si mwanasheria lakini jee haimpi loophole mhusika kusema mimi nilidhani ana umri wa miaka 16 na siku moja? Watahakikishaje kuwa mtuhumiwa alifanya hivyo akijua thika kuwa anayemuuzia ulabu ana chini ya miaka 16? Ukizingatia jinsi hasa mabinti zetu siku hizi wanavyopevuka mapema!
 

...Na tukizungumzia pombe, jee tunaunganisha na pombe za kienyeji?


THE INTOXICATING LIQUORS ACT, 1968/28
PART I


Preliminary: Interpretation


''Intoxicating liquor'' means liquor or local liquor;

''Liquor'', means

(a) wine, ale, beer, porter, cider, perry. hop beer and any liquor, containing more than two per centum by weight of absolute alcohol except any bona fide medicine containing intoxicating, liquor as herein defined administered or sold by any duly qualified medical practitioner or pharmacist, or administered by any person purely for medicinal purposes; and​
(b) spirits of any description other than industrial spirits as Cap. 222 defined in section 2 of the Spirits Ordinance...​

''Local liquor'' means
pombe, fermented asali, tembo, ulanzi and all liquors (other than beer, spirits and wines to which the East African Excise Management Act, 1952 applies or moshi) of a kind prepared by the indigenous people of Tanganyika which contain more than one per centum by weight of absolute alcohol and any liquor which the Minister may, by notice in the Gazette, declare to be local liquor.​
Tumeongelea loophole ya muuza pombe kutegemewa kukisia umri wa mnunuaji. Li loophole lingine la hapa ni kwamba hii sheria inawabana Licensees, lakini wapika Wanzuki na La Mnazi wa vichoroni hawahitaji kuwa Licensees kutegemeana na vipimo vya ukali wa pombe yao (ukirejea definition ya Local liquor). Tatizo ni kwamba...aaaah, right, you got it, ...hawana vipimo!!
 

Attachments

  • SHERIA YA POMBE.pdf
    174.2 KB · Views: 629
Hapana Ogah.Hautuelewi.
Hakuna mtu anayepinga msanifu original kuwa consulted. Tatizo ni pale wanaposema kuwa mabidiliko yoyote yalitakiwa kufanywa na msanifu original. Hii ndiyo tunayoona kuwa ni kupenyeza ulaji maana si lazima msanifu original apewe kila kazi itakayofanyika katika jengo aliloli-design. Huu ni uamuzi wa mshitiri na hapaswi kulazimishwa. Kwa kumlazimisha amchukue mtu ambae pengine hakumridhia ndio tunaona inaweza kuwa ni njia ya kumtengenezea ulaji msanifu original. Huyu bwana/bibi atakuwa amepata kazi in perpetuity kwa sababu tuu ali-design jengo la awali! Huku ni kum-hold to ransom mshitiri! Mshitiri awe na uhuru wa kumpa kazi yeyote amtakaye (hata msanifu original) bila kushinikwa. Hii ni haki yake maana yeye ndiye anayeingiza pesa yake na ni lazima aridhike kuwa anapata value for his/her money. Mbaya anapochukua short cut na kuacha kutumia wataalamu waliohalalishwa kihalali kwa kazi anayokusudia!

Si Tanzania peke yake ambapo mabadiliko yanafanywa na asiye msanifu original. Hii inatokana na pengine mshitiri kutopendezwa na kazi aliyomfanyia msanifu original au wakati mwingine ni kutaka mtazamo mpya tuu. Inaruhusiwa na haina noma. Ila kama huyo anayembadili msanifu original ni competent ni lazima ataheshimu na kutilia maanani alichokikuta.

Kilichofanyika katika jengo hili ni interior design na si kazi ngumu isipokuwa walioifanya hawakuwa competent. Hauhitaji kuwa msanifu original kujua umuhimu wa escape routes katika public space!



...one thing "somehow" naridhishwa na argument yako unaposema..........ni busara msanifu original akawa consulted..........while Kuhani ana-dispute kwa kusema ni "flawed" kusuggest kumtumia msanifu original........hence the report is not credible!!!!.........thats where the difference btn us.........sasa na wewe....unaleta za kusema..........sijui ulaji......that is very weak indeed...........

.....hey hey hey.......taratibu Fundi..........that (quoted in red) was not my point of discussion with you and Kuhani........amenities za safety are very obvious for any layperson to realize..............

......anyhow.........well well well.......now thats where Mwanakijiji comes in...........
unasema mshitiri alikubali incompetent interior designer ku-modify matumizi ya jengo!!!!...........once again..........tell me now about design liability........je itakuwa kwa huyo incompetent interior designer.......as you had suggested.........?
 
Ogah. Kama alitumika interior designer au mtaalamu yeyote, ndio. Yuko liable. Lakini nina wasiwasi kama hata huyo incompetent interior designer alitumika! Sitoshangaa kama mshitiri hakuchukua mafundi tuu mtaani na kufanya aliyoyataka. Tanzania bado hatuheshimu Professionals. Tunaona wanatulia pesa tu. Humu jamvini tuu, ni wangapi wametumia wataalamu katika kujenga vibanda vyao? Michoro tunaitoa kwenye magazeti na kwenye mtandao. Mkandarasi ni mzee mwenye uzoefu. Msimamizi ni mke, mme, mdogo, baba, mama, rafiki yetu n.k.!
 
Watu wanachoshindwa kuelewa ni kuwa ripoti imesema Bubbles na 110 discos hawakuwa na leseni za kufanya shughuli za sanaa. Lakini pili ripoti inasema pia kuwa Mkataba wa NSSF na hayo makampuni ulikuwa ni kwa shughuli za kiofisi na siyo madisko. Lakini mnataka kujadili pombe!
 
Katika hotuba yake ya kufunga mwezi wa kumi Rais Kikwete hakuzungumzia vifo vya watoto 19 Tabora, wala ripoti ya Mkuu wa Mkoa wala mpango wa kutekeleza mapendekezo ya ripoti ile ili tukio hilo lisijuridie tena katika mazingira yale yale. Akazungumza mengi isipokuwa watoto 19! Nimedokewa kuwa alisahau!

Katika mjadala wa wabunge wa JMT kwa wiki mbili wakiwa Dodoma, mjadala ulioanza mwishoni mwa mwezi wa kumi sijui ulifunguliwaje lakini hakukuwa na mjadala motomoto kuhusu mazingira yaliyosababisha vifo vya watoto wale na kelele za kutaka wahusika wote wawajibishwe kwa mujibu wa ripoti na hata kuitisha uchunguzu huru zaidi (ambao ungechunguza ofisi ya mkuu wa mkoa na Mkuu wa Polisi). Hawakufanya hivyo; Wakazungumza mengi kweli isipokuwa ya watoto 19 au hata kutaka ile ripoti ijadiliwe Bungeni. nimeambiwa wabunge karibu 320 (wa CCM na wa UPinzani) walisahau vifo vya watoto hao!

Wakati wa hotuba yake ya kuliahirisha Bunge Waziri Mkuu Pinda naye alizungumza kwa kirefu lakini kama wenzake na yeye hakugusia kabisa vifo vya watoto wale 19 na wengine kujeruhiwa katika mazingira ya kizembe, aibu na ya kutokuwajibika kama yale tena siku ya Sikuu kubwa ya Idi El Fitr. Akazungumza mambo mengi ya kusifia shughuli za Bunge na kuuza utendaji kazi wa serikali yake. Lakini na yeye kama wenzake hakugusia vifo vya watoto 19 Tabora. Naambiwa na yeye alipitiwa.

NIkasema labda waandishi wetu wanaweza kukumbuka; na wao vile vile wakasahau hata kuhoji kwenye magazeti kwanini Rais, Bunge, Waziri Mkuu hawakuzungumzia vifo vya watoto 19 Tabora? Nikajiuliza kwanini waandishi wa habari hawakuichambua ripoti hiyo, kuhoji maswali na kupiga kelele watu wawajibishwe. Nikaambiwa na wao wamesahau!

Nikasubiri kwenye mtandao maarufu wa Watanzania kuona kama kuna mtu hata mmoja aliyeona mapungufu hayo kwenye hotuba ya Rais, ya Waziri Mkuu, mjadala wa Bunge na kwenye Magazeti. Hakuna aliyekumbuka vifo vya watoto hawa. Nimeambiwa wote wamesahau.


Nikabakia najiuliza, kwanini ninakumbuka? Nikaenda kutafuta majibu. Nilipoyapata na kujua kilichomo nikajikuta na mimi naletewa vidonge viwili nichague kimoja chekundu kingine cha bluu:

11956181_ecade765cd.jpg


Nikaambiwa kwa maneno ya Morpheus katika Matrix:

You have to see it for yourself. This is your last chance. After this there is no turning back. You take the blue pill, the story ends, you wake up in your bed and believe whatever you want to believe. You take the red pill, you stay in Wonderland, and I show you how deep the rabbit hole goes. Remember, all I’m offering is the truth, nothing more

Sasa mimi kama vile ilivyokuwa kwa Rais, Bunge, Waziri Mkuu, Waandishi, na wanachama wa mitandao mbalimbali ya Wabongo na wananchi kwa ujumla natakiwa nami nifanye uamuzi. Uamuzi ambao nitaishi nao. Naamini kuwa kidonge cha bluu kitakomesha hii njozi mbaya. Chekundu hata hivyo kinahitaji ujasiri maana unaweza kujikuta uko peke yako katika tandabui ya njama ya ukimya!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mwanakijiji,

Wengi tumesahau hili la watoto wa Tabora,hata mimi nashangaa ni nini kilichotufanya tusahau haraka hivi? ni makusudi? hapana! la hasha! pengine hili la EPA kwasababu tulikuwa tunaliimba sana kwa muda mrefu limechangia kutusahaulisha kila mtu akawa yuko busy na Jeetu Patel na Johnson Lukaza. Haiwezi kuwa sababu iliyochangia hii mkuu? Kila mtu yuko kisutu huku kila mtu akisubiri lini Kagoda ataenda mahakamani!
 
Mkuu Mwanakijiji,

Wengi tumesahau hili la watoto wa Tabora,hata mimi nashangaa ni nini kilichotufanya tusahau haraka hivi? ni makusudi? hapana! la hasha! pengine hili la EPA kwasababu tulikuwa tunaliimba sana kwa muda mrefu limechangia kutusahaulisha kila mtu akawa yuko busy na Jeetu Patel na Johnson Lukaza. Haiwezi kuwa sababu iliyochangia hii mkuu? Kila mtu yuko kisutu huku kila mtu akisubiri lini Kagoda ataenda mahakamani!

Kwa sababu maafa haya hayakutokea Dar. Ingekuwa yametokea hapo dar basi ingekuwa wimbo ila kwa sababu ni kule wenzetu Wakenya wanaita OSHAGOO basi, hadithi imeshaisha zamaniiiiiiiiiii. Waulize wazazi wa wale watoto, wanawakumbuka sana lakini ni nani wa kuwauliza? Wote tuko mjini tunagagaa na upwa tu!
 
Kwa sababu maafa haya hayakutokea Dar. Ingekuwa yametokea hapo dar basi ingekuwa wimbo ila kwa sababu ni kule wenzetu Wakenya wanaita OSHAGOO basi, hadithi imeshaisha zamaniiiiiiiiiii. Waulize wazazi wa wale watoto, wanawakumbuka sana lakini ni nani wa kuwauliza? Wote tuko mjini tunagagaa na upwa tu!

Ndugu Eeka Mangi, sio kwa sababu halikutokea Dar, nchi yetu kitu kinapotokea ndio utasikia kila kauli, lakini mara nyingi ukipita muda yote yanaachwa (kumbuka Tabora Mkuu wa Mkoa alikiri tatizo kama hilo liliwahi tokea na ikaundwa tume). Na hili halihusu Dar es Salaam tu. Kumbuka Dar lilianguka jengo Temeke (nadhani Chang'ombe) ikaundwa tume, lakini hatujui lililokuwemo katika ripoti yao. Japo kuna kesi ilifunguliwa kwa waliionekana wana hatia baada ya jengo kuanguka, sijui imefikia wapi. Pia juzijuzi lilianguka tena jengo Dar, akafa mtu mmoja, lakini hatuoni hatua zilizo wazi kuchukuliwa. hivyo si Tabora tu, hata Dar yanatokea na watu wanaendelea na masuala yao kama kawaida. Tutabaki kuunda tume mpaka ifikie wakati tume ni nyingi kuliko matukio!.
 
Mfumwa, how does that explain Rais wa nchi anayezungumza kuhusu Mwezi wa kumi kushindwa kukumbuka vifo vya watoto 19 vilivyotokea mwezi wa kumi?
 
Back
Top Bottom