Rasimu hajakidhi bado sana

May 4, 2010
77
12
RASIMU YA KATIBA MPYA
MAONI NA MSIMAMO BINAFSI WA AWALI KUHUSU RASIMU
SEHEMU YA KWANZA: MAONI YA JUMLARasimuhii ukiangalia juu juu tu na kwa kupitia propaganda ya vyombo vya habari ambavyovinalipwa kufanya hivyo, kupitia fedha za wafadhili za 'watch dog’ utaisifiakuwa ni nzuri na haina kasoro yeyote. lakini ukiisoma ukiwa umetulia utaona nirasimu hatari kwa usalama na mustakabali wa taifa hili ambalo limekuwa ni mfanowa kuigwa na nchi nyingi duniani kwa misimamo yake amani na utulivu. Kwa kifupi bado hatujapata Rasimu ya kuwapa wananchiwaijadili na kuitolea maamuzi ya kuikubali au kuikataa kutokana na mapungufumakubwa yanayoonekana katika Rasimu hii kama ifuatavyo;
  • Rasimu haijibu kero za mungano na wala ki mantiki haiimarishi muungano. Ni njia ya kisayansi ya kuua Muungano na sijui atakeye wanadganya wa Tanzania kuwa kuimarisha muungano ni kuwa na serikali tatu ni nani na anatupa insurance gani? Watanzania hawakuwa na lengo la kudai serikali tatu kama ilivyopendekezwa na Rasimu hii, lakini tatizo kubwa la muungano lilikuwa utata wa utekelezaji wa mambo makuu ya kimsingi ya muungano.

  • Kuna kila dalili kuwa Tume inayoongozwa na Mh. Jaji Warioba imezidiwa ujanja na makundi maalum ambayo ni hatari katika jamii yetu ya watanzania. Itakumbukwa kuwa kabla ya serikali kuamua kuunda tume tayari genge la wasomi wakiongozwa na Issa Shivji wa Kigoda cha Mwalimu, Kitila Mkumbo aliyekuwa makamu mwenyekiti UDASA na wengine wanaojiita waumuni wa Azimio la Arusha walikwisha anza kutu brainwash wakitumia mijadala ya kisomi iliyoonyeshwa moja kwa moja kwa wananchi kupitia TV, mijadala iliyofanyika kwenye ukumbi maarufu wa Nkrumah, Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (live coverage pale Nkurumah Hall). Mambo yote waliyokuwa wanaropoka pale yameingia kwenye hii rasimu. Swali kwa nini yameingia kirahisi bila hata kuchujwa? Kweli mabilioni ya pesa yaliyotengwa kwa tume kufanya kazi ndo yameishia kunakili taarifa zilizokuwapo na kutuletea wananchi tuzijadili?

  • Rasimu haijatimiza kiu ya wananchi wa Tanzania. Rasimu hii imetimiza kiu ya makundi ya watu wachache hususan Kigoda cha mwalim, CHADEMA, LHRC, Haki Elimu, MCT na MTF na Tanganyika Law Society. Kwa uhakika zaidi ya asilimia 90 ya Watanzania hawajasikika na wamepigwa butwaa na matokeo ya Rasimu.
Nivema Rasimu hii warudishiwe ijiridhishe katika mambo yafuatayo; 1. Jambo lolote wanaloshaurilazima liwe na maslahi kwa wa Tanzania waliowengi na liwe ndani ya uwezo waTanzania kwa kuzingatia hali halisi, bajeti na malengo mengine ya kimaendeleo,mila na desturi za kitanzania.2. Si vema kuirudisha nchikatika malumbano ambayo kila mmoja anafahamu kuwa hayana majibu. Mfanokitendawili cha moja na moja ni tatu. Lazima wajumbe wa Tume wazingatiemtikisiko wa kisiasa uliowahi kuikumba nchi hii katika kujadili mambo ambayosasa wanataka kuyarudisha kama yale ya G55, na mkanganyiko uliopelekea Mh AboudJumbe kujiuzulu nyadhifa zake zote.3. Tanzania kwa sasa inapigahatua kuondoa umasikini. Sasa lazima kwenye katiba kuwe na mwelekeo wa kiuchumikwa vitendo. Kuwa na serikali yenye gharama ndogo na fedha nyingi kwenda kwenyeshughuli za kimaendeleo. 4. Maoni au mawazo mapyalazima yazingatie kuwa Tanzania ina maadui wengi wa kisiasa, kiuchumi nakisaikolojia. Kuna mambo yameiwezesha Tanzania kuheshimika duniani hasa ikiwemoMuungano wa Tanganyika na Zanzibar, kuwa kisiwa cha amani. Tayari juhudi kubwa zimekuwa zikifanywakupotosha mantiki ya muungano na utulivu nchinikwa uongo eti Muungano uliasisiwa na CIA. Watu hawa enye mtazamo hafifu wanashindwakusema ukweli kuwa uhusiano wa udugu naukaribu wa Tanganyika na Zanzibar ulianza wakati wakoloni hao wanaotaka leo hiimuungano uvunjike wakiwepo. Kwa ufupi utamaduni wa barana visiwani ulishabihiana sana hasa kama vile lugha ya Kiswahili nk. Utamadunihuu wa kuongea lugha moja ndio uliyotusaidia sana kutambua kuwa sisi(Tanganyika na Zanzibar) ni watu wamoja na kusaidia muungano kukubaliwa maramoja hata bila ya mjadala mrefu. Lakini kuna ushahidi kuwa kulikuwa na mambomengi yanayofanyanana katika sehemu hizi kabla ya muungano kwa mfano,kila lililotokea Tanzania Bara lilikuwa na mbadala wake visiwani. Mfano halisi wa hiki tunachojaribu kukiandika ni mfano wa1954 kuzaliwa Tanganyika AfricanNational Union (TANU), chama kilichoanzishwa Tanganyika kutokana naTanganyika African Association, kwa ajili ya kudai uhuru kwa upande waTanganyika. Zanzibar nako 1957 ilianzishwa Afro Shirazi Party (ASP), kutokanana kuungana kwa African Association na Shirazi Association na MwalimuNyerere alikuwepo kushuhudia uanzishwaji wa ASP, MBONA HAWA wasomi VISHOKA HAWASEMIkiundani hii historiahalisi ya siasa ya Tanzania???. 5. Pia wana-tume wazingatie kuwa miungano mingi dunianiimesambaratika na wasifumbe macho kusema kuwa kati ya mambo yaliyofanya hiyomiungano kusambaratika ni kuwa na serikali nyingi ambazo baadaye zinakosa utawala bora na kuwa kikomo cha utawala bora wa kisayansi inaozingatiachai of command kwa kuwa kila mtu kujiona anaweza kwenda mwenyewe? Mfano ni kuvunjika kwa muungano wa Malaysia naSingapore, China na Taiwan, Gambia na Senegal na mifano mingi ambayo historiaimeshudia ikivujika kama wa Korea Ksn na Korea Kzn nk
6. Tume hii ilipewa takribanshilingi bilioni 50 ili kufanya kazi, kuhoji watu na kutafsiri maoni yaokisayansi. Haitegemewi maoni yakeyatokane na taarifa ambazo ziliwahi kuandikwa hapo Zamani mfano NyalaliCommission au Kisanga Commission au Warioba Commission au Tanganyika LawSociety au Midahalo ya Katiba iliyokuwa ikiandaliwa pale Nkrumah Hall chuokikuu cha Dar-es-Salaam. Kufanya hivyo ni kuwanyima wa Tanzania waliowengikusikika. Kwa mshangao Tume imekiri kuwakuna wa Tanzania walitaka serikali mbili wengine nne wengine tatu. Lakiniyenyewe ikaamua kuchukua serikali tatu. Hii ni kosa kisayansi. Ilibidi kwanzaiainishe ni watu wangapi walisema tatu wangapi walisema nne wangapi walisemambili. Kamani kweli wanayotushauri basi wawe na ujasiri huo huo wa kunakiri maoni ya tumeya NYALALI NA KISANGA NA WARIOBA CORRUPTION COMMISSION WATUELEZE KWA NINI HAYOMAWAZO HAYAKUCHUKULIWA. Mbona hawatuelezi yaliyojiri wakati wa Jumbe na NjeruKasaka maana ilikuwa ni suala nyeti sana kama hilowaliloleta juu ya serikali tatu. Si busara kutumia taarifa ambazo zilitolewa na serikali hiyo hiyozikakataliwa hii ni kuleta kiburi cha kutaka kuilazimisha serikali mambo ambayoina sababu za msingi kuyakataa wakati huo ilipopewa hizo taarifa za Nyalali naKiasanga. SEHEMU YA PILI: · SERIKALIYA TANGANYIKA NA SUALA NYETI LA MUUNDO WA MUUNGANO WA SERIKALI TATU HAYAYANATOKEA WAPI?Tumeilisheheni wataalamu wengi wanaoheshimiwa sana nchinikutokana na umilisi wao mkubwa katika maeneo ya elimu waliyobobea. Lakini inaelekea hawakujisumbuakufanya utafiti wa kina juu ya sehemu hii iliohusu serikaliya Tanganyika na muundo mpya wa serikali tatu walioupendekeza. Hii inaonyesha wamekujana mawazo yao na mawazo ya vikundi ambavyo vimetajwa hapo mwanzo na kutaka kutulazimisha jamii yote ya wa Tanzania tuyaamini. Kwamfano;
  1. Suala nyeti la muungano. Inabainishwa katika tafiti mbali mbali ambazo tulitegemea Tume inayoongozwa na Jaji Warioba wazisome na kutupa mwongozo wa nini tujadili. Kwa watanzania wengi ambao hawakuwapo wakati muungano ukiasisiwa wangeweza kuelewa kuwa kuna kitu kinaitwa Article IV ambacho kwenye machapisho mbalimbali kinasema;
ArticleIV of the Articles of union had specified the reserved union matters. ThisArticle reads: “Thereshall be reserved to the parliament and Executive of the United Republic thefollowingmatters:(i) TheConstitution and government of the united Republic;(ii)External affairs;(iii)Defense;(iv)Police;(v)Emergency powers;(vi)Citizenship;(vii)Immigration;(viii)External trade and borrowing;(ix)The public service of the United Republic;(x)Income tax, corporation tax, customs and excise duties; and(xi)Harbors, civil aviation, posts and telegraph. Hapa tume ingeweza kutuambia tujadili matatizo ya muungano ilituyapatie ufumbuzi. Mtazamo wa serikali ya CCM katika kunusuru mijadala yakisiasa isiyokuwa na TIJA kwa watanzania zaidi ya kuwaongezea matatizo ya maisha nikuchunguza kama orodha ya mambo ya muungano inaweza kuwa ni sababu. Kuna watuwameonesha kuwa inawezekana chokochoko za muungano inatokana na mambo ambayohayakuwapo kwenye makubaliano ya awali kuongezwa kwenye orodha. Ama kamailivyotanguliwa kusemwa kuwa tatizo kubwa la muungano ni kutokutekelezwa kwamambo muhimu yaliyokubaliwa kuwa ni ya kimuungano. Kuna ukweli kuwa upande waZanzibar umekuwa una makundi ya watu tofauti tofauti waliokuwa siku zotewakidai kuwa muungano hauna maana kutokana na kupuuza kutekeleza Articles ofUnion. Kwa mfano ugavi sawa wa rasilimali fedha nk zilizotokana na mikopo yanje, misaada mbalimbali kama FIFA GOALS na rasilimali fedha zilizotakana navyanzo mbalimbali vya ndani ya nchi. Hii tulitegemea tume itueleza kinaga ubaga moja baada ya jinginelakini siyo kutuambia tu kuwa sasa mambo ya muungano yatakuwa saba. Nani kawapamamlaka kuamua mambo makubwa kama haya kwa niaba ya watanzania Millioni45?.
  1. Suala nyeti la Muundo wa Muungano: Muungano ni suala nyeti na tukufu ambalo ni lazima lilindwe kwa gharama yeyote ile kwa usalama wan chi yetu tukufu. Kwa kweli na mtu yeyote aneonekana kutaka kutikisa nguzo zake haina budi kumtolea uvivu ili kusambaratisha nguvu zake na kundi lake kwa kutumia rasilimali zenye gharama yeyote ile kwa maslahi ya taifa hili. Kama ilivyotanguliwa kuanishwa kwenye maandiko haya kuwa mifano ya mataifa kadhaa ambayo yamefuata serikali za shirikisho zimeenda na maji kwa kushindwa kusonga mbele kutokana na shida za utawala wa serikali za shirikisho. Hivyo Tume ilitakiwa kuwa ubunifu wa hali ya juu katika kufanya tafiti na uwasilishaji wa wanayoyaota mawazo ya watanzania ya kutaka serikali tatu. Udhaifu mkubwa katika taarifa ya rasimu ya katiba ni kushindwa kuwa wabunifu na kuchambua kwa kina muundo wa serikali. Kwa kiwango kikubwa uamuzi wao hautokani na maoni ya watu waliowahoji. Hii inatokana na ukweli kuwa mara baada ya kuchapisha taarifa kila mtu aliyehojiwa ameshangazwa na serikali tatu. Waliokataa sababu kubwa zaidi ya asilimia 90 ikawa ni kwamba Muungano utavunjika mara moja, ni gharama ambayo watanzania walipa kodi wata twikwa kuendesha serikali tatu badala ya kuelekeza fedha hizo kwenye barabara, shule na hospitali. Onyo hapa kuna wale wakosaji wanasema bora nchi iharibikiwe tukose wote. Hawa wanasaidiwa sana na coverage ya vyombo vya habari na ni hatari kwa usalama wa nchi hii. Wengi ni wapinzani na wana harakati ambao wanaishi hapa Tanzania lakini mishahara yao yote inatoka Ulaya. Hao wanasema bora Tanganyika ije na kwenye huu msafara kuna wanasiasa, kuna maprofessa walioshiwa hoja ambao wamekuwa wakiranda randa kwenye korido za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kujikosha kwa vijana wa kizazi kipya wasiowafahamu. Wengi wanatumia kofia ya kumnadi Mwalimu Nyerere. Lakini Nyerere gani angependa serikali tatu? Ni vinara wa makongamano na Majukwaa ya wahariri, katiba nakadharika LHRC kupitia live coverage ya vyombo fulani vya habari.
Hii inatoa wasiwasi nakutaka kujua kiini cha kushauri serikali tatu. Tukiingia kwenye literaturereview ambayo Tume ya Jaji Warioba tungetegemea iisome na kutupa mwongozo, tunabaini kuwa tangu wakati wa Nyerere kumekuwapo wana zuoni ambao wamekuwawakichokonoa chokonoa habari za Mungano na kuandika mambo yao mengine ni sahihimengine siyo sahihi. Lakini kwa kifupi wanataka kuhadaa kuwa chanzo cha Muunganoilikwa ni CIA ya marekani kutaka kuzuia wa Cuba wasiingie Zanzibar. Hatufahamuukweli wa hizo porojo lakini hata kama ni kweli hatunasababu ya kujua nakuziamini au kuaminishwa. Kwanza hao wa Cuba walikuwapo Tanzania Bara na ndiowalijenga shule ya sekondari Ruvu, Kilosa, Kwiro na hata Fidel Castromwenyewe aliwahi kuja Tanzania. Watanzania wengi walisoma Cuba, na hataMadaktari wengi wa Cuba walitibu wa Tanzania. Hadi sasauhusiano wa Tanzania na Cuba ni nzuri na hauhatarishi amani ya nchi hii Mawazo haya potofu juu yaMuungano na CIA yameonyesha jinsi gani baadhi ya watu hao walivyoshindwakubaini kuwa KUSOMA HISTORIA ya siasa za nchi hii. Bahati nzuri inaonekanakwenye taarifa nyingine kuwa kuna ushahidi wa harufu ya muungano hata kabla yamapinduzi. “Nyerere had theintention to unite Tanganyika and Zanzibar for many years back toIndependence …………… he dared to sent Ali. M.Tambwe and Bibi Titi Muhammed toassist ASP campaign as to facilitate his ambition…”
  1. Tume haikuzingatia athari za mapendekezo yake: Pamoja kuwa tume ina majaji na wasomi waliobobea na wanafahamu yaliyotokea juu ya Muungano wa Serikali za Shirikisho kama hii ya Warioba Model itakuwa ni sababu kubwa muungano kufa kama ilivyotokea kwenye baadhi ya nchi duniani, hapa kuna mifano michache.
Muungano wa Malaysia na Singapore ulidumu miaka miwili tu kutoka1963 mpaka 1965. Hii ilitokana na kufuata mfumo wa muungano kama hawawaheshimiwa wanaotaka Tanzania ifuate. Bunge la Malaysia lilikaa wakapiga kurana kusema hatutaki muungano basi ukafa kirahisi sana. China na Taiwanhakikueleweka pia walikuwa na muungano wao na serikali zao lakini leo hiihakuna kitu. Muungano wa Senegal na Gambia ulidumu miaka saba tu 1982 mpaka1989 4. Tumeimewakilisha Mawazo ya Wana-Tume na Makundi Fulani: Tume haikutendea haki watanzania wengi imechukua zaidi maono yaobinafsi na makundi fulani yenye ujanja ujanja wa kutaka kuamua mambo yawatanzania kutumia TV na vyombo vilivyo kwenye mtandao wa MCT kama magazeti na stesheni za radio binafsi na Mashirika ya wanaharakati. Kuna mchambuzi fulani wa masuala ya kisiasa aliandika hivi karibuni kuwa; TUMENimeangaliamjadala hivi karibuni katika moja ya vituo vya televisheni nchini, kuhusuMuungano na Tanzania tuitakayo, wazungumzaji wakuu wakiwa kutoka CCM, CHADEMAna Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS). v CCM kwa upande wake walitaka muundo wa sasa wa Muungano(serikali mbili), yaani Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Muungano. v CHADEMA wanataka Serikali tatu, yaani Serikali ya Zanzibar,Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Muungano. Lakini pia wapo wachachewanaoshabikia muundo wa Serikali moja.Hoja inayotolewa na CHADEMA na wenginewanaopendelea Serikali tatu (kikiwamo chama cha upinzani cha CUF) ni ukwelikwamba; kuna mambo ya Muungano, mambo ya Zanzibar na Mambo ya Tanganyika.
<!--if (window.adgroupid == undefined) { window.adgroupid = Math.round(Math.random() * 1000);}document.write('<scr'+'ipt language="javascript1.1" src="http://adserver.adtech.de/addyn/3.0/1332/4486816/0/357/ADTECH;loc=100;target=_blank;grp='+window.adgroupid+';misc='+new Date().getTime()+'"></scri'+'pt>');//-->
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kuwa kimekwenda visiwani Zanzibar, kuwapelekea wananchi serikali ya tatu. Kauli hiyo imetolewa jana visiwani humo na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, alipokuwa akizungumza na wazee wa jimbo la Uzini kabla ya kuzindua kampeni za kuwania ujumbe wa Baraza la Wakilishi. Alisema CHADEMA inawataka Wanzanzibari waamue aina ya Muungano wanaoutaka tofauti na huu wa sasa ambao umezusha manung’uniko makubwa. Aliongeza kuwa chama hicho kinaamini muundo wa serikali tatu yaani ile ya Tanganyika, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Muungano.
Hapa Tume itusaidie kujibu masuala yafuatayo walihoji watu wangapi, waliwapata vipi, profile zao zikoje na asilimia ngapi walisema nini na kwa nini? SEHEMU YA TATU KASORO NYINGINE ZA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA KATIBA MPYA
  1. Mfumo wa Utawala wa Serikali: inaonesha kuwa TUME imeshindwa kuweka bayana mfumo gani wa serikali wanataka Tanzania tuufuate Presidential System tunayoifahamu, au Parliamentary system au cocktail?
Ukiangalia Rasimu inaipa madaraka makubwa Bunge. Mpaka kuna kipengele cha Bunge kumuondoa Rais madarakani. Hii kwa nchi za kiafrika ni kutaka kutusambaratisha. Ni mawazo yanayoletwa kwetu na wafadhili wa NGO na WATCHDOGS zinazo fufuka kama Uyoga. Wanachofanya ni kutumia njaa za hao wana NGOs kama wakina Deus Kibanda, wakina Kajubi wakina Rakesh na sasa kuna wana habari nao wanapewa hizo pesa. Bosi mkubwa ni Baba Paroko na anaetumia helikopta mpaka uchaguzi wa madiwani?? ITV nayo inatusikitisha. Kwa hili suala tume iambiwe haliwezekani kwani Tanzania inafuata Presidential system. Hao waliowatuma hayo mawazo wengi wao wako huko Ulaya Magharibi tunafahamu wana Parliamentary system kwao ni valid kwetu NO. Tuache mambo ya kunakili kila kitu kutoka nchi nyingine bila kuangalia mazingira yetu. 2. Katiba imejaa vitu vingi. Lakini uzito wake unatofautiana sana na mambo mengine ya muhimu hayapo. Mfano mambo ya mahakama, maadili ya watumishi wa umma na viongozi na rushwa yameelezwa kwa kirefu bila sababu ya msingi. Tunajiuliza je haya ndiyo mambo ya msingi ya kuwasaidia wa Tanzania waliowengi?? Tusingependa wa Tanzania waendelee kushika tama na kukaa juu ya vinu wakituangalia tulio mijini tukiendelea kuukata. Yawezekana kuna upendeleo wa wana-Tume wengi kuwa wanasheria na viongozi wastaafu au waliowahi kufanyia kazi mambo ya rushwa na walijisahau wakapoteza mwelekeo wa adidu za rejea. Mfano wa vitu hivyo ni vilivyokuwemo ndani ya Azimio la Arusha. Hata kama mambo haya ni muhimu kuna impression kuwa yanaeelezwa kwa zama zilizopitwa na wakati. Mambo ya miiko ya uongozi tuwe makini. Tusitake tu unafiki wa kusema tumeua Azimio la Arusha na kuanzisha la Zanzibar, sasa tume inakuja kuokoa jahazi na kuirudisha Tanzania kwenye mstari. Huu ni mtazamo wa kinafiki kwa baadhi ya wanazuoni na wanahabari ambao siku za karibuni wamekuwa wakitafuta umaarufu kwa kulitaja sana Azimio la Arusha na kigoda cha Mwalimu Nyerere, lakini ukiangalia ni kutafuta public sympathy isiyo na evidence. Kwanza hawafanani na Nyerere kwa vitendo na waliowengi ni mashabiki wa CHADEMA, ni maswahiba wa mitandao ya kikoloni ikiwemo consetvarive union ambayo Nyerere mwenyewe alipambana nayo na kuishinda wakati ikiwasaidia RENAMO na Makaburu kule Zimbabwe na Afrika ya Kusini. Itakuwa ni ndoto leo kuweka miiko ya uongozi ambayo siyo realistic na haitekezeki. Kwenye Rasimu wanazungumzia watumishi wa umma wasiwe na hisa kwenye makampuni wakati sheria za nchi zimeshabadilika tuna masoko ya hisa tuna uchumi huria na kuna sababu za msingi kuwa nazo. Ukiwabana kupitiliza watumishi wa umma una risk kuwa watu wenye uwezo ambao hawataki shida wataamua kufanya kazi sekta binafsi na labda nchi za nje kama ilivyokuwa wakati huo wanaotaka kuturudisha ambapo wataalamu wengi waliamua kwenda Botswana, Namibia, hata Ulaya na Marekani. Jamani hatuingalii dunia hata viongozi wa Chama cha Kikominist cha China wanafanya biashara halali itakuwa sisi, hata familia ya Rais wa Zamani wa Marekani George walker Bush inafanya biashara halali na hata mgombea wa Chama cha Republic ambacho ni Grand Old Party (GOP) Senata Mitt Romney ni mfanya biashara maarufu ndani ya Marekani, kampuni zake zimejaa nchini China zikifanya biashara. Tume italeta rushwa ikiwanyima viongozi wasifanye biashara. Kilichotakiwa ni kuweka Sheria ya Kikatiba ya kuwabana viongozi na kuwawekea mashariti ya ufanyaji biashara na kazi za Serikali. Kwa mfano kama kiongozi ana kampuni ambayo inaomba tenda ya kutoa huduma serikali ndani ya kitengo ambacho yeye anaongoza, iweje? Lakini si kuwakataza, ukiwakataza wataingia kwenye rushwa kubwa kubwa za kuhatarisha amani ya nchi. 3. Kuhusu rushwa: Ndani ya rasimu ya katiba mpya kuna mambo mengi yametoka kwenye ile Tume ya Kwanza ya Mh. Jaji Warioba iliyopewa kazi ya kuchunguza mambo ya rushwa. Kwanza hiyo ropiti ilikuwa na sababu zake kwa hiyo haikuwa sahihi kuinakili kama ilivyo na kuiweka kwenye Katiba. Hata kama ina mantiki nimeona kwenye Rasimu wanazungumzia kuwa mtumishi akipewa zawadi aipeleke kwa Katibu Mkuu Kiongozi, lakini mazingira na aina ya zawadi vinatofautiana na nani anamfuatilia nani na kuwa na uhakika nani anafanya nini nk, hii itakwa ni vigumu.
  1. Haki za Raia: Ni fikira ya kila mtu kuwa Rasimu hii haijitoshelezi katika eneo hili. Inazungmziwa juu juu tu na haki ni nyingi zingine ni contradictions. Elimu haiwezi kuwa ni haki isiyotafsiriwa. Haya ni mambo ya msingi na kuyaweka kwenye wajibu wa Serikali. Pia hapa tunapata shida maana hii imekuwa ikiimbwa kila mara na Slaa na wana majukwaa eti ohoo watanzania mnahaki ya kuihoji serikali kwa nini hamkupatiwa elimu? Wote tunajua kuwa elimu ya primary school ni ya lazima. Ukiweka kwenye katiba haki kama hizi uwe muangalifu usije ukajikuta unadaiwa kitu ambacho hauna uwezo nacho. Nadhani nivema kutafuta namna ya kuiweka.

  1. Mgawanyo wa Rasilimali: Kuna mambo ya msingi kwa wananchi ambayo katiba inatakiwa iyaangalie. Mfano sasa kuna kelele za rasilimali. Kwanza lazima katiba itamke wazi kuwa rasilimali zote ni mali ya wa Tanzania wote. Pia kwa wawekezaji ni lazima asilimia 30 ya mavuno ya rasilimali yabaki nchini au thamani yake. Mfano tumekuwa tukivuna tani 50 za dhahabu kila mwaka, katiba inaweza kusema angalau tani 15 lazima zibaki nchini wauziwe Masonara na Benki Kuu. Hii itakuwa na faida kwa masikini wengi kuliko mambo ya mamlaka, maadili, haki na tawala yaliyojaa kwenye rasimu iliyowasilishwa.

  1. Rasilimali Ardhi: Kuna hatari ya nchi kupoteza ardhi kupitia multinationals na land grabbing via FDIs. Rasimu ya Katiba haioneshi ni kwa jinsi gani ardhi yetu imelindwa. Nivema kusema ni marufuku mtu wa nje kuwa na ardhi Tanzania na kuwa na Land Lease ya zaidi ya miaka 20. Hivi sasa kuna uwekezaji unakuja na kusema land leass ya miaka 50, hii ni sawa tu na kununua ardhi kwani wa Tanzania waliopo sasa baada ya miaka 50 ni wachache sana watakao kuwapo. Hii iingie kweny rasimu.

  1. Katiba Mpya iende smabamba na Uchumi wa Kisasa: Uchumi wa Tanzania hivi sasa umeshikiliwa na sekta binafsi, informal sector na biashara. Lakini rasimu inaendeleza yale yale ya wakulima na wavuvi kwa mkazo. Hii ibadilike na pia mipango ya maendeleo hasa miaka mitano na 10 iingizwe kwenye katiba ili kuifanya serikali kila mara ilazimike kuwa na mipango. Haya ni muhimu kama vile walivyochukua nafasi kuubwa kuelezea mahakama.

  1. Idadi ya Wabunge ni Kituko: Katika rasimu idadi ya wabunge inayopendekezwa ni kituko. Labda tume itoe tafsiri mpya ya kazi za wabunge. Inataka kuturudisha miaka 50 nyuma. Tanzania ina wilaya zaidi ya 130 leo hii inasema mbunge mmoja kwenye mkoa mwanamke na mwanaume. Hii wameitoa wapi duniani?? Lengo ni uwakilishi kweli?? Hata suala la elimu siyo vema kuwabana sana watu. Hivi sasa siyo majungu zaidi ya asilimia 70 ya wabunge wa CHADEMA hawana elimu ya chuo kikuu mpaka Mbowe, Mnyika, Lema, Sugu, na wengine wengi. Je TUME imegundua nini kwenye viwango vya elimu.
SEHEMU YA NNE HITIMISHO NA MAPENDEKEZO MAPYA
  1. Muundo wa Muungano: Muundo wa Serikali tatu utaliangamiza taifa. Utakuwa ndio mwisho wa muungano. Hiyo tusijidanganye maana tumeona Malaysia na Singapore, Senegal na Gambia na mifano mingine. Tuangalie namna ya kuondoa kero za muungano. Tubaki na Serikali zetu mbili maana hapo hawa wanaomuimba Nyerere tuwaambie tunamuenzi kwa yale ambayo mpaka anakufa alikuwa akiyapigania kama ya muundo wa sasa wa muungano na isiwe ni unafiki tu. Kuna uhakika mkubwa hata kama angekuwa hai leo, mambo yote angewaachia kuyajadili na kufanya mtakavyo, lakini hili la muungano asingekubali angekuala na hao vishoka sahani moja mpaka angewateketeza wote bila kumuacha hata mmoja. Na labda hata Jaji Warioba ingekuwa ndio mwisho wake wa kuwepo kwenye medani za siasa za Tanzania. Kwani kwa mapendekezo haya asingemsamehe yeyote aliyehusika. Zanzibar isikilizwe na wanayoyataka na kuyalalamikia yafanyiwe kazi iwe aibu kwa hao mbwa koko wanaosubiri muungano ufe. Wengine ndo wanashabikia Mtwara na Southern States. Labda Tume itumie ujasiri kusema imeangalia kuwa Tume zote zilizopita zilipendekeza serikali tatu kusema kwa nini hazikusikilizwa. Hatuja sahau kwa nini Aboud Jumbe alipelekea kujiuzulu ni kile kitendawili cha 1+1 ni 3 alichoshindwa kumjibu Mwalimu Nyerere akasema 3. Wakaja wale waliojiita G55 hatuna shaka kama kwenye hii tume hawamo nao wakaja na jibu la 3 wakaenda na maji. Vipi wakina Kolimba na Malecela walipoambiwa hawamsaidii Rais. Nini msimamo wa Nyerere katika haya tume iwe wazi pia kuliko kukimbilia taarifa za jaji Kisanga na Nyalali. Nakumbuka msimamo wa CCM wakati Tume inayoongozwa na Mh. Jaji Warioba inakabidhiwa hadidu za rejea ulikuwa Muundo wa sasa wa muungano usijailiwe wala kutafutiwa maswali yeyote. Nia ya CCM ilikuwa Tume ikita ngivu zake kutafutia ufumbuzi juu ya kero za muungano wetu huu mtukufu na si vinginevyo. Msimamo wa CCM ni pamoja na msimamo wa Rais waJamhuri ya Muungano ambaye ni mwana CCM na Mwenyekiti wa Chama. Na ikumbukwe kuwa Jaji Warioba ni mwanaCCM, swali kuu kwake kashindwa kuitetea nafasi ya chama chake, kashindwa vipi kutetea msimamamo wa Mwenyekiti wake ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Nchi? Jaji Warioba na Tume yake wameboronga kuliko ilivyotegemewa kwenye suala hili la mfumo na muundo wa sasa wa Muungano wetu adhimu kabisa. Makosa haya kwa watu wanaopigania muungano wetu hausemeki na wala hausameheki kirahisi. Wangeweza kuhoji U-CCM wa Jaji Warioba na uadilifu wake kwa Chama na Serikali yake.

  1. Vipindi vya Urais kati ya Tanzania bara na Zanzibar: Katika kushughulikia kero za Muungano Tume ingejaribu kupendekeza kupitia Rasimu yake kuwa baada ya vipindi vya viwili viwili vya marais wa wawili wa Tanzania bara basi nafasi hiyo iende Zanzibar kwa rais mmoja atakaepatiwa vipindi viwili vya miaka mitano mitano. Kwa mfano Kupitia CCM, baada ya Tanzania bara kupata fursa ya kutoa Marais wawili (Rais Mkapa na Rais Kikwete) waliokaa kwa kipindi cha miaka 20, basi Wa Zanzibar wapate nafasi hii baada ya Rais JK watoe Rais atakae kaa kwa miaka 10. Kwa ufupi wa maelezo haya ni kuwa kwenye kipindi cha miaka 30 basi Bara wapate miaka 20 ya kuongoza nchi na 10 iende Zanzibar. Jambo hili lingefanyika na kuwekwa kwenye katiba basi tusingepata tabu leo ya kuona makundi mengi yakigombana kutafuta ujiko ndani ya mitaa yetu kwa minajili ya kupata Urais 2015. Kila mtu angetupa jicho upande wa zanzibari leo kuangalia ni mtu gani miongoni mwetu wana CCM ambaye anaweza kuwa amiri Jeshi Mkuu wa kuchukua kijiti cha Uongozi adhimu wan chi kwa minajili kulinda uhuru, amani na usalama wan chi yetu tukufu iliyoundwa na muungano wa watu wenye mtizamo mmjoja. Tunaomba viongozi wa juu wa Chama na Serikali, wakiungana na wale wa Vyombo vya juu vya Ulinzi na Usalama wan chi hii wamuulize haya kayatoa wapi? Mawazo haya yanamuwakilisha nani? Chadema na CUF hawa ni wasaliti wakubwa waanagaliwe sana. Mapendekezo haya siyo tu yametikisa nguzo za muungano wetu bali yamezivunja nguzo hizi, kwa hiyo Muungano umepwaya na una nyufa nyingi na za hatari kuvunjika.

  1. Nini hatari ya Kuvunjika Muungano: Tuna mkumbusha Jaji Warioba kuwa siasa za Zanzibari ziko salama kwa kwa ajili ya Muungano ambao umeimarika. Kama Muungano ukivunjika leo basi Zanzibari itanuka damu ya ajabu. Nawaomba wakuu wa Chama na Serikali na wale wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wan chi warejee Mkutano wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika Zanzibar (Unguja) tarehe 04.11.2012. Kumbukumbu za Mkutano huu ziko kwenye CDs Ambazo sisi tunazo kama hawana sisi tutawapa waone wenyewe. Katika mkutano huo CCM walikuwa wanajibu kauli mbalimabli zilizokuwa zimetolewa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, wana CCM hawakuuma maneno kwa kauli za Matusi ambazo haziwezi kutukanika. Katibu wa Vijana wa Wilaya ya Mjini Magharibi aliweza kusema waziwazi kuwa wana Uamsho na viongozi wa CUF hasa maalimu Seif na Jussa wanakazwa au wanatiwa. Matusi haya yalipokuwa yanatolewa kulikuwa na nderemo zikiambatana na shamra shamra na vifijo na kadhalika. Kwa jinsi walivyokuwa wanazidi kutukana ndio furaha za wana CCM ziliwafanya waendelee kuwashangilia wasemaji, hasa huyu kijana Katibu wa Vijana na Mgeni wa heshima wa Mkutano huo ambaye alikuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Mzee Borafia. Mkutano huo ulifanywa siku mbili kabla Mkutano Mkuu wa CCM taifa wa taerehe 06.11.2012. Ni matumaini yetu kuwa Tume ya Jaji Warioba italiangalia hili kwa makini na kuibadilisha Rasimu kabla haijaenda kwa wananchi kujadiliwa na kutolewa mapendekezo.

  1. Kupoteza Legacy ya Utwala Bora wa Rais JK: Muungano ukija kuvunjika kwa ajili Muundo mpya wa Muungano unaopendekezwa na Rasimu itakuwa na athari kwa utawala wa mpendwa wetu Mh. JK . Tunawashauri wasaidizi wa karibu wa Mh. JK wasishindwe kumshawishi ili atumie kila linalowezekana aipige chini hii Rasimu ili kama watu wanataka muundo huo wa Muungano ambao ni hatarishi kwa uhuru, usalama na uhai wa taifa letu tukufu wasubiri rais mwingine asiye yeye. Kwani huo sio msahafu lakini kwa sisi ni wapenzi na wanachama wa CCM hatutopenda hili litokee kwa Kiongozi yeyote wa CCM anayeongoza nchi hii. Naogopa kuwa legacy ya mpendwa Rais wetu JK kuja kufananishwa na ile ya Rais Gorbachev wa USSR ya zamani iliyosambaratika.

  1. Tume ipewe muda irekebishe rasimu kabla haijaenda kwa wananchi. Hii ni kwa Mh Rais aliyewakabidhi kazi atengeneze jopo la wataalamu makini na waadilifu kutoka Bara na visiwani waipitie Rasimu na kwarudishia mapendekezo wana TUME ili warekebishe hasa yale mambo ambayo yanweza kuhatarisha amani, usalama na uhai wa Taifa hili lilioundwa na Muungano mtukufu wa Serikali tukufu za Zanzibar na Tanganyika KABLA YA KUWASHIRIKISHA WANANCHI KWENYE MJADALA wa rasimu ya kupata Katiba Mpya.

  1. Articles of Union: TUME IKUMBUSHWE KUWA HAINA UWEZO WA KUGUSA NAKUBADILISHA MAMBO YALIYOKWENYE MUUNGANO. IMEYAPUNGUZA NA KUBAKI SABA KWA KUTUMIA KIGEZO KIPI? KWA RUHUSA YA NANI?? HAYA YANAONDOAJE KERO ZA MUUNGANO??

  1. Kwa sasa kuna umuhimu wa kufuatilia kwa karibu nyendo za Tume, watu wanao-infulence na mitazamo yao huwezi kumuamini kila mtu tuna wakina GORBACHEVU wanataka tuingie kwenye historia ya kuibadili Tanzania mwelekeo. Inashangaza MCT kupewa kipaumbele kwenye maoni ya Katiba kuwemo kwenye Mabaraza ya Katiba. Ni wazushi na wasaliti wanaodunduliza pesa za wafadhili kuja ku BRAIN WASH WATANZANIA. Kimsingi MCT si chombo cha kubeza. Kina watu wachache wanaoweza kuwa hatarishi kwa namna moja au nyingine. Baadhi ya wajumbe wa bodi zao wanaandika makala katika magazeti tata kama vile Mawio au Mwanahalisi ambalo kwa kiburi limeamua kurudi mitaani kwa kubadilisha jina. Wananchi wa kawaida tunajiuliza nani anawapa kiburi magazeti kama haya?? Kuna kila dalili kuwa haya magazeti ni miradi ya watu wenye nafasi katika nchi ambao labda vyombo vilivyopewa mamlaka kusimamia habari ikiwemo wizara wanawaogopa. Kama si kweli inashangaza kuona wanaandika habari ambazo haziwezi kuvumiliwa na mtu yeyote Yule kwa sababu yeyote. Ushauri kwa Waziri husika ni kufungia haya magazeti na kuwafanya waandishi wa habari wajue kuwa hawako juu ya sheria. Ikisuburiwa mpaka 2015 haitawezekana kuwanyamazisha kwanza watakuja na dharau kubwa kwa serikali hivyo maamuzi YOTE yafanyike sasa. Kwa mawaziri wanaokwenda mwendo wa kinyonga ni wa kati wa kuwapumzisha na kutafuta wakina Magufuli, Muhongo, Mwakyembe, Kagasheki na Tibaijuka wengine wapo wengi tu CCM kina Hazina kubwa.
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika
Ahsanteni Sana
 
Hapa mada kubwa ni Muungano: Tukubali kwamba tangu wakati wote katika muungano, serikali mbili imekuwa kero kwa pande zote mbili na kama kuna mambo ya kufikiria kuweka sawa basi na hayo mambo hayarekebishiki na ndiyo maana watu wamependekeza kwa tume serikali tatu. Bila kumung'unya maneno muda huu tunapashwa kuamua kuwa na serikali moja au muungano kuvunjika.
 
Back
Top Bottom