RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

Wana jamii

katika mapendekezo ya Rasimu ya Katiba mpya limo suara la raisi kuteua majaji. Sote tumeshuhudia jinsi majaji vihiyo walivyokuwa wanateuriwa na rais pamoja na kwamba kuna tume ya mahakakama inayomshauri Rais katika teuzi za majaji. Kama majaji watendelea kuteuriwa na rais basi tutaendelea kushuhudi muhimili huu ukiendelea kudhibitiwa ipasavyo na mhimili mwingine yaani Selikali kama ilivyo sasa. tukatae pendekezo hili ikiwezekana tuchukue utaratibu wa kuwapata majaji katika katiba ya majirani zetu wakenya.
 
Rasimu hii bado mambo mengine yanahitajiufafanuzi, pamoja na viti maalumu kuondolewa lakini inapendekezwa kila jimbo litakuwa na wabunge wawili wa kike na kiume, sasa wanapatikanaje? au kila mgombea atakuwa na mgombea mwenza? wenye rasimu watfafanulie.
Duh! Acha niwahi jimboni kwangu nianze kutafuta perfect match. Mgombea mwenza wa ubunge. It sounds good. Kama kuna vyama 20 wagombea watakuwa 40. Safi.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
mm naona hapo kwenye kinga ya raisi iondolewe,maana hao wabunge uwezo wa kumshitaki haupo maana ni wanachama wake.
 
Wanajf,
moja kati ya vitu vilivyopendekezwa kuwepo kwenye rasimu ya katiba na tume ya warioba ni kufutwa kwa viti maalum the utaratibu uwe kwamba wanachaguliwa kutoka kwenye majimbo kama wawakilishi wa wanawake,
kama ilivyo utaratibu wa sasa kuwapata hawa wabunge kwa asilimia kubwa ilitegemea ni jinsi gani unawafurahisha mabwana zako(wakubwa wa vyama) na wala si wananchi maana wao hawakuwa na maamuzi kwenye kukufanya kuwa mbunge!

Lakini kwa sasa wananchi wana maamuzi katika kuchagua hawa wabunge(wanawake) kwa hiyo ushawishi wao ndo utawafanya wachaguliwe na wananchi,
tukiongelea kwa chama kama CCM kuwafurahisha mabwana na wapiga kura at the same time ni kitu kigumu sana,
sasa swali langu ni kwamba tutegemee kuona mabadiliko gani kwa hawa wabunge ambao kwa sasa wengi wao ni wale wa (ndiooooo, namsifu sana rais, namsifu sana waziri, naunga hoja mkono mia kwa mia wakati amoerodhesha matatizo kibao e.t.c)??????
Tukizingatia kuna suala la kuruhusiwa mgombea binafsi kwa maana kwamba hata kama chama hakitakuteua bado una chance ya kugombea kama mgombea binafsi na kama wananchi wamekukubali then utapita!

So tutegemee nini bungeni kwa sasa kwa hawa wabunge?
Je wataanza kutetea kwa nguvu zote maslahi wa wananchi hata kama watawakera wakubwa wa chama????? Wakiwa wanajua kabisa kwamba hata wakitoswa watgombea kama wagombea binafsi?
Mkuu nadhani hilo ndilo litakalotokea. Tutegemee kuwapata akina Filikunjombe kibao Bungeni kuanzia sasa. Watu sasa watajitoa kwenye utumwa wa vyama watakuwa watumwa wa wananchi. Tume imeenda mbali zaidi na kuruhusu kuwafuta wabunge kazi kabla ya uchaguzi basi hapa utegemee wabunge kujituma kwa wananchi wao aliowachagua
 
Naona kuna msamiati mpya. Washirika wa Muungano. Kina nani hawa?
Halafu hiki kipengele kimekaaje?
Tume pia, inapendekeza haki mpya ziingizwe kwenye Katiba ikiwa ni pamoja na haki ya wafanyakazi, , haki ya mtoto, haki za Watu wenye Ulemavu, Haki za Wanawake, Haki za Wazee, Haki za Makundi Madogo katika Jamii, Haki ya Elimu na Kujifunza, Haki ya kupata habari, Haki na uhuru wa habari na vyombo vya habari na kadhalika.

mkuu raia fulani hapo kwenye red. isije ikawa ni haki za maliberali!
 
Wana jamii

katika mapendekezo ya Rasimu ya Katiba mpya limo suara la raisi kuteua majaji. Sote tumeshuhudia jinsi majaji vihiyo walivyokuwa wanateuriwa na rais pamoja na kwamba kuna tume ya mahakakama inayomshauri Rais katika teuzi za majaji. Kama majaji watendelea kuteuriwa na rais basi tutaendelea kushuhudi muhimili huu ukiendelea kudhibitiwa ipasavyo na mhimili mwingine yaani Selikali kama ilivyo sasa. tukatae pendekezo hili ikiwezekana tuchukue utaratibu wa kuwapata majaji katika katiba ya majirani zetu wakenya.

Ni bora hii tume ya mahakama ipewe meno ya kuwahoji wanaotaka kuwa majaji na kupendekeza kwa Rais. Hapa kunatakiwa kuwe na uwazi kama ilivyo kwa Kenya na si kufanya mapendekezo kimya kimya. Kumbuka sakata la Zanzibar.
 
Wana jamii

katika mapendekezo ya Rasimu ya Katiba mpya limo suara la raisi kuteua majaji. Sote tumeshuhudia jinsi majaji vihiyo walivyokuwa wanateuriwa na rais pamoja na kwamba kuna tume ya mahakakama inayomshauri Rais katika teuzi za majaji. Kama majaji watendelea kuteuriwa na rais basi tutaendelea kushuhudi muhimili huu ukiendelea kudhibitiwa ipasavyo na mhimili mwingine yaani Selikali kama ilivyo sasa. tukatae pendekezo hili ikiwezekana tuchukue utaratibu wa kuwapata majaji katika katiba ya majirani zetu wakenya.

Mkuu itapendeza ukatowa mapendekezo tuwapate kwa mfumo upi?
 
Pamoja na mapendekezo mengi kwenye TUME kuwa mazuri, lakini bado kuna mapangufu makubwa, mfano madaraka ya rais bado hayajaainishwa vizuri, RAIS kuteua majaji, kwanini huo Mhimili usiteuwe wenyewe na mambo mengine mengi.

Swali langu je hii rasimu inaweza kufanyiwa marekebisho kabla ya kupigiwa kura ya NDIYO NA HAPANA?

Marekebisho yatafanywa kupitia mabaraza ya katiba na bunge la katiba. Lakini mi ninawasiwasi kwa nini madaraka ya rais hayapunguzwi? Eti kila jimbo kuwe na wagombea wawili -ke na -me,sisi tunataka wabunge wapunguzwe wao wanazid kuwaongeza si bora hata wangesema kila nch iamue aina ya wabunge kwenye katiba zao kuliko huu upuuzi. Wametumia garama kuuubwa rasmu yenyewe ya kawaida tu,si bora hata wangeteuliwa watu kadhaa tu wakaanda rasmu kuliko hizo garama zote walizotumia na mambo waliyoleta ni ya kawaida tu,anyway wamejaribu na hii ndo Tanzania!
 
Lakini kuna ukweli usiopingika kuwa mikoa na wilaya zetu zimewekewa mipaka kikabila. Hata hii mipya iliyotengwa siku za karibuni! Nani anabisha?
 
Hii rasimu hapo kwenye hii mihimili ya dola kujitegemea bado haija paweka vizuri...hasa hapo kwenye mahakama...kwenye bunge pako fresh...
 
mkuu Matola mimi mwenyewe jambo hili siliafiki hata kidogo,mbunge mmoja anatosha sana,kama wameweza kutoa viti maalumu kwa nini wanatuletea tena huu mzigo mwingine?ni nini mantiki ya kuwa na wabunge wa jinsia zote ktk kila jimbo?ni ktk harakati za kutafuta usawa au ni nini?na je usawa unatafutwa kwa kufanya km sisi tunavyotaka kufanya?we have to be very keen here na sio kukurupuka.

wamekopi katiba ya kenya!this is absurd.hata G7,nchi tajiri sana duniani hawana mfumo huu.
 
Ni bora hii tume ya mahakama ipewe meno ya kuwahoji wanaotaka kuwa majaji na kupendekeza kwa Rais. Hapa kunatakiwa kuwe na uwazi kama ilivyo kwa Kenya na si kufanya mapendekezo kimya kimya. Kumbuka sakata la Zanzibar.

Raisi kwakuwa ndiye mkuu wa mhimili mmoja wa dola-serikali haruhusiwi hata kidogo kuweka mkono wake katika kuteua ama kuchagua watumishi wa mhimili mwingine wa dola-mahakama.

Raisi abaki kudeal na serikali yake na tume ya utumishi wa mahakama ndiyo ifanye kazi ya kuajiri majaji ikiwa ni pamoja na Jaji Mkuu na Naibu wake.
 
Haki za akina Mdee na Mbatia

Tume ya warioba wamejitahidi kwa kweli.Madaraka ya raisi ndiyo hawajaliweka vizuri.Rais anatakiwa kuwapendekeza mawaziri/majaji baada ya hapo kuwe na tume huru itakayo wafanyia mchujo (vetting) na baada ya hapo majina ya watakaofaulu yapelekwe bungeni kuwa approved na kurudishwa kwa raisi kwa ajili ya kuwatangaza. Hili la kusema raisi awateue na baada ya hapo wapitishwe na bunge naona bado halijakaa vizuri kwani wabunge wa chama anachotokea rais wanaweza kuwa ni wengi na wakawapitisha hata wale ambao hawafai.
 
Mkuu itapendeza ukatowa mapendekezo tuwapate kwa mfumo upi?

Nafasi za kazi zitangazwe na kisha wenye sifa waombe. Kisha kamati maalumya majaji iwafanyie usaili bila kuingiliwa na mamlaka yo yote.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Si Kikwete aliwambia Dodoma muianzishe lakini muiendeshe wenyewe na nyie mmekomalia iingie kwenye katiba?
Hakuna aliyekataza katiba kuwepo, shida ni kwamba mnataka wale wanaodaiwa kuibeba bakwata iwabebe!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom