Rais Magufuli awaapisha Mabalozi wateule Kipilimba, Bana, Mbennah na Milanzi

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,908
51,907

1578995369792.png


Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli awaapisha Mabalozi wateule wafuatao :-

4EB5AFA9-B168-408F-9E5C-47026908CD72.jpeg


1. Meja Jenerali Mstaafu Gaudence Milanzi kuwa Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini

2. Dkt. Modestus Francis Kipilimba kuwa Balozi wa Tanzania Nchini Namibia

3. Profesa Emmanuel David Mwaluko Mbennah kuwa Balozi wa Tanzania Nchini Zimbabwe

4. Dkt. Benson Alfred Bana kuwa Balozi Tanzania Nchini Nigeria.

Hafla ya uapisho inafanyika Ikulu Jijini Dar es salaam.



Rais Magufuli awakataza Mabalozi kuaga aga ovyo ”Ikiwezekana ndani ya wiki 2 muwe mmeshaenda kwenye nchi mkatuwakilishe”

Rais Magufuli ameyabainisha hayo leo Januari 14, 2020, mara baada ya zoezi la kuwaapisha Mabalozi wa nchi nne ikiwemo Zimbabwe, Nigeria, Afrika Kusini pamoja na Namibia, hafla iliyofanyika Ikulu ya Jijini Dar es Salaam, na kumuagiza Waziri wa Mambo ya Nje kuhakikisha barua za Mabalozi hao zinapatikana haraka ili waweze kwenda kufanya majukumu yao waliyopangiwa.

“Ninajua siku za nyuma kulikuwa na tabia ya watu, akishateuliwa Ubalozi atakaa tena anazunguka maofisi kwenda kuaga kwa Rais, Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Nje wengine wanaenda hadi kwa Wakurugenzi na Wakuu wa Mikoa, ikiwezekana ndani ya wiki 2 muwe mmeshaenda kwenye hizo nchi ambazo mtatuwakilisha” amesema Rais Magufuli.

F7953C81-F9D9-429F-979D-DE87C29EAB16.jpeg


Walioapishwa leo ni Meja Jenerali Mstaafu, Gaudence Milanzi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Dkt Modestus Francis Kipilimba kuwa Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Profesa Emmanuel David Mwaluko Mbennah, kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe pamoja na Dkt Benson Alfred Bana kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria.

=====

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 14 Januari, 2020 amewaapisha Mabalozi 4 aliowateua hivi karibuni kuiwakilisha Tanzania katika nchi za Afrika Kusini, Namibia, Zimbabwe na Nigeria.

Walioapishwa ni Mej. Jen (Mstaafu) Gaudence Salim Milanzi anayekuwa Balozi wa Tanzania Pretoria - Afrika Kusini, Dkt. Modestus Francis Kipilimba anayekuwa Balozi wa Tanzania Windhoek – Namibia, Prof. Emmanuel David Mwaluko Mbennah anayekuwa Balozi wa Tanzania Harare – Zimbabwe na Dkt. Benson Alfred Bana anayekuwa Balozi wa Tanzania Abuja – Nigeria.

Baada ya kuwaapisha, Mhe. Rais Magufuli amewataka kuripoti katika vituo walivyopangiwa ndani ya wiki 2 kuanzia sasa na amewasisitiza kwenda kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria, kwa kuzingatia maslahi ya Taifa hasa kiuchumi na kuwawezesha Watanzania kupata ajira katika fursa zilizopo katika nchi hizo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amewataka Mabalozi hao kufuatilia maeneo yote ambayo Mhe. Rais Magufuli alikubaliana na Waheshimiwa Marais wenzake alipotembelea nchi hizo hivi karibuni, na pia kuitangaza vyema Tanzania ambayo kwa sasa inapiga hatua kubwa katika maeneo mengi.

Hafla ya kuapishwa kwa Mabalozi hao imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.

Kabla ya kuwaapisha Mabalozi hao, Mhe. Rais Magufuli ameongoza kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

14 Januari, 2020
 
Wangempeleka kenya, South Africa au Marekani akaibe technology na kujifunza

Kwanini wote tulitawaliwa wote na wenzetu wametuacha mbali ? Au ujasusi maana yake nini?

Tunatakiwa kuinvest sana kwenye ujasusi wa kiuchumi. sio utekaji! Nchi ya kijinga sana mtu kama Kapilimba aliyebobea kwenye IT anatumika kuteka watu badala ya kwenda kuiba technolojia angalau ya kutengeneza hata wembe.
 
Ni katika muendelezo wa kutekeleza ahadi yake ya kuimarisha diplomasia ya Tanzania kwa lengo la kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili Watanzania.

Leo Rais Magufuli amewaapisha wateule wanne ambao watakua mabalozi wa Tanzania katika nchi mbalimbali barani Afrika.

Wateule hao ni Meja Jenerali (MST) Gaudence Milanzi (Afrika Kusini), Dkt. Modestus Kipilimba (Namibia), Prof. Emmanuel Mbennah (Zimbabwe), na Dkt. Benson Bana (Nigeria).

Katika miaka minne ya uongozi wake uliotukuka, zaidi ya Watanzania 500 wamepata ufadhili wa kusoma nje ya nchi ambapo fursa za biashara baiana ya Tanzania na nchi mbalimbali zimeimarika sana.
 
Sijawaona wakuu wa mihimili mingine, yaani Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai na Mahakama Mh.Jaji Mkuu kuwepo ktk shughuli za kawaida za kiserikali kama hii ya leo, je maoni ya wanaJamiiforums yameanza kuzingatiwa ?

Tutegemee sasa viongozi wa mihimili ya dola kukosekana ktk shughuli kama hizo kinyume ilivyokuwa mazoea ya siku za karibuni wanaCCM kushurutisha uwepo wao kwa manufaa ya CCM kufifisha utendaji huru wa kazi za mihimili hiyo muhimu ktk kujenga dola na taifa imara.
 
Back
Top Bottom