Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,311
- 9,739
Ndugu Zangu Hivyo Ndivyo unavyoweza kusema kuwa Rais Mama Samia Ni Dereva Mahiri na shupavu Sana katika kuliendesha gari hili la Safari ya maendeleo ya Tanzania, Ni dereva Ambaye ameonyesha umaridadi na uzoefu wa kuendesha gari,ameonyesha umakini mkubwa katika safari,ameonyesha kuwajari abiria wake,ameonyesha usikivu,unyenyekevu ,busara ,hekima na upendo mkubwa Sana kwa abiria wake.
Ameonyesha kufahamu na kutambua kuwa amebeba Roho za watu na siyo wanyama,ameonyesha kutambua umuhimu wa Roho alizozibeba ndani ya gari yake, ameonyesha kutambua kuwa Roho zote zipo mikononi mwake,ameonyesha kutambua kuwa kosa dogo na moja linaweza hitimisha uhai wa abiria wake, ameonesha kutambua kuwa uhai wa Mwanadamu haununuliwi kwa Fedha ya aina yoyote Ile, Rais Samia amekidhi kiu ya abiria wake,amewaondolea hofu na Mashaka,Amewapa matumaini ya kufika salama bila uchovu Wala hofu,hakuna aliyeshika Roho mikononi maana Dereva ameonyesha kuzifahamu vyema njia aipitayo na mahali anakokwenda
Mwendo ni wakuridhisha, sauti za abiria Ni za furaha na amani,maongezi ya abiria Ni pongezi na sifa kwa Dereva wao,kwa hakika Hakuna mwenye kutamani kushuka,Hakuna mwenye kutamani kupanda gari jingine,hakuna mwenye kujuta na safari,Hakuna mwenye kujutia Nauli yake,hakuna mwenye kujilaumu kusafiri naye.
Kila abiria anatamani kupanda gari hili Tena, kila abiria anamuombea Maisha marefu na Afya njema Dereva huyu.
Tanzania Ni Gari aiongozayo na kuliendesha mama Samia,Hakuna anayejuta kuzaliwa Tanzania kwa Sasa,hakuna anayetamani kuhama Tanzania kwa Sasa, Hakuna anayehofu juu ya kesho yake ndani ya Tanzania, Kwa sasa Tanzania Ni nchi inayotoa matumaini kwa kila mtanzania mwenye kutumia fursa za kiuchumi zilizopo, Ni nchi inayomiminisha fursa kila mahali, Ni nchi ambayo kwa Sasa Ni Tumaini kwa wanyonge katika kuinuka kiuchumi, Ni nchi na mahali palipo salama kwa kila mmoja wetu kusonga mbele na kupiga hatua za kimaendeleo.
Rais Samia anazidi kuchanja mbuga katika mioyo ya watanzania, anazidi kueleweka na watanzania, Anaendelea kukubalika na watanzania kwa kuwa ameonyesha kuyatambua matatizo na kero za watanzania na kuwa Tayari kupambana nazo,Ameonyesha uzalendo kimaneno na kimatendo katika kuwatumikia watanzania,ameonyesha Ushupavu na ujasiri katika kuliongoza Taifa letu, ametupatia matumaini ya kesho iliyo Bora Zaidi ya leo
Watanzania Tuendelee kumuunga mkono mh Rais wetu, Tuendelee kumwombea Afya njema na nguvu za Kuendelea kututumikia, Tuendelee kuwa naye bega kwa bega, Tuendelee kumpa faraja na kumtia moyo mama yetu, Tuendelee kusimama Naye katika Hatua zote za ujenzi wa Taifa letu , Tuendelee kumpa ushirikiano na kuonyesha upendo kwake Kama anavyoonesha kwetu watanzania.
Watanzania Tutambue na kufahamu kuwa viongozi aina ya Rais Samia Hawazaliwi kila Siku na hawapatikani kila mahali, Viongozi Wa aina yake wenye upendo,uzalendo kwa nchi zao huwa Ni nadra sana Sana kuwapata. Watanzania Tumepata bahati ya kumpata Mama Samia. Ambaye ameonyesha ujasiri, uzalendo,ushupavu na umahili katika kuliongoza Taifa hili, Amelibeba Taifa hili kwa moyo wake wote katika mabega take kuhakikisha kuwa analifikisha salama na mbele zaidi kimaendeleo mahali ambapo kila mtanzania ataguswa kiuchumi nakuondoka katika umaskini wa kipato.
Kazi iendeleee,mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627
Ameonyesha kufahamu na kutambua kuwa amebeba Roho za watu na siyo wanyama,ameonyesha kutambua umuhimu wa Roho alizozibeba ndani ya gari yake, ameonyesha kutambua kuwa Roho zote zipo mikononi mwake,ameonyesha kutambua kuwa kosa dogo na moja linaweza hitimisha uhai wa abiria wake, ameonesha kutambua kuwa uhai wa Mwanadamu haununuliwi kwa Fedha ya aina yoyote Ile, Rais Samia amekidhi kiu ya abiria wake,amewaondolea hofu na Mashaka,Amewapa matumaini ya kufika salama bila uchovu Wala hofu,hakuna aliyeshika Roho mikononi maana Dereva ameonyesha kuzifahamu vyema njia aipitayo na mahali anakokwenda
Mwendo ni wakuridhisha, sauti za abiria Ni za furaha na amani,maongezi ya abiria Ni pongezi na sifa kwa Dereva wao,kwa hakika Hakuna mwenye kutamani kushuka,Hakuna mwenye kutamani kupanda gari jingine,hakuna mwenye kujuta na safari,Hakuna mwenye kujutia Nauli yake,hakuna mwenye kujilaumu kusafiri naye.
Kila abiria anatamani kupanda gari hili Tena, kila abiria anamuombea Maisha marefu na Afya njema Dereva huyu.
Tanzania Ni Gari aiongozayo na kuliendesha mama Samia,Hakuna anayejuta kuzaliwa Tanzania kwa Sasa,hakuna anayetamani kuhama Tanzania kwa Sasa, Hakuna anayehofu juu ya kesho yake ndani ya Tanzania, Kwa sasa Tanzania Ni nchi inayotoa matumaini kwa kila mtanzania mwenye kutumia fursa za kiuchumi zilizopo, Ni nchi inayomiminisha fursa kila mahali, Ni nchi ambayo kwa Sasa Ni Tumaini kwa wanyonge katika kuinuka kiuchumi, Ni nchi na mahali palipo salama kwa kila mmoja wetu kusonga mbele na kupiga hatua za kimaendeleo.
Rais Samia anazidi kuchanja mbuga katika mioyo ya watanzania, anazidi kueleweka na watanzania, Anaendelea kukubalika na watanzania kwa kuwa ameonyesha kuyatambua matatizo na kero za watanzania na kuwa Tayari kupambana nazo,Ameonyesha uzalendo kimaneno na kimatendo katika kuwatumikia watanzania,ameonyesha Ushupavu na ujasiri katika kuliongoza Taifa letu, ametupatia matumaini ya kesho iliyo Bora Zaidi ya leo
Watanzania Tuendelee kumuunga mkono mh Rais wetu, Tuendelee kumwombea Afya njema na nguvu za Kuendelea kututumikia, Tuendelee kuwa naye bega kwa bega, Tuendelee kumpa faraja na kumtia moyo mama yetu, Tuendelee kusimama Naye katika Hatua zote za ujenzi wa Taifa letu , Tuendelee kumpa ushirikiano na kuonyesha upendo kwake Kama anavyoonesha kwetu watanzania.
Watanzania Tutambue na kufahamu kuwa viongozi aina ya Rais Samia Hawazaliwi kila Siku na hawapatikani kila mahali, Viongozi Wa aina yake wenye upendo,uzalendo kwa nchi zao huwa Ni nadra sana Sana kuwapata. Watanzania Tumepata bahati ya kumpata Mama Samia. Ambaye ameonyesha ujasiri, uzalendo,ushupavu na umahili katika kuliongoza Taifa hili, Amelibeba Taifa hili kwa moyo wake wote katika mabega take kuhakikisha kuwa analifikisha salama na mbele zaidi kimaendeleo mahali ambapo kila mtanzania ataguswa kiuchumi nakuondoka katika umaskini wa kipato.
Kazi iendeleee,mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627