Rais Kikwete azindua Sera ya Elimu na Maabara

Serikali jana imetangaza elimu bure kuanzia primary hadi sekondary na kwa shule za private bei elekezi kutolewa! Pia baada ya maabara nguvu kuelekezwa nyumba za walimu! Elimu ya msingi miaka 10.

Hilo ni jambo jema kabisa nakubali, lakini je kwanini limekuja wakati huu kuelekea uchaguzi mkuu? Je, ilisubiri uchaguzi tu? Kama si kampeni ya CCM ni nini?

Ukitaka kujua yaliyojiri jana soma magazeti ya leo : Majira, Mtanzania....n.k
Kwa upande mwingine ni Afadhali kulipia karo kuliko hii bure inayotangazwa. Unajua shule ya msingi ni bure, lakini hiyo michango ni zaidi ya karo na ni kero kweli kweli. Sekondari ada inayofutwa ni 20,000/= lakini pia kulikuwa na michango ya karo; na hivi sasa Ikiondolewa hiyo basi ujue michango itaongezeka. Waulize hata BRN wanalijuwa hilo maana ni moja ya mikakati yao.
 
Ulinzi watalinda askari,
Hakuna Tour,
ujenzi inajenga serikali,
mock bure kwanza siyo Lazima,
Hakuna mahafari,
Ukarabati kazi ya serikali,
Afya hospital zipo.
Unafikri kwa kutumia kigegedwa!!
 
Sisi Watanzania sio wakweli hata kidogo,huwezi sema elimu ya sekondari na msingi bure. wakati huo hupeleki ruzuku ya uendeshaji kwenye shule,hivi sasa utaona kwa mwezi kwa kichwa cha mtoto wa wanapeleka ruzuku shilingi 200,itaboresha vipi elimu? Unakuta shule haina vyoo vya wanafunzi na ina vyumba 2 au 5. Vya madarasa,nyumba moja ya walimu,halafu watu wote wapo kimya sio watumishi wa umma,wanasiasa wala raia.Elimu ya Tanzania iko njia panda!
 
Kwa upande mwingine ni Afadhali kulipia kero kuliko hii bure inayotangazwa. Unajua shule ya msingi ni bure, lakini hiyo michango ni zaidi ya kero na ni kero kweli kweli. Sekondari ada inayofutwa ni 20,000/= lakini pia kulikuwa na michango ya kero; na hivi sasa Ikiondolewa hiyo basi ujue michango itaongezeka. Waulize hata BRN wanalijuwa hilo maana ni moja ya mikakati yao.

Duh! Nimepata shida hapo kwenye neno kero, mwanzo nilijua umechapia kumbe unamaanisha kuwa Karo au ada ndo kero hiyo hiyo kwa maana inakera wananchi! Kama hivyo ndivyo basi ni sawa! Nimekusoma mkuu!
 
Kuna mambo yanatia kichefuchefu na ni ngumu sana kuamini kama maamuzi ya namna hii yanafanywa kupitia tafiti za kitaalamu au ni mihemko ya kisiasa ambayo italigharimu taifa siku za usoni:

a) Walimu na madarasa/nyumba hawatoshi kwa shule zilizopo sasa, tumesharukia kuzipeleka shule za msingi kuwa za sekondari pia!! Kuna shule hazina vyumba vya kutosha, walimu wenye taaluma (achilia mbali idadi), hatuna maabara wala vitabu vya kiada na ziada.
b) Kufuta mitihani ya darasa la 7 na msisitizo kuwekwa kwenye mtihani wa form 4. Kama watu wanafika darasa la 7 bila kujua kusoma wala kuandika, mtu huyu anastahili vipi kuingia elimu ya sekondari??
c) Inashangaza umuhimu uliowekwa kwa kiswahili, lugha ambayo inatumika katika mawasiliano ya kijamii lakini matumizi yake si ya kitaaluma kwa kiasi kikubwa. Dunia imeshatekwa na Kiingereza, na uamuzi huu si tena wa vita ya "colonial legacy" bali ni kujichimbia shimo refu hatutaweza kutoka. Wakati dunia inaenda kuwa kijiji kimoja, sisi tunaona ni muda muafaka kurudi kwenye shimo letu na kukaa huko. Imesemwa mara nyingi kuwa ni kuenzi lugha ya Kiswahili lakini ni ukweli sasa kuwa wakubali wameshindwa kuendeleza kiingereza kutokana na udhaifu wa kiutendaji. Na sasa wanapanua matumizi ya kiswahili ambayo yatawaondoa watu katika ulimwengu wa kisasa!!

d) Utaona mlolongo wa uuaji wa makusudi wa elimu. Kuwa na Div. 5, kufuta mitihani ya Darasa la 7 na sasa elimu kuwa ya miaka 11 mfululizo bila mitihani ya kuchuja!! Wanachotaka ni kuwa na watu watakaojiita wamemaliza form 4. Hao wamefikishwa hapo na matatizo lukuki ya mfumo wetu wa elimu!!

A sad day indeed!!
 
Hata barabara nyingi zilizokuwa mbovu kwa miaka yote 4 sasa zinakarabatiwa kama si kuwekwa lami mpya ya kichinachina.
 
Hii michango atalipa nani,,?
1. Caution money
2. Ulinzi
3. Afya
4. Ujenzi.
5. Thamani
6. Vifaa vya usafi
7. Mahafali.
6. Tour
7. Ukarabati
8. Mitihani ya MOCK, INTER SCHOOL
9. ETC.

Utalipa ww mzazi!!!
 
  • Thanks
Reactions: 999
Hali ya shule za msingi ni mbaya sana sasa wakati wazazi wanachangia. Itakuwaje hii michango ikiondolewa? Au wakisema elimu ni bure maana yake ni kuwa wamefuta ada lakini michango mingine inaendelea kutegemeana na mahitaji ya shule?

Kuhusu kufutwa kwa mtihani wa darasa la saba (kama ni kweli), lengo ni nini? Tunataka kuwa na watu wengi waliomaliza sekondari au walioelimika? Sujaisoma lakini inaonekana Sera hiyo inahimiza quantity bila kujali ubora (quality).
 
Nakumbuka kwenye uchaguzi Wa 2010 Waziri Maghembe alitoa tangazo la kufuta mtihani Wa darasa la saba kienyeji kwa lengo la kujipatia kura. Safari hii wamewahi kidogo kutangaza.
 
Kuna mambo yanatia kichefuchefu na ni ngumu sana kuamini kama maamuzi ya namna hii yanafanywa kupitia tafiti za kitaalamu au ni mihemko ya kisiasa ambayo italigharimu taifa siku za usoni:

a) Walimu na madarasa/nyumba hawatoshi kwa shule zilizopo sasa, tumesharukia kuzipeleka shule za msingi kuwa za sekondari pia!! Kuna shule hazina vyumba vya kutosha, walimu wenye taaluma (achilia mbali idadi), hatuna maabara wala vitabu vya kiada na ziada.

Kwenye dunia inayobadilika, kila kitu kinabadilika pia. Miaka ya 60 kuna elimu ya darasa la nne kulitosha kukupa kazi ya usimamizi.juu ya hapo hata umeneja ulikuwa size yako.

Marekani miaka ya 60, asilimia ndogo sana ya wananchi wake walikuwa na Master's degree, Specialization haikuwepo. Ukifanya SEARCH kidogo tu@ utagundua kuwa 50 years later, asilimia ya wenye Master's sasa hivi marekani ni sawa na asilimia ya waliokuwa na bachelors degree miaka ya 60. Sasa Tanzania ikiendelea kuifanya elimu ya sekondari kuwa "luxury" watakuwa wanafanya makosa. Tunahitaji watu wengi zaidi wafike sekondari, ikiwezekana kila mtoto anayezaliwa Tanzania afike walao elimu ya sekondari.

Ukitazama hata sasa hivi Tanzania, kuwa na degree ya kwanza si lolote tena, kwani specialization inafanyika kwenye Master level. Hivyo kuendelea kuchuj awatu wasifike chuo kikuu sio suluhisho, suluhisho ni kuongeza quality ya wanaofika,pamoja na kuwawezesha walimu.

If i were in their position, i would allocate over 20% of national budget on basic education, kuanzia "high school",private sector wanaweza ku-cover hili gap. Serikali ihakikishe kuwa kila mtanzania anayesoma kwa miaka 11, anafahamu kitu flani. Hili haliwezekani kwa kuweka focus kwenye mitihani isiyo na kichwa wala miguu

b) Kufuta mitihani ya darasa la 7 na msisitizo kuwekwa kwenye mtihani wa form 4. Kama watu wanafika darasa la 7 bila kujua kusoma wala kuandika, mtu huyu anastahili vipi kuingia elimu ya sekondari??

Kama walimu hawajawezeshwa na focus ipo kwenye mitihani, hili ni rahisi kutokea, focus ya walimu irudi kwenye process, na sio kwenye results. Hakuna mtu mjinga kabisa duniani asiyefundishika, wengi huchukua muda tofauti kujifunza.

Napongeza uamuzi wa kuondoa focus kwenye mitihani, katika level ambayo mwanafunzi anatakiwa a-focus kwenye kuelewa na kupata ujuzi-basic, hivi humu kila mtu angewekewa mtihani wa kujifunza jinsi ya kutembea,kula,kuongea lugha inayotumika alipo, si ingekuwa problem?wengine wakisikia mtihani appetite ya kusoma inapotea.
Marekani wamefanikiwa kwa hili, na hata nchi kama Japan zenye mitihani, participation ya darasan (continuous) assesment ina uzito mkubwa sana, kiasi kwamba mtu anayeshiriki 100% darasani kwa maana ya mahudhurio,mazoezi ya kila siku anakuwa guarranteed at least 60% which is already passing grade.

Mitihani iwepo, ila isiwe alfa na omega.

Kwa sasa hivi huo mtihani wa darasa la saba umepoteza maana kwa private schools kwa kuwa nyingi huweka mitihani yao.wazazi wanalifahamu hili.

c) Inashangaza umuhimu uliowekwa kwa kiswahili, lugha ambayo inatumika katika mawasiliano ya kijamii lakini matumizi yake si ya kitaaluma kwa kiasi kikubwa. Dunia imeshatekwa na Kiingereza, na uamuzi huu si tena wa vita ya "colonial legacy" bali ni kujichimbia shimo refu hatutaweza kutoka. Wakati dunia inaenda kuwa kijiji kimoja, sisi tunaona ni muda muafaka kurudi kwenye shimo letu na kukaa huko. Imesemwa mara nyingi kuwa ni kuenzi lugha ya Kiswahili lakini ni ukweli sasa kuwa wakubali wameshindwa kuendeleza kiingereza kutokana na udhaifu wa kiutendaji. Na sasa wanapanua matumizi ya kiswahili ambayo yatawaondoa watu katika ulimwengu wa kisasa!!

This is one of the best decisions me thinks, Kiswahili hakiwezi kukua, kama tutaendelea kukitumia kama accessory, Hakuna maana kumlazimisha mtu ajifunze kwa kiingereza, halafu anafika form 4 hajaelewa kitu kwa kuwa lugha matatizo. Bora umfundishe kwa lugha anayoielewa, ili umuondolee barrier.

Mwanzo itakuwa ngumu, sana lakini baada ya miaka kadhaa tutafika. Wazazi wenye ku-prioritise kiingereza watapeleka watoto english medium.
Naamini kwa mtoto mwenye uwezo wa kujifunza kiingereza na kuelewa hahitaji kwenda english medium ili kuongea kiingereza vizuri.

d) Utaona mlolongo wa uuaji wa makusudi wa elimu. Kuwa na Div. 5, kufuta mitihani ya Darasa la 7 na sasa elimu kuwa ya miaka 11 mfululizo bila mitihani ya kuchuja!! Wanachotaka ni kuwa na watu watakaojiita wamemaliza form 4. Hao wamefikishwa hapo na matatizo lukuki ya mfumo wetu wa elimu!!

A sad day indeed!!

Big decisions are always controversial and will guarantee to shock, this could be the best thing to our education system, or it could be the worst.The devil is in the details and implementation.
I argue the government to push serious money in fundamental education, lets prioritize education in our budget. Lets make teaching something every intelligent Tanzanian aspires to do. lets go back to basics and inspire our youngsters to love reading and learning just for the sake of it.lets keep our youngsters think about their learning process more than they think about the results and the outcomes, for the best outcomes comes from good learning process.

I would start by increasing teachers remunerations, enhance schools budgets,expand schools auditing and priotritise learning infrastructures.

Kwa waajiri, it's time focus is put on students entire learning career not just 2 or 3 exams. lets make transcripts worthy and continuous assessment crucial.if it works in college education we can tickle it down to basic education.

NOTE:
I have strong reservations on these changes, and for me it takes someone with a lifetime mission and complete ownership of the process. I will respect our ministry if they pull this off in 10 years time,but i will never blame them for trying. for continuing in our current state is expressway to irrelevancy.
 
Last edited by a moderator:
Hii michango atalipa nani,,?
1. Caution money
2. Ulinzi
3. Afya
4. Ujenzi.
5. Thamani
6. Vifaa vya usafi
7. Mahafali.
6. Tour
7. Ukarabati
8. Mitihani ya MOCK, INTER SCHOOL
9. ETC.

9. Maji
10. Chakula

Huu ni utapeli wa kutosha.
Nasomesha mtoto shule ya kata lkn wakati anaingia form one nililipa more than 340, 000 Tshs ada ikiwa ni 20, 000 Tshs.
Nilijiuliza hii ndiyo shule ya kata?
Prof adanganye vilaza wenzake.
Kwa wale wasiojua shule ya kata wajiandae ku-less 20, 000 Tshs kwenye hiyo figure then ndiyo watamsoma prof kilaza vizuri
 
we mbugila kunandege inaenda kipawa?

ipo Inayoenda Uarabuni na CHINA kupeleka TWIGA na meno ya tembo toka Tanzania

View attachment 226794

Twiga.jpg

View attachment 226795


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
....sera za kichizi kwa machizi....elimu Tanzania sio bure.Mzazi na mtoto wanabeba gharama kubwa sana,mzazi gharama ya kuchangia,mtoto gharama ya kuwa maimuna.
 
Ndo sera inayorasimisha Kiswahili kuwa lugha ya kujufunzia na mawasiliano kwa sekondari na elimu ya juu? ? Au! !

Another bogus policy from a bogus government. Can Tanzanians seize the 2015 elections opportunity to help flush out of government these stooges! Lest we are all drowning!.
 
Ndugu wana bodi nimesoma kwenye magazaeti ya leo kuhusu kuongezwa kwa umri wa elimu ya msingi kutoka miaka saba mpaka kufikia miaka 13,

Kwangu ninachokiona hapa ni kuwa na ombwe ya kati ya walionacho na wasiokuwa nacho kutokana na mfumo waliouweka na kuweka kiswahili kiwe ndio lugha mama ya kufundishia wakati huu ulimwengu umekuwa kama kijiji hapa si lazima kumshika mtu sikio ni kujidanganya mchana kweupeee,

Turudi nyuma miaka ya sitini,sabini na themanini elimu Tanzania ilikuwa ndio msingi na ilikuwa bora tofauti na sasa hakukuwa na huyu ni mtoto wa masikini huyu ni mtoto wa tajiri akili na maarifa , juhudi na walimu wazalendo na makini waliokuwepo ndio ulimwezesha mtoto au msomi kufikia malengo tofauti na sasa.

Elimu ya sasa bila kumungunya maneno ukitaka mwanao apate elimu bora na ya uhakika basi mzazi huna budi kujiminya na kujinyima ili kumtafutia mwanao shule iliyo bora ambayo hupatikana shule binafsi, au za kidini na hapa ndipo yule mtoto wa mlalahoi anaposhindwa kupita kutokana na umasikini uliopo.


Zipo wapi zile.shule za vipaji maalumu zilizokuwepo enzi hizo ? Ambazo angalao zilikuwa ndio kimbilio la mtoto wa mnyonge? Inawezekana zilififishwa kwa makusudi ili upande wa pili uweze kuneemeka kwa kuwa shule nyingi zinawahusu watu wakubwa ama viongozi na nyingi zimekuwa zikiendeshwa kibiashara zaidi bila kuangalia wale wasiokuwa nacho wao waende shule za kata.

Nakuwa nahofu na hizi shule zetu zilizo chini ya serikali kama zitaweza kutupa kile tulicho hitaji ilituweze kwenda sawa katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia ilhali watoto wao wakisoma shule za kimataifa na academic halafu uje useme wataiboresha elimu hii ni ndoto na imekaa kisiasa zaidi

Aliyeshiba hawezi mkumbuka mwenye njaa na hapa ndipo tulipo kwa sasa tuna janga la elimu ya mlalahoi.
 
Suluhisho fanya kazi kwa bidii jikomboe pata fedha msomeshe mtoto wako ng'ambo. Inauma lakini ndio ukweli!
 
Back
Top Bottom