Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,262
- 9,714
Ndugu zangu Watanzania,
Kwa hakika Rais samia ni mpango wa Mungu mwenyewe,ni Mungu ndiye amtumiaye Rais samia kuwatumikia watanzania,ni Mungu ndiye ambaye anampatia njia na maarifa ya kuongoza Taifa letu,ni mkono wa Mungu ulio mbele ya Rais samia. palipo na Mungu pana baraka,pana neema ,pana mafanikio,pana pangwa pakapangika,pana nuru,mwanga,njia,furaha, Tabasamu,upendo na mikakati yenye Tija. ndani ya Taifa letu kuna kutamalaki kwa amani na utulivu kwasababu ya uwepo wa Mungu aliye amua kumuinua na kumtumia Rais samia kuongoza Taifa letu,.ndio maana mnaona kinywa cha Rais samia kikitoa maneno ya upendo kwa watu wote na kuhubiri haki wakati wote.
Sasa Rais huyu mcha Mungu na mwenye hofu ya Mungu amekuja na jambo la kipekee na lililokonga nyoyo za watu kwa kuamua kugawa buree vyandarua kwa wanafunzi wote mashuleni ili kuwakinga na kuwalinda dhidi ya ugonjwa wa malaria ambao umekuwa hatari sana.hii maana yake nini? Jibu ni kuwa Rais samia anataka watoto wote wakue pasipo kitisho cha magonjwa hasa malaria,wasikatize masomo kwa sababu ya kuumwa,wasikose masomo kwa sababu ya kuugua,wahudhurie vipindi vyote darasani,wawe wenye kujiamini na wenye utayari wa kuja kulitumikia Taifa letu na kutoa Elimu kwa jamii inayowazunguka.
Mwingine anaweza kusema mbona miaka fulani serikali iligawa vyandarua kwa watanzania wote? Jibu ni kuwa Rais samia ameshuka chini kabisa kwa kumpatia kila mwanafunzi chandarua chake.jiulize familia moja yenye baba na mama hapo mtaani pako ina wanafunzi wangapi wanaosoma ? Kila familia ina wastani wa wanafunzi wangapi wanaosoma? Ifahamike kuwa Mpango huu unawapa wanafunzi wote vyandarua bila kujali wapo wangapi katika familia.
Wana Mbeya ambako zoezi hili limeanza tayari wamefurahi sana na kumpongeza sana Rais samia,wanafunzi wamemshukuru sana Rais wao kipenzi na kuwasihi wazazi wao kumpigia kura za ndio kwa kishindo uchaguzi ujao ili waweze kutimiza ndoto zao za Elimu kupitia Rais samia. Ikumbukwe ya kuwa tayari Rais samia alishafanya maajabu mengine ya kujenga vyumba vya madarasa zaidi ya elfu ishirini pamoja na kuweka mikakati ya kujenga vingine zaidi ya elfu moja.inakuja huku watanzania wakishuhudia serikali ya Rais samia ikitoa elimu buree hadi kidato cha sita huku wanafunzi wote wenye sifa wakipewa mikopo ya elimu ya juu, lakini akiwa ametoa maelfu ya ajira kwa kada ya Elimu ili kuboresha na kurahisisha hali ya ufundishaji shuleni.
Huyu ndiye Rais samia mama wa shoka ,chuma cha Reli,shujaa wa Afrika,kioo cha Afrika, jasiri muongoza njia na nuru ya wanyonge akiendelea kufanya maajabu ya kipekee ambayo yalionekana kama hayawezekani.kwake hakuna lisilowezekana au kushindikana,kwake hakuna kufuri lisilo na funguo,hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea,hakuna mlima usio na kilele,hakuna usiku usio kucha,hakuna changamoto isiyo na jibu ,hakuna mtihani usio na majibu.kwake yote yanawezekana na ndio maana Anaendelea kuchanja mbuga kwa mafanikio makubwa katika kila Eneo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Kwa hakika Rais samia ni mpango wa Mungu mwenyewe,ni Mungu ndiye amtumiaye Rais samia kuwatumikia watanzania,ni Mungu ndiye ambaye anampatia njia na maarifa ya kuongoza Taifa letu,ni mkono wa Mungu ulio mbele ya Rais samia. palipo na Mungu pana baraka,pana neema ,pana mafanikio,pana pangwa pakapangika,pana nuru,mwanga,njia,furaha, Tabasamu,upendo na mikakati yenye Tija. ndani ya Taifa letu kuna kutamalaki kwa amani na utulivu kwasababu ya uwepo wa Mungu aliye amua kumuinua na kumtumia Rais samia kuongoza Taifa letu,.ndio maana mnaona kinywa cha Rais samia kikitoa maneno ya upendo kwa watu wote na kuhubiri haki wakati wote.
Sasa Rais huyu mcha Mungu na mwenye hofu ya Mungu amekuja na jambo la kipekee na lililokonga nyoyo za watu kwa kuamua kugawa buree vyandarua kwa wanafunzi wote mashuleni ili kuwakinga na kuwalinda dhidi ya ugonjwa wa malaria ambao umekuwa hatari sana.hii maana yake nini? Jibu ni kuwa Rais samia anataka watoto wote wakue pasipo kitisho cha magonjwa hasa malaria,wasikatize masomo kwa sababu ya kuumwa,wasikose masomo kwa sababu ya kuugua,wahudhurie vipindi vyote darasani,wawe wenye kujiamini na wenye utayari wa kuja kulitumikia Taifa letu na kutoa Elimu kwa jamii inayowazunguka.
Mwingine anaweza kusema mbona miaka fulani serikali iligawa vyandarua kwa watanzania wote? Jibu ni kuwa Rais samia ameshuka chini kabisa kwa kumpatia kila mwanafunzi chandarua chake.jiulize familia moja yenye baba na mama hapo mtaani pako ina wanafunzi wangapi wanaosoma ? Kila familia ina wastani wa wanafunzi wangapi wanaosoma? Ifahamike kuwa Mpango huu unawapa wanafunzi wote vyandarua bila kujali wapo wangapi katika familia.
Wana Mbeya ambako zoezi hili limeanza tayari wamefurahi sana na kumpongeza sana Rais samia,wanafunzi wamemshukuru sana Rais wao kipenzi na kuwasihi wazazi wao kumpigia kura za ndio kwa kishindo uchaguzi ujao ili waweze kutimiza ndoto zao za Elimu kupitia Rais samia. Ikumbukwe ya kuwa tayari Rais samia alishafanya maajabu mengine ya kujenga vyumba vya madarasa zaidi ya elfu ishirini pamoja na kuweka mikakati ya kujenga vingine zaidi ya elfu moja.inakuja huku watanzania wakishuhudia serikali ya Rais samia ikitoa elimu buree hadi kidato cha sita huku wanafunzi wote wenye sifa wakipewa mikopo ya elimu ya juu, lakini akiwa ametoa maelfu ya ajira kwa kada ya Elimu ili kuboresha na kurahisisha hali ya ufundishaji shuleni.
Huyu ndiye Rais samia mama wa shoka ,chuma cha Reli,shujaa wa Afrika,kioo cha Afrika, jasiri muongoza njia na nuru ya wanyonge akiendelea kufanya maajabu ya kipekee ambayo yalionekana kama hayawezekani.kwake hakuna lisilowezekana au kushindikana,kwake hakuna kufuri lisilo na funguo,hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea,hakuna mlima usio na kilele,hakuna usiku usio kucha,hakuna changamoto isiyo na jibu ,hakuna mtihani usio na majibu.kwake yote yanawezekana na ndio maana Anaendelea kuchanja mbuga kwa mafanikio makubwa katika kila Eneo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.