dah bosi Wangu Ludigija
Huyo alikuwa anasema Magufuli ni mjomba wake akawekwa Kigamboni Mkurugenzi alitudhulumu sana mali zetu alikuwa anatuma afisa ardhi kupima ardhi za watu kwa mabavu na dereva wake alikuwa anatembeza wateja kwenye ardhi alizopora tunashangaa hajafukuzwa
 
Rais Samia Suluhu Hassan ameteua wakuu wapya wa wilaya 37, kuwahamisha vituo vya kazi 48 na wengine 55 kubakia kwenye vituo vyao.

Kati ya Wakuu wa Wilaya hao 140, Wanawake ni 40 na Wanaume ni 100

View attachment 2494967View attachment 2494968View attachment 2494970View attachment 2494971View attachment 2494972View attachment 2494973View attachment 2494974View attachment 2494975
Sara Msafiri malkia wa Kigamboni akaenda kibaha hayupo?? Hasara aliyotia Tanzania kwa ujinga wake ndio mzigo kwa walipa kodi
 
Hawana kitu ,kila kitu bure nyumba hadi usafiri,hela ya likizo,bima bure, hela za vikao,pia status inamsaidia popote pale kufanikisha mambo yake.
Off course but Bora nifanye kazi yangu ya kuajiriwa kuliko hizo ambazo hazina uhakika japo Zina kupa guarantee ya mapesa mengi yanatokana na hadhi hiyo na kiukweli hawategemea salary hizo maana mapesa haramu ni mengi
 
Hao wapya namba nane hapo Grace Kingalame si mwandishi wa habari huyo? Au wanafanania majina.
Juma Issa Chikoka kabaki, ni yule mchekeshaji wa zamani na huwa naamini anafanya kazi vizuri.

Wake wa vigogo naona wanabaki na hawapelekwi mbalimbali uko Tandahimba.
Na yule Nick wa Weusi jina lake nani sijui, vipi tena
Wanahabari TBC huwa wanapata teuzi sana. Nimeona pia Japhar Haniu poa kapata
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya Wapya 37, kuwahamisha vituo vya Kazi Wakuu wa Wilaya 48 na wengine 55 kubakia kwenye vituo vyao.

Kati ya Wakuu wa Wilaya hao 140, Wanawake ni 40 na Wanaume ni 100 ambao ni kama ifuatavyo:

A) WAKUU WA WILAYA WAPYA:

1. Felician Gasper Mtahengerwa – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha

2. Marko Henry Ngu’mbi – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido

3. Emmanuela Kaganda Mtatifikolo – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.

4. Gerald R. Mongella – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chemba

5. Kanali Boniphace Magembe – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Geita

6. Leah Lucas Ulaya – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe

7. Deusdedith Josephat Katwale – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya Chato

8. Grace Henry Kingalame – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nyang’halwe

9. Dkt. Linda Peniel Salekwa – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mufindi

10. Dkt. Abel Mwendawile Nyamahanga – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Muleba

11. Japhet Mosses Maganga – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa

12. Erasto Yohana Sima – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba

13. Julius Kalanga Laiser – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Karagwe

14. Dinah Elias Mathamani – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Uvinza

15. Dkt. Christopher David Timbuka – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Siha

16. Amir Mohamed Mkalipa – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai

17. Kasilda Jeremia Mgeni – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Same

18. Goodluck Asaph Mlinga – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Liwale

19. Chistopher E. Ngubiagai – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilwa

20. Beno Morris Malisa – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbeya

21. Josephine Keenja Manase – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kyela

22. Jaffar Mohamed Haniu – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rungwe

23. Rebeca Sanga Msemwa – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro

24. Shaka Hamdu Shaka – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilosa

25. Rachel Stephen Kasanda – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Magu

26. Hassan Omary Bomboko – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe

27. Victoria Charles Mwanziva – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ludewa

28. Kanali Joseph Samwel Kolombo – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibiti

29. Zephania Stephan Sumaye – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mafia

30. Lazaro Killian Komba– Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kalambo

31. Dkt. Jane Chacha Nyamsenda – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga

32. Wilman Kapenjama Ndile – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Songea

33. Mboni Mohamed Mhita – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama

34. Farida Salum Mgomi – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ileje

35. Solomon Jonas Itunda – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Songwe

36. Zakaria Saili Mwansasu – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Uyui

37. Naitapwaki Lumeya Tukai – Ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nzega



B) WAKUU WA WILAYA WALIOHAMISHWA VITUO VYA KAZI:

1. Suleiman Yusufu Mwenda – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba.

2. Edward Jonas Mpogolo – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Same.

3. Halima Abdallah Bulembo – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Muheza.

4. Hashim Abdallah Komba – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea.

5. Mwanahamisi Athumani Mukunda – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Bahi.

6. Saadi Ahmed Mtambule – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mufindi.

7. Sophia Mfaume Kizigo – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkalama.

8. Godwin Crydon Gondwe – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bahi. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.

9. Veronica Arbogast Kessy – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Misungwi.

10. ACP Advera John Bulimba – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Nzega.

11. Majid Hemed Mwanga – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mlele. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilosa.

12. Salum Hamis Kalli – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Magu.

13. Kisare Matiku Makori – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Uyui.

14. Mohamed Hassan Moyo – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa.

15. Kherry Denis James – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbulu. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo.

16. Dkt. Vicent Naano Anney – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Rungwe.

17. Kanali Denis Filangali Mwila – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbarali. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe.

18. Sebastian Muungano Waryuba – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Malinyi. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga.

19. Danstan Dominic Kyobya – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilombero. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara.

20. Dkt. Julius Keneth Ningu – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ulanga. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo.

21. Judith Martin Nguli – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mvomero. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Liwale.

22. Hanafi Hassan Msabaha – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara. Alikuwa Mkuu wa Wilaya Uvinza.

23. Lauter John Kanoni – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe.

24. Matiko Paul Chacha – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Misungwi. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kaliua.

25. Ng’wilabuzu Ndatwa Ludigija – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kwimba. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala.

26. Claudia Undalusyege Kitta – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi.

27. Fatma Almas Nyangasa – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni.

28. Nick Simon John – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe.

29. Halima Habib Okash – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mvomero.

30. Filberto Hassan Sanga – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nyasa. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mlele.

31. Ngollo Ng’waniduhu Malenya – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ulanga.

32. Johari Musa Samizi – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kwimba.

33. Simon Peter Simalenga – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Songwe.

34. Anna Jerome Gidarya – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Busega. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ileje.

35. Moses Joseph Machali – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkalama. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba.

36. Thomas Cornel Apson – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Siha.

37. Kemilembe Rose Lwota – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Manyoni. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo.

38. Joshua Samwel Nassari – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda.

39. Esther Alexander Mahawe – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbozi. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma.

40. Simon Kemori Chacha – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Sikonge. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Chemba.

41. Dkt. Mohamed Rashid Chuachua – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kaliua. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbeya.

42. Said Mohamed Mtanda – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha.

43. Louis Peter Bura – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo.

44. Jokate Urban Mwegelo – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Korogwe. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke.

45. Albert Gasper Msando – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

46. Juma Said Irando – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Muheza. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai.

47. Zainab Abdallah Issa – Amehamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Pangani. Alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo.



C) WAKUU WA WILAYA WANAOENDELEA NA VITUO VYA KAZI:

1. Dadi Horace Kolimba – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Karatu

2. Raymond Stephen Mangwala – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro.

3. Dkt. Khamis Athumani Mkanachi – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kondoa.

4. Remedius Mwema Emmanuel – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa.

5. Jabir Mussa Shekimweri– Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma.

6. Gift Isaya Msuya – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chamwino.

7. Said Juma Nkumba – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukombe.

8. Peres Boniphace Magiri– Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilolo.

9. Kanali Wilson Christian Sakullo – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Misenyi.

10. Kanali Mathias Julius Kahabi – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ngara.

11. Jamila Yusuph Kimaro – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpanda

12. Onesmo Mpuya Buswelu – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika.

13. Kanali Michael Masala Ngayalina – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe.

14. Kanali Evance M. Mallasa – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kakonko.

15. Kanali Aggrey John Magwaza – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibondo.

16. Kanali Issac Anthony Mwakisu – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kasulu.

17. Kanali Hamis Mayamba Maiga – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rombo.

18. Abdallah Musa Mwaipaya – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mwanga.

19. Shaibu Issa Ndemanga – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi.

20. Hassan Nassor Ngoma – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa.

21 Janeth Peter Mayanja – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hanang.

22. Lazaro Jacob Twange – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Babati.

23. Mbaraka Alhaji Batenga – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kiteto

24. Dkt. Suleiman Hassan Serera – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro.

25. Dkt. Halfan Boniface Haule – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma.

26. Mwl. Moses Ludovick Kaegele – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Butiama.

27. Dkt. Vincent Biyegela Mashinji– Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Serengeti.

28. Juma Issa Chikoka – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rorya.

29. Lt. Kanali Michael Mangwela Mtenjele – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya Tarime.

30. Mayeka Simon Mayeka – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chunya.

31. Jabir Omari Makame – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Gairo.

32. Lt. Kanali Patrick Kenan Sawala – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba.

33. Mwangi Rajab Kundya – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Newala

34. Mariam Khatib Chaurembo – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu.

35 Amina Nassoro Makilagi – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana.

36. Hassan Elias Massala– Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela

37. Senyi Simon Ngaga – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema.

38. Juma Samwel Sweda – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Makete.

39. Kissa Gwakisa Kasongwa – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Njombe.

40. Khadija Nassir Ali – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga.

41. Meja Edward Flowin Gowele – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rufiji.

42. Peter Ambrose Lijualikali – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nkasi.

43. Julius Sunday Mtatiro – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru.

44. Aziza Ally Mangosango – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbinga.

45. Joseph Modest Mkude – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kishapu.

46. Aswege Enock Kaminyonge– Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa.

47. Faiza Suleiman Salim – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Itilima.

48. Fauzia Hamidu Ngatumbura – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Meatu.

49. Paskasi Damian Murangili – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Singida.

50. Fakii Raphael Lulandala – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Momba.

51. Sauda Salum Mtondoo – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Igunga.

52. Abel Yeji Busalama – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi.

53. Hashim Shaib Mgandilwa – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga.

54. Kalist Lazaro Bukhay – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Lushoto

55. Kanali Maulid Hassan Surumbu – Anaendelea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga.
Walioachwa je mkeka wao uwapi...hapo ndio ujue wewe ni mbumbu mbu mbususu
 
Mkuu wa Wilaya Simalenga aliyetuhumiwa kumpiga na kumjeruhi msichana anaadhibiwa kwa kuhamishwa kituo? Ni ujumbe gani unaotumwa? Kuwa ruksa kwa viongozi wa kisiasa kuwapiga watoto? Inasikitisha sana.

Amandla...
 
Zainab karudishwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Pangani ambapo pia ndio alipoanzia wadhifa huo,ni mke wa Waziri Jumaa Aweso ambae pia ni Mbunge wa Pangani,hii haitakua na conflict of interest kiutendaji?
 
Mpaka leo watu wanawaza ukristo na uislamu duu.
Kwa humu JF teuzi nyingi za raisi zikiwa zimeelemea kwa waislamu, basi anaitwa mdini

Ikiwa teuzi zimeelemea kwa upande wa wakristo, member wote wanaufyata.

Ona sasa, raisi kateua wakuu wa wilaya wapya 37, 6 kati ya hao ni waislamu, 31 ni wakristo lakini huwezi sikia ajenda ya udini hapa. Na hutokuja sikia waislamu wa humu JF wakilalamikia udini ktk hili, wapo kimyaaa wanaendelea na harakati zao kama kawa.

Great Thinkers wameshanielewa
 
Alikuwa na mdomo mchafu Sana, wanakuwa wamemfanyizia
Hari yake si nzuri sana na huenda ni matendo yake maana watu wengi wameumizwa sana na maamuzi yake yasiyo fair hata kidogo.

Kwenye hilo kapu wanaougulia sahivi yuko mmama mwingine wa chama kata fulani naye yuko hoi, pia za ndani na DED naye mambo yao ni magumu
 
Hari yake si nzuri sana na huenda ni matendo yake maana watu wengi wameumizwa sana na maamuzi yake yasiyo fair hata kidogo.

Kwenye hilo kapu wanaougulia sahivi yuko mmama mwingine wa chama kata fulani naye yuko hoi, pia za ndani na DED naye mambo yao ni magumu
DED wa Kigamboni??Yaani huyo Sara Msafiri kweli itabidi aombe watu msamaha kwa sababu alikuwa hana adabu na wala staha alikuwa anafanya ushenzi bila kuwa na aibu na alikuwa na yule Makonda kudhulumu watu Kigamboni
 
Back
Top Bottom