Rais Magufuli: Siwezi kusikiliza madai ya malipo yoyote wakati kuna malipo hewa kila kona

Afadhali yao hao waalimu walau viongozi wao wanajinasibu kuwatetea. Viongozi wa vyama vingine hawasikiki kabisa utafikiri hawapokei makato ya wanachama. Nina wasiwasi sana na mienendo ya hivi vyama vya wafanyakazi, wanachama mwishowe wataona hakuna haja ya kuchangia chama kisichoweza kuwatetea. Haiwezekani wafanyakazi wanakatwa madeni ya mikopo ya HESLB kinyume na kiwango walichoafikiana napia zaidi ya kiwango cha makato halafu hivyo vyama havikemei wala kuwatetea.
Umesema vizuri mkuu. Kama vyama vyote vingechachamaa kudai haki za wanachama wao serikali ingesikiliza tu. Tukumbuke umoja wetu ndio nguvu yetu. Watumishi wote nchi hii wakigoma serikali haitakuwa na namna zaidi ya kulipa stahiki zao.

Sent from my TECNO P5 using JamiiForums mobile app
 
Umesema vizuri mkuu. Kama vyama vyote vingechachamaa kudai haki za wanachama wao serikali ingesikiliza tu. Tukumbuke umoja wetu ndio nguvu yetu. Watumishi wote nchi hii wakigoma serikali haitakuwa na namna zaidi ya kulipa stahiki zao.

Sent from my TECNO P5 using JamiiForums mobile app
Ni kweli kabisa. Ipo haja ya kuangalia upya aina ya viongozi wa vyama vya wafanyakazi tulio nao. Wameshapoteza sifa za kuongoza na wengi wanaonekana kama mamluki. Haiwezekani mtu anajitapa kwa kutokujali stahiki za wafanyakazi halafu wakae kimyaa kama hawasikii na kuona kinachoendelea. Halafu mtu huyohuyo anaalikwa na wafanyakazi kuja kuwasanifu sikukuu ya Mei Mosi! Hapa tuna mamluki sio viongozi.
 
Kwa walimu wanyooshwe tu maana wakati wa kampeini huwa wanaweka akili mfukoni japo siyo wote ila wengi wa walimu hawajielewei. Mliahidiwa laptop mkashangilia, wacha namba isomwe tu.
 
mnyonge mnyongeni lkn haki yake mpeni.. ikiwa mtu anastahili kulipwa n alipwe tu ,hakuna namna.
 
Kwa nafasi yake rais JMT ni mkuu wa menejiment ya utumishi wa uma, yaan ndio mwajiri wa watuishi wa umma. Sasa ana mwaka na zaidi ofisini, kama kuna malipo hewa bado hana tofauti na waliotengeneza malipo hewa aliyoyakuta, maana kama bado kuna malipo hewa yanatokea chini ya utawala wake. La pili ni kujitangaza kuwa u kiongozi dhaifu kupita kiasi. unajua unalipa watu hewa na bado unaendelea kufanya hivyo tukueleweje. La tatu siyo isu ya kutishana wala kubembelezana. Malipo kwa watumishi wa serikali kama ilivyo kwa sekta binafsi ni ya kisheria wala si ya kukuomba. Ni nidhamu ya woga kiongozi wa nchi kutangaza hutishi na mtu wakati watu wanadai malipo yao ambayo yapo kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma. Tafakari chukua hatua kisheria na sio kutisha watu
 
Duh mimi nilihamishwa mwaka 2013 sijalipwa hela ya uhamisho mpaka sasa kwa kauli hii ya Mhe.Rais basi tena
 
mambo mengine ni ya ki.jinga kweli,hewa hewa utadhani wao wnaolipwa malipo hewa walikuwa chini ya uongozi wa chama cha chadema
 
hivi unawezaje kutumia mwaka mzima kuhakiki watumishi wasio zidi 500,000 huku uhakiki unafanyika kwa njia ya mtando! mbona huyu JPM anataka kutufanya watu wote ni wajinga wasio jielewa
 
JPM akihutubia umati wa watu Leo hii Mjini Lindi amesema serikali yake siyo ya kutishwa tishwa na hivyo hawezi kusikiliza madai yoyote wakati kuna Malipo hewa kibao kila Kona.

Mishahara Hewa, Matibabu Hewa, Malipo ya Uhamisho Hewa.. Hewa hewa hewa!


Maoni yangu:

Juzi nilisikia viongozi wa walimu wakitangaza mgogoro na Serikali. Kwa hotuba hii poleni sana walimu wote kwani mkuu hatishwi kabisa na kelele za Nyau.

Mtalipwa tukimaliza Hewa! Poleni Sana.

Inaonesha kipind cha nyuma walikuwa wanakioana kizembe kizembe sana...... Taaratbu za malipo si zina fahamika kwann zisifuate, pale wanapogundua kuna udanganyfu... Taaratbu zipo
 
Sasa bila kusikiliza unajuaje kama ni hewa au sio hewa? Je, uhakiki ukiiisha hewa haiwezi kurudi? Je, hiyo hewa inadhibitiwa vipi? Kwa nini malipo yasilipwe kwa sasa wakati hewa ikidhibitiwa? Je, mfano madai hayo kama sio hewa, fedha ipo ya kuwalipa kwa sasa?
 
Kama tutasimama upande wa haki, basi tutakubaliana Kwamba anacho fanya Rais ni sahihi kwa sbb idara, wizara, taasisi,manispaa, n.k zilikuwa zimeoza na zilikuwa zikifanya malipo/matumizi ya hovyo hovyo. Hivyo lawama zote za awamu hii zipelekwe awamu iliyopita
 
Jamaaa ana roho mbaya sana anatamani hata hiki kidogo atunyang'anye. Yeye lengo ni wananchi wawe masikini wa kupitiliza ili kumrahisishia kwenye uchaguzi w@ 2020.si unaona anagawa pesa kwa kila anapopita. Anatamani yeye awe wazir, bunge, mahakama, polisi . Hii ni hatariii sana. Amejigeuza ni mtawala wa kiimla na si kiongozi aliechaguliwa na watu.Daaah waswas wangu asije akazuia mishahara ya watumishi mpaka 2020.
 
Back
Top Bottom