Elections 2010 Raslimali za Tanzania Zinatosha Watanzania Wote Milioni 43 - Zinakwenda Wapi?

niweze

JF-Expert Member
Oct 21, 2009
1,008
116
Tukianza Kuchambua Kila Kona na Kutafuta Raslimali za Nchi Yetu ya Tanzania Unaweza Ukapatwa Butwaa. Nchi Yetu ya Tanzania Iliwepewa Hizi Raslimali ili Ijijenge na Kuwa Nchi Bora Duniani. Wengi Tukianza Kuangalia Haya Madini Yanauzwa Bila Hata Risiti Zozote na Mikataba Inayojulikana na Kikundi cha Bank kuu na Chama CCM ni Tatizo Tupu Hapa. Ukifuatilia Sana Haya Madini Yaligunduliwa Mwaka Gani Utacheka Zaidi. Inchi Yetu Imekanyagwa na CCM na Wanashindwa Hata Kutueleza Funds Zinapatikana Kiasi Gani na Zaidi Mipango Gani Wanafanya Kuwaelimisha Hao Wananchi Wanaoishi Pembeni Mwa Migodi. Kichekesho Kingine na Upotofu ni Kutofanya Njia Yeyote Kuelimisha Taifa ili Watanzania Waweze Kuinvest, Kumiliki na Kuuza kwa Faida Hii Raslimali Yao. Hakuna Hii Mipango Yoyote ya Kuinvest kwa Wananchi Wako Kuijenga Nchi...Ukienda Upande wa Mashamba na Kilimo Maswala ni Yale Yale. Mpaka Leo Hii Wananchi Wengi Wanalima kwa Mikono Kilimo cha Kizamani na Kitu Serikal ya CCM Imefanya ni Kuwaangalia na Kula Pesa za Kuwaelimisha na Kutoa Mikopo Kwao. Sasa Hii Inchi Itaendelea Vipi? Tanesco na Sources Zingine za Energy Zinapiganiwa na Hawa CCM Kila Leo ili Nani Ashikilie ili Wale Badala ya Kufikiria Miaka Ishirini Ijayo Watanzania Wataconsume Umeme Kiasi Gani. Tangu Tanesco Ifunguliwe, CCM Hawakujua Population ya Tanzania na Itahitaji Umeme Kiasi Gani? Ni Maswala Mengi Wameiangusha Nchi Lakini Wao Wanaona Wanahaki ya Kushika Usukeni wa Gari Wakati Gari Linaingia Porini.

"Tuamke Tuamke Watanzania Hakuna Nchi Yeyote Utatusaidia Kuwaondoa Sisiem ni Sisi Wenyewe"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom