BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,020
Date::11/3/2009Rais Mstaafu Benjamin Mkapa atajwa katika kesi ya kina Mramba
Rais Mstaafu awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, jina lake limetajwa katika kesi ya akina Mramba.
Na Tausi Ally
Mwananchi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana ilielezwa kuwa Rais mstaafu Benjamin Mkapa ndiye aliidhinisha mchakato wa kuiajiri Kampuni ya Alex Stewart uendelee kwa haraka.
Hayo yalielezwa mbele ya jopo la mahakimu watatu lililokuwa likiongozwa na hakimu John Utamwa wakati Wakili Hurbet Nyange alipokuwa akimhoji shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka Godwin Nyelo (4.
Nyelo ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na masuala ya Uchumi wa Wizara ya Nishati na madini ni shahidi wa kwanza kwa upande wa mashtaka kutoa ushahidi wake katika kesi ya kutumia madaraka vibaya na kuisababishia hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni serikali inayowakabili Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Gray Mgonja.
Hata hivyo shahidi huyo alisema Rais Mkapa alihusika katika kukubali mchakato huo uendelee haraka baada ya Wakili Nyange kumuonyesha dokezo na kumtaka asome sehemu ya dokezo hilo naye kufanya hivyo mahakamani hapo.
Dokezo hilo lilikuwa limeandikwa kutoka kwa Daniel Yona ambaye kwa wakati huo alikuwa Waziri wa Nishati na Madini kwenda kwa Rais huyo wa serikali ya awamu ya tatu.
Akimhoji shahidi huyo, Wakili Hurbert na mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo:
Wakili Nyange: Waziri wako Daniel Yona alikuwa na wajibu wa kutii wakubwa wake?.
Nyelo: Ndiyo.
Wakili Nyange: Mkubwa wake wa kazi akisema jambo hili lina uharaka na wewe unasema halina uharaka atamsikiliza nani?.
Nyelo: Mkubwa wake.
Wakati mahojiano hayo yakiendelea Wakili Nyange alimuonyesha Nyelo dokezo aliloliandika Yona kwenda kwa Rais na kumtaka shahidi huyo asome jibu linalodaiwa kuwa ni la Rais.
Shahidi huyo alilisoma kuwa “Nakubali endeleeni haraka.
Wakili Nyange: Baada ya kusoma Waziri angeweza kusitisha huo mchakato?.
Shahidi: Waziri asingeweza kusitisha huo mchakato kwa sababu ya uharaka.
Wakili Nyange: Uliwahi kuuona mkataba uliotengenezwa na kwenye upande wa malipo ulikuwa na tofauti na jinsi mlivyopendekeza kama kamati?.
Shahidi Nyelo: Hapana.
Wakili Nyange: Katika ule mkataba ambao serikali iliingia na Alex Stewart uliona kama kuna kipengele kilikuwa na matatizo au tofauti na mlivyokubaliana?.
Shahidi: Kipengele kilichokuwa na matatizo ni cha ada tu vingine vilikuwa sawa.
Wakili Nyange: Maneno yako ya kuwa hapakuwepo na bajeti kati ya mwaka 2003 na 2004 ya kuilipa kampuni ya Alex Stewart, wewe na ripoti ya bunge kipi ni sahihi?.
Shahidi: Yote ni sahihi.
Wakili Nyange: Nikikwambia kuwa kampuni ya Alex Stewart ilishindwa kufanya kazi yao kutokana na makampuni ya madini kukataa kukaguliwa hadi hapo walipoonywa na waziri wa fedha?.
Shahidi: Ni sawa kabisa waziri wa fedha aliwaonya.
Wakili Nyange: Unakumbuka kampuni ya Alex Stewart ilikataa taarifa za hesabu za makampuni yaliyoonyesha hasara?.
Shahidi: Hilo sikumbuki.
Wakili Nyange: Unakumbuka sababu iliyoongeza mkataba wa Alex Stewart toka mwaka 2005 hadi 2007 ili kuwawezesha kumaliza kazi yao ni kutokana na ukosefu wa ushirikiano kati yake na wachimbaji hao.
Shahidi: Hiyo ni moja ya sababu.
Wakili Nyange: Unafahamu Nyaraka zaidi ya 6000 zilifichwa ili kampuni ya Alex Stewart isizione katika kuhakiki?.
Shahid: Inawezekana ikawa hata zaidi ya hiyo.
Wakili Nyange: Hivi una habari nyaraka hizo zilikuwa zikifichwa na kampuni hizo kwa ajili ya kukwepa kodi na kwamba hilo liligunduliwa na kampuni ya Alex Stewart?.
Shahidi: Hilo najua.
Wakili Nyange: Unajua kama kampuni ya Alex Stewart iligundua kampuni za Blacr Dom na kampuni ya Resolute zilishindwa kuthibitisha matumizi yao ya dola 160 ambayo yalikuwa hayaeleweki kwa sababu nyaraka husika zilikuwa katika makao makuu yao ambayo hayapo hapa Tanzania?.
Shahidi: Hapana.
Wakili Nyange: Unajua Nyaraka hizo ilitakiwa zibaki hapa hapa nchini.
Shahidi: Najua
Wakili Nyange: Wewe ulishauri vipi?.
Shahidi: Alex Stewart asipewe mkataba.
Wakili Nyange: Unamsaliti Waziri , Katibu Mkuu na kamati nzima mliyokaa?.
Shahidi: Hapana.
Wakili Nyange: Picha unayotaka mahakama iioneni ipi?.
Shahidi: Kile nilichokishauri kwenye kamati ndicho nilichomshauri Waziri.
Kwa upande wa mahojiano kati ya wakili Casbert Tenga na Shahidi Nyelo yalikuwa kama ifuatavyo;
Wakili Tenga: Hayo mapendekezo uliyoyatoa yanaashiria zoezi zima lifutwe?.
Shahidi: Sawa.
Wakili Tenga: Unakubali kuwa mapendekezo hako ya kufuta zoezi zima na wakati wa kusaini mkataba ulikuwa umefika hiyo aina madhara kwa kamati?.
Shahidi: Itakuwa na madhara.
Hakimu Utamwa aliiahirisha kesi hiyo hadi leo mahojiano hayo kati ya mawakili wa upande wa utetezi na shahidi yatakapoendelea.
Shahidi huyo wa kwanza kwa upande wa mashtaka ambaye kwa sasa ni mwajiriwa wa kampuni ya madini ya Uranes Tanzania Limited awali akitoa ushahidi wake alidai ushauri wake wote alioutoa kuhusiana na mchakato huo wa kuiajili kampuni ya Alex Stewart haukuzingatiwa kwa sababu mambo mengi aliyaona katika utendaji wa kampuni ya hiyo na kwamba aligundua hawakusaidia kuimarika kwa udhibiti na usimamizi wa maandizi.
Alidai hakukuwepo na mabadiliko yoyote katika utendaji uliokuwepo awali kabla ya kampuni hiyo kuajili, ilipoajiliwa na ilipomaliza muda wake na kufanyiwa tathmini(Evaluation).
Alidai katika dokezo la Mei 26,2003 la majadiliano ya kuweka mfumo wa kudhibiti uzalishaji wa dhahabu kuwa kutokana na mambo yalikuwa yanajitokeza ilibidi kufanywe mabadiliko kwenye zabuni za awali ili ziendane na matakwa yao.
Kwa mujibu wa dokezo hilo, Nyelo alidai majadiliano waliyofanya na wadau wengine yalionyesha kuwa hawakuwa na uharaka wa kuingia mkataba na kampuni hiyo kabla ya kuona utaratibu uliokuwa unatumiwa na nchi nyingine. Alidai kwa kuwa lengo lilikuwa ni kuongeza mapato ya serikali kulipa kampuni asilimia 1.9 ni sawa na kupunguza mapato na hivyo kuondoa maana ya zoezi zima na kwamba kwa kuwa kunadalili ya kampuni hiyo ya Alex Stewart kutokuwa wawazi kwa maelezo yao alipendekeza wasipewe kazi hiyo.
Rais Mstaafu awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, jina lake limetajwa katika kesi ya akina Mramba.
Na Tausi Ally
Mwananchi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana ilielezwa kuwa Rais mstaafu Benjamin Mkapa ndiye aliidhinisha mchakato wa kuiajiri Kampuni ya Alex Stewart uendelee kwa haraka.
Hayo yalielezwa mbele ya jopo la mahakimu watatu lililokuwa likiongozwa na hakimu John Utamwa wakati Wakili Hurbet Nyange alipokuwa akimhoji shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka Godwin Nyelo (4.
Nyelo ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na masuala ya Uchumi wa Wizara ya Nishati na madini ni shahidi wa kwanza kwa upande wa mashtaka kutoa ushahidi wake katika kesi ya kutumia madaraka vibaya na kuisababishia hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni serikali inayowakabili Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Gray Mgonja.
Hata hivyo shahidi huyo alisema Rais Mkapa alihusika katika kukubali mchakato huo uendelee haraka baada ya Wakili Nyange kumuonyesha dokezo na kumtaka asome sehemu ya dokezo hilo naye kufanya hivyo mahakamani hapo.
Dokezo hilo lilikuwa limeandikwa kutoka kwa Daniel Yona ambaye kwa wakati huo alikuwa Waziri wa Nishati na Madini kwenda kwa Rais huyo wa serikali ya awamu ya tatu.
Akimhoji shahidi huyo, Wakili Hurbert na mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo:
Wakili Nyange: Waziri wako Daniel Yona alikuwa na wajibu wa kutii wakubwa wake?.
Nyelo: Ndiyo.
Wakili Nyange: Mkubwa wake wa kazi akisema jambo hili lina uharaka na wewe unasema halina uharaka atamsikiliza nani?.
Nyelo: Mkubwa wake.
Wakati mahojiano hayo yakiendelea Wakili Nyange alimuonyesha Nyelo dokezo aliloliandika Yona kwenda kwa Rais na kumtaka shahidi huyo asome jibu linalodaiwa kuwa ni la Rais.
Shahidi huyo alilisoma kuwa “Nakubali endeleeni haraka.
Wakili Nyange: Baada ya kusoma Waziri angeweza kusitisha huo mchakato?.
Shahidi: Waziri asingeweza kusitisha huo mchakato kwa sababu ya uharaka.
Wakili Nyange: Uliwahi kuuona mkataba uliotengenezwa na kwenye upande wa malipo ulikuwa na tofauti na jinsi mlivyopendekeza kama kamati?.
Shahidi Nyelo: Hapana.
Wakili Nyange: Katika ule mkataba ambao serikali iliingia na Alex Stewart uliona kama kuna kipengele kilikuwa na matatizo au tofauti na mlivyokubaliana?.
Shahidi: Kipengele kilichokuwa na matatizo ni cha ada tu vingine vilikuwa sawa.
Wakili Nyange: Maneno yako ya kuwa hapakuwepo na bajeti kati ya mwaka 2003 na 2004 ya kuilipa kampuni ya Alex Stewart, wewe na ripoti ya bunge kipi ni sahihi?.
Shahidi: Yote ni sahihi.
Wakili Nyange: Nikikwambia kuwa kampuni ya Alex Stewart ilishindwa kufanya kazi yao kutokana na makampuni ya madini kukataa kukaguliwa hadi hapo walipoonywa na waziri wa fedha?.
Shahidi: Ni sawa kabisa waziri wa fedha aliwaonya.
Wakili Nyange: Unakumbuka kampuni ya Alex Stewart ilikataa taarifa za hesabu za makampuni yaliyoonyesha hasara?.
Shahidi: Hilo sikumbuki.
Wakili Nyange: Unakumbuka sababu iliyoongeza mkataba wa Alex Stewart toka mwaka 2005 hadi 2007 ili kuwawezesha kumaliza kazi yao ni kutokana na ukosefu wa ushirikiano kati yake na wachimbaji hao.
Shahidi: Hiyo ni moja ya sababu.
Wakili Nyange: Unafahamu Nyaraka zaidi ya 6000 zilifichwa ili kampuni ya Alex Stewart isizione katika kuhakiki?.
Shahid: Inawezekana ikawa hata zaidi ya hiyo.
Wakili Nyange: Hivi una habari nyaraka hizo zilikuwa zikifichwa na kampuni hizo kwa ajili ya kukwepa kodi na kwamba hilo liligunduliwa na kampuni ya Alex Stewart?.
Shahidi: Hilo najua.
Wakili Nyange: Unajua kama kampuni ya Alex Stewart iligundua kampuni za Blacr Dom na kampuni ya Resolute zilishindwa kuthibitisha matumizi yao ya dola 160 ambayo yalikuwa hayaeleweki kwa sababu nyaraka husika zilikuwa katika makao makuu yao ambayo hayapo hapa Tanzania?.
Shahidi: Hapana.
Wakili Nyange: Unajua Nyaraka hizo ilitakiwa zibaki hapa hapa nchini.
Shahidi: Najua
Wakili Nyange: Wewe ulishauri vipi?.
Shahidi: Alex Stewart asipewe mkataba.
Wakili Nyange: Unamsaliti Waziri , Katibu Mkuu na kamati nzima mliyokaa?.
Shahidi: Hapana.
Wakili Nyange: Picha unayotaka mahakama iioneni ipi?.
Shahidi: Kile nilichokishauri kwenye kamati ndicho nilichomshauri Waziri.
Kwa upande wa mahojiano kati ya wakili Casbert Tenga na Shahidi Nyelo yalikuwa kama ifuatavyo;
Wakili Tenga: Hayo mapendekezo uliyoyatoa yanaashiria zoezi zima lifutwe?.
Shahidi: Sawa.
Wakili Tenga: Unakubali kuwa mapendekezo hako ya kufuta zoezi zima na wakati wa kusaini mkataba ulikuwa umefika hiyo aina madhara kwa kamati?.
Shahidi: Itakuwa na madhara.
Hakimu Utamwa aliiahirisha kesi hiyo hadi leo mahojiano hayo kati ya mawakili wa upande wa utetezi na shahidi yatakapoendelea.
Shahidi huyo wa kwanza kwa upande wa mashtaka ambaye kwa sasa ni mwajiriwa wa kampuni ya madini ya Uranes Tanzania Limited awali akitoa ushahidi wake alidai ushauri wake wote alioutoa kuhusiana na mchakato huo wa kuiajili kampuni ya Alex Stewart haukuzingatiwa kwa sababu mambo mengi aliyaona katika utendaji wa kampuni ya hiyo na kwamba aligundua hawakusaidia kuimarika kwa udhibiti na usimamizi wa maandizi.
Alidai hakukuwepo na mabadiliko yoyote katika utendaji uliokuwepo awali kabla ya kampuni hiyo kuajili, ilipoajiliwa na ilipomaliza muda wake na kufanyiwa tathmini(Evaluation).
Alidai katika dokezo la Mei 26,2003 la majadiliano ya kuweka mfumo wa kudhibiti uzalishaji wa dhahabu kuwa kutokana na mambo yalikuwa yanajitokeza ilibidi kufanywe mabadiliko kwenye zabuni za awali ili ziendane na matakwa yao.
Kwa mujibu wa dokezo hilo, Nyelo alidai majadiliano waliyofanya na wadau wengine yalionyesha kuwa hawakuwa na uharaka wa kuingia mkataba na kampuni hiyo kabla ya kuona utaratibu uliokuwa unatumiwa na nchi nyingine. Alidai kwa kuwa lengo lilikuwa ni kuongeza mapato ya serikali kulipa kampuni asilimia 1.9 ni sawa na kupunguza mapato na hivyo kuondoa maana ya zoezi zima na kwamba kwa kuwa kunadalili ya kampuni hiyo ya Alex Stewart kutokuwa wawazi kwa maelezo yao alipendekeza wasipewe kazi hiyo.