Rais Ramaphosa amuahidi Rais Magufuli kwamba atachukua Walimu wa Kiswahili toka Tanzania

Shigganza

Senior Member
May 24, 2018
160
412


Leo tarehe 26 Mei 2019, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Joseph Magufuli amekutana na kufanya Mazungumzo na Rais wa Afrika kusini, mhe. Cyril Ramaphosa Ikulu jijini Preteria. Katika Mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine amempongeza kwa kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya tano wa Afrika kusini na amemhakikishia kuwa Tanzania itadumisha uhusiano na ushirikiano wa kindugu na kihistoria ulioasisiwa na Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere na Hayati Nelson Mandela kupitia vyama vya ANC na CCM.

Kadhalika mhe Rais alibainisha kuwa anatarajia kukua kwa uhusiano wa Tanzania na Afrika kusini utakua katika masuala ya kiuchumi pamoja Kiswahili. Kabla ya Mazungumzo hayo Wazir wa Mambo ya Nje Palamagamba Kabudi alimkabidhi mhe. Ramaphosa zawadi ya vitabu vya kusoma na kufundishia Lugha ya Kiswahili kutoka Chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM)

Kwa upande wake Rais wa Afrika kusini alimshukuru Rais Magufuli kwa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwake na kufuatia uamuzi wa Afrika kusini kuanza kufundisha Lugha ya Kiswahili, Nchi yake itachukua walimu wa Kiswahili kutoka Tanzania ili watumike kufundisha katika shule za Msingi na Sekondari.

Nampongeza sana mhe. Rais wa ushawishi wake alioufanya ili kurejesha fursa ya Watanzania kupata ajira za kufundisha Lugha ya Kiswahili Nchini Afrika kusini ambayo wakenya walitaka kuijuchukua ambapo hivi karibuni iliripotiwa wakenya kadhaa kuajiriwa Nchini Afrika kusini kufundisha Kiswahili, licha ya ukweli kwamba linapokuja suala la umahiri wa Lugha kitaaluma watanzania tupo vizuri ikilinganishwa na majirani zetu hao kwa kuwa Lugha hiyo ni ya pili kwa Watanzania wengi na inatumika kufundishia kwa elimu ya Msingi, na ni somo mojawapo kwa ngazi ya kidato cha Sita na vyuo vikuu.

Rai yangu ni kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Wizara ya kazi, Ajira na Maendeleo ya vijana, ziandae utaratibu mzuri utakaowezesha kupatikana kwa walimu wenye sifa nzuri na watakapo kwenda huko wahakikishe wanafanya kazi kwa bidii, maarifa na ubunifu ili kujenga imani kubwa kwa Afrika Kusini dhidi ya walimu kutoka Tanzania, wasipofanya hivyo tusishangae, Nchi hiyo ikachukua uamuzi wa kujaribu walimu kutoka Mataifa mengine ambao wanaweza kujituma zaidi ya wa kwetu na hivyo kuchukua fursa hiyo.

Mabalozi wetu mlioko katika mataifa ya Nje wekeni kipaumbele cha kwanza kwenye Diplomasia ya uchumi, kila hafla ya kuapishwa kwa balozi Rais amekuwa anasisitiza mabalozi wetu kusaka fursa za kiuchumi zilizopo nje kwa taifa letu lakini nashawishika kuamini baadhi yao bado wamepiga usingizi wa pono, msaidieni Rais ili Watanzania wengi tunufaike na taifa kwa ujumla.

IMG_1838.jpg
IMG_1837.jpg
IMG_1839.JPG
 
Soma heading na ulichoandika kama vinafanana...S.Africa imeahidi kuajiri waalimu wangapi kutoka Tanzania? Wataanza kazi lini? Nijibu kwanza hayo maswali mawili...
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 26 Mei, 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Mhe. Cyril Ramaphosa, Ikulu Jijini Pretoria.

Katika Mazungumzo hayo, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mhe. Rais Ramaphosa kwa kuapishwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Afrika Kusini na amemhakikishia kuwa Tanzania itadumisha uhusiano na ushirikiano wa kidugu na kihistoria na nchi hiyo ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Mwl.Julius Kambarage Nyerere na Hayati Nelson Mandela kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha ANC (African National Congress).

Mhe. Rais Magufuli amemshukuru, Mhe Rais Ramaphosa kwa kumkaribisha kufanya nae mazungumzo siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Afrika Kusini na amebainisha kuwa anatarajia uhusiano wa Tanzania na Afrika Kusini utaimarishwa zaidi katika masuala ya uchumi na kukuza lugha ya Kiswahili.

Kwa upande wake, Mhe. Rais Ramaphosa amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwake, na amemhakikishia kuwa Afrika Kusini inatambua mchango mkubwa wa Tanzania katika ukombozi wa Taifa hilo na kwamba katika kipindi chake cha uongozi wake atauendeleza na kuuza zaidi uhusiano huo.

Mhe. Rais Ramaphosa amesema kufuatia uamuzi wa Afrika Kusini kuanza kufundisha lugha ya Kiswahili, nchi yake itachukua walimu wa Kiswahili kutoka Tanzania ili watumike kufundisha somo hilo katika shule za msingi na sekondari.

Aidha, Mhe. Rais Ramaphosa ameahidi kufanya Ziara Rasmi ya Kitaifa nchini Tanzania kabla ya Mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) uliopangwa kufanyika mwezi Agosti 2019 nchini Tanzania Na pia atahudhuria mkutano huo.

Kabla ya mazungumzo hayo Mhe. Rais Magufuli ambaye ameongozana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amemkabidhi Mhe. Rais Ramaphosa zawadi ya vitabu vya kusoma na kufundishia lugha ya Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Mhe. Rais Magufuli na Mhe. Rais Ramaphosa wamefanya mazungumzo hayo ikiwa ni kabla Mhe. Rais Ramaphosa hajatangaza Baraza lake la Mawaziri.
61145615_110608370037716_2143124710811313675_n.jpeg
IMG_20190526_180309.jpeg
IMG_20190526_180312.jpeg
 
Tulizembea sana, any way hongera zake rais

Isipokuwa umekosea ulioandika nafasi zetu.... hapana sio zetu Ila niushindani anaeshinda soko anapata ajira, iwe Kenya ama Tanzania
 
Soma heading na ulichoandika kama vinafanana...S.Africa imeahidi kuajiri waalimu wangapi kutoka Tanzania? Wataanza kazi lini? Nijibu kwanza hayo maswali mawili...

..alipokuja Waziri Mkuu wa ETHIOPIA zilitolewa ahadi kama hizi.

..Ni hivi, bila kujua KIINGEREZA itakuwa vigumu sana kupata ajira ya kufundisha Kiswahili huko nje.

..Wakenya wanatupiga bao kwasababu wanajua Kiingereza na Kiswahili, sisi waTz tumeng'ang'ania Kiswahili peke yake.
 
Leo tarehe 26 mei 2018 Rais wa Jamhuru ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Joseph Magufuli amekutana na kufanya Mazungumzo na Rais wa Afrika kusini, mhe. Cyril Ramaphosa Ikulu jijini Preteria. Katika Mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine amempongeza kwa kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya tano wa Afrika kusini na amemhakikishia kuwa Tanzania itadumisha uhusiano na ushirikiano wa kindugu na kihistoria ulioasisiwa na Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere na Hayati Nelson Mandela kupitia vyama vya ANC na CCM.

Kadhalika mhe Rais alibainisha kuwa anatarajia kukua kwa uhusiano wa Tanzania na Afrika kusini utakua katika masuala ya kiuchumi pamoja Kiswahili.

Kwa upande wake Rais wa Afrika kisini alimshukuru Rais Magufuli kwa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwake na kufuatia uamuzi wa Afrika kusini kuanza kufundisha Lugha ya Kiswahili, Nchi yake itachukua walimu wa Kiswahili kutoka Tanzania ili atumike kufundisha katika shule za msingi na Sekondari.
Hii ni 2019 sio 2018 chalii alafu maongezi yachai usiyakurupukie kutaftia credits nikama nimwambie mtoto ntakuletea gari babake aadithie ukoo wake wote. Acheni upimbi
 
Vizuri....faida za kusafiri ni kama hizo, unakutana na watu wanakupa madili
Nilikuwa napata tabu kuelewa kenya itoe waalimu wa kiswahili kwenda kufundisha Afrika Kusini , wakati hapa nchini tuna hazina ya kutosha ya wataalamu wa lugha hii ya kiswahili, sina shaka na Kenya lakini ingekuwa si sahihi kwa Afrika kusini kusahau mchango wa Tanzania wakati wanapigania uhuru wao kutoka kwa wakoloni, sasa hivi kidogo wamefanya jambo jema, cha msingi nadhani ni wakati sasa wa Mheshimiwa Rais kuanza kutembea duniani , fursa haziji ila hutafutwa, asingesafiri sidhani kama hiyo fursa ingepatikana Tanzania, Shukrani🙏🏼
 
Nilikuwa napata tabu kuelewa kenya itoe waalimu wa kiswahili kwenda kufundisha Afrika Kusini , wakati hapa nchini tuna hazina ya kutosha ya wataalamu wa lugha hii ya kiswahili, sina shaka na Kenya lakini ingekuwa si sahihi kwa Afrika kusini kusahau mchango wa Tanzania wakati wanapigania uhuru wao kutoka kwa wakoloni, sasa hivi kidogo wamefanya jambo jema, cha msingi nadhani ni wakati sasa wa Mheshimiwa Rais kuanza kutembea duniani , fursa haziji ila hutafutwa, asingesafiri sidhani kama hiyo fursa ingepatikana Tanzania, Shukrani🙏🏼
Kenya nao wana waalimu wa Kiswahili mkuu,waliposikia walipeleka watu wao kwenda ku lobby huko
Tanzania kama wamelala usingizi wa pono mi sitawalaumu Afrika Kusini kwa kuchukua Kenya
 
Hapa kuna kitu mwandishi kakosea kwa vijana wa humu,
Kuna kachama kakataja basi hapo mada yote imehalibika.
 
Ongera mheshimiwa raisi kwa kwenda huko na kukutana na fursa muhimu ila tunaomba utembee na nchi nyingine tofauti tofauti hili tupate fursa tofauti na iyo ya uko south Africa
 
Back
Top Bottom