Rais Samia aongeza muda mpango wa TASAF, zaidi ya kaya 173,076 zaondokana na umaskini

kalacha mateo

Senior Member
Sep 27, 2021
118
237
NAIBU Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deo Ndejembi amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wanufaika wa mradi wa kunusuru kaya maskini (TASAF) kwa kuuongezea muda mradi huo hadi mwaka 2025 ambapo awali ulikua uishie mwaka 2023.

Moja ya manufaa ya mpango huo ni kuendelea kuwanusuru wananchi na umaskini uliokithiri ambapo Kaya 173,076 zimehitimu zinaweza kujitegemea bila ruzuku. Kaya hizo zinaweza kumudu gharama za matibabu, kusomesha watoto na zina vitega uchumi na biashara za uhakika zinazoongeza pato la familia na zinakopesheka kwa kuwa na rasilimali zalishi.

Kaya hizo zilizohitimu ni miongoni mwa kaya 886,724 zilizohakikiwa na kuongeza kuwa kaya 730,138 bado zina hali duni kiuchumi na hivyo zinaendelea kuwepo katika kipindi cha pili cha mpango na kupokea ruzuku huku kaya nyingi zikiwa ni zile za wazee na zinaoongozwa na watoto.

2c1e1e97-c9ae-4f50-b687-83f3990901a5.jpg
 
Nadhani kuna watu huko serikalini hawajui tafsiri ya umaskini.

Huwezi kuondowa umaskini kwa ruzuku ya Tasaf, ni Utapeli tu.

Ukiona serikali imeongeza muda wameona fursa ya taasisi ya kuchota pesa za kampeni 2025 ambazo hazina kazi zipo zipo tu.
 
NAIBU Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deo Ndejembi amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wanufaika wa mradi wa kunusuru kaya maskini (TASAF) kwa kuuongezea muda mradi huo hadi mwaka 2025 ambapo awali ulikua uishie mwaka 2023.

Moja ya manufaa ya mpango huo ni kuendelea kuwanusuru wananchi na umaskini uliokithiri ambapo Kaya 173,076 zimehitimu zinaweza kujitegemea bila ruzuku. Kaya hizo zinaweza kumudu gharama za matibabu, kusomesha watoto na zina vitega uchumi na biashara za uhakika zinazoongeza pato la familia na zinakopesheka kwa kuwa na rasilimali zalishi.

Kaya hizo zilizohitimu ni miongoni mwa kaya 886,724 zilizohakikiwa na kuongeza kuwa kaya 730,138 bado zina hali duni kiuchumi na hivyo zinaendelea kuwepo katika kipindi cha pili cha mpango na kupokea ruzuku huku kaya nyingi zikiwa ni zile za wazee na zinaoongozwa na watoto.

2c1e1e97-c9ae-4f50-b687-83f3990901a5.jpg
Hii ndio Tanzania ya CCM kutafuta ulaji. Idadi hiyo yote imeondoka umasikini kweli!!
Nyumba nyasi maji tope kuchangia na Ngombe! Umeme huduma ya afya.
Shule watoto wanacheza vumbi Darasani kweli!!??
 
Wahusika wa TASAF,Ni muda wa kujiongezea ulaji tu,baadhi wanapiga hela sana,yaani basi tu.
 
Ni Bora fedha zikajenge viwanda, mashamba hao maskini wakafanye kazi huko wajipatie vipato Halali. Hakunaga vya Bure vikunudaishe
 
Back
Top Bottom