Rais Samia ajiuzulu na kama hataki kujiuzulu basi asigombee tena, ni janga kwa Taifa kiuchumi na kiustawi wajamii!

kipumbwi

JF-Expert Member
Feb 3, 2015
3,057
8,722
20240123_184254.jpg
Update14 February;baada ya mwezi kuanza kuranguliwa wananchi sukari.. Je mkoa ulipo sukari kilo shs ngapi?!!
20240214_124316.jpg

Hoja kuu:
Kwenye uchumi wowote hupimwa kwa mfumko wa bei(inflation rate) wa bidhaa sokoni, mfumuko wa bei unapozidi zaidi ya 50% uchumi unakua hatarini.

Kwa hali ya nchi hivi Sasa ilivyo basi kwa nchi za wenzetu na watu walio serious na ustawi wa jamii na uchumi basi serikali kuu ilipaswa kuachia ngazi, aidha kwa rais kuvunja Baraza la mawaziri na kusuka upya ama Rais mwenyewe kujiuzulu.

Yaliwahi kutokea haya pale Uingereza pindi nchi ilipoyumba kiuchumi kwa mfumuko mkubwa wa bidhaa baada ya suala la BREXIT, hali iliyopelekea Waziri Mkuu Boris kujiuzulu na Mawaziri wakuu wawili wakajiuzulu ndani ya mwaka mmoja na nusu na ikapelekea Uingereza kua na Mawaziri wakuu watatu ndani ya miaka miwili.

Hapa kwetu kila kitu kwa sasa bei ghali, mfumuko wa bei ni maradufu,kuanzia daladala, mabasi ya mikoani, vifurushi vya simu (uhuni zaidi huku package zimepunguzwa unavhopata ila unalipia hela ile ile automatically ni mfumuko wa bei kwani unapata MB 500 kwa shs 1000 ilihali zamani ilikua unapata 1GB).

Tunapoongea hapa sasa hivi kununua sukari Tanzania hii ni anasa, bei ya sukari kilo moja unapata bia 3 na chenji inabaki, mfuko mmoja wa Cement kutoka Tsh. 13,000 mpaka Tsh. 17,000 mpaka 23,000 mikoa ya Kanda ya ziwa.

Serikali inatazama tu,waziri anasingizia mafuriko ya mvua,miaka yote mvua inanyesha na mfumuko mkubwa hivyo hakuna,kama sio wizi ni nini?!!

Mvua zinanyesha kila mahali, bado umeme ni wa mgao ilihali tunaambiwa mabwawa hayana maji- kama sio wizi ni nini? Yote haya ili watu wale hela za umma kupitia mitambo ya SONGAS, IPTL na mitambo ya gesi ndio maana umeme wa mabwawa ambayo 100% ni ya serikali wanahujumu kwani hakuna mabilioni ya kugawana.

Hali ya uchumi kwa Watanzania inahujumiwa na serikali? Kama Rais Samia hanufaiki na hafurahii haya kwa nini hatokezi kulisimammia?

Enzi za Magufuli Sukari iliadimika kwa wiki kama 2 na bei ikafika shs 4000-5000 na mara moja Magufuli alitoa tamkoa kua atafuta vibali vyote vya wauza sukari kama hawatoshusha bei, bei ilishuka na ikauzwa Tsh. 2800 mpaka alipoingia madarakani Rais Samia ambapo bei imekua maumivu kwa Watanzania.

Kuna watu wanasema Samia hana uchungu na Tanganyika, ndio maana hajali, kwani Zanzibar sukari kilo moja ni Tsh. 2000-2500 ilihali bara huku 5000-6000. Zanzibar hakuna mgao wa umeme, huku Tanganyika ambapo kunazalishwa umeme na kupeleka Zanzibar umeme mgao mtupu.

Rais Samia hafai kuongoza tena, anawaza uchaguzi tu na ya kubaki madarakani na ndio maana tumemsikia akitoa tamko Majeshi yajiandae.

Viongozi bora huwaza current and next generation, viongozi wabovu huwaza kufanya miradi ya corruption na how to rig next election!
 
Achawehu wako wewe. Kwa hiyo umetoka huko na kichaa chako na kuanza kubandika hivyo vikaratasi vyako.

Suala la sukari serikali ilishalitolea ufafanuzi kupitia wizara ya kilimo ,ikiwa ni pamoja na kuelezea sababu ya upungufu wa sukari hapa nchini pamoja na hatua ambazo serikali imechukua kukabiliana na Changamoto hiyo. Ambapo serikali imeagiza na inaingiza nchini tani za sukari zaidi ya laki moja kuanzia mwezi huu na kuanza kusambazwa nchini.kumbuka kuwa kwa sasa tuna upungufu wa Tani elfu 30 kwa hiyo zikija hizo tani laki moja maana yake suala la upungufu wa sukari litakwisha mara moja.

Fahamu ya kuwa matumizi ya sukari hapa nchini kwa siku ni tani 1500. Kwa hiyo kuingia kwa maelfu ya tani hizo nchini yatafanya bei ya sukari kushuka chini haraka sana na kurejea katika hali yake ya kawaida.

Serikali ya Rais Samia imefanya kazi kubwa sana katika kukabiliana na mfumuko nwa bei katika bidhaa mbalimbali hapa nchini. kama unazo akili kichwani mwako na huna matatizo ya kupoteza kumbukumbu basi embu jaribu kuangalia na kufuatilia bei ya kilo moja ya unga ilikuwa shilingi ngapi mwezi kama huu mwaka jana na sasa bei ya unga ni shilingi ngapi sokoni.utakachogundua ni kuwa hali ya bei ya mwaka huu ni nzuri na isiyo na maumivu kwa mwananchi.

Ukienda katika kila eneo unaona namna ambavyo Mheshimiwa Rais na serikali yake wamefanyia Kazi suala la mfumuko wa bei na kuwa katika hali nzuri
 
Achawehu wako wewe. Kwa hiyo umetoka huko na kichaa chako na kuanza kubandika hivyo vikaratasi vyako.

Suala la sukari serikali ilishalitolea ufafanuzi kupitia wizara ya kilimo ,ikiwa ni pamoja na kuelezea sababu ya upungufu wa sukari hapa nchini pamoja na hatua ambazo serikali..

Matusi hayasaidii,wehu na vichaa kama nyie ambao mnalipwa kutetea mambo ya hovyo na propaganda mnazidi kumchafua mnaemtetea,jifunzeni kwa @pascalmayala
 
Kwa kifupi kabisa, Mama amepoteza kabisa mwelekeo. Shida yake kubwa ni kukaribisha MAJOKA chumbani. JPM aliyafukuza MAJOKA yoye na hakutaka kuyapa nafasi kabisa, lakini mama alipopata tu nafasi hiyo akayatafuta MAJOKA yote popote yalipokuwa na kuyasogeza miguuni pake. Sasa yanalitafuna Taifa.

Kwa hakika mama hawezi tena kuyakemea MAJOKA hayo. Kujikomboa kutoka katika hali hii ngumu ya maisha inayosababishwa na haya MAJOKA ni kupitia njia kadhaa tu:

1. Watanzania wote kuvaa ujasiri na kusema "sasa basi" kwa kauli ambayo mtu yeyote awaye yote ataelewa.

2. Mungu mwenyewe aingilie kati.
 
Naunga mkono hoja msingi wa matatizo yote uliyoyataja ni weak government ya Samia.

Ila hapo kwa ‘Boris Johnson’ hakujiuzuru kwa ridhaa yake wala sababu ulizotaja.

Kilichomtoa ni shinikizo kutoka ndani ya chama chake na media influence on public opinion kwa kupakwa matope kwa vitu ambavyo ‘havina kichwa wala miguu’ (mbinu zao za usalama wa taifa), wakishakuona ni threat for national security.

Kwanini usalama wao walimtoa, japo ‘civil service’ ya U.K. aina mandate ya kuongoza nchi ila wana influence kubwa kwenye siasa zao. Fanya yote usiende kinyume na national security advice.

Boris ana rafiki yake anaitwa ‘Evgeny Lebedev’ ni mfanyabiashara tajiri mzaliwa wa uingereza (na raia) lakini wazazi wake (baba anaitwa, Alexander Lebedev) walikwenda U.K. kama wahamiaji kutoka Russia ni matajiri.

Sasa fanya yote U.K. lakini sio kumiliki mainstream media hasa widely circulating news papers au news channel. Awachukulii huo uwekezaji poa unapofanywa na foreigners kwa sababu wanaelewa nguvu ya media kwenye ku influence social thinking.

Huyo ‘Alexander Lebedev’ alinunua moja ya magazeti ambalo popular ila lilikuwa linatengeneza hasara kwa muda, ivyo biashara ikawa kama anaiendesha kwa hela yake mfukoni. Hapo sasa waingereza wakashuku zaidi lazima kuna mkono wa Kremlin sio bure.

Baba mtu amesharudi Russia huyo kijana wake ‘Evgeny Lebedev’ ndio anamiliki hizo assets kwa sasa na ni rafiki wa karibu wa Boris. Urafiki wao ni wa karibu sana to the point of dislike from national security ya U.K. kwa mtu mwenye nafasi nzito kama Boris toka akiwa waziri wa mambo ya nje.

Mara kadhaa Boris akiwa waziri wa mambo ya nje alikuwa akienda Crimea baba mtu anapoishi kwa sasa. Anaenda bila wasaidizi kwa sababu ni private trips anafikia kwenye hotel ya kifahari wanayomiliki hao Lebedev’s.

Jamaa wa usalama wakawa na wasiwasi na Boris anaweza kuongea UK international policies akiwa mwenyewe huko bila ya kuangaliwa. Baadae tena wakati wa uchaguzi wa mwisho huyo rafiki yake alimchangia kwenye campaign ya uchaguzi wakati anatetea kiti cha uwaziri mkuu, hela ambazo wanadai zimechangishwa kwa warusi.

Aliposhinda uchaguzi Boris akapendekeza rafiki ‘Evgeny Lebedev’ awe lord. Baada ya kufanyiwa vetting usalama ukamkataa kwa madai baba yake yupo karibu sana na Kremlin. Boris akakataa hoja zao kwa madai wanamzushia tu akamteua ivyo ivyo.

Hapo sasa ndio usalama wakamuanzishia vitimbi vya party gate, wasaidizi wake (civil servant) wengine waliokuwa watu wake wa karibu nao wakaanza kumponda kwa vitu vya kijinga, mara wabunge wa chama chake hawana imani nae, anapigwa na bad publicity kwenye media zao hasa bbc kwa vitu vya kijinga, mpaka mwenyewe akakubali yaishe; I love U.K. politics.
 
Achawehu wako wewe. Kwa hiyo umetoka huko na kichaa chako na kuanza kubandika hivyo vikaratasi vyako.

Suala la sukari serikali ilishalitolea ufafanuzi kupitia wizara ya kilimo ,ikiwa ni pamoja na kuelezea sababu ya upungufu wa sukari hapa nchini pamoja ...
Unawaita watu hawana akili ila wewe ni kiazi sana. Hili suala la sukari ni la kutengenezwa ambalo mmelitengeneza wenyewe.

Kuna watu waliomba kuruhusiwa kuingiza sukari ni zaidi ya miezi minne Sasa na wakanyimwa Vibali. Binafsi namjua mfanya biashara aliomba kibali cha kuingiza Tani laki 2 akakosa Vibali.

Kwa taarifa yako Hadi hivyo Vibali vinavyotolewa watu wamevifanya mtaji bila kuwa na pesa hupati kibali. Na inasemekana Abdul ndio amepata pa kupigia dili. Ili update kibali unamuona Abdul kwanza.

Nimalize Kwa kusema sukari kutoka Brazili ni tsh1450 CIF ikifika mtaani watu wanafnaya yao.
 
Kwa kifupi kabisa, Mama amepoteza kabisa mwelekeo. Shida yake kubwa ni kukaribisha MAJOKA chumbani. JPM aliyafukuza MAJOKA yoye na hakutaka kuyapa nafasi kabisa...
Hiyo namba 1 nafasi yake kesho tokeni tukaandamane
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom