Rais wa Tanzania na Kiingereza, wa Ujerumani na Kijerumani!

Sijui kwanini sisi Watanzania hatuthamini vilivyo vyetu, ikiwemo lugha yetu adhimu ya Kiswahili. Lugha yenyewe tunayoing'ang'ania ya Kiingereza wengi wetu hatuimudu vyema. Baadhi ya ofisi za serikali pia utakuta wanafanya mawasiliano ya barua baina yao kwa kutumia Kiingereza na kuiacha lugha ya Kiswahili.

Jambo hili huwa linanikera sana. Ndio maana mimi huwa nikipokea barua ya kiofisi ambayo najua imetoka kwenye taasisi/ofisi ya Kitanzania na watumishi wake ni Watanzania na inahitaji majibu huwa naijibu barua hiyo kwa Kiswahili.

Watanzania wenzangu tuamke tuache kuwa watumwa wa lugha za watu. Mungu katujalia kuwa na chetu, basi tukienzi na kukitunza.
 
Ni shida ya huyo mjerumani kutokujua kingereza. Sasa mjerumani mzima hata kingereza hajui anakuja kuongea kijerumani chake.
 
kikwete alishadharau vitu vya kwetu ndio maana hawezi kaa zaidi ya mwezi nchini, hawezi tibiwa nchini, anapenda na kuthamin wawekezaji kuliko wazawa hata wahujumu uchumi wa nchi! juz kadharau pesa zetu anaona za madafu!
 
Wakuu,
Katika dhifa ya kitaifa aliyondaliwa Rais wa Ujerumani, Jk kwanini hakuhutubia kwa Kiswahili chetu, ilihali mgeni wake kahutubia kikwao? Wapi kuthamini vya kwetu jama!

Achana na wajeruman, wako smart sana na vitu vyao, TZ tunayumba tu hatuna uelekeo. Na sio kwamba hawajui kiingereza, wanajua sana, but hawataki kuongea, wanajivunia vya kwao tu.
Mimi nafanya nao shule huku Ujeruman, but kila kitu iwe matangazo, ni lugha yao tu, hakuna kusema eti kuna foreigner huku, foreigner utajua mwenyewe nini ufanye kuhakikisha unajua kilichotangazwa.
Sasa wabongo, kiingereza chenyewe hovyo, bado mtu yuko kwako, lugha yako unaiona hovyo, yaani bure kabisa.
 
Hata katiba inayopendekezwa bado haijachapishwa na mpiga chapa wa serikali mpaka kwanza iandikwe kwa kingereza kisha itafsiriwe kwa kiswahili!
 
Hata katiba inayopendekezwa bado haijachapishwa na mpiga chapa wa serikali mpaka kwanza iandikwe kwa kingereza kisha itafsiriwe kwa kiswahili!

Ni aibu kudharau utamaduni wako then ukatukuza utamaduni wa wenzako!
 
Ni shida ya huyo mjerumani kutokujua kingereza. Sasa mjerumani mzima hata kingereza hajui anakuja kuongea kijerumani chake.

Mkuu mwache aongee tu kijerumani chake maana kimempa mafanikio makubwa tangu enzi izo na kama kuendelea walishaendelea wenzetu tangu miaka iyo wewe unaeongea icho kiingereza umepata maendeleo gani mana hata kutengeneza sindano atuwezi kazi kulalamika njaa tu na kukinga vibakuli kuomba misaada.
 
Sijaona tatizo kuongea kiingereza. Tatizo ninaloliona ni sisi Watanzania kukariri kwamba kwasababu iki hivi basi inatakiwa kwenda hivi.



hauna uzalendo. Kiswahili ni lugha yetu(lugha ya taifa) kama taifa lina lugha yake kwa nini lisiitumie badala yake kung'ang'ana na lugha ya kigeni? Kiswahili ni kibantu.
 
hauna uzalendo. Kiswahili ni lugha yetu(lugha ya taifa) kama taifa lina lugha yake kwa nini lisiitumie badala yake kung'ang'ana na lugha ya kigeni? Kiswahili ni kibantu.
 
Nakumbuka alikuja Rais wa china aliongea kichina lakini rais aliongea kingereza ni aibu sana. Jiulize watu wangap wanajua kichina kulinganisha n kiswahil dunian tunapuuzia tunafikir ni vitu vidogo hiv ni vitu vya muhim sana kama taifa tatizo hatuna dira tupotupo tuu. kama mgeni ni Muingereza angeongea 'kingereza chake lakini kwa jana angeongea kiswahili hata kama ni maskini inaonyesha unajithamini na kujiamini hata wenyewe wanapenda tujidhamini na tutaheshimika
 
Huwezi kuamini mahakamani Jaji/Hakimu wanaposikiliza kesi huandika kwa kiingereza hata kama waliombele yake wanaongea kiswahili!
 
Nakumbuka alikuja Rais wa china aliongea kichina lakini rais aliongea kingereza ni aibu sana. Jiulize watu wangap wanajua kichina kulinganisha n kiswahil dunian tunapuuzia tunafikir ni vitu vidogo hiv ni vitu vya muhim sana kama taifa tatizo hatuna dira tupotupo tuu. kama mgeni ni Muingereza angeongea 'kingereza chake lakini kwa jana angeongea kiswahili hata kama ni maskini inaonyesha unajithamini na kujiamini hata wenyewe wanapenda tujidhamini na tutaheshimika

mr somji ukweli kichina kina wazumgumzaji wa asili.kuzidi kiingereza au kihispania au hata kifaransa
kwa hyo sio ajabu aongee kichina .lakini jakaya kiingereza chenyewe broken bado anang'an'ania tu bora mkapa alikuwa fluent
 
Ramon sawa lakini me simlahumu jk kutokua fluent English yake kwasababu siyo mwingereza na watanzania wanatakiwa wabadilike kingereza ni lugha siyo akili na siyo lazima mtanzania ajue fluent kwan lugha yake eti mtu akikosea anachekwa ni ujinga na unajita msomi jiulize wajeruman wangap wanjua kingereza.. kujifunza siyo mbaya lugha ili mradi maelewano baina y watu wanaowasiliana tu
 
Mkuu mwache aongee tu kijerumani chake maana kimempa mafanikio makubwa tangu enzi izo na kama kuendelea walishaendelea wenzetu tangu miaka iyo wewe unaeongea icho kiingereza umepata maendeleo gani mana hata kutengeneza sindano atuwezi kazi kulalamika njaa tu na kukinga vibakuli kuomba misaada.

Ni kweli na sawa kabisa. Na vile vile Rais achwe azungumze vile aonavyo kwake ni sawa, badala ya kila mara hili kila mara lile. Lugha yoyote utakayotumia kama ni utajiri utaendelea kuwepo kama ni umaskini utaendelea kuwepo tu.
 
Wakuu,
Katika dhifa ya kitaifa aliyondaliwa Rais wa Ujerumani, Jk kwanini hakuhutubia kwa Kiswahili chetu, ilihali mgeni wake kahutubia kikwao? Wapi kuthamini vya kwetu jama!
Jambo hili la kung'ang'ania kiingereza na kukiacha kiswahili, ni jambo analolipenda sana raisKikwete sijui kwa nini. Alipokuja rais wa china, kikwete alihutubia kwa kiingereza pia.
 
Back
Top Bottom