Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,264
- 9,715
Ndugu zangu watanzania,
Ukiwa kiongozi Tanzania hasa ngazi ya Urais inahitaji kifua kipana,moyo mkubwa,moyo wa uvumilivu, upendo, huruma na moyo wa msamaha katika kuwaongoza na kuwatumikia watanzania,kwa kuwa sisi watanzania kwa kiwango kikubwa ni walalamishi, vigeugeu, tunaofanya mambo na kazi kwa kusukumwa na kuvizia vizia,. watanzania haturidhiki wala kuwa na shukurani hata pale tunapotendewa mema.
Chukua dakika moja kufikiri ni kiongozi yupi wa ngazi ya urais ambaye wakati wa utawala wake hakulaumiwa, kutukanwa, kusingiziwa, Kumchonganisha na wananchi,kumuombea mabaya ,kumlaani,kumtukana kuanzia utawala na uongozi wa Hayati mwalimu nyerere mpaka mh Dr Mama Samia suluhu Hasssan?ni yupi ambaye hakuitwa Dikteta? Yupi ambaye hakuambiwa ana mipango mibovu ya uchumi? Yupi ambaye hakuambiwa amalize haraka miaka yake madarakani ili akalee na kucheza na wajukuu zake? Yupi ambaye hakuambiwa anawafukarisha watanzania?
Ni watanzania wangapi kwa masikio yenu watanzania wenzangu wazalendo mmesikia kila utawala mmoja ukipita huanza kukumbukwa ukilinganishwa na unaokuwepo wakati huo? Ilikuwa hivyo wakati wa mwinyi watu wakasema bora mwalimu nyerere arejee madarakani,ikawa hivyo wakati wa hayati Benjamin mkapa ambapo watu wakasema bora mwinyi kuliko mkapa, ikaendelea hivyo kwa mh mzee wangu Dr Jakaya mrisho Kikwete ambapo watu wakasema bora Benjamini mkapa mambo yalikuwa sawa,ikaja kwa Hayati Mwalimu Dr John pombe Joseph Magufuli watu wakalalama na kulaani na kusema bora Mh Dr Jakaya Kikwete mambo yalikuwa safii na sasa Tupo na mama yetu kipenzi shujaa wa Afrika Nembo ya Tanzania na Nuru ya wanyonge mama samia suluhu Hasssan ,watu wale wale waliompinga kwa nguvu zao zote, kwa matusi, kejeri, dharau, dhihaka, hila, udhalilishaji na chuki sasa wameanza kumshambulia mama yetu na kusema bora Hayati Magufuli.
Midomo ile ile iliyotanuka kama ya akina Tundu lissu kumtukana Hayati magufuli ndani na nje ya mipaka ya Tanzania ,sasa wanamuona shujaa wakati walimuua kimaneno na kimaombi akiwa angali bado hai.Hii maana yake nini? Jibu ni kuwa sisi watanzania ni wanafiki wa kiwango cha juu sana,ni vigeugeu sana na tunaohitaji kiongozi mwenye moyo wa chuma asiye tazama nyuma wala kujali makelele na aliyeamua kuziba masikio kama alivyosema mama yetu kipenzi mama samia alipokuwa jijini Arusha, watanzania ukiwasikiliza sana lazima ukwame tu,lazima uyumbe kiuongozi,lazima upoteze dira na muelekeo wako,lazima uchelewe kuwafikisha nchi ya asali na maziwa ,lazima ujute kuwafahamu,lazima usosononeke moyoni mwako,lazima uwe na mawazo mengi ya nini ufanye kuwaridhisha watanzania,kwa kuwa watanzania hawaridhiki wala kutosheka,inabidi wakati mwingine uwaswage kwenda mbele na ukiwafikisha ng'ambo ya pili ya mto ndio watajuwa kuwa dhamira yako ilikuwa njema.
Mama yangu na Rais wangu mama samia Songa mbele kwa kishindo,usitazame nyuma wala kugeuka,kama ulivyotuasa kutazama mbele kwa matumaini badala ya hofu ya kupasa nawe kutazama mahali ulipodhamilia kuwafikisha watanzania kimaendeleo pasipo kujali maneno yao,acha waongee wewe chapa kazi na Songa mbele tuu, Tembea na dira yako,tazama Malengo yako na mtangulize Mungu wetu aliye hai katika shughuli na majukumu yako yote ya Urais maana siyo wote wanaofurahia mafanikio yako japo wanaweza kuwa katikati yako kati ya wale unaowaamini na kuwasikiliza,wapo wanaosubiri na kutamani kuona anguko lako ,lakini nakupa imani kuwa Mungu Aliyekuinua kiuongozi yupo upande wako na upande wa Taifa letu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa,kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Ukiwa kiongozi Tanzania hasa ngazi ya Urais inahitaji kifua kipana,moyo mkubwa,moyo wa uvumilivu, upendo, huruma na moyo wa msamaha katika kuwaongoza na kuwatumikia watanzania,kwa kuwa sisi watanzania kwa kiwango kikubwa ni walalamishi, vigeugeu, tunaofanya mambo na kazi kwa kusukumwa na kuvizia vizia,. watanzania haturidhiki wala kuwa na shukurani hata pale tunapotendewa mema.
Chukua dakika moja kufikiri ni kiongozi yupi wa ngazi ya urais ambaye wakati wa utawala wake hakulaumiwa, kutukanwa, kusingiziwa, Kumchonganisha na wananchi,kumuombea mabaya ,kumlaani,kumtukana kuanzia utawala na uongozi wa Hayati mwalimu nyerere mpaka mh Dr Mama Samia suluhu Hasssan?ni yupi ambaye hakuitwa Dikteta? Yupi ambaye hakuambiwa ana mipango mibovu ya uchumi? Yupi ambaye hakuambiwa amalize haraka miaka yake madarakani ili akalee na kucheza na wajukuu zake? Yupi ambaye hakuambiwa anawafukarisha watanzania?
Ni watanzania wangapi kwa masikio yenu watanzania wenzangu wazalendo mmesikia kila utawala mmoja ukipita huanza kukumbukwa ukilinganishwa na unaokuwepo wakati huo? Ilikuwa hivyo wakati wa mwinyi watu wakasema bora mwalimu nyerere arejee madarakani,ikawa hivyo wakati wa hayati Benjamin mkapa ambapo watu wakasema bora mwinyi kuliko mkapa, ikaendelea hivyo kwa mh mzee wangu Dr Jakaya mrisho Kikwete ambapo watu wakasema bora Benjamini mkapa mambo yalikuwa sawa,ikaja kwa Hayati Mwalimu Dr John pombe Joseph Magufuli watu wakalalama na kulaani na kusema bora Mh Dr Jakaya Kikwete mambo yalikuwa safii na sasa Tupo na mama yetu kipenzi shujaa wa Afrika Nembo ya Tanzania na Nuru ya wanyonge mama samia suluhu Hasssan ,watu wale wale waliompinga kwa nguvu zao zote, kwa matusi, kejeri, dharau, dhihaka, hila, udhalilishaji na chuki sasa wameanza kumshambulia mama yetu na kusema bora Hayati Magufuli.
Midomo ile ile iliyotanuka kama ya akina Tundu lissu kumtukana Hayati magufuli ndani na nje ya mipaka ya Tanzania ,sasa wanamuona shujaa wakati walimuua kimaneno na kimaombi akiwa angali bado hai.Hii maana yake nini? Jibu ni kuwa sisi watanzania ni wanafiki wa kiwango cha juu sana,ni vigeugeu sana na tunaohitaji kiongozi mwenye moyo wa chuma asiye tazama nyuma wala kujali makelele na aliyeamua kuziba masikio kama alivyosema mama yetu kipenzi mama samia alipokuwa jijini Arusha, watanzania ukiwasikiliza sana lazima ukwame tu,lazima uyumbe kiuongozi,lazima upoteze dira na muelekeo wako,lazima uchelewe kuwafikisha nchi ya asali na maziwa ,lazima ujute kuwafahamu,lazima usosononeke moyoni mwako,lazima uwe na mawazo mengi ya nini ufanye kuwaridhisha watanzania,kwa kuwa watanzania hawaridhiki wala kutosheka,inabidi wakati mwingine uwaswage kwenda mbele na ukiwafikisha ng'ambo ya pili ya mto ndio watajuwa kuwa dhamira yako ilikuwa njema.
Mama yangu na Rais wangu mama samia Songa mbele kwa kishindo,usitazame nyuma wala kugeuka,kama ulivyotuasa kutazama mbele kwa matumaini badala ya hofu ya kupasa nawe kutazama mahali ulipodhamilia kuwafikisha watanzania kimaendeleo pasipo kujali maneno yao,acha waongee wewe chapa kazi na Songa mbele tuu, Tembea na dira yako,tazama Malengo yako na mtangulize Mungu wetu aliye hai katika shughuli na majukumu yako yote ya Urais maana siyo wote wanaofurahia mafanikio yako japo wanaweza kuwa katikati yako kati ya wale unaowaamini na kuwasikiliza,wapo wanaosubiri na kutamani kuona anguko lako ,lakini nakupa imani kuwa Mungu Aliyekuinua kiuongozi yupo upande wako na upande wa Taifa letu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa,kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.