Wakuu kwa yeyote mwenye ile listi ya mafisadi 11 iliyotajwa na dr. Slaa mwaka 2007 atuwekee hapa!
Mkuu mwambie mzee wako ajitangaze magazetini na redion Lakini kwa njia hizi mnazotumia wala haziwezi kufua dafu ufisadi ni kashifa kubwa sana hapa duniani,Wengi wamekuwa wakijaribu kulizungumzia jambo hili kwa namna mbalimbali. sitaki kuwarudisha nyuma kwenye historia mpaka Lowassa kufika hapa alipo kisiasa. tunakumbuka mwaka 2005 ambapo kulikuwa na makubaliano ya Mh lowassa na kikwete kuwa atakapoingia kikwete kama mgombea na hatimaye kuchukua urais kwa kupitia CCM baada ya miaka 10 iwe zamu ya Lowassa. katika kipindi kile cha mtandao Sitta alisukwa kuwa angekuwa waziri mkuu na mambo yalikuja kuharibika mwishoni pale uwaziri mkuu alipopewa Lowassa. sitta alijenga chuki kwa lowassa pamoja na kuwa akikuja kupozwa kwa kupewa uspika bado hakuwa ameridhika na nafasi ile.
Lowassa alionekana mtendaji sana na hata kuonekana akimfunika rais kikwete. alipangua sadu za watendaji wengi na kuweka wale ambao aliona wangeendana na kasi yake. rais akiwa nje ya nchi mara nyingi aliporud alikuta wale watu wake wamewekwa pembeni na wamewekwa wengine ambao waliweza kuendana na kasi ya lowassa. rejea kwenye ujenzi wa shule za kata.
jambo hili usalama walio upande wa kikwete walimshtua kuwa jamaa yako ana speed sana na watu wanamwona kila kona akipiga kazi mpaka wewe unasahaulika. hivyo jiangalie. rais kweli alitizama na kuona jamaa amejijenga sana kisiasa.ukaandaliwa ule mpango wa richmond. katika hilo sitta alishirikishwa sana na ukichangia na chuki zake kwa lowassa akaona ni nafas nzuri ya kumbomoa. lilipozuka la kuzuka rais alimwambia Lowassa kuwa ajiuzulu na yeye atamsafisha. lakini rais alikuwa na lengo la kumtosa lowassa katika meli kwa maana ya kwamba abebe mzigo wa dhambi zao zote na baadaye waje kumtua.
kumbe rais alikuwa na malengo yake mengine. kuwa amwache lowassa azame na lile zigo na hapo hapo haraka rais kikwete akawageukia wale walio kuwa wapinzani wa lowassa na kuanza kuwapa nafasi watu kama akina nape, akina malecela,akina mangula,akina kinana n.k rais aliamua kuwa promote hawa ili sasa kuunda mtandao mpya baada ya kuona ule uliomwingiza madarakani ameusaliti.hivyo akaamua kutafuta marafiki wapya ambao pia watakuja kumlinda.
usalama wa taifa kwa kiasi kikubwa ndio waliokuwa wakishirikiana na ikulu kupanga mikakati ya kumwangusha lowassa hasa baada ya rais kufanya mabadiliko makubwa ya kuweka watu "wake" ili sasa waweze kuendana na mambo yake "rejea kutekwa na kuteswa kwa dr ulimboka na wafanyakazi wa ikulu kuhusika. usalama ukagwanyika ktika sehemu kuu mbili. moja ni yenye kufata maslah ya rais na nyingine yenye kuangalia maslah ya taifa na hii ikaonekana kama ipo upande wa lowassa. wengi wakatolewa katika nyadhifa zao na hata kubadilishiwa vitengo halafu wakaingizwa vijana waodogo wadogo wasio hata na uelewa mzuri ili hawa wawe walamba miguu wa rais na kufata matakwa yake.tumeyaona mengi.
kwenye moja ya mikutano ya NEC ilifikia hatua kidogo Mh Lowassa apasue jipu la ukweli wa Richmnond na kama si busara za Mkapa leo yangekuwa mengine. ila kwa busara mkapa na mwinyi walimshauri Lowassa anyamaze asizungumzie suala la Richmond. na wengi wamekuwa na hamu ya yeye kuja kuuweka wazi ukweli wa jambo hili. wengi wamekuja kugundua kuwa kwa yeye ilimpasa afe kwa ajili ya wengi. hivyo wengi kwa sasa wanakula matunda ya kazi aliyofanya lowassa kwa kujidai yeye anapenda sana cham kwa lengo la kukiokoa na wenzie wanaitumia karata hiyo kumdidimiza kisiasa.
Ngoja wajaribu lakini vikundi vyao vitapoteana mapema sana mwezi wa tano kama siyo wa sita.Vijibwa vya Lowasa mnashida sana kusafisha huyu mzee wenu tangu nizaliwe sijawahi kuona wala kusikia lowasa kafanya jema zaidi ya ufisadi wake anafanya kila siku kwenye jamii.