sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 645
WAKATI fulani wakuu wa mikoa na wilaya walihudhuria mafunzo maalum ya siku kumi mjini Dodoma ambapo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliwaasa kutokujihusisha na ushabiki wa kivyama hasa kipindi hiki cha mfumo wa vyama vingi. Badala yake, Pinda aliwataka wawe huru bila kuegemea upande wowote wa chama cha siasa huku wakitekeleza tu kwa ufanisi mkubwa sera za chama tawala.
Waziri Mkuu alisema: Ninawaonya msitumbukie katika siasa na wala msijaribu kabisa. Huko kuna vyama vingi vitumikieni vyote ingawa kwa sehemu kubwa mtatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi, hivyo simameni kidete ndugu zangu.
Katika mafunzo hayo, Pinda aliwasihi wakuu hao wa mikoa na wilaya kutokukaa tu ofisini badala ya kuwafuata wananchi na kutambua na kisha kushughulikia kero zao. Pia aliwataka kutumia fursa za kiuchumi zilizopo mikoani ili zitumike kumsaidia mwananchi kuondokana na umasikini.
Kimsingi, huo ndio ulipaswa kuwa wajibu wa wakuu wa mikoa na wilaya huko waendako; kuwatumikia wananchi bila kujali itikadi zao za kivyama, kidini na kikabila lakini ukweli umekuwa tofauti kama makala hii itakavyojaribu kueleza.
Gazeti moja linalotoka kila siku hapa nchini limeandika hivi majuzi kwamba Mkuu wa Mkoa wa Arusha (RC), Magesa Mulongo, alivunja ukimya akaeleza namna alivyofurahishwa na maamuzi ya Mahakama Kuu ya kumvua ubunge aliyekuwa mbunge wa jimbo la arusha mjini, Godbless Lema.
Gazeti hilo, toleo Na. 2724 la Mei 18, katika ukurasa wa tatu, linaandika: Mkuu wa Arusha, Magesa Mulongo, ameonesha furaha yake ya kuenguliwa kwa mbunge wa Arusha Mjini, Gobles Lema kulikofanywa na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha akidai kuwa kumesaidia kudumisha amani katika mkoa huo.
Gazeti hilo likazidi kuandika: Akizungumza mara baada ya kuwaapisha wakuu wapya wa wilaya sita katika hafla fupi iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, Mulongo alisema kwa sasa Mji wa Arusha umetulia na alimpongeza Jaji Gabriel Rwakibarila ambaye alitoa hukumu iliyomnyanganya ubunge Lema.
Kama ni kweli matamshi hayo yametoka kwenye kinywa cha kiongozi huyo wa serikali kulingana na taarifa hiyo, basi hii ni hatari kabisa kwa nchi iliyoridhia utawala wa demorasia na siasa za vyama vingi kwani kwa kufanya hivyo kiongozi huyo wa serikali atakuwa anawagawa watu anaowatawala kwa mujibu wa itikadi za vyama vyao. Kadhalika haendani kabisa na wosia wa Pinda.
Waziri Mkuu alisema: Ninawaonya msitumbukie katika siasa na wala msijaribu kabisa. Huko kuna vyama vingi vitumikieni vyote ingawa kwa sehemu kubwa mtatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi, hivyo simameni kidete ndugu zangu.
Katika mafunzo hayo, Pinda aliwasihi wakuu hao wa mikoa na wilaya kutokukaa tu ofisini badala ya kuwafuata wananchi na kutambua na kisha kushughulikia kero zao. Pia aliwataka kutumia fursa za kiuchumi zilizopo mikoani ili zitumike kumsaidia mwananchi kuondokana na umasikini.
Kimsingi, huo ndio ulipaswa kuwa wajibu wa wakuu wa mikoa na wilaya huko waendako; kuwatumikia wananchi bila kujali itikadi zao za kivyama, kidini na kikabila lakini ukweli umekuwa tofauti kama makala hii itakavyojaribu kueleza.
Gazeti moja linalotoka kila siku hapa nchini limeandika hivi majuzi kwamba Mkuu wa Mkoa wa Arusha (RC), Magesa Mulongo, alivunja ukimya akaeleza namna alivyofurahishwa na maamuzi ya Mahakama Kuu ya kumvua ubunge aliyekuwa mbunge wa jimbo la arusha mjini, Godbless Lema.
Gazeti hilo, toleo Na. 2724 la Mei 18, katika ukurasa wa tatu, linaandika: Mkuu wa Arusha, Magesa Mulongo, ameonesha furaha yake ya kuenguliwa kwa mbunge wa Arusha Mjini, Gobles Lema kulikofanywa na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha akidai kuwa kumesaidia kudumisha amani katika mkoa huo.
Gazeti hilo likazidi kuandika: Akizungumza mara baada ya kuwaapisha wakuu wapya wa wilaya sita katika hafla fupi iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, Mulongo alisema kwa sasa Mji wa Arusha umetulia na alimpongeza Jaji Gabriel Rwakibarila ambaye alitoa hukumu iliyomnyanganya ubunge Lema.
Kama ni kweli matamshi hayo yametoka kwenye kinywa cha kiongozi huyo wa serikali kulingana na taarifa hiyo, basi hii ni hatari kabisa kwa nchi iliyoridhia utawala wa demorasia na siasa za vyama vingi kwani kwa kufanya hivyo kiongozi huyo wa serikali atakuwa anawagawa watu anaowatawala kwa mujibu wa itikadi za vyama vyao. Kadhalika haendani kabisa na wosia wa Pinda.