Mwanachama Sahihi
JF-Expert Member
- Apr 3, 2015
- 536
- 164
Hizo ndege atapanda nyingi tu
Jambo la kufurahisha ni kwamba amefuta karibu mashangingi yote. Msafara una toyota hilux double cabin za kutosha! Haya ni mabadiliko makubwa.
So what's the big deal here?
KAMA MLINUNULIWA NA MAJIZI mlitaka tufanyeje! hamkuwa na mgombea mlikuwa na pazia mtegemee kwenda ikulu! ifikie hatua mjitambue mliingia mkengeKama kuna mtanzania anafikiri atapata mabadiliko kupitia CCM atasubiri sana. Sana sana ni mabakora, mabomu ya machozi, n.k. Yaani tunadanganywa kiasi hata cha kwenda kupiga kura huku tukijua ni danganya toto tu. Unaekuja hapa ukibeza utalibeza hata kaburi lako, ila utajikuta ndani na kufunikwa na udongo kidogo tu kama utakuwa umebakia. Ninasema hivyo kwa sababu makaburu wanajua tuna dhahabu nyingi sana na wana miaka mitano bado ya kujibebea bure. Tembo walishaishia sasa ni kobe.
Kama yalishanunuliwa usipoyatumia unaokoa nini?
Hapana, hatuwezi kudanganyika kirahisi. Alipaswa kuanza na mabilioni ya pesa za kwenda kutibu chunusi India. Kutumia barabara ni kuokoa pesa kiogo sana , pengine sawa na nauli ya mh mmoja kwenda London
Hizi ni stunt za kuamsha taifa baada ya kuona, kuna huzuni, kutoridhika, manung'uniko na taifa limegawanganyika
Anachotakiwa ni kuliunganisha taifa si kuanza na vitu vidogo vidogo vya kumjengea umaarufu wa haraka
Asimame na kuangalia taifa lilipo na ajiulize kama ndivyo wenzake walivyopokea nchi siku za nyuma
Asikimbie ukweli kuwa uchaguzi , kampeni, matokeo n.k. vimeacha makovu makubwa makuba sana katika umoja wa taifa
Huo ni ukweli anaotakiwa kukabiliana nao na si popularity ya vitu vidogo vidogo
Tatizo si spea wala vipuri, ni jinsi taifa lilivyogawanyika na changamoto ya kukosa kuungwa mkono na sehemu ya jamii
Ni jinsi wananchi wanavyoangaliana kwa misingi ya kubaguana, chuki n.k. Jinsi chuki ilivyobobea na kuleta yale ya Geita
Aunganishe taifa hili lililogawanyika kwanza ili aungwe mkono. Kinyuime chake kila jambo analofanya litakuwa Big G
Mwacheni ajiamlie, angenunua labda ndege nzuri au kutumia ndege mngesema kakimbia barabara alizosimamia
Sasa kawapiga bao na kuonyesha wananchi na dunia alichosimamia kinafaida mnaanza kubwetuka na maajabu yenu.
Mumuache Rais wetu.
Eti foleni aaagh leteni lingine
Mtanyooka tu
Ikija A mnaongea B, ikija B mnasema ni X na ikiletwa mnang'aka eti ni Z ..yaaani mpaka Mungu mwenyewe mnamchanganya
Du, hili povu latoka wapi?Hatutaki wala hatuna haja ya kujuwa ulichomaanisha.
Unachomaanisha/ulichomaanisha wewe kitatusaidia nini sisi zaidi ya wewe kujaribu kutujaza ujinga ulionao?
Tunataka ukweli.
Hivi wewe ni mwandishi wa habari za ukweli? Au udaku?
Wengine huwa hatudanganyiki.
angetumia helcopter angepunguza zile vurugu za misongamano isiyo na lazima
kuna watu wataponda tu yaani kila kitu wao ni kupinga kila kinachofanywa na JPM