johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 85,095
- 143,945
Dar es Salaam kuna mgao mkubwa wa maji kwa sababu mto Ruvu umevamiwa na binadamu na kuchepusha maji.
Pili maelfu ya mifugo yanayoingizwa kwenye mito kunywa maji yamepunguza kiasi cha maji kwani ng'ombe mmoja kwa mfano hunywa lita 40 za maji kwa siku.
Tatu ni ukataji miti hovyo hali inayoharibu ikolojia ya nchi.
Nne ni tatizo la tabia nchi.
Hivyo mgao wa maji hauepukiki
Na kwahiyo naagiza Wakuu wote wa mikoa kuweka ulinzi katika mito yote ili kulinda maji ya watu wetu.
========
Rais Samia Suluhu Hassan amesema anatambua Miji mingi mikubwa inakabiliwa na uhaba wa maji unaopelekea mgao wa maji na upungufu wa umeme
Amesema hiyo imetokana na mambo mawili makubwa ambayo ni Ubishi na ukaidi wa wanadamu na Kudra za Mungu
Amefafanua, "Bado kuna wananchi wengi wameendelea kuvamia vyanzo vya maji kwa kuyachepusha kwa ajili ya matumizi mengine. Pia, kuna watu wanalima karibu na vyanzo vya maji. Haya yote yanapelekea Vyanzo vya Maji kupungua"
"Nimefatana na viongozi wote hawa wa dini kwanza, kufuatana na viongozi wa dini wote hawa ni baraka kama kuna mapepo huko njiani yanapeperuka, pili nimeipa heshima Mwanza, tutaanza hapa dua za kuomba mvua zenye neema kwa Taifa letu"-Rais Samia.
Pili maelfu ya mifugo yanayoingizwa kwenye mito kunywa maji yamepunguza kiasi cha maji kwani ng'ombe mmoja kwa mfano hunywa lita 40 za maji kwa siku.
Tatu ni ukataji miti hovyo hali inayoharibu ikolojia ya nchi.
Nne ni tatizo la tabia nchi.
Hivyo mgao wa maji hauepukiki
Na kwahiyo naagiza Wakuu wote wa mikoa kuweka ulinzi katika mito yote ili kulinda maji ya watu wetu.
========
Rais Samia Suluhu Hassan amesema anatambua Miji mingi mikubwa inakabiliwa na uhaba wa maji unaopelekea mgao wa maji na upungufu wa umeme
Amesema hiyo imetokana na mambo mawili makubwa ambayo ni Ubishi na ukaidi wa wanadamu na Kudra za Mungu
Amefafanua, "Bado kuna wananchi wengi wameendelea kuvamia vyanzo vya maji kwa kuyachepusha kwa ajili ya matumizi mengine. Pia, kuna watu wanalima karibu na vyanzo vya maji. Haya yote yanapelekea Vyanzo vya Maji kupungua"
"Nimefatana na viongozi wote hawa wa dini kwanza, kufuatana na viongozi wa dini wote hawa ni baraka kama kuna mapepo huko njiani yanapeperuka, pili nimeipa heshima Mwanza, tutaanza hapa dua za kuomba mvua zenye neema kwa Taifa letu"-Rais Samia.