TaiPei
JF-Expert Member
- Aug 4, 2022
- 421
- 328
DC Shaka Hamdu Shaka akitatua Mgogoro Kati ya Wafugaji na Wakulima huko huko Porini,
===
Kuelekea Uchaguzi Mkuu huru wa Serikali za Mitaa & Vijijini wa 2024 tunahitaji kuwa na DCs & RCs vibrant na waliosheheni Ushawishi hasa wa kisiasa ( Political influence )
Tunahitaji Wakuu wa Wilaya na Mikoa wanaoweza kushawishi zaidi ya kutumia police na migambo katika kupata matokeo ya kishindo 2024 & 2025,
Tunahitaji mkuu wa Mkoa anayeweza kubeba vyote kwa maana ya Siasa na Serikali kwa wakati mmoja huku akiacha wananchi wake wakiwa wamoja na waliojaa matumaini juu ya Serikali & Rais wao,
Shaka kwa Uzoefu wake wa karibu miongo miwili kwenye Chama na Uimara wake katika kujenga hoja anaweza kuwa RC mzuri sana katika Tanzania hii ya Kidemokrasia na akakiletea Chama Ushindi mkubwa kwenye chaguzi za usoni,
Watu wote ni mashahidi kwa kipindi chake hiki kifupi cha kuwa mkuu wa Wilaya ya Kilosa tayari ameanza kuyaunganisha makundi yote kwa falsafa yake ya Maendeleo kwa Wote nahapa naamini kuwa Uongozi ni kipaji ( inborn ) hakika huyu Bwana anakipaji cha Uongozi,
Kuendelea kumweka Shaka kwenye Wilaya ni matumizi mabaya ya rasilimali watu hasa kipindi hiki cha Siasa huru za mikutano ya hadhara na Chaguzi Huru na Haki,
CCM kwa sasa lazima itumie zaidi watu wenye ushawishi wa kisiasa na mvuto kwa wapigakura/Wananchi zaidi ya CV na majina yaliyozoeleka Serikali kwa miongo yote Kama tunania ya kukivusha salama Chama 2024 & 2025,
WanaJf Mtakumbuka Upinzani walifurahi sana baada ya Shaka kuondolewa kwenye Uenezi wa Chama huku CCM wakipigwa na butwaa,Siku zote ukiona adui yako anafurahia maamuzi yako rudi kayatazame Upya maamuzi hayo,
Kunamambo yakubishaniwa Ila kamwe sio Uhodari na Uchapakazi wa kijana huyu Mzalendo wa kweli kwa Taifa lake na Rais wake Shaka Hamdu Shaka,