Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Huyu RC bila shaka alikuwa anajipendekeza mbele ya rais wakati JK anajiandikuisha sensa leo. alisema mbali na viongozi wachache wa dini ya Kiisilamu na waumini wengine wa dini hiyo wanaoeneza ushawishi kwamba Waisilamu wasikubali kuandikisha, pia kuna viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani wenye heshima zao mbao pia wanaeneza ushawishi huo. Hawa hakuwataja.
Tunaomba awataje kwa majina viongozi wa siasa wanaofanya hivyo ama sivyo RC huyo aachane na kujipendekleza kwa Rais.
isitoshe RC huyo ametangaza waumini kadha wa dini ya Kiisilamu waliokamatwa kutokana na kushawishi wenzao wasijiandikishe, lakini swali kubwa ni kwa nini hadi sasa serikali haijamtia mbaroni Sheikh Ponda ambaye wazi wazi alikuwa akiwashawishi Waisilamu wasijiandikishe.
Serikali inamuogopa Ponda na kukimbilia kukamata vidagaa?
Tunaomba awataje kwa majina viongozi wa siasa wanaofanya hivyo ama sivyo RC huyo aachane na kujipendekleza kwa Rais.
isitoshe RC huyo ametangaza waumini kadha wa dini ya Kiisilamu waliokamatwa kutokana na kushawishi wenzao wasijiandikishe, lakini swali kubwa ni kwa nini hadi sasa serikali haijamtia mbaroni Sheikh Ponda ambaye wazi wazi alikuwa akiwashawishi Waisilamu wasijiandikishe.
Serikali inamuogopa Ponda na kukimbilia kukamata vidagaa?