Rashidi Lema na hatima ya mashahidi katika mahakama za Tanzania!

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,598
Kufuatia hukumu ya Jaji Masati ambaye amewaachia watuhumiwa wote kwamba hawana hatia ya mauaji, na kwamba hakuna mtu ambaye ameithibitishia mahakama bila kuacha chembe ya shaka kwamba watuhumiwa waliua; na kwamba ushahidi wa Lema (ungamo) ni batili kwa kuwa hakupata nafasi ya kuutetea mbele ya mahakama. Na kutokana na maoni ya utetezi kuwa Lema alikufa na ushahidi wake ambao ndio ungethibitisha wapi mauaji yalifanyika, nani aliyafanya na kwa amri ya nani. Kwa mazingira ya kesi hii, kifo cha Lema kilikuwa cha kawaida au ni mpango maalumu wa kuinyima ushahidi mahakama? Na je haiwezekani kuanzisha ujunguzi maalumu kuhusu kifo hicho sambamba na kumtafuta muuaji? Nimepata maswali mengi sana ila nahofia sasa kwamba kwa mwenendo wa kesi nyingi katika mahakama zetu itakuwa ngumu kupata watu wakaojitolea kuwa mashahidi.
 
Dar City

pole kwa maswali yasiyo na majibu. Nami pia nimekumbwa na tatizo hilo. Jana binafsi nilipata mshtuko kwa hukumu hiyo.

Nafikiri hapa ningekuwa nimambiwa nitoe hitimishi ningesema yafuatayo:

- Ofisi ya DPP ivunjwe naye ashtakiwe kwa kuwa mzembe na kuiletea hasara serikali kwa kushindwa kumkamata muuwaji kwa muda huo wote. Pia watendaji wa ofisi hiyo waangaliwe taaluma zao kama zimekaa vizuri sababu wataendeshaje kesi muda wote huo bila kujua watashindwa. Unless waniambie wameshinikizwa.

- IGP ajiuzulu sababu ofisi yake imeshindwa kuwalinda usalama wa raia ambayo ndio majukumu yake makuu.

- Serikali iwajibike kwa kushindwa kuwalinda raia mpaka wanauwawa na watu wasiojulikana.

- Tume ya awali iliyoundwa kuchunguza sakata hili itoe maelezo kwa nini uliudanganya umma kwamba zombe aliuwa. Otherwise waje na strong defence ya ripoti yao.

Namalizia: UDIKTETA MARA NYINGINE UNAFAA
 
MUNGU NDIYE HAKIMU WA KWELI!! Kwa yote yaliyotokea, mimi naamini kuwa Mungu anayafahamu na kwa kweli hukumu yake itatokea hapa hapa duniani! Hakuna atakayeishi milele maana sote sisi ni wapitaji HATUNA MJI UDUMUO!!!
 
MUNGU NDIYE HAKIMU WA KWELI!! Kwa yote yaliyotokea, mimi naamini kuwa Mungu anayafahamu na kwa kweli hukumu yake itatokea hapa hapa duniani! Hakuna atakayeishi milele maana sote sisi ni wapitaji HATUNA MJI UDUMUO!!!

Edwinito,

Mimi ni muumini ninayemwamini Mungu. Lakini sitaki na kamwe sipendi tabia ya kumtwisha Mungu mizigo inayotokea kwa sababu ya uzembe wetu. Kama serikali haiwezi kuwajibika kwa sababu wanazojua wao, ni jukumu letu kuifanya iwajibike au kuitoa tukaweka nyingine itakayotimiza matakwa yetu kama wananchi wa Tanzania. Hii inahusu hata mihimili mingine ya dola. Tukimkabidhi Mungu uzembe wetu tunajichimbia kaburi zetu wenyewe. Na haya tunayoshuhudia ni matunda ya ushenzi wetu. Huu mwanzo tu, ngoma bado haijaanza!
 
Mkuu DC, maana ya maneno yangu ni kuwa yeye mwenyewe (Mungu), kupitia vitabu tunavyoviamini alisema kisasi ni cha kwake yeye, mimi ninaamini katika HAKI yake! Jumapili tulikuwa somo zuri lililohusu HAKI, neno lilisema..."HAKI HUINUA TAIFA, BALI DHAMBI NI AIBU YA WATU WOTE"! Narudia tena hakuna atakayeishi milele, fikiria tangu umepata ufahamu, wangapi walikuwepo (wema na wabaya), lakini leo hii hawapo! Simtwishi Mungu mizigo inayotokea, isipokuwa nimesema YEYE NI HAKIMU WA KWELI NA ATAAMUA KWA HAKI! Yeye hakawii wala hawai, anakuja kwa WAKATI wake!
 
hapa hakuna sababu kabis aya kumlaumu huyu hakimu hata kidogo, hakimu hata kama anajua una kosa lakini haukumu kwa hisia zake bali kwa ushahidi unaowekwa mahakamani, sasa kesi imekuja bila ushahidi ulioshiba hata kama wewe ungekuwa ni hakimu ungefanya nini?
tatizo kubwa liko kwa DPP, pamoja na jeshi zima la police kwa kushindwa kupeleka ushahidi unaoleweka mahakamani
 
Yani haiwezi mwingia mtu yeyote akilini kuwa watu wote wale wameachiwa huru tujiulize wale askari walioenda kupika risasi kule tegeta na kumletea zombe maganda walikuwa wanafanya hili iweje? tujiulize kulikuwa na kundi la askari walikwenda msitu wa pande kufanikisha azma ya mkubwa au inamaana wakikubaliana watu watatu kwenda kuua mmoja akashika miguu mingine mikono mwingine akachinja kwa Sharia za Tanzania muuaji ni yule aliyechinja
Ohoh my God! Mungu hirehemu hii nchi yaangalie machozi ya waja wako....!!
 
nitashangaa sana endapo wananchi wa Mahenge hawatawaadhibu CCM, Dr. Ngasongwa na Celin Komban ktk uchaguzi 2010.
 
hapa hakuna sababu kabis aya kumlaumu huyu hakimu hata kidogo, hakimu hata kama anajua una kosa lakini haukumu kwa hisia zake bali kwa ushahidi unaowekwa mahakamani, sasa kesi imekuja bila ushahidi ulioshiba hata kama wewe ungekuwa ni hakimu ungefanya nini?
tatizo kubwa liko kwa DPP, pamoja na jeshi zima la police kwa kushindwa kupeleka ushahidi unaoleweka mahakamani
unadhani jeshi na DPP wameshindwa kupeleka ushahidi?si ndio hapo yanakuja maswali mengi yasiyo majibu hiyo ni mipango ya kulindana ambayo imesukwa vizuri sana.si DPP,washauri,polisi hakimu wala nani wote wameshirikiana kupindisha sheria ili hao jamaa wawe huru,wameshindwa kupeleka ushahidi wa maana kisha wakawahi kwa wingi kwenda kuwachukua mabosi wao mahakamani utafikiri msafara wa harusi,ndo hivyo tena changa la macho lishapigwa na tujue kabisa wanyonge hatuna haki bongo hata tufanyeje na miuaji isharudi mtaani na wataendelea kuua kisingizio kile kile wameua majambazi.
 
jaji hakutaka kusikiliza ushahidi/ungamo la lema kwa sababu zake mwenyewe. alijua lema amelemewa na alikuwa ana kuja mahakamani kwa kusaidiwa na washitakiwa wenzake kushuka kutoka kwenye karandinga. hata baada ya mashahidi wengine kumaliza kutoa ushahidi angeweza kusikiliza ushahidi wake pamoja na ugonjwa wake. mara ngapi mahakama huwa zinahamia hospiltali. badala yake masati aliagiza kesi iahirishwe hadi lema 'atakapopona' na ndio kesi ikaisha. umuhimu wa ushahidi wa lema masati alikua anaujua, alifanya makusudi kuruhusu lema afe na ushahidi wake. miafrika ndivyo tulivyo

macinkus
 
jaji hakutaka kusikiliza ushahidi/ungamo la lema kwa sababu zake mwenyewe. alijua lema amelemewa na alikuwa ana kuja mahakamani kwa kusaidiwa na washitakiwa wenzake kushuka kutoka kwenye karandinga. hata baada ya mashahidi wengine kumaliza kutoa ushahidi angeweza kusikiliza ushahidi wake pamoja na ugonjwa wake. mara ngapi mahakama huwa zinahamia hospiltali. badala yake masati aliagiza kesi iahirishwe hadi lema 'atakapopona' na ndio kesi ikaisha. umuhimu wa ushahidi wa lema masati alikua anaujua, alifanya makusudi kuruhusu lema afe na ushahidi wake. miafrika ndivyo tulivyo

macinkus

Poa mkuu,

Sasa kama mtu muhimu anaachwa afe (sina hakika kweli kama alikufa kifo cha kawaida au aliuawa) na kwa hiyo ushahidi wake ukapotea; kuna haja kwa mtu yeyote kuungama? Na kwa mazingira ya kesi hii na kama kifo hiki siyo cha kawaida (i.e Lema aliuawa), je kuna usalama kwa mashahidi wanaoitwa kuisadia mahakama iweze kutoa hukumu za haki?
 
yule aliyeua sijui Afande nani atafutwe kwa nguvu zote na kifo cha lema kichunguzwe,

hapa kuna moshi mweusi
 
haya Mahakimu ndivyo yalivyo . Hata ya usukumani yanahongwa ma'ngombe yanapindisha sheria . hiyo haishangazi kwa Dar ambako mafisadi yamejaa kila kona .
 
Kifo cha shahidi muhimu sana kwenye kesi ya Zombe, Rashid Lema, kweli kinatatanisha japokuwa hatuwezi kusema moja kwa moja kama aliuawa au la! Hata hivyo tusiache wala kuogopa kutoa ushahidi ili tuache haki itendeke. Pia ukikataa kutoa ushahidi ni kosa la kuidharau mahakama (contempt of court), kwa hiyo tusije tukakwepa jukumu hili muhimu la kutoa ushahidi tukaingia kwenye matatizo na tukahukumiwa na mahakama kwa ajili hiyo!
 
Back
Top Bottom