Tutafika
JF-Expert Member
- Nov 4, 2009
- 1,443
- 631
Watanzania kwa ndoto za mchana! Nani huyo anatakiwa ampe DCI Manumba amri ya kufungua police inquiry(PI)... hao hao wanufaika wa hizo account? Unapomtaja Ngeleja kama Ngeleja, unakosea sana kwani unasahau jambo moja muhimu...mfumo unaobariki/unaoruhusu mambo kama haya kutendeka. Je vijisenti vya Chenge vilirudishwa? Juzi hukushuhudia mfumo ukimwongezea majukumu na sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha bungeni na bado! Unacheza na CCM!
Sasa naona kuna haja ya kuwa mpambanaji active zaidi!,
Hospitali hazina maji wala umeme, shuka hazifuliwi na magodoro ni yale tuliyoyakuta mwaka 1961. Madakitari na waalimu wameamua kuwa walevi wa gongo kwasababu ya maisha magumu. Mbaya zaidi wanywa gongo wanafungwa wakati wale wa madawa ya kulevya wanashangiliwa! Mkulima ndio usiseme make huyu ndio ngazi ya kupandia, anakanyagwa kichwani. Analima kwa tabu sana halafu anazuwiwa kuuza!
Hivi hatujachoka hii hali?